Rais Samia sikiliza na kubali ushauri kuhusu mkataba wa Bandari

VYEMELO

JF-Expert Member
Jul 21, 2020
348
459
Kwa asili Mwanawake amejaliwa kwa neema ya mwenyezi Mungu kuwa msikivu. Ni msikivu mzuri na hasa 'anaposomeshwa' na mwanaume. vinginevyo, ndoa zisingekuwepo duniani.

Tumeshuhudia siku za hivi karibuni mjadala mkali kuhusu bandari zetu zilizopo upande wa pili wa Muungano. Wabongo tumegawanyika ktk makundi kadhaa kwa mjadala huu unaohusu (kubinafsishwa/kuuzwa/ubia?) kwa bandari zote za baharini, maziwani, (na, mitoni, kama zipo) zilizopo Tanzania bara.

Mjadala huu umetufikia na hata umegusa mioyo na hisia zetu watu tuliopo mikoa, wilaya, tarafa, kata, na vijiji vya pembezoni mwa Bongoland kabisa. Inashangaza. Mitandao ni maendeleo ila imeleta mambo; utasikia mwanakijiji cha ndani kabisa uswekeni, ... Umemsikia profesa Shivji! ... Ulimsikia Jenerali! .... Mama Tibaijuka kaongea kwa hisia leo, yule mama ni moto wa kuotea mbali!... Leo nimemsikia Jaji mwanamke akimshutumu Rais, mmh, ni hatari! Umewasikia wapinzani wanavyo uchambua mkataba, hasara na faida zake? Mmh, huyu 'Mama' anataka kuiuza Nchi.

Maneno ni mengi; mengi kweli kweli. Tupo watu tunaoiunga mkono Serikali kwa kuchukuwa hatua hiyo na tuna sababu zetu nzuri; sasa kama bandari zetu zimegeuzwa kuwa 'shamba la bibi' tena na Watanzania "wazalendo' wenzetu kabisa, ndio wanaonekana kufaidi keki ya Taifa peke yao, Si tuwape waarabu labda taabu zetu za maisha zitapungua kama siyo kwisha kabisa. Wengine wanakwenda mbali kwa kusema eti, Serikali ishiishie kwenye bandari tu, ije ibinafsishe na hili 'Dubwana' Halmashauri za wilaya.

Ni jipu kama inawezekana wapewe 'waarabu'. Suala la mikopo ya vikundi vya wanawake (CRDB) kanjanja ktk Halmashauri na benki wamekwishatengeneza kamfumo kenye 'mifereji' ya kunufaika na mabilioni hayo. Walengwa hawafikiwi. Chezea wabongo weye! Mungu aiponye Nchi hii jamani.

Tupo tunaopinga kabisa kabisa hatua hiyo ya Serikali kwa hofu kwamba, ... sasa Nchi inauzwa sawasawa na alivyowahi utahadharisha umma Spika wa Bunge mstaafu hata ikamgharimu ajira yake. Kwamba, Serikali itupilie mbali Makubaliano hayo ya (awali?)

Tupo tunataka Serikali yetu sikivu iupitie IGA upya na kuuchambua tena kwa makini na kina ili kutenga mchele, mawe, pumba na kuviweka mahali pake stahili; Ili mwisho wa siku tuibuke na mkataba utakaokuwa na sifa zote za kuitwa MKATABA.

Tupo tunaojua faida na hasara za Makubaliano haya, lakini kwa sababu ya mazingira ya labda kulinda ajira zetu, au, tumefaidi, au, tutafaidi (isivyo haki - i.e. kupitia wizi na milungura) kuwepo kwa uwekezaji, tumekaa kimya boti liendelee majini.

Tupo tusiojua kabisaa juu ya kinachoendelea; akina tia mchuzi pangu pakavu.

Lakini kwa mukhtadha huo, mambo yoote yanamwangukia maskini Mama yetu huyu wa kizanzibari, ambaye alikubali kuichukuwa Nchi wakati ikiwa na changamoto lukuki za kufikwa na msiba mkubwa wa Rais, Uviko, madeni, miradi makubwa, hali mbaya ya uchumi, watanzania hawana pesa za kutosha kukidhi mahitaji yao ya kila siku, hali mbaya ya hewa, wizi na ufisadi Serikalini, na nyingine nyingi zinazofanana na hizo.

Mimi sijui niwe upande gani jamani kwa maana nikisikiliza pande zote naona kama zote ziko sahihi na sawa tu; sasa si kuchanganyikiwa huku jamani? Nimechanganyikiwa!

