Sandinistas
JF-Expert Member
- Jul 5, 2013
- 2,616
- 1,778
Kwa hakika anayetafuta political mileage Arusha kwenye msiba hawezi kuwa Lema aliyeshinda uchaguzi kwa kishindo, tena muda mrefu baada ya uchaguzi mkuu kumalizika. Wanaotafuta kick watakuwa walewale wanaotumia mahakama kumkomoa Lema. Sasa wameanza kutumia misiba kama platform ya kumdhalilisha na hata kumuingiza Mbowe bila kujua kwenye mipango yao ovu. But one thing I am sure about is that in all this they are shooting themselves in the foot. Wanafanya chama chao kionekane kama cha kishetani. Wanawaonyesha wana Arusha kwa vitendo kuwa, hata kama Lema siyo kiongozi mzuri sana, lakini angalau ni binadamu mwenzao wa kawaida; siyo jitu katili linaloweza kuwaumiza wenzake ili tu yeye ajifariji kwamba amewakomesha. Kwa watu wa aina hii busara za VP ni usaliti wa kupuuzwa!