Reginald Mengi aungwe mkono, Bakhresa, Dewji Mh!!

Mkuu kwenye kutoa kuna mambo mawili, kuna wanaotoa kwa kutafuta sifa mbele ya jamii ili wakubalike. na ambao wanatoa kidini (ibada). Anayetoa kwa nia ya kukubalika mbele ya jamii atafanya kila njia kile anachotoa kionekane. Anayetoa kiibada (uislam na ukristo zote zina ibada ya kutoa) atatoa bila mbwembwe na huenda kwa kificho. Kuna watu leo hata wakitoa sahani ya wali wataalika media. Hata hivyo mi nimeshuhudia shule ambayo baadhi ya vyumba vimejengwa na SS Bakhresa eneo furani jijini dar ambapo pia ana kiwanda cha kuoka mikate kwenye eneo hilo. lakini huyu ndugu pia kuna raia wanamsubiri kila siku kwenye vituo vyake vya biashara na anawapa cash ili wajikimu na maisha
Ni sahihi kabisa mkuu, hata kwa sisi wakristo tunaambiwa unapotoa msaada ama sadaka hata mkono wa kushoto hupaswi kujua mkono wa kuume/kulia umetoa kiasi gani.kwa hiyo kwa wanaozingatia maadili kweli wanapotoa misaada hawatangazwi.
 
Mkuu upo Biased. Kwanza hii thread umeielezea kishabiki na kinyume chake, tajiri wa kwanza hapa bongo anaesaidia masikini na ameajiri wafanyakazi wengi ni BAKHRESA. huyu mzee hujui siri zake, ni mtu ambae anatoa mkono wa kushoto haujui kinachoedelea, sasa mkuu unataka dunia nzima wajuwe fulani katoa ili iweje, huyu jamaa hapendi misifa kama huyo mengi, na anaibiwa sana tu lakini hadropu,na biashara zake zinazidi kunawiri kuliko huyo mengi. Huyu mzee namkubali katika wafanyabiashara wote tanzania
Kweli mkuu bakhresa anatoa misaada mingi ila si wa kujitangaza kama Mr machache afanyavyo nadhan mleta mada huenda anatoka kanda moja na bwana huyo ndio maana anamfagilia. Pia huku singida Mr MO ametoa misaada mingi kama ujenzi wa mashule, kuchimba visima vya maji, kujenga misikiti n.k lakini hapendi kujitangaza. Kiimani ( kwa wakristo na waislam ) tunaambiwa unapotoa msaada usijitangaze tena hata mkono wa kushoto hupaswi kujua mkono wa kulia umetoa nn/ kiasi gan
 
Yaani huyu mengi hajaonekana miezi halafu anaibuka na kick ya tumilioni 25?,

Huyu mzee namfananisha na striker mmoja ivi anapenda sana sifa. Sasa hiyo m25 hata muuza ndizi anauwezo wa kuzitoa na asitangazwe. Inakera sana
 
As u said kuongozwa na dini, backhresa huwa hatangazi misaada yake kamwe! Mo dewji ana foundation kabisa.. Mengi kutangaza ndio style na hakuna kosa.
 
Bila shaka wee ni mchaga maan watu wa kaskazin kwa kumpgiaga upatu uyu mengi mpo vizuri..mtu anatajwa kuwa na utajiri zaid ya USD 300M kutoa msaada wa Tshs.25M ndo kelele zote hizo..misaada ya mzee mengi mingi lazima itangazwe,mm ni rc pure ila mbona naonaga mitaan bakhresa anawajengea muslim misikitin mingi tu yenye thaman zaid ya hyoo pesa kam msaada na sionagi wakimtangaza kwenye tv
Its true, juzi ametoa msaada wa orphage centres shinyanga almost 15 Mil lakini alikataa isitangazwe.
 
Bila shaka wee ni mchaga maan watu wa kaskazin kwa kumpgiaga upatu uyu mengi mpo vizuri..mtu anatajwa kuwa na utajiri zaid ya USD 300M kutoa msaada wa Tshs.25M ndo kelele zote hizo..misaada ya mzee mengi mingi lazima itangazwe,mm ni rc pure ila mbona naonaga mitaan bakhresa anawajengea muslim misikitin mingi tu yenye thaman zaid ya hyoo pesa kam msaada na sionagi wakimtangaza kwenye tv
Its true, juzi ametoa msaada wa orphage centres shinyanga almost 15 Mil lakini alikataa isitangazwe.
 
Kweli mkuu bakhresa anatoa misaada mingi ila si wa kujitangaza kama Mr machache afanyavyo nadhan mleta mada huenda anatoka kanda moja na bwana huyo ndio maana anamfagilia. Pia huku singida Mr MO ametoa misaada mingi kama ujenzi wa mashule, kuchimba visima vya maji, kujenga misikiti n.k lakini hapendi kujitangaza. Kiimani ( kwa wakristo na waislam ) tunaambiwa unapotoa msaada usijitangaze tena hata mkono wa kushoto hupaswi kujua mkono wa kulia umetoa nn/ kiasi gan

Haswaa
 
Nimeona kwenye taarifa ya habari ITV kuwa Reginald Mengi amechangia ujenzi wa kitua cha afya huko Mbeya shilingi milioni 25. Najiuliza huyu mzee ana moyo wa aina gani, au dini yake ndio imemjenga kuwa na huruma ya kuguswa na matatizo ya watu? Ameshachangia sehemu nyingi tu zaidi ya hiyo.