Kwa hali yangu hii isiyofaa, Namshauri 'Mama' (lakini iwapo hakuna 'Jambo la mtu' bali ni uzalendo wa kupambana na Umaskini; watu 'vyuma vimekaza'), chonde chonde wasikilize wazee wako hawa (kwa umri) na tena inawezekana ni walimu wako pia wa Chuo Kikuu, akina Anna Tibaijuka ((Prof), Shivji (Prof); Jaji nani yule mwanamama nimesahau jina lake, akina Dr. Tibenda, akina Tundu, wakili Mwabukusi, n.k. Waalike na kuwasikiliza wanasheria na mawakili woote maarufu Nchini, wanaharakati na wanasiasa kama Dokta Slaa, Ulimwengu; woote nashauri kutoka sekta binafsi kwani wale wa Serikalini wao walikwishafanya kazi yao tumeiona.

Kwa nini wewe Mama? Rais kwa mujibu wa Katiba yetu ndiye Mbeba maono yoote ya Nchi; sasa, jahazi lisije hama na kugonga mwamba na kupasuka vipande vipande chini ya unahodha wako. Nchi na mbingu zitakulilia Mama yangu na hutokwepa adhabu ya mwenyezi Mungu, adhabu ya Jehanamu. Dunia hii pamoja na fahari yake vyote vinapita tutaviacha kwani tupo hapa duniani kwa kitambo kifupi tu. Sisi ni wapitaji na wasafiri ktk dunia.

Makao Mungu alotuandalia ni Mbinguni, jehanamu binadamu tunakwenda kwa ujinga wetu kama hivi. Mungu kwa mujibu wa Biblia ametupatia wanadamu miaka 70 ya kuishi, na tukiwa na nguvu 80, lakini miaka yoote hiyo haina furaha ya kweli bali imejaa huzuni, shida, na masumbufu kibao. Kwa hesabu hiyo ya Kimungu, piga hesabu mama umebakiza miaka mingapi duniani?

Iwapo IGA hii itatupeleka kama Nchi kwenye kufanya Makubaliano yatakayokuwa hayana afya kwa Maendeleo na ustawi wa Tanzania,. Utupie mbali! Hatuna cha kukosa kama Watanzania. Tutaendelea na Umaskini wetu, tulikwishazoea, mpaka pale kitakapokuja kizazi kitakachoona inafaa kuwekeza ktk bandari kwa namna hiyo.

Hili suala mama siyo la kisiasa hao wajasiriasiasa wanaokuzunguka akina nap, sukuma, bajaji, hamna kitu, nachelea kusema ni wachumiatumbo tu hao. Simama sasa na utembee na Watanzania mamangu. Utakaja kunikumbuka siku moja, kama si hapa duniani, itakuwa ahera.

Wasalaam!
 
Hivi mtu hushauriwa kabla ya kuamua, au huamua kwanza ndipo ashauriwe?

Tuanzie hapo.
 
Hivi mtu hushauriwa kabla ya kuamua, au huamua kwanza ndipo ashauriwe?

Tuanzie hapo.
Agreement ni proposal ambayo lazima yapitiwe watu wakubaliane kwanza , agreement unapokea kwanza na kupitia sio mkataba huo kama kuna kutu hakipo sawa unawaambia wabadilisha na kama mkataba mzima ni hovyo unaweza kuukataa na hakuna kitu watafanya.

Ingekuwa ni mkataba kwamba ameshasaini hao waarabu ungeshawaona hapo na wangekuwa na umiliki tayar ,ukisaini mkataba tu basi umekwisha na ukitaka kuwatoa unaweza kushtakiwa na kulipa fidia.

Mkataba uko hatua ya agreement na wasomi kibao wameshirikishwa wengine wanatoa maoni ,we presha yako na nn ? hakuna kimesainiwa sio rahisi kwa vile agreement ni mlolongo mrefu mpaka pande zote zikubali wanaweza kufuta au kuongeza vitu fulani .

Hamna kitu kinafanya watu wawe na hofu zaidi ya kutokujua
 
Agreement ni proposal ambayo lazima yapitiwe watu wakubaliane kwanza , agreement unapokea kwanza na kupitia sio mkataba huo kama kuna kutu hakipo sawa unawaambia wabadilisha na kama mkataba mzima ni hovyo unaweza kuukataa na hakuna kitu watafanya...
Hujui kuwa Kuna shughuli za Awali zilishaanza kabla ya azimio kuleta bungeni?

