RC Gambo ameikosea Mamlaka, aondolewe haraka

RC Gambo ameikosea Mamlaka, aondolewe haraka

kabombe: Gambo alikuwa kisiasa zaidi ya kitaifa kwenye ule msiba. Sote wenye akili zaidi ya kujua kusoma na kuandika tulijionea. Hatuambiwi na mtu, tuliona kwa macho yetu mchana kweupe! Ile ni aibu ya mwaka aliyoifanya huyu mteule wa jamaa, bwana yule, Sizonje.
 
Ndani ya Sheikh Amri Abeid Arusha. Kuaga miili ya waliofariki kwenye ajali ya basi dogo. Watu 35 wakiwemo wanafunzi 32, walimu 2 na dereva 1 wa Shule ya Lucky Vicent.

Nilikuwa Jukwaa kuu. Karibu na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan. Muda wa salamu za rambirambi ukafika. Wakuu wa kiserikali na kisiasa wakawa wanakaribishwa. Mkaribishaji ni RC Mrisho Gambo wa Arusha. Mwenyeji

Wasaidizi wa Mama Samia wakapata ujumbe mfupi kutoka kwa Mbowe. Wakamletea Mama Samia. Mama Samia akamuagiza mmojawapo amuite RC Gambo ili amuagize jambo. Jambo muhimu la kisiasa na kiserikali. Amri

Mama Samia,Gambo alipokuja, akamuagiza Gambo awaongeze Mbunge Lema na Meya Lazaro kwa watoa salamu za rambirambi. Wakati huo,mzungumzaji alikuwa Ndugu Simbachawene. RC Gambo akatikisa kichwa kumkatalia Mama Samia. Akina Lema hawakuongezwa

Amri ikakataliwa. Mamlaka ikakosewa. Kinachotakiwa sasa ni kumuondoa Gambo kwakuwa Makamu wa Rais,kama taasisi ya pili ya juu nchini,lazima alindiwe heshima yake. Who is RC!?

Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)
Hata mimi ningekuwa Gambo nisingeruhusu Lema na Lazaro wake kuropoka pale jukwaani, maana ni viumbe wanaotembea na laana. Hongera sana Gambo!
 
WILE: Wewe binafsi huoni ni jambo la ajabu Mkuu wa Mkoa kugomea maagizo ya Makamu wa Rais? Hii ni aibu ya Mwaka. Lakini uzuri ni kwamba huo ukuu wa mkoa hatazeeka nao. Kesho tu tutakuwa wote mtaani tukisoma namba. Na ujue hakuna ajira ya mtu anayejua tu kusoma na kuandika.
 
Simiyu Yetu: Ninyi watu wa kanda ya 'siwa' hatukuelewa kwamba mna roho mbaya kiasi hiki. Mna ukabila na ukanda nyie. Ovyo kabisa
 
Kila kitu mnakimbilia kusema muondoe haraka madarakan kisa upinzan umenyimwa nafas ya kutoa Neno msibani aiseeeee.
 
Kama ni kweli, RC Gambo apigwe chini la sivyo mama yetu makamu wa rais achukue maamuzi magumu!
 
Ramli chonganishi hii
Bavicha bana,wewe ulimsikia wakati anamuelekeza Mrisho amuingize Lema?Je kama ndio alikuwa anaelekeza Lema asiongee?
Halafu sio lazima Lema aongee,Mbowe bosi wake ameshaongea inatosha kabisa.
Chadema acheni kutafuta kiki kupitia misiba
Endeleeni hivyo hivyo,kebehini hivyo hivyo,tukaneni hivyo hivyo,dharauni hivyo hivyo ,zidisheni kwa wingi muwezavyo .....but time comes tutaheshimiana...siku hiyo anaewapa jeuri atakuwa uhamishoni kwenye ulingo tupo sisi mwenyewe tukifundishana adabu.
Time comes......
 
Wangesaini kitabu cha maombolezo, hiyo inatosha, zaidi ya hapo ni ujinga wa kufanya msiba uwanja wa siasa.

This whole thing is such a big zoo.

Wananchi wote (au tuseme wanachama wote wa CHADEMA) wa jimbo la Arusha wakasaini hicho kitabu cha maombolezo?
Je hao wengine waliopewa fursa ya kuzungumza hawajui kusaini kitabu cha maombolezo?
 
Huu sio msiba wa CCM ila hawa CCM wameonyesha political immaturity kupitia utoto uliofanywa na huyo Gambo.

Kweli huyo RC ameonesha utoto wa akili yake kwa kiwango cha juu kabisa na hao wanaomshabikia kama si kumdhihaki nao hawajitambui au hawaijui hiyo 'protokali' wanayoizungumzia .
Makamu wa Rais alikuwepo msibani kuwakilisha TAIFA. Kitendo cha kumdharau yeye ni kulidhalilisha TAIFA kupitia Rais
 
Acheni ushabiki heshima ya makamu wa rais inavunjwa hivyo na sijui nani atabaki bila kuvunjiwa heshima.hata kama hawakubali akina lema alipaswa kumheshimu bosi wake
 
Swali la muhimu kabisa, tutadhibiti vipi hizi ajali,silioni.