Hapa bongo tunao matajiri ambao tunakula bidhaa zao kila siku kama Bahresa na Mo Dewji na Manji. Hawa kazi yao ni kukusanya pesa tu lakini hakuna mrejesho kwa wananchi, mnatulisha masoda na majuice ambayo hayajengi afya bora zaidi ya kuleta magonjwa! kwanini basi msirudishe faida zenu japo sehemu kidogo kwa kusaidia sehemu zenye mahitaji kama shule, vituo vya afya nk?

Sijawahi kusikia hawa jamaa wamesaidia public au dini zao hawa zinafanana kwamba ukifanya biashara na kulipa kodi inatosha? kuna faida gani ya kuwa na tajiri namba moja kijana Katika Afrika ambaye hata maskini hawajivunii uwepo wako.

Fedha nyingi hazileti afya wala long life, sioni necessity ya ku accumulate wealth kiasi kikubwa bila kuwapa nafuu maskini somewhere kutoka katika faida unazozipata kwenye biashara zako. Mengi angekuwa na biashara ndogo ndogo wallahi ningeamua kumuunga mkono kwa kuuza bidhaa zake.

Bidhaa za Mo na Azam zimejaa kila kona nchini, lakini mrejesho hakuna zaidi ya ule wa kiuchumi kwamba ametengeneza ajira. Hawa matajiri wengine wanaona kitu cha maana kuchangia kwenye michezo kuliko kugusa roho za watu. Kwa kweli Mzee Mengi anapaswa kuungwa mkono kwa kila jambo.
mengi yupo vizuri anatoa msaada kukiwa na kamera kibao.....huo sio msaada tena ni kiki ndugu....au kwa imani yake ni sahihi kufanya hivyo....lkn kwa imani ya hao wengine uliowataja ukitoa msaada mbele ya kamera unapata nothing mbele ya mola wako...ukitoa iwe siri yako wewe na anayepewa tu...
 
Misaada kama hii uliyosema sio endelevu inazidi kuwafanya wabweteke. Msaada kama huo wa kusaidia shule kama anatoa hiyo ndio endelevu na pongezi kwake.

Mkuu unajuaje bakhressa hatoi misaada katika mahospitali,mashule nk? Au unataka dunia nzima ijue katoa? Dini yake hairuhusu hivyo unavyotaka wewe
 
Damu ni nzito kuliko maji

Mwarabu misaada yake anaipeleka uarabuni huko

Tummunge tu mkono ndugu yetu reginald mengi

Hao masinga singa wamekuja kuchuma kwa Wajinga

Na Bado kina makonda anawapa tenda hao wehu anawadharau wazawa
 
Musikiti inaleta tija gani kwenye jamii zaidi ya kuwa dojo za karate.
Misikiti inapunguza watoto wa zinaa,inapunguza wauza unga,inapunguza wavuta unga,inapunguza mimba za utotoni,inasaidia kukemea kukeketa,inakemea ufisadi,inamfundundisha mwanadamu dhima yake hapa duniani. Misikiti inamsaidia mwandamu kutafuta mali kwa njia za halali. Mkuu ukipata nafasi kiuchumi jenga misikiti na wahimize watu wahudhurie kwa wingi, maana humo ndimo jamii inapewa miongozo sahihi ya maisha
 
kuna jipu kubwa sana hapo katika udini huyu jamaa misaada imekaa kiudini sio kwa wote hata ajira zake kusa sifazote ila kuwa na moja tuu ya dini utapewa kazi

kwanzia mfagiaji hadi top ni muslim na je wasio na imani waajiriwe wapi?
Ni sahihi kabisa hasa yule Charles Hillary ni muislam tena mjahidina hasaaa
 
Bila shaka wee ni mchaga maan watu wa kaskazin kwa kumpgiaga upatu uyu mengi mpo vizuri..mtu anatajwa kuwa na utajiri zaid ya USD 300M kutoa msaada wa Tshs.25M ndo kelele zote hizo..misaada ya mzee mengi mingi lazima itangazwe,mm ni rc pure ila mbona naonaga mitaan bakhresa anawajengea muslim misikitin mingi tu yenye thaman zaid ya hyoo pesa kam msaada na sionagi wakimtangaza kwenye tv
shida za watanzania nikuwajengea misikiti na kuwagawia hela? kwanini mna akili ndogo ivi nimeona hata diamond anajisifu kajenga misikiti, watu hawana maji , hawana dispensary , watoto wanasomea chini ya miti eti mnajisifu kuwajengea misikiti
 
Matajiri wengi wa kiislam wao misaada yao ni kujenga misikiti na madrasa basi!