Hujui pia kuwa Azimio la Bunge linayafanya makubaliano hayo kuwa SHERIA?
 
una hakika mkataba umesainiwa ?
Uwe unaelewa,

Azimio la Bunge linaweka makubaliano hayo ya Awali kuwa SHERIA, na kuweka Serikali yetu kwenye mtego wa kushindwa kuvunja makubaliano haya au mikataba ijayo.

Wewe mbwiga unaweza kuwa na maarifa ya kisheria zaidi ya Professor Shivji, NGULI tangu Awamu ya Mwl Nyerere?
 
Uwe unaelewa,

Azimio la Bunge linaweka makubaliano hayo ya Awali kuwa SHERIA, na kuweka Serikali yetu kwenye mtego wa kushindwa kuvunja makubaliano haya au mikataba ijayo.

Wewe mbwiga unaweza kuwa na maarifa ya kisheria zaidi ya Professor Shivji, NGULI tangu Awamu ya Mwl Nyerere?
sema wamekubali hayo makubali yaliyowasilishwa ili kuandaa mkataba hata hyo sheria hujui maana yake ni nn?

Unajua maana ya mkataba au upo tu kupelekwa na wasomi uchwara..Mkataba ukipita tayar jamaa wanakuwa na mamlaka ya kuendesha hiyo bandari yaani tayari ni wamiliki.

Je umeona wapi huo umiliki ?tumia akili yako shule hukuenda kukaa kweny madawat
 
WEWE NI TATIZO ZAIDI YA DIPI DABILIYU DUBAI KAMA HAUJAWAELEKA WAFUATAO;-

Haujamwelewa@Father Kitime
Haujamwelewa@Dr Slaa
Haujamwelewa@Freeman Mbowe,
Haujamwelewa@Mwanasheria Dr Nshala Rugemeleza.
Haujamwelewa@Prof Shivji
Haujamwelewa@Prof Anna Tibaijuka
Haujamwelewa@Tundu Lissu
Haujawaelewa@Shirika la haki za binadamu.
Haujawaelewa@Tanganyika law school.
Haujawaelewa@Baraza la Waislamu Tanzania
Haujawaelewa@Baraza la Wakristo Tanzania
Haujamwelewa@Maria Sarungi.
Haujamwelewa@Mange Kimambi.

Basi wewe ni tatizo kuliko hao Di pi Dabiliyu Dubai.
 
WEWE NI TATIZO ZAIDI YA DIPI DABILIYU DUBAI KAMA HAUJAWAELEKA WAFUATAO;-

Haujamwelewa@Father Kitime
Haujamwelewa@Dr Slaa
Haujamwelewa@Freeman Mbowe...
Kuna watu wengi wanaamini tatizo ni waarabu,uwekezaji au dini,lakini hawajibu hoja za IGA na HGA.

Kuna kitu hakipo sawa kwenye IGA lakini watu wanaamini eti kwa kuwa Dii Pii Wooodi ni kutoka kwa waarabu na kwenye uislamu, basi tunaopinga huo mkataba ni "Wagalatia".

Tuna tatizo kubwa sana la udini kuliko vile tulivyokuwa tunaona hapo awali,hii issue ya DP - World imeliweka hili swala wazi zaidi. Na tatizo hasa lipo upande mmoja tu wa dini moja tuu,ndio wao wanaona kama wanaonewa.

Hili sakata limeweka wazi kuhusu elimu na uelewa wa pande mbili hizi.
 
Mm nataka hao uliowataja wapiganie katiba mpya ili kupata Suluhu ya kudumu ya matatizo haya
 
WEWE NI TATIZO ZAIDI YA DIPI DABILIYU DUBAI KAMA HAUJAWAELEKA WAFUATAO;-

Haujamwelewa@Father Kitime
Haujamwelewa@Dr Slaa
Haujamwelewa@Freeman Mbowe...
Ngoja waje wazee wa hashtag ya DP world wakiongozwa na... Lord denning Faizafoxy na covax!!
 
sema wamekubali hayo makubali yaliyowasilishwa ili kuandaa mkataba hata hyo sheria hujui maana yake ni nn?

Unajua maana ya mkataba au upo tu kupelekwa na wasomi uchwara..Mkataba ukipita tayar jamaa wanakuwa na mamlaka ya kuendesha hiyo bandari yaani tayari ni wamiliki.

