RC Gambo ameikosea Mamlaka, aondolewe haraka

RC Gambo ameikosea Mamlaka, aondolewe haraka

WEWE NI NANI MPAKA USIKIE ALICHOONGEA MAKAMU WA RAISI NA RC GAMBO..!?
 
Ni kweli kama mbunge mwenyeji alistahili kupewa nafasi ya kuwasalimu na kuwapa pole wapiga kura wake katika msiba huo mzito

Lakini tukumbuke mkuu wa mkoa naye ni binadamu, huwezi mtukana matusi ya nguoni kiongozi mwenzako, bila hata kuomba msamaha, leo unataka utu wako hueshimiwe wakati wewe uheshimu utu wa kiongozi mwenzio

Mbunge wa Arusha alikosea sana pale alipomtolea kashfa kiongozi mwenzie, anapaswa amuombe radhi mwenzie, mambo yaishe wafanye kazi pamoja katika kuwaletea maendeleo wana Arusha
Personal issues hazipaswi kuletwa kwenye kazi
 
Mkuu zaidi ya hao wanasiasa waliokuwepo jukwaa kuu hukuona umati wa wananchi ulifurika uwanjani?

Kama uliuona basi elewa kuwa si ITIFAKI wananchi wote wale kunyimwa haki ya kuongea.na sio ITIFAKI kuongea wote kwa pamoja .

SAUTI zao zingewakilishwa ma VIONGOZI wao waliowachagua ambao ni MEYA wa jiji MBUNGE wao
Wangesaini kitabu cha maombolezo, hiyo inatosha, zaidi ya hapo ni ujinga wa kufanya msiba uwanja wa siasa.

This whole thing is such a big zoo.
 
Gambo anapewa kiburi na Rais,ndio maana kapata nguvu ya kumdharau Makamu wa Rais.
Makamu wa Rais alipaswa kuonesha kwamba kakerwa na Gambo kwa kuwapa nafasi Lema na Meya kusalimia mara tu alipokaribishwa.Hii ingesaidia sana kulinda heshima yake kwa wateule hawa na hata kwa mteuzi mwenyewe.Pia Rc huyu angepata meseji ni jinsi gani mama Samia kachukizwa na upuuzi wake kiasi cha kuvunja protocal ili tu asimamie alichokiona kinafaa.

Tatizo ninaloliona hapa ni ile kupewa cheo kama bahati fulani tu hivi kwa hiyo kila mara anajihisi kutomkwaza bwana mkuu.Naamini kwa makamu wa rais aliyejiamini kama marehemu Dr Omary Ally Juma asingekubali ujinga huu wa kina Gambo na anayewapa kiburi.
 
Watu kutojiuliza haya maswali, imenifanya nianze kuogopa sana kama taifa tunaelekea wapi au labda tumefika wapi. Kutwa mijadala yetu ni mambo ya kitoto tu.
Kwa kweli mi naona aibu sanaaa, Kwanza wengine ifahamike maiti ikwa tayari, kisha ikawa haiziki bali zaendelea ngonjera nyiiingi twaona ni kama kumnyima haki yake ya msingi ya kuwahishwa kuzikwa, Zikeni kisha endeleeni kuongea hadi asubuhi hakuna noma, hekima ni kuweka jambo mahali pake! Binafsi namwomba Allah awapokee maiti wetu, atujaze subra kwa msiba huu, atupe badala iliyo ya kheri zaidi kuliko alowachukua, YAA ALLAH WALA USITUFARAKANISHE KUPITIA MTIHANI HUU ULOTUPATIA.............................Amen.
 
Vyovyote mtakavyosema achili mbali itikadi za vyama vyenu, Lema kwa jana hakuwa mbunge wa kawaida, ndiye muwakilishi wa wananchi wa Jimbo lenye msiba, alipaswa kupewa nafasi ya kuwapa pole wananchi wake lkn kwa visa na siasa zetu ndio ikawa hivyo, huo ndio ukweli.
 
Mimi sikuona umuhimu wa mtu alievaa gwanda la chama kuzungumza pale, kwanza angejitambua kuwa alipaswa kujiheshimu yeye kwa kuvaa mavazi yanayoendana na shughuli husika ndio aombe kuheshimiwa,
Yanayoendelea arusha RC ndio anayajua,
Na mtu anaekuja kichama kwenye business ya kitaifa ni wa kupigwa chini tu.
 
Chagueni sasa
kati ya Mbowe na Lema yupi awe muongeaji misibani
maana Hata kwenye msiba mnatafuta kiki
ķiki kwa faida gan?tulipanga folen kumchagua na ndio mwakilishi wetu,mkuu wa mkoa tumeletewa tu..acheni ubaguzi.
 
Swali la muhimu kabisa, tutadhibiti vipi hizi ajali,silioni.