Hata Diamond kila akiulizwa katoa msaada gani kwa jamii atakutajia orodha ya misikiti aliyojenga ,na si orodha ya dispensary au visima vya maji au madarasa aliyojenga.Naona ndo dini yao inavyowafundisha kwamba misaada yao isiwaguse wakiristo
Unamjua Mustafa Sabodo, unajua aliwapa kiasi gani chadema wakachimbe visima? Tunasema kwamba MO na SSB ni walipa kodi wakubwa na wanachangia sana kwenye jamii lakini dini wanayoifuata haiwaruhusu kufanya matangazo wakati wa kutoa.
 
Unamjua Mustafa Sabodo, unajua aliwapa kiasi gani chadema wakachimbe visima? Tunasema kwamba MO na SSB ni walipa kodi wakubwa na wanachangia sana kwenye jamii lakini dini wanayoifuata haiwaruhusu kufanya matangazo wakati wa kutoa.
Mbona ni issue ndogo, sio lazima kusaidia, ni hiari,pia ni hiari kutangaza au kutotangaza. Sio kosa
 
Unamjua Mustafa Sabodo, unajua aliwapa kiasi gani chadema wakachimbe visima? Tunasema kwamba MO na SSB ni walipa kodi wakubwa na wanachangia sana kwenye jamii lakini dini wanayoifuata haiwaruhusu kufanya matangazo wakati wa kutoa.

Nimekupata vyema
 
shida za watanzania nikuwajengea misikiti na kuwagawia hela? kwanini mna akili ndogo ivi nimeona hata diamond anajisifu kajenga misikiti, watu hawana maji , hawana dispensary , watoto wanasomea chini ya miti eti mnajisifu kuwajengea misikiti
Mkuu hawa matajiri wanalipa kodi, hivyo usije na hasira zako kwakuwa tu kijiji unachoushi hakina zahanati na madarasa ya kutosha.watatoa zakka na sadaka zao kama wanavyotaka wenyewe, mahitaji mengine kamuone mkurugenzi wa wilaya yako
 
Mkuu unajuaje bakhressa hatoi misaada katika mahospitali,mashule nk? Au unataka dunia nzima ijue katoa? Dini yake hairuhusu hivyo unavyotaka wewe
Mkuu hujanielewa, nimemnukuu mtu pale akisifia misaada ya kuwapa omba omba pesa kila ijumaa nikasema hiyo sio endelevu. Nikasifia msaada wa kujenga baadhi ya vyumba vya madarasa ya mojawapo ya shule zilizo jirani na kiwanda chake (Mzee SSB). Ukikuta comment na ukiona mtu kamnukuu mtu kasome comment zote ili uelewe vizuri. Yaonesha wewe ulisoma kile kipande cha misaada midogo ya omba omba na kwa vile ulikuwa unasoma kwa hisia simpendi SSB nampondea basi hisia zako zikakufanya usione zile pongezi nilizompa mwishoni kwa ujenzi wa madarasa ktk comment hiyohiyo. Soma vizuri usiweke hisia mbele.
 
Nimeona kwenye taarifa ya habari ITV kuwa Reginald Mengi amechangia ujenzi wa kitua cha afya huko Mbeya shilingi milioni 25. Najiuliza huyu mzee ana moyo wa aina gani, au dini yake ndio imemjenga kuwa na huruma ya kuguswa na matatizo ya watu? Ameshachangia sehemu nyingi tu zaidi ya hiyo.

Hapa bongo tunao matajiri ambao tunakula bidhaa zao kila siku kama Bahresa na Mo Dewji na Manji. Hawa kazi yao ni kukusanya pesa tu lakini hakuna mrejesho kwa wananchi, mnatulisha masoda na majuice ambayo hayajengi afya bora zaidi ya kuleta magonjwa! kwanini basi msirudishe faida zenu japo sehemu kidogo kwa kusaidia sehemu zenye mahitaji kama shule, vituo vya afya nk?

Sijawahi kusikia hawa jamaa wamesaidia public au dini zao hawa zinafanana kwamba ukifanya biashara na kulipa kodi inatosha? kuna faida gani ya kuwa na tajiri namba moja kijana Katika Afrika ambaye hata maskini hawajivunii uwepo wako.

Fedha nyingi hazileti afya wala long life, sioni necessity ya ku accumulate wealth kiasi kikubwa bila kuwapa nafuu maskini somewhere kutoka katika faida unazozipata kwenye biashara zako. Mengi angekuwa na biashara ndogo ndogo wallahi ningeamua kumuunga mkono kwa kuuza bidhaa zake.

Bidhaa za Mo na Azam zimejaa kila kona nchini, lakini mrejesho hakuna zaidi ya ule wa kiuchumi kwamba ametengeneza ajira. Hawa matajiri wengine wanaona kitu cha maana kuchangia kwenye michezo kuliko kugusa roho za watu. Kwa kweli Mzee Mengi anapaswa kuungwa mkono kwa kila jambo.
pumba kweli wewe Mengi anatumia media zake kujikweza Bahresa na Dewji wanatoa zaidi ya huyo Mchaga ila hawapendi umaarufu

Fikili kabla hujatoka povu
 
Back
Top Bottom