Je umeona wapi huo umiliki ?tumia akili yako shule hukuenda kukaa kweny madawat
Kwamba Professor Shivji ni msomi uchwara?

Ngoja niache kujibizana nawe usijeniambukiza ujinga.
 
Kwamba Professor Shivji ni msomi uchwara?

Ngoja niache kujibizana nawe usijeniambukiza ujinga.
Wapi professor shivji kasema unayosema kama hujui kaa kwa kutulia ...yeye kasema bunge limepitisha ila mkataba bado lazima upitiwe na wasomi wengine kwan bungeni wote wasomi?

Sasa umepelekwa huko Udsm kujadiliwa usifikrie ni rahsi lazima agreement ilipitiwe kwa watu tofauti ,hatua ya kwanza ni bunge.

Msomi mchwar sio shivji ni wewe hujui hta kuchanganua hapo jamaa kaongelea kuhusu agreement ila mkataba bado ...Unajua tofauti ya agreement na mkataba?

Bado wasomi wanachambua na kwa vile nchi yetu inaushiriki wa viongozi wa dini nao pia watato maoni yao
 
Kwa asili Mwanawake amejaliwa kwa neema ya mwenyezi Mungu kuwa msikivu. Ni msikivu mzuri na hasa 'anaposomeshwa' na mwanaume. vinginevyo, ndoa zisingekuwepo duniani.

Tumeshuhudia siku za hivi karibuni mjadala mkali kuhusu bandari zetu zilizopo upande wa pili wa Muungano. Wabongo tumegawanyika ktk makundi kadhaa kwa mjadala huu unaohusu (kubinafsishwa/kuuzwa/ubia?) kwa bandari zote za baharini, maziwani, (na, mitoni, kama zipo) zilizopo Tanzania bara.

Mjadala huu umetufikia na hata umegusa mioyo na hisia zetu watu tuliopo mikoa, wilaya, tarafa, kata, na vijiji vya pembezoni mwa Bongoland kabisa. Inashangaza. Mitandao ni maendeleo ila imeleta mambo; utasikia mwanakijiji cha ndani kabisa uswekeni, ... Umemsikia profesa Shivji! ... Ulimsikia Jenerali! .... Mama Tibaijuka kaongea kwa hisia leo, yule mama ni moto wa kuotea mbali!... Leo nimemsikia Jaji mwanamke akimshutumu Rais, mmh, ni hatari! Umewasikia wapinzani wanavyo uchambua mkataba, hasara na faida zake? Mmh, huyu 'Mama' anataka kuiuza Nchi.

Maneno ni mengi; mengi kweli kweli. Tupo watu tunaoiunga mkono Serikali kwa kuchukuwa hatua hiyo na tuna sababu zetu nzuri; sasa kama bandari zetu zimegeuzwa kuwa 'shamba la bibi' tena na Watanzania "wazalendo' wenzetu kabisa, ndio wanaonekana kufaidi keki ya Taifa peke yao, Si tuwape waarabu labda taabu zetu za maisha zitapungua kama siyo kwisha kabisa. Wengine wanakwenda mbali kwa kusema eti, Serikali ishiishie kwenye bandari tu, ije ibinafsishe na hili 'Dubwana' Halmashauri za wilaya.

Ni jipu kama inawezekana wapewe 'waarabu'. Suala la mikopo ya vikundi vya wanawake (CRDB) kanjanja ktk Halmashauri na benki wamekwishatengeneza kamfumo kenye 'mifereji' ya kunufaika na mabilioni hayo. Walengwa hawafikiwi. Chezea wabongo weye! Mungu aiponye Nchi hii jamani.

Tupo tunaopinga kabisa kabisa hatua hiyo ya Serikali kwa hofu kwamba, ... sasa Nchi inauzwa sawasawa na alivyowahi utahadharisha umma Spika wa Bunge mstaafu hata ikamgharimu ajira yake. Kwamba, Serikali itupilie mbali Makubaliano hayo ya (awali?)

Tupo tunataka Serikali yetu sikivu iupitie IGA upya na kuuchambua tena kwa makini na kina ili kutenga mchele, mawe, pumba na kuviweka mahali pake stahili; Ili mwisho wa siku tuibuke na mkataba utakaokuwa na sifa zote za kuitwa MKATABA.

Tupo tunaojua faida na hasara za Makubaliano haya, lakini kwa sababu ya mazingira ya labda kulinda ajira zetu, au, tumefaidi, au, tutafaidi (isivyo haki - i.e. kupitia wizi na milungura) kuwepo kwa uwekezaji, tumekaa kimya boti liendelee majini.

Tupo tusiojua kabisaa juu ya kinachoendelea; akina tia mchuzi pangu pakavu.

Lakini kwa mukhtadha huo, mambo yoote yanamwangukia maskini Mama yetu huyu wa kizanzibari, ambaye alikubali kuichukuwa Nchi wakati ikiwa na changamoto lukuki za kufikwa na msiba mkubwa wa Rais, Uviko, madeni, miradi makubwa, hali mbaya ya uchumi, watanzania hawana pesa za kutosha kukidhi mahitaji yao ya kila siku, hali mbaya ya hewa, wizi na ufisadi Serikalini, na nyingine nyingi zinazofanana na hizo.

Mimi sijui niwe upande gani jamani kwa maana nikisikiliza pande zote naona kama zote ziko sahihi na sawa tu; sasa si kuchanganyikiwa huku jamani? Nimechanganyikiwa!

Kwa hali yangu hii isiyofaa, Namshauri 'Mama' (lakini iwapo hakuna 'Jambo la mtu' bali ni uzalendo wa kupambana na Umaskini; watu 'vyuma vimekaza'), chonde chonde wasikilize wazee wako hawa (kwa umri) na tena inawezekana ni walimu wako pia wa Chuo Kikuu, akina Anna Tibaijuka ((Prof), Shivji (Prof); Jaji nani yule mwanamama nimesahau jina lake, akina Dr. Tibenda, akina Tundu, wakili Mwabukusi, n.k. Waalike na kuwasikiliza wanasheria na mawakili woote maarufu Nchini, wanaharakati na wanasiasa kama Dokta Slaa, Ulimwengu; woote nashauri kutoka sekta binafsi kwani wale wa Serikalini wao walikwishafanya kazi yao tumeiona.

Kwa nini wewe Mama? Rais kwa mujibu wa Katiba yetu ndiye Mbeba maono yoote ya Nchi; sasa, jahazi lisije hama na kugonga mwamba na kupasuka vipande vipande chini ya unahodha wako. Nchi na mbingu zitakulilia Mama yangu na hutokwepa adhabu ya mwenyezi Mungu, adhabu ya Jehanamu. Dunia hii pamoja na fahari yake vyote vinapita tutaviacha kwani tupo hapa duniani kwa kitambo kifupi tu. Sisi ni wapitaji na wasafiri ktk dunia.

Makao Mungu alotuandalia ni Mbinguni, jehanamu binadamu tunakwenda kwa ujinga wetu kama hivi. Mungu kwa mujibu wa Biblia ametupatia wanadamu miaka 70 ya kuishi, na tukiwa na nguvu 80, lakini miaka yoote hiyo haina furaha ya kweli bali imejaa huzuni, shida, na masumbufu kibao. Kwa hesabu hiyo ya Kimungu, piga hesabu mama umebakiza miaka mingapi duniani?

Iwapo IGA hii itatupeleka kama Nchi kwenye kufanya Makubaliano yatakayokuwa hayana afya kwa Maendeleo na ustawi wa Tanzania,. Utupie mbali! Hatuna cha kukosa kama Watanzania. Tutaendelea na Umaskini wetu, tulikwishazoea, mpaka pale kitakapokuja kizazi kitakachoona inafaa kuwekeza ktk bandari kwa namna hiyo.

Hili suala mama siyo la kisiasa hao wajasiriasiasa wanaokuzunguka akina nap, sukuma, bajaji, hamna kitu, nachelea kusema ni wachumiatumbo tu hao. Simama sasa na utembee na Watanzania mamangu. Utakaja kunikumbuka siku moja, kama si hapa duniani, itakuwa ahera.

Wasalaam!
Mwambie Fr. Kitima atueleza mkataba kati ta TEC na serikali wa hospital ya Bugando ukomo wake ni lini?
 
Rais Samia kumbuka mbingu huongea na ardhi nayo huongea

Toka hii aibu ya TANGANYIKA kutaka kuuzwa kwa waarabu

Mbingu za TANGANYIKA zipo kimya
Ardhi ya TANGANYIKA ipo kimya

Naomba ukiwa pekee yako fikiria hili

Fikiria sana hili

Unayo nafasi ya kurudi kwenye mstari kila binadamu hukosea


Tunaomba Mungu akuongoze ujiondoe
 
Back
Top Bottom