Rais Samia ni komandoo aliyeiva

Lucas Mwashambwa

JF-Expert Member
Jul 28, 2022
15,340
9,767
Ndugu zangu watanzania,

Mtu kufikia hatua ya ukomandoo anakuwa amepitia mafunzo mengi Sana magumu,yenye kuhitaji nguvu na akili,maarifa na upeo,ufahamu na utambuzi,uvumilivu na ujasiri,ukakamavu na ushupavu,Dhamira na malengo,Dira na muelekeo.

Komandoo Ni mpambanaji na Jasiri Sana,mkakamavu na mvumilivu wa Hali ya juu katika magumu na mateso yote apitiayo.Hakati Tamaa mpaka atimize lengo ,yupo tayari kuishi na kukaa katika mazingira ya aina yoyote yale,hatazami nyuma kwa hofu Bali hutazama mbele kwa matumaini na moyo wa ushindi kwa Taifa lake,yupo Tayari kuhatarisha maisha yake kwa ajiri ya Taifa lake ,Ni mtu aliye jitoa na kujitolea Kama sadaka kwa ajili ya maisha na uhai wa Taifa lake na watu wake.

Kamandoo hachoki kupigana,hachoki kupambana,kazi yake ni kusonga mbele kwa maarifa ,akili,ujuzi,ujasiri, ushupavu,ukakamavu na umadhubuti wa Hali ya juu Sana

Hivi Ndivyo alivyo Rais wetu mama Samia suluhu Hassani,Ni kiongozi mpambanaji Sana,Jasiri, mkakamavu,Hodari, mvumilivu, aliyejitoa na kujitolea kuwatumikia watanzania,hatazami nyuma kwa hofu Bali hutazama mbele kwa matumaini makubwa Sana,hateteleki Wala kuteteleshwa.hayaogopi matatizo ya kiuongozi Bali huyakabili kwa moyo wa ujasiri na ushupavu,hayakwepi matatizo Bali hutazama na kuyamaliza kiweledi Sana.

Ndio maana tumefika hapa Kama Taifa ,ndio maana tumeshinda Vita vyote vya kiuchumi,ndio maana tumevuka mitihani yote migumu,ndio maana tumewashinda maadui wote waliojitokeza mbele yetu Kama Taifa. kwa kuwa mbele yetu alikuwepo na yupo Rais wetu mpendwa na Jasiri mama Samia suluhu Hassani kipenzi Cha watanzania na Tumaini la wanyonge.ni kwa kuwa mbele yetu Kama Taifa alikuwepo mama yetu na Rais wetu alietushika mkono,kutufariji,kututia moyo,kutuunganisha,kutufuta machozi ,kutushauri,kutