Al-Watan
JF-Expert Member
- Apr 16, 2009
- 11,891
- 14,596
Unawezakuweka barabara za lami halafu barabara za lami hizo ndizo zikawa kichocheo cha mwendokasi zaidi.Kudhibiti kunategemeana na CHANZO CHA AJALI.
Najua wengi watasema chanzo ni MWENDO KASI au UZEMBE WA DEREVA.
Wengi husahahu kwamba GARI LENYEWE na hata BARABARA pia ni vyanzo vya ajali.
Tuboreshe barabara kama tunahitaji kusafiri salama kwa magari. Lazima tuwekeze kwenye barabara za lami ZENYE VIWANGO.
Barabara za lamizinatakiwa, na serikali imejitahidi kiasi chake, lakini tunahitaji zaidi ya barabara za lami.
Katika nchi ambayo uhai wa mtu hauna thamani na uelewa wa watu kwamba gari ni chombo cha hatari unaweza kutiliwa shaka pale abiria wanapomhimiza dereva aende kasi, aukushindwa kumkemea dereva anapoenda kasi, tunahitaji zaidi ya barabara za lami.
Kwa mfano.
Shule ilihakikishaje kwamba basi lililochukua wanafunzi ni salama? Waliopanga safari walihakikisha gari limefanyiwa fullcheckup hivi karibuni? Waliangalia rekodiza kampuni/ dereva kuhusu usalama? Walichukua tahadhari kutojaza watu zaidi ya kiwango? Walijipa muda wa kutosha kusafiri ili kusihitajike kwenda kwa mwendokasi?
Wazazi wana ufuatiliaji gani katika haya mambo? Au mtoto akiwa shule kila kitu anaachiwa mwalimu tu?