Reginald Mengi aungwe mkono, Bakhresa, Dewji Mh!!

Reginald Mengi aungwe mkono, Bakhresa, Dewji Mh!!

kuna jipu kubwa sana hapo katika udini huyu jamaa misaada imekaa kiudini sio kwa wote hata ajira zake kusa sifazote ila kuwa na moja tuu ya dini utapewa kazi

kwanzia mfagiaji hadi top ni muslim na je wasio na imani waajiriwe wapi?

Kwa wafanyakazi tunaowajua kwa kuwaona kwenye Azam TV sijaona suala la udini. Udini unaleta wewe. Na hapo juu nilikwambia kuwa Bakhresa anatoa msaada kimya kimya sio kwa waislamu pekee ila dini yake ndo inamtaka asijitangaze.
 
Media ni kitu kizuri na kibaya sana: hakuna dini inayopenda mtu akitoa msaada kujitangaza, na kufanya hivyo ndio unatoka nje ya kusudio la kutoa msaada na badala yake kuonekana kama umejitangaza.
Sio wote watoao misaada wanapenda kijulikane walichotoa au kujulikana.
Tofautisha msaada na sadaka
 
Msitumie mgongo wa dini kama kisingizio, kiufupi ukishakua mfanyabiashara moja kwa moja unaingia kwenye kundi la matapeli, huwezi ukawa tapeli halafu ujidai unashika dini. Kama unafanya biashara, na hatukusikii umetoa msaada, basi hutoi, msijifiche kwenye dini, toeni misaada na tuione mkitoa, otherwise ni misaada hewa.
Wewe udini tu ndo unakusumbua wala hakuna kingine.

Endelea kuamini unachoamini ila wanaonufaika na misaada hiyo nao wanaamini kivyao. Pia chuki zako kwao ni chanzo cha maradhi ya moyo kwako na sehemu ya neema kwao kwani Mungu ndio anajua ukweli na Ataendelea kuwapa utajiri zaidi na zaidi
 
Nimeona kwenye taarifa ya habari ITV kuwa Reginald Mengi amechangia ujenzi wa kitua cha afya huko Mbeya shilingi milioni 25. Najiuliza huyu mzee ana moyo wa aina gani, au dini yake ndio imemjenga kuwa na huruma ya kuguswa na matatizo ya watu? Amesha changia sehemu nyingi tu zaidi ya hiyo. Hapa bongo tunao matajiri ambao tunakula bidhaa zao kila siku kama Bahresa na Mo Dewji na Manji. Hawa kazi yao ni kukusanya pesa tu lakini hakuna mrejesho kwa wananchi, mnatulisha masoda na majuice ambayo hayajengi afya bora zaidi ya kuleta magonjwa! kwanini basi msirudishe faida zenu japo sehemu kidogo kwa kusaidia sehemu zenye mahitaji kama shule, vituo vya afya nk? sijawahi kusikia hawa jamaa wamesaidia public au dini zao hawa zinafanana kwamba ukifanya biashara na kulipa kodi inatosha? kuna faida gani ya kuwa na tajiri namba moja kijana Katika Afrika ambaye hata maskini hawajivunii uwepo wako. Fedha nyingi hazileti afya wala long life, sioni necessity ya ku accumulate wealth kiasi kikubwa bila kuwapa nafuu maskini somewhere kutoka katika faida unazozipata kwenye biashara zako. Mengi angekuwa na biashara ndogo ndogo wallahi ningeamua kumuunga mkono kwa kuuza bidhaa zake. Bidhaa za Mo na Azam zimejaa kila kona nchini, lakini mrejesho hakuna zaidi ya ule wa kiuchumi kwamba ametengeneza ajira. Hawa matajiri wengine wanaona kitu cha maana kuchangia kwenye michezo kuliko kugusa roho za watu. Kwa kweli Mzee Mengi anapaswa kuungwa mkono kwa kila jambo.
anakulisha wewe na watanzania bila yeye mngekufa. unga chapa h. maziwa, ngano, chapati, mkate n.k
anakuletea mpaka nyumbani kwako, analipa kodi
 
Bila shaka wee ni mchaga maan watu wa kaskazin kwa kumpgiaga upatu uyu mengi mpo vizuri..mtu anatajwa kuwa na utajiri zaid ya USD 300M kutoa msaada wa Tshs.25M ndo kelele zote hizo..misaada ya mzee mengi mingi lazima itangazwe,mm ni rc pure ila mbona naonaga mitaan bakhresa anawajengea muslim misikitin mingi tu yenye thaman zaid ya hyoo pesa kam msaada na sionagi wakimtangaza kwenye tv
Unalenga nini?
 
