Ratiba inaendelea: Waraka wa TEC unasomwa leo kwa mara ya tatu

Unaweza kujiuliza kwanini TEC wakachagua kuusoma waraka wa kupinga kugawa bandari za Tanganyika kwa DPW kwa wiki sita na si pungufu ama zaidi?
Hili limekaa kiroho na kihesabu zaidi.. Dunia inaendeshwa na tarakimu na hesabu kupitia kanuni maarufu ya MAGAZIJUTO (BODIMUS)!

Mara sita inawakilisha siku sita za uumbaji, yaani siku sita za wiki.. Jumatatu mpaka Jumamosi! Kwahiyo ilipaswa waraka usomwe kila siku kwa siku sita mfululizo, lakini wanaosomewa ni waumini na waamini kanisani na siku pekee ya kuweza kuwasomea katika wingi wao ni siku ya ibada ambayo ni Jumapili
Kwahiyo ndio maana zikatengwa Jumapili sita mfululizo za kusomewa waraka husika, na leo hii ni Jumapili ya tatu
Waraka mpaka sasa umeonesha mafanikio makubwa sana! Dondoo zilizoandaliwa kisomi na kwa weledi mkubwa hazikutoka nje ya mstari wa katiba ya taifa

Zimejitokeza taasisi, vikundi na watu binafsi waliojaribu kuukosoa na kuupinga waraka lakini wakashindwa vibaya sana, kwakuwa badala ya kukosoa ama kupinga kilichomo kwenye waraka husika, wao wakaishia kutoa shutuma, kutuhumu na kukejeli watu binafsi, taasisi iliyoandaa waraka, imani ya waandaaji nk

Hawa wote walikuwa na haki kamili ya kufanya hivyo kwa mujibu wa katiba yetu, kakini kuna kila dalili kwamba hawakusukumwa na uzalendo na dhamira njema bali kwa maelekezo maalum na kwa malipo! Mbaya zaidi wakakurupuka sana na kuongea ujinga mtupu kisha haoo wakasepa zao kukinga mikono!

TEC hawakutetereka kwenye hilo na wala hawakuthubutu kunyanyua mdomo kujibizana nao! Walibaki na focus yao kukamilisha ratiba.. Na wanatambua wazi kwamba debe tupu haliishi kutika..!

Waraka wenye manufaa kwa watanganyika wote bila kujali
Itikadi zao
Imani zao
Makabila yao
Kipato chao nk nk unaendelea kusomwa leo kwa mara ya tatu, na ili kukamilisha ratiba bado mara zingine tatu. Wanaotumwa kuujibu kwa malipo wajitahidi kuujibu kwa hoja na si vioja

Watanganyika sio wapumbavu! Tunajitambua!!!!View attachment 2737210
ila sisi wa misa ya kwanza saa 12 hatujasomewa, sijapenda
 
Pengine nina uwezo mdogo sana wa kufikiri (sio kosa langu kwani elimu ni ndogo sana) lakini lazima niseme kuwa Sehemu hiyo inaonyesha ni kwa namna gani fasihi ni ngumu sana. Unaweza kujipanga weee kuachia kombora mara hamadi unakuta fasihi imebadilisha uelekeo wa kombora lako na kukurudia mwenyewe
.......it fuckks you back just the same way it fuckks others!

● waraka unasomwa kwa mara ya ngapi vilee?!!! Hizo sio kelele?!! Uwafikie ujumbe huu huko?!!!

● Mama Samia Suluhu Hassan, The Mother of Modern Tanzania, amesema chochote mpaka sasa?!!! Atumie ujumbe huu kudescribe wapiga kelele?!! Hapana, hawezi kwani ye ni kiongozi na amestaarabika.

Mimi nasema usomwe hadi October 2030 atakapomaliza muda wake.
Ukiamua kukiweka kwenye lugha picha hiki ulichoandika kitaonekana hivi ama hivi
1868a2fd48e9cec7d1321601256fa88f.jpg
312394b532e2b47198ae348dfbdbabc8.jpg
 
Huo ni uongo mnaongeza chumvi ili kusambaza sumu kwa raia, wewe usijifanye una akili kuliko wa bunge wote Tanzania na wewe sio mtaalamu wa mikataba.
Hoja hujibiwa kwa hoja. Hapa unapinga tu hoja huna
 
Hoja hujibiwa kwa hoja. Hapa unapinga tu hoja huna
Kwani hapo kuna hoja au tuhuma, hoja ni argument kwa kulete hivyo vipengere katika huo mkataba, sio kuongea lolote bila udhibitisho, na mimi naweza nitaja chochote bila udhibitisho wowote.
 
Wasabato wanapaelewaje hapa maana kwao siku ya saba na ya mapumziko kiuumbaji ni Ijumaa
Kila imani ina siku yake ya kuabudu kwahiyo hapo unaweza hata ukaanzia hiyo Jumamosi na kuishia Ijumaa
Muhimu ni idadi ya siku na si mpangilio wa siku
 
Kama hawa kuchaguliwa mbona hatukuona waraka kutoka kanisani wakumshauri au kumlaani alio wa teuwa bila kuchaguliwa, tukiwambia hao watu ni wadini amna uzalendo wowote mnabisha.
Mujahideen wengi ndio walipita bila kupingwa

Walipitishwa kuweka usawa 😄😄🔥🐼
 
Back
Top Bottom