Rais Samia, usiichukue hiyo pesa Tsh. Milioni 120,000,000 ya fomu ya kugombea Urais

Rwebo

JF-Expert Member
Oct 17, 2015
981
1,146
Nimeshtushwa na habari kuwa wanawake kwenye kongamano lao lililokutana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, wamekuchangia sh 120,000,000 kwa ajili ya form ya Urais 2025.

Pamoja na kuwa form hiyo ina gharimu sh milioni 1 tu. Mama tunaujua fika kuwa Una uwezo wa kujilipia gharama ya form hiyo yaani sh milioni moja tu.

Wanawake hao wangekuchangia kiasi halisi sh milioni moja tu na zinazozidi waelekeze ziende ziwasaidie wanawake na wasichana Watanzania wenye uhitaji mkubwa zaidi lakini siyo wewe Rais Samia.

Mfano kwenye Radio Free Africa tarehe 10 March 2024 asubuhi, walirusha habari ya mama mmoja amelazwa hospitali ya Seketoure huko Mwanza yuko hoi.

Mama huyo hana pesa ya matibabu, hana chakula na hana hata mtu wa kumuudumia.

Mama huyo anaudumiwa na mtoto wake wa kiume wa miaka 10 kwa kila kitu hata kumuosha akijisaidia maana hajiwezi kabisa.

Kongamano hilo la wanawake lingemsaidia mama mwenzao kama huyo ambaye anakosa matibabu, chakula na huduma ya kujisitili.

Rais wangu Kataa pesa hizo ziende kwa wanawake wenzenu na wasichana wanaokosa ada vyuoni.
 
Unampangiaje mama wa watu cha kufanya acha yeye mwenyewe aamue sio mjinga au hajui anachofanya..

Alafu hayo mambo ni yawanawake kwenye events yao na unajua wanawake hasa wa pwani na kutunzana kwenye sherehe ni kama uji na mgonjwa.

Waachie wenyewe..
 
Nimeshtushwa na habari kuwa wanawake kwenye kongamano lao lililokutana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, wamekuchangia sh 120,000,000 kwa ajili ya form ya Urais 2025. Pamoja na kuwa form hiyo ina gharimu sh milioni 1 tu. Mama tunaujua fika kuwa Una uwezo wa kujilipia gharama ya form hiyo yaani sh milioni moja tu. Wanawake hao wangekuchangia kiasi halisi sh milioni moja tu na zinazozidi waelekeze ziende ziwasaidie wanawake na wasichana Watanzania wenye uhitaji mkubwa zaidi lakini siyo wewe Rais Samia. Mfano kwenye Radio Free Africa tarehe 10 March 2024 asubuhi, walirusha habari ya mama mmoja amelazwa hospitali ya Seketoure huko Mwanza yuko hoi. Mama huyo hana pesa ya matibabu, hana chakula na hana hata mtu wa kumuudumia. Mama huyo anaudumiwa na mtoto wake wa kiume wa miaka 10 kwa kila kitu hata kumuosha akijisaidia maana hajiwezi kabisa. Kongamano hilo la wanawake lingemsaidia mama mwenzao kama huyo ambaye anakosa matibabu, chakula na huduma ya kujisitili. Rais wangu Kataa pesa hizo ziende kwa wanawake wenzenu na wasichana wanaokosa ada vyuoni.
Inasikitisha sana ushauri mzuri, ila hawezi kuufuata, ashalewa madaraka,angekuwa anajitambuwa asingegombea tena uraisi angewaachia na yeye akae pembeni kuitafuta akhera yake,
 
Unampangiaje mama wa watu cha kufanya acha yeye mwenyewe aamue sio mjinga au hajui anachofanya..

Alafu hayo mambo ni yawanawake kwenye events yao na unajua wanawake hasa wa pwani na kutunzana kwenye sherehe ni kama uji na mgonjwa.
Waachie wenyewe..
Usilete mambo ya wanawake yule ni raisi. Hebu kuwa na heshma
 
Pale Jangwani alipe fidia stahiki kwa mujibu wa sheria kwa watu wenye hati. Kamwe wale wananchi wasidhulumike
Kuna eneo la wazi pale, Yanga ndio watalitumia kujenga Uwanja wa Kisasa.

1969, Late Abeid Karume alijenga Jengo la Yanga.
2025/2026. Mama Samia atajenga uwanja wa Yanga.
 
Nimeshtushwa na habari kuwa wanawake kwenye kongamano lao lililokutana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, wamekuchangia sh 120,000,000
Basi utashtuka sana hadi kifo kama habari ya namna hiyo imekushtua.
 
Hivi Tqnzania hakuna campaign finance law?

Tunajuaje hizi hela hazina lengo la kumnunua rais (influence buying)?
 
Nimeshtushwa na habari kuwa wanawake kwenye kongamano lao lililokutana kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, wamekuchangia sh 120,000,000 kwa ajili ya form ya Urais 2025. Pamoja na kuwa form hiyo ina gharimu sh milioni 1 tu. Mama tunaujua fika kuwa Una uwezo wa kujilipia gharama ya form hiyo yaani sh milioni moja tu. Wanawake hao wangekuchangia kiasi halisi sh milioni moja tu na zinazozidi waelekeze ziende ziwasaidie wanawake na wasichana Watanzania wenye uhitaji mkubwa zaidi lakini siyo wewe Rais Samia. Mfano kwenye Radio Free Africa tarehe 10 March 2024 asubuhi, walirusha habari ya mama mmoja amelazwa hospitali ya Seketoure huko Mwanza yuko hoi. Mama huyo hana pesa ya matibabu, hana chakula na hana hata mtu wa kumuudumia. Mama huyo anaudumiwa na mtoto wake wa kiume wa miaka 10 kwa kila kitu hata kumuosha akijisaidia maana hajiwezi kabisa. Kongamano hilo la wanawake lingemsaidia mama mwenzao kama huyo ambaye anakosa matibabu, chakula na huduma ya kujisitili. Rais wangu Kataa pesa hizo ziende kwa wanawake wenzenu na wasichana wanaokosa ada vyuoni.
Uko sahihi kabisa, Hao akina mama hata hawajui watendalo. Kuna watu wengi wenye uhitaji waliostahihili mchango huo, kama vile watu wanao poteza maisha kwa kukosa pesa 'kidogo sana' kwa ajili ya matibabu na pia kuna watoto wengi yatima wanaishi mazingira ya kusikitisha kwenye vituo vya kulelea watoto yatima vinavyoendeshwa na watanzania wachache 'wasamalia wema'.​
 
Huenda Mama atatumia busara yake kuona hiyo fedha anailekeza iende kwa wahitaji.
 
Back
Top Bottom