Tofautisha msaada na sadaka
Sadaka ni kutoa chochote ulichonayo na kumpa yeyote, sio lazima awe muhitaji.

Msaada ni kutoa fungu lolote katika uwezo wako kwa ajii ya watu wenye uhitaji kwenye jamii au watu wenye mahitaji maalum.
Babumwerevu shkamoo[emoji15] [emoji15]
 
Mzee S.S Bakhresa umemuonea mkuu. Nilishawahi kuwa na mgonjwa alilazwa hospital ya Mwananyamala,kila asubuhi niliyokuwa pale kuna wafanyakazi wa Azam walikuwa wanapita wodini asubuhi na kugawa juice,keki na mikate kwa wagonjwa bureeee. Nilipohoji nikaambiwa huo ni utaratibu wa Azam katika baadhi ya Hospitali za umma.
Wadanganyika bana,mtu anapiga hela kibao mnapewa mandazii mnafurahiii! Huyu jamaa sina uhakika km analipa kodi kwy hayo majengo anayoyatumia!Mo km sikosei anadaiwa ni tra
 
Hao wote ulowataja ni Waislam, Katika dini ya kiislam ni mwiko kabisa kujionesha pale unapotoa Msaada (Swadaka). Kama upo Dar es Salaam nenda Ocean Road kawaulize wagonjwa wa Ocean Road Bakhrsa huwa anawapeleka nini pale Ocean Road wale wagonjwa kila mwenzi ! na MIDA GANI HUWA ANAENDA ! halafu rudi hapa ! na si hivo tu BAkhrsa ameajiri watanzania wangapi ambao wamebeba vichwa vingapi katika familia zao! halafu njoo hapa useme ! Kama hujui kitu bora ukae kimya!
 
Maelezo tata haya, jaribu kuyatia nyama kidogo maana wapo wenye mawazo potofu.

Hayo mawazo yao kila ramadhani bakheresa anagawa pesa na vyakula zaidi ya hapo anatoa sana misaada kwenye mahospital uzuri wa bakheresa hapendi kujitangaza ila tunaomjua tunajua ndio maana hata yeye mwenyewe wengi hawamjui
 
Sasa ukitoa then ukanyamaza wengine watajifunza vipi kuwa kuna ulazima wa kutoa jamani. Hapo mnaongelea suala la dini kutorusuhu kuonekana wakati wa kutoa lakini sio kweli kuwa dini inaruhusu kukwepa kulipa kodi, vile vile suala la kuwalipa wafanya kazi kiwango kidogo cha mshahara, ubaguzi wa dini na jamii ya watu fulani dini hairuhusu pia, kuajiri wahindi pekee na kuwaacha wazawa dini hairuhusu.
Mimi naona tukitoa misaada lazima tujitangaze ili wengine waige mfano.
 
Mkuu naona umekaa kidini zaidi kuliko kuelezea kijamii bila kujali dini Wala kabila ya mtu.

Kwa ufupi ni kuwa R. MENGI chochote akitaka kukifanya kituo chake cha Itv hakitaacha kurusha kama vile TBC kwa sizonje hata fake news wanatangaza bila kufanya uchunguzi.

Hao watu uliowataja kasoro Manji kwa sababu sina uhakika na itikadi yake ya kidini. Huwa wanatoa sana misaada ya kijamii na hakuna media inajua au hata wakijua hawatangazi.

Huku kwetu kuna mambo mengi tu Bakhresa amefanya kwa ajili ya ustawi wa jamii maskini so weka udini pembeni wahukumu kwa matendo Yao kwa sababu hakuna dini inayofundisha tajiri asimsaidie masikini.
 
Back
Top Bottom