RC Gambo ameikosea Mamlaka, aondolewe haraka

RC Gambo ameikosea Mamlaka, aondolewe haraka

Acheni Ku discus tatizo ambalo limetokea na kugeuza mtaji kisiasa huku mkijitoa ufahamu na kuleta topic za ajabu,embu fkria ndo yamekukuta hayo yaliyowakuta wenzetu ungejisikiaje?embu tuangalie chanzo cha matatizo na namna ya kuyatatua au kupunguza.hili suala sio la kisiasa tuwafariji ndugu zetu Leo kwao kesho kwako tuache kutumika kisiasa.msishangae sana viongozi hayo ni malezi waliyopata ndio maana wanafanya ivo lkn utu kwanza.
ab69fc4fa793cc35c1b5405338b98a96.jpg
 
Ndani ya Sheikh Amri Abeid Arusha. Kuaga miili ya waliofariki kwenye ajali ya basi dogo. Watu 35 wakiwemo wanafunzi 32, walimu 2 na dereva 1 wa Shule ya Lucky Vicent.

Nilikuwa Jukwaa kuu. Karibu na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan. Muda wa salamu za rambirambi ukafika. Wakuu wa kiserikali na kisiasa wakawa wanakaribishwa. Mkaribishaji ni RC Mrisho Gambo wa Arusha. Mwenyeji

Wasaidizi wa Mama Samia wakapata ujumbe mfupi kutoka kwa Mbowe. Wakamletea Mama Samia. Mama Samia akamuagiza mmojawapo amuite RC Gambo ili amuagize jambo. Jambo muhimu la kisiasa na kiserikali. Amri

Mama Samia,Gambo alipokuja, akamuagiza Gambo awaongeze Mbunge Lema na Meya Lazaro kwa watoa salamu za rambirambi. Wakati huo,mzungumzaji alikuwa Ndugu Simbachawene. RC Gambo akatikisa kichwa kumkatalia Mama Samia. Akina Lema hawakuongezwa

Amri ikakataliwa. Mamlaka ikakosewa. Kinachotakiwa sasa ni kumuondoa Gambo kwakuwa Makamu wa Rais,kama taasisi ya pili ya juu nchini,lazima alindiwe heshima yake. Who is RC!?


Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)
Haya maongezi mubashara yalioneshwa television gani?
 
Yaani JPM atengue uteuzi wa RC kwa kuwa tu Lema hakupewa kipaza sauti kusalimia Wafiwa?

Yeye ni Mbunge anaweza kuandaa Mkutano wake wa kuomboleza na amnyime Kipaza sauti Mrisho Gambo
 
Bashite alikuwepo Arusha.. yawezekana ni yeye aliyempenyezea Kijana yule..
Wasicho jua watu wengi ni kwamba Gambo kapokea maelekezo kutoka juu Mbinguni kuwa Lema Mbunge wa Arusha mjini asipate fursa ya kuwapa pole wafiwa! Tupo msibani wengine wanawaza kukomoana. Unapo muona RC Gambo na RC BASHITE ujue mkomoaji yupo katikati yao.
 
Ndani ya Sheikh Amri Abeid Arusha. Kuaga miili ya waliofariki kwenye ajali ya basi dogo. Watu 35 wakiwemo wanafunzi 32, walimu 2 na dereva 1 wa Shule ya Lucky Vicent.

Nilikuwa Jukwaa kuu. Karibu na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan. Muda wa salamu za rambirambi ukafika. Wakuu wa kiserikali na kisiasa wakawa wanakaribishwa. Mkaribishaji ni RC Mrisho Gambo wa Arusha. Mwenyeji

Wasaidizi wa Mama Samia wakapata ujumbe mfupi kutoka kwa Mbowe. Wakamletea Mama Samia. Mama Samia akamuagiza mmojawapo amuite RC Gambo ili amuagize jambo. Jambo muhimu la kisiasa na kiserikali. Amri

Mama Samia,Gambo alipokuja, akamuagiza Gambo awaongeze Mbunge Lema na Meya Lazaro kwa watoa salamu za rambirambi. Wakati huo,mzungumzaji alikuwa Ndugu Simbachawene. RC Gambo akatikisa kichwa kumkatalia Mama Samia. Akina Lema hawakuongezwa

Amri ikakataliwa. Mamlaka ikakosewa. Kinachotakiwa sasa ni kumuondoa Gambo kwakuwa Makamu wa Rais,kama taasisi ya pili ya juu nchini,lazima alindiwe heshima yake. Who is RC!?

Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)
Mna uhakika kama kweli mh makamu wa Rais alimwambia aongeze majina hayo mkuu wa mkoa?????
Acheni ushabiki wa kipuuzi, mkuu wa mkoa hawezi kunkatalia mtu anayeto ndani ya mamlaka yake ya uteuzi
Makamu wa Rais yupo ndani ya taasisi ya Urais

Tuache kushabikia mambo yasio na tija,
 
Swali la muhimu kabisa, tutadhibiti vipi hizi ajali,silioni.