Ila nani aliitwa kutoa ngonjera na nani hakuitwa naona sana mazungumzo yake.

Inaonyesha jinsi gani jamii yetu inavyojali ngonjera na risala kuliko kutatua matatizo.
Yaani,watu wameumia na ajali mbaya iliyoondoa uhai wa watoto wetu tena wenye umri mdogo,wanasiasa wako wanataka nafasi ya kuongea.

Je,wangeongea wangepunguza machungu ya wazazi?

Je kuongea kwao kungerudisha pumzi za watoto wetu?

Kila kitu siasa,kukaa kimya ni uamuzi sahihi kwa kipindi hiki kigumu kwa wazazi na watanzania kwa ujumla
 
Kiutawala mama samia yupo chini ya mkuu wa mkoa na mratibu wa shughuli za msiba ni mkuu wa mkoa na kamati yake


Bingwa wa kufunika makosa,

Hebu tuambie na hili.
Tulifahamishwa kuwa Rais anawakilishwa hapo msibani na Samia Suluhu Hassan.
Je, huyo aliyewakilishwa (JPM) ,"kiutawala" yupo chini ya mkuu wa mkoa?
 
Hiyo ARASII mpuuzi sana. Alikuwa anafanya kazi mahali fulani akatengeneza bifu na wachaga fulani mahali pale. Mpuuzi sana na ana negativity sana na wachaga....! Lakini yote yana mwisho. Huwezi kutegemea sasa kuendesha maisha. Iko siku atatemwa na ndio mwishoake.
 
Swali la muhimu kabisa, tutadhibiti vipi hizi ajali,silioni.

Ila nani aliitwa kutoa ngonjera na nani hakuitwa naona sana mazungumzo yake.

Inaonyesha jinsi gani jamii yetu inavyojali ngonjera na risala kuliko kutatua matatizo.
Wenye kusimamima hoja na balance za kisiasa ndio watunga sheria na wasimamia katiba ndio wattage maamuzi na wapindisha sheria hatujakosea tuko tunapostahili
 
Mbowe na Kinana wangejua kuwa kuna hii protocali ya kitoto wasingehudhuria tukio hilo au wasingekubali kuongea. Yaani Mbowe sasa ndiyo anatumika kuwanyima viongozi wa Arusha kutoa pole kwa wananchi wao? Somebody somewhere is prostituting Tanzania, to paraphrase KK.
 
Ndani ya Sheikh Amri Abeid Arusha. Kuaga miili ya waliofariki kwenye ajali ya basi dogo. Watu 35 wakiwemo wanafunzi 32, walimu 2 na dereva 1 wa Shule ya Lucky Vicent.

Nilikuwa Jukwaa kuu. Karibu na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan. Muda wa salamu za rambirambi ukafika. Wakuu wa kiserikali na kisiasa wakawa wanakaribishwa. Mkaribishaji ni RC Mrisho Gambo wa Arusha. Mwenyeji

Wasaidizi wa Mama Samia wakapata ujumbe mfupi kutoka kwa Mbowe. Wakamletea Mama Samia. Mama Samia akamuagiza mmojawapo amuite RC Gambo ili amuagize jambo. Jambo muhimu la kisiasa na kiserikali. Amri

Mama Samia,Gambo alipokuja, akamuagiza Gambo awaongeze Mbunge Lema na Meya Lazaro kwa watoa salamu za rambirambi. Wakati huo,mzungumzaji alikuwa Ndugu Simbachawene. RC Gambo akatikisa kichwa kumkatalia Mama Samia. Akina Lema hawakuongezwa

Amri ikakataliwa. Mamlaka ikakosewa. Kinachotakiwa sasa ni kumuondoa Gambo kwakuwa Makamu wa Rais,kama taasisi ya pili ya juu nchini,lazima alindiwe heshima yake. Who is RC!?

Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Arusha)


Kwa taarifa yako Makamu wa Rais ni mdogo kuliko Mkuu wa Mkoa wa Arusha au Dar.
 
Wenye kusimamima hoja na balance za kisiasa ndio watunga sheria na wasimamia katiba ndio wattage maamuzi na wapindisha sheria hatujakosea tuko tunapostahili
Hapana. Si kweli. Kusimamia hoja na balance za kisiasa ni jukumu la wanancho wote.

Tatizo mmewaachia watu fulani tu jukumu hilo. Kwa sababu tu wao ni wawakilishi.

Hilo ni tatizo la msingi kabisa.
 
Back
Top Bottom