Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,651
- 218,131
Ikumbukwe kwamba siku ya Jumamosi ya 17/7/2021 lile Kongamano kubwa kabisa la Katiba mpya litafanyika Jijini Mwanza , Tunawashukuru Chadema na wadau wote waliowezesha Makongamano haya kufanikiwa .
Sina haja sana na kongamano hili ambalo halijafanyika bado , Bali ninachotaka kuwaomba viongozi wanaoratibu kongamano hili , baada ya kutoka Mwanza walielekeze Singida , na hasa Wilaya ya Ikungi . Nimetaka liende Ikungi ili tuone huo uchafu alioropoka DC mzigo wa Wilaya hiyo anayeitwa Jerry Muro kama ataweza kuufanya .
Jerry Muro mtu duni aliyeokotwa kutoka Yanga na kupachikwa kwenye Ukuu wa Wilaya kama bakshishi baada ya kumhujumu Yusuph Manji ( sitafafanua ) , ametangaza kwamba ni marufuku kwa mtu yeyote kujadili umuhimu wa katiba mpya kwenye Wilaya anayoongoza , Ukweli ni kwamba Jerry Muro hana mamlaka hayo aliyojipa , na hakuwahi kuwa nayo na wala hatokuja kuwa nayo hadi anaingia kaburini .
Ndio maana tunawaelekeza Chadema kubadili ratiba ya kongamano la Katiba mpya na kulielekeza Ikungi ili tuone hiyo jeuri ya Jerry Muro itakakoishia .
Sina haja sana na kongamano hili ambalo halijafanyika bado , Bali ninachotaka kuwaomba viongozi wanaoratibu kongamano hili , baada ya kutoka Mwanza walielekeze Singida , na hasa Wilaya ya Ikungi . Nimetaka liende Ikungi ili tuone huo uchafu alioropoka DC mzigo wa Wilaya hiyo anayeitwa Jerry Muro kama ataweza kuufanya .
Jerry Muro mtu duni aliyeokotwa kutoka Yanga na kupachikwa kwenye Ukuu wa Wilaya kama bakshishi baada ya kumhujumu Yusuph Manji ( sitafafanua ) , ametangaza kwamba ni marufuku kwa mtu yeyote kujadili umuhimu wa katiba mpya kwenye Wilaya anayoongoza , Ukweli ni kwamba Jerry Muro hana mamlaka hayo aliyojipa , na hakuwahi kuwa nayo na wala hatokuja kuwa nayo hadi anaingia kaburini .
Ndio maana tunawaelekeza Chadema kubadili ratiba ya kongamano la Katiba mpya na kulielekeza Ikungi ili tuone hiyo jeuri ya Jerry Muro itakakoishia .