Ila nani aliitwa kutoa ngonjera na nani hakuitwa naona sana mazungumzo yake.

Inaonyesha jinsi gani jamii yetu inavyojali ngonjera na risala kuliko kutatua matatizo.
Hayo yamezungumzwa...na haya lazima yazungumzwe kwa kuwa yana athari zake pia.
Usitupotoshe makusudi
 
Mna uhakika kama kweli mh makamu wa Rais alimwambia aongeze majina hayo mkuu wa mkoa?????
Acheni ushabiki wa kipuuzi, mkuu wa mkoa hawezi kunkatalia mtu anayeto ndani ya mamlaka yake ya uteuzi
Makamu wa Rais yupo ndani ya taasisi ya Urais

Tuache kushabikia mambo yasio na tija,
Lakini unaonaje lema kutokupewa haki yake ya kiprotokali ya kutoa neno akiwa ni mbunge mwenyeji?
Ukiacha ushabiki pembeni.
 
Vyama vya upinzani visiishi kuwa matukio
 
Ninyi nyote huwa nawafananisha na kopo la kuchambia kazi yenu ni moja tu kusafisha uchafu matak*ni na kuyaacha mat*ko yakiwa safi. na mnaiweza kazi hiyo hongereni kwa umahiri mkubwa.
Uwiiiiiiii, wamekoma huko waliko
 
Hii Tanzania siju tunaenda wapi. Tunabaguana mpaka kwenye msiba?
 
kama ni kweli kuna mawili either mama mpendwa ajiuzulu au RC atolewe leo kufikia jioni.
 
Mama anadharaulika saana,km wanamdharau hivo basi huko maofisini kazi ipo
 
Weka video hicho komemo tuone!!! Otherwise how can we trust you nyie wabadili gia angani?
 
Uwezo Wao wa kufikiri umegota mwisho, kwasababu ya udogo wa ubongo Wao mdogo ka kidonge cha pirton
 
Bila ya kujali chochote kama kweli Gambo alikataa kutii amri ya Makamo wa Rais basi hafai kuna mgogoro wa Ki Muungano unafukuta
 
Na hiyo ndiyo ingekuwa funzo kwa Gambo.Lakini mama naye muoga.


Sio muoga.
Mhe.Makamu wa Rais ,Samia Suluhu, msomi ametumia busara kutoshindana na mjinga hadharani.
Tumpe muda tuone atafanya , atachukua hatua gani kwa huu utovu wa nidhamu
 
Lakini unaonaje lema kutokupewa haki yake ya kiprotokali ya kutoa neno akiwa ni mbunge mwenyeji?
Ukiacha ushabiki pembeni.

Ni kweli kama mbunge mwenyeji alistahili kupewa nafasi ya kuwasalimu na kuwapa pole wapiga kura wake katika msiba huo mzito

Lakini tukumbuke mkuu wa mkoa naye ni binadamu, huwezi mtukana matusi ya nguoni kiongozi mwenzako, bila hata kuomba msamaha, leo unataka utu wako hueshimiwe wakati wewe uheshimu utu wa kiongozi mwenzio

Mbunge wa Arusha alikosea sana pale alipomtolea kashfa kiongozi mwenzie, anapaswa amuombe radhi mwenzie, mambo yaishe wafanye kazi pamoja katika kuwaletea maendeleo wana Arusha
 
Unajua kusoma?

Mimi sioni umuhimu wa mwanasiasa yeyote kuongea katika msiba, labda kama msiba wa mwanasiasa mwenzao na wanaongea kwa kuwa wanamuongelea mtu wa kada yao.

Vinginevyo, msiba wa raia, haitakiwi rais, mbunge, mkuu wa mkoa au mwanasiasa yeyote kuongea.

Wanasiasa wakitaka kuongea wafanye press conference zao. Watoe hotuba zao, kwao, si msibani.

Kwa sababu wakisema maneno msibani, wataugeuza msiba kuwa sehemu ya siasa na hilo litaondoa maana ya msiba ya kufariji waliofiwa. Watu ndiyo wataanza kuongea siasa za vyama.

Sasa hapo sijabagua chama, nimewalundika wanasiasa wote.

Tangu awali.

Nakushangaa unanipa majina ya wanasiasa fulani wa chama fulani kama nimetetea wanasiasa wa chama fulani.

Ndiyo maana nikauliza, unajua kusoma?

Mkuu ,
zaidi ya hao wanasiasa waliokuwepo jukwaa kuu ,hukuona umati wa wananchi uliofurika uwanjani?

Kama uliuona basi elewa kuwa si ITIFAKI wananchi wote wale kunyimwa haki ya kuongea.na sio ITIFAKI kuongea wote kwa pamoja .

SAUTI zao zingewakilishwa na VIONGOZI wao waliowachagua ambao ni MEYA wa jiji na MBUNGE wao
 
Back
Top Bottom