Mbona hiyo video ni kama ya 2008 au macho yangu yana kijani sana?!!
Bw. John hebu jiulize maswali mepesi yafuatayo:-
- Kwa mwaka huo 2008, RC wa Arusha alikuwa nani?
- DC wa Arumeru alikuwa nani?
- RC wa sasa 2017 Gambo na DC Mnyeti mwaka huo walikuwa wapi?
- Rais wa sasa 2017 John Magufuli alikuwa na cheo gani wakati huo?
- Na mwisho, huyo E.P. Mollel alikuwa nani mwaka huo???
Mungu ni mwema sana, maovu na unafiki wa CCM wanaoufanya gizani kwa siri ametupa nafasi ya kuuona na kuusikia, angalau kwa sehemu ndogo tu. Hapo ni Arumeru, je Tanzania ina wilaya ngapi? Idara ngapi na kata na vijiji vingapi uhuni huu unaendelea kila siku?? Tanzania haiendelei kwa sababu ya
tatizo moja kubwa nalo ni CCM. Hicho kinachoitwa CCM ki ukweli ni furushi (chama?) moja kubwa lililobeba fitna, ujinga, chuki, rushwa na ufisadi, ushirikina nk nk. Ndugu zangu Watanzania hilo furushi mkikubali na kuamini kuwa mnaweza kuling'oa na kulitupa kunakostahili mtakuwa mmetenda jambo kubwa sana la ushujaa kwa Taifa na vizazi vyenu sasa na baadaye. Inawezekana kwa kulitoa hilo dubwana mkawa pia mmeondoa matatizo yenu kwa asilimia 50% automatically and immediately. Haya matatizo tunayoyafahamu mfano umaskini, ujinga na rushwa ni kazi na matokeo ya CCM 100%. CCM haina nia wala uwezo wa kubadilika wala kujisafisha hivyo inatakiwa tu kuondolewa madarakani.
Ukweli na historia ya CCM ndivyo ilivyo toka miaka ile ya themanini; CCM ni rushwa, dhuluma, ukatili na hila dhidi ya Taifa na wananchi. Ni vile tu sehemu kubwa ya Watanzania hawana elimu ya kutosha (ujinga) na taarifa sahihi za wanayotendewa na hao mumiani.