Ila nani aliitwa kutoa ngonjera na nani hakuitwa naona sana mazungumzo yake.

Inaonyesha jinsi gani jamii yetu inavyojali ngonjera na risala kuliko kutatua matatizo.
chukua likes zote!
 
Ndani ya Sheikh Amri Abeid Arusha. Kuaga miili ya waliofariki kwenye ajali ya basi dogo. Watu 35 wakiwemo wanafunzi 32, walimu 2 na dereva 1 wa Shule ya Lucky Vicent.

Nilikuwa Jukwaa kuu. Karibu na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan. Muda wa salamu za rambirambi ukafika. Wakuu wa kiserikali na kisiasa wakawa wanakaribishwa. Mkaribishaji ni RC Mrisho Gambo wa Arusha. Mwenyeji

Wasaidizi wa Mama Samia wakapata ujumbe mfupi kutoka kwa Mbowe. Wakamletea Mama Samia. Mama Samia akamuagiza mmojawapo amuite RC Gambo ili amuagize jambo. Jambo muhimu la kisiasa na kiserikali. Amri

Mama Samia,Gambo alipokuja, akamuagiza Gambo awaongeze Mbunge Lema na Meya Lazaro kwa watoa salamu za rambirambi. Wakati huo,mzungumzaji alikuwa Ndugu Simbachawene. RC Gambo akatikisa kichwa kumkatalia Mama Samia. Akina Lema hawakuongezwa

Amri ikakataliwa. Mamlaka ikakosewa. Kinachotakiwa sasa ni kumuondoa Gambo kwakuwa Makamu wa Rais,kama taasisi ya pili ya juu nchini,lazima alindiwe heshima yake. Who is RC!?

Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)
mtu wa meza kuu karibu na makamu wa rais hawezi kuandika haya uliyoyaandika!
 
Mimi sikuona umuhimu wa mtu alievaa gwanda la chama kuzungumza pale, kwanza angejitambua kuwa alipaswa kujiheshimu yeye kwa kuvaa mavazi yanayoendana na shughuli husika ndio aombe kuheshimiwa,
Yanayoendelea arusha RC ndio anayajua,
Na mtu anaekuja kichama kwenye business ya kitaifa ni wa kupigwa chini tu.
wewe ndio ziro kabisa.
 
Gambo anapewa kiburi na Rais,ndio maana kapata nguvu ya kumdharau Makamu wa Rais.

Angesimama mama samia mwenyew amaa ilkua haina ulazima wakumpeleka mtu ambae hana nguvu

Gambo na rais wote mandaz tuu
Tena 2020 wajipange *****
 
Ni kweli kama mbunge mwenyeji alistahili kupewa nafasi ya kuwasalimu na kuwapa pole wapiga kura wake katika msiba huo mzito

Lakini tukumbuke mkuu wa mkoa naye ni binadamu, huwezi mtukana matusi ya nguoni kiongozi mwenzako, bila hata kuomba msamaha, leo unataka utu wako hueshimiwe wakati wewe uheshimu utu wa kiongozi mwenzio

Mbunge wa Arusha alikosea sana pale alipomtolea kashfa kiongozi mwenzie, anapaswa amuombe radhi mwenzie, mambo yaishe wafanye kazi pamoja katika kuwaletea maendeleo wana Arusha


Wananchi wa jimbo la Arusha (inawezekana kabisa kuwa hata baadhi ya wazazi wafiwa ni miongoni mwao)
ndio walionyimwa fursa ya kuongea kupitia kwa wakilishi wao MEYA na MBUNGE wao na sio Godbless Lema na C.Lazaro
Tukubali Mhe. Gambo ana kisasi au hampendi Lema , je ni sababu ipi iliyozuia MEYA wa jiji la Arusha kuongea kama si kuwa ni wa CHADEMA?
 
Ha ha ha
RC wa Arusha,
RC wa Dar

Ni shidaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa!!!!
Hawa jamaa inawezekana wana asili ya Kihutu na Kitutsi. Tusije shangaa kwa sasa wako kwenye maandalizi kabambe ya Kimbari ya Tanzania. God Forbid!
 
Mama yetu Samia kakosewa sana! Gambo anamgomea Makamu wa Rais! Sasa nimeamini kama wengine wanavyosema kwamba kwa awamu hii mfululizo wa wakubwa 11 (First eleven) nchini ni hawa:

1. Mkuu wa Kaya
2. Bashite
3. Gambo
4. Kijazi
5. Mama Samia
6. Majaliwa
7. Janet
8. Mhagama
9. Simbachawene
10. Ndugai
11. Kaimu Jaji mkubwa.
 
MOTOCHINI: Naona umesahau tu kusema "Gambo piga kazi, achana na ngonjera za mama Samia". Si ndio lilikuwa lengo lako?
 
Back
Top Bottom