RC Gambo ndani ya sakata la rushwa Arusha

RC Gambo ndani ya sakata la rushwa Arusha

Uharamu wa video kwa tarehe unaharamisha mazungumzo yaliyorekodiwa. Ushahidi mwingine unaokosekana ni kutokuwepo makabidhiano ya pesa kukamilisha suala la rushwa.

Kulingana na matamshi ya Nasari, ni kwamba ni kithibiti kisicho na mashaka, kwa kutumia teknolojia ya kisasa. Inashangaza kuona kuwa wameshindwa hata kurekebisha tarehe za hiyo video.

Hivyo basi, ni sahihi mtu yeyote kukanusha uhalali wa hiyo video.
Kwa mtazamo wako video ilirekodiwa 2008 na watabiri ambao walijua Gambo atakuja kuwa RC Arusha?Au Mnyeti D.C Meru?
 
Nikiongea naitwa mchochezi nikinyamaza kimya naitwa muogopaji!????
Hv hakuna namna nyingine tukafanya ili ukoloni urudi upya!??
 
Kuna vitu hata kuuliza kunaonyesha IQ ilivyo ndogo, wewe huwezi ku reason Je Wanaotajwa hapo Kama Gambo,Mnyeti,Magufuli Walikuwa na nyadhifa hizo 2008?
Kiushaidi wamekosea nafikili ndio maana wameamua kutopeleka takukuru wameita press conference kwa sababu ushahidi huo Una tatizo
 
Kw
Kiushaidi wamekosea nafikili ndio maana wameamua kutopeleka takukuru wameita press conference kwa sababu ushahidi huo Una tatizo
kwa akili yako hao takukuru wangeangalia tarehe ya camera? Halafu kesi ya Nyani unategemea ngedere afanye nn
 
Kuna vitu hata kuuliza kunaonyesha IQ ilivyo ndogo, wewe huwezi ku reason Je Wanaotajwa hapo Kama Gambo,Mnyeti,Magufuli Walikuwa na nyadhifa hizo 2008?
Sasa kama aliyerekodi hiyo video alikuwa mzembe kiasi cha kutozingatia wakati, inadhihirisha jinsi alivyokuwa " hajui" anachokifanya. Hii unaweza ukaiona nyepesi kwenye jicho la kisiasa lakini mbele ya sheria ni tofauti kabisa!! Wewe huwezi kujiuliza kwanini tarehe haikutiliwa maanani au kwa IQ yako unaamini ni bahati mbaya?!! Unadhani Nassari ni mjinga kukimbilia kwa waandishi wa habari badala ya Takukuru wanakomsubiri?!! Kama nywele zimekizidi kichwa zinyoe akili ipumue!
 
Kama viongozi wake wananunuliwa na CCM tena kwa viela mbuzi,tukiwapa nchi wakaja mabepar na mipesa yao si watauza nchi hawa?wameshindwa uzalendo ndan ya chama chao tena kwa Aibu wananunuliwa na CCM,wataweza kweli kuwa WAZALENDO kwa taifa zima?

Dhana ya uzalendo ndani ya chama tu imefeli,vip kwa taifa?TUNAHITAJI CHAMA IMARA CHA KUONGOZA NCHI SIO CHAMA KINAZUNGUKA MITAANI KUPIGA KELELE OOOOH VIONGOZI WETU WANANUNULIWA. KWANINI WANUNULIWE?
 
Acha umburula wewe, 2008 Gambo alikuwa R.C?,Magufuli alikuwa rais?, Mnyeti alikuwa D.C? Kifaa chochote usiposet tarehe itabaki vile vile tafuteni majuha wakudanganya.Utawala uneshafitinika.

Sijui uma cheo gani CHADEMA ila kitasubiri sana kutawala nchi kama aina ya viongozi ndio hao wanaodai wana ushahidi hata wasiuweke sawa. Maalim hadi leo anaaminisha kuwa atapewa utawala muda si mrefu. Hahahaaa, Wajinga ndio waliwao. Mtakumbuka blanketi kumekucha
 
Video ya miaka 7 iliyopita, then angalia sauti na mdomo kama vinaendana.ila kwa chadema ni wanywa viroba hawatakaa waekewe
 
Hii kitu hatari sana, basi tu watu watajenga hoja za kuteteana ila mioyoni mwao sivyo,wataalamu wa mikakati wasio wanasiasa wamekunywa maji mengi,wafegi kavuta fegi,wakileo kapiga fundo na wakukuna vichwa wamekuna. Eee mwenyez Mungu tujaalie hekima na busara.
 
Hiyo tarehe siyo ishu, ni factory setting hiyo, mwenye Camera hakuifanyia resetting!. Hata hivyo hiyo time haiathiri Contents!. Kama shauri likienda mahakamani expert opinion itaelezea resetting ya time haiwezi kuinvalidate content!

Hata digital camera usipoireset time ukipiga picha itaonyesha picha ya zamani lakini hiifanyi picha kuwa ni ya zamani!!
 
Kweli ushabiki ni kama uwendawazimu ndio maana wale mashabiki wa mpira hufikia hatua ya kutoa roho!

Wewe utajua kabisa jambo unalo investigate ni jambo nyeti sana na litahitajika kutumika kwenye vyombo vya kisheria halafu unafanya uzembe kama huo ambao wengi wanatetea eti ni setting za kamera "hivyo haina shida"!? Tujiulize maswali kadhaa hapa :-

I. Hivi kwa jinsi hiyo clip ilivyo inaweza kupokelewa mahakamani kama kielelezo!?

II. Tukitaka kujua siku na saa halisi kudhibitisha mazungumzo hayo tutajuaje (jambo muhimu kabisa ili kudhibitisha na supporting information nyingine) wakati tarehe ni 9.01.2008!?

Umakini ni muhimu sana katika jambo la msingi kama hili, hapa itoshe tu kusema Nasari amejitahidi ila itabaki kuwa propaganda tu iliyokosa umakni kuwatia watuhumiwa hatiani
 
..Duh!!

..mpaka mambo ya kuchoma shule?

..hatua lazima zichukuliwe hapa.

..kuchoma shule ni kesi kubwa sana.
 
Mbona hiyo video ni kama ya 2008 au macho yangu yana kijani sana?!!

Hawakurekebisha tarehe ya kutengenezwa kwa kamera. hata camera yangu hapa home ukipiga picha au video inaandika mwaka 2015. Niliinunua mwaka 2016 Ujerumani.
 
Back
Top Bottom