Ray na wenzake wameukashifu ukatoliki

Ray na wenzake wameukashifu ukatoliki

Kyenju

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2012
Posts
5,303
Reaction score
2,853
Binafsi siyo msomaji wa magazeti ya udaku, ila leo asubuhi wakati naangalia gazeti la kununua ndipo nimeona habari inayowahusu Ray au VINCENT KIGOSI pamoja na wenzake akina JOHARI.

Picha zao ziko ukurasa wa mbele kwenye gazeti la KIU wakiwa wamevalia mavazi ya kikatoliki, ila sijajua kama ni habari ya kweli au ya kutungwa.

Pia kwenye maelezo yao wanasema Wakatoliki wanapanga kuandamana, kama ni kweli sioni haja ya kuandamana kwa ajili ya mtu kama RAY, bali aombe msamaha au watafutwe wachapwe viboko
attachment.php
 

Attachments

  • rey.jpg
    rey.jpg
    66.3 KB · Views: 9,473
Binafsi siyo msomaji wa magazeti ya udaku, ila leo asubuhi wakati naangalia gazeti la kununua ndipo nimeona habari inayomuhusisha Ray au VINCENT KIGOSI pamoja na wenzake akina JOHARI.

Picha zao ziko ukurasa wa mbele kwenye gazeti la KIU wakiwa wamevalia mavazi ya kikatoliki, ila sijajua kama ni habari ya kweli au ya kutungwa.

Pia kwenye maelezo yao wanasema Wakatoliki wanapanga kuandamana, kama ni kweli siono haja ya kuandamana kwa ajili ya mtu kama RAY, bali aombe msamaha au watafutwe wachapwe viboko.
Bado sijakupata, ni kwa namna gani wameukashifu ukatoliki? Kuvaa hayo mavazi au kuna jambo jingine? Nijuwajuwavyo wakatoliki hawana ujinga huo wa kuandamana kwa namna hiyo...
 
Hahaa umenifurahusha kwa kawaida watu wanasema tumbiri akimaliza miti huja majumbani sasa kwa wasanii wqkimaliza ubunifu wao huaza kupotosha jamii na huyu ray kazoeya mara ya 1 aliwaingilia waislamu kwa mchezo wake wa talaka 3 dini hata c yake ila pengine mara hii kaamua kwenda ukatoliki vumilieni tuu mlio na hio dini wenzake wote wanafanya km hivyo
 
Ni mavazi tu au kuna kingine,yule ni msanii tu wala sioni tatizo hapo,mbona kwenye muvi yake fulani amepiga kanzu na baraghashia na tena ni mkristo mzuri tu.
 
...
Pia kwenye maelezo yao wanasema Wakatoliki wanapanga kuandamana, kama ni kweli sioni haja ya kuandamana kwa ajili ya mtu kama RAY, bali aombe msamaha au watafutwe wachapwe viboko

Lengola gazeti la udaku ni kukujaza jazba na hamas ili ununue gazeti lao. Wakatoliki hawawezi kuandamana kwa ajili ya gazeti la UDAKU, wao wako busy kujenga shule za maana, zahanati, makanisa, madaraja na vyuo vya ufundi. Huo muda wa kuandamana hakuna kabisa!
 
Kwa nini mtu uandamane kupinga uovu uliofanywa na mtu asiyejua afanyacho? Njia nzuri zaidi ni kumuelimisha juu ya ukatoliki ili aongoke.
 
Ni mavazi tu au kuna kingine,yule ni msanii tu wala sioni tatizo hapo,mbona kwenye muvi yake fulani amepiga kanzu na baraghashia na tena ni mkristo mzuri tu.

Binafsi hiyo move sijaiona, lakini inategemea na kilicholengwa nda ya muvi hiyo.
 
Wadesaji wakuu, watakuwa wameona nigeria, wasamehe bure wamegandamizia bila hata wao kujua.
 
Kwani mavazi ya kikatoliki ni yapi?
Kuna mkatoliki anaweza kupata nafasu ya kuandamana kweli
 
kama kayatumia kuchezea filamu sioni tatizo.....hata kama wangechezea filamu ya porn mwisho wa siku ni mavazi tu na hao ni wasanii waacheni wafanye "sanaa" yao
 
kama kayatumia kuchezea filamu sioni tatizo.....hata kama wangechezea filamu ya porn mwisho wa siku ni mavazi tu na hao ni wasanii waacheni wafanye "sanaa" yao

Hii inaonyesha jinsi gani wakristo walivyokomaa kiimani, maana ni upepo utapita na kusahaulika.
 
Mleta mada unapaswa kuwaomba radhi wakatoliki, Wakatoliki hawajawahi kuwa na kaswende ya Ubongo na haitokuwa hivyo Daima.

Angalia movie za Hoolywood wanavyotumia makanisa kukamilisha Movie zao tena kwenye matukio ambayo yanaweza kuharibu mtazamo kwa muangaliaji juu ya mapadri au kanisa lakini hakuna hata siku moja waumini waliwahi kupatwa na kaswende ya Ubongo.

Shigongo anaharibu sana kizazi hiki cha watu wavivu wa kufikiri na wanaodhani Global Publishers ni reliable source of information.
 
Labda wangekuwa akina nanihii mngeskia maandamano, lakini kwa wakristu sijapata kuskia
 
Binafsi siyo msomaji wa magazeti ya udaku, ila leo asubuhi wakati naangalia gazeti la kununua ndipo nimeona habari inayowahusu Ray au VINCENT KIGOSI pamoja na wenzake akina JOHARI.

Picha zao ziko ukurasa wa mbele kwenye gazeti la KIU wakiwa wamevalia mavazi ya kikatoliki, ila sijajua kama ni habari ya kweli au ya kutungwa.

Pia kwenye maelezo yao wanasema Wakatoliki wanapanga kuandamana, kama ni kweli sioni haja ya kuandamana kwa ajili ya mtu kama RAY, bali aombe msamaha au watafutwe wachapwe viboko
attachment.php

... Siyo mavazi ya kikatoliki haya...
 
hakuna mkristu mwenye muda huo labda wewe mtoa mada ambaye nakufahamu fika kuwa ni muislamu.
hao ni wasanii na hilo ni gazeti la udaku so kiufupi hapo hakuna habari yoyote.
 
Kama umesoma vizuri nafikiri utanielewa, kwanza nimekuambia mi si msomaji wa magazeti haya pia nimekwambia sijui kama ni habari za kweli ua la. Ebu soma kwa utulivu utanielewa.
 
Back
Top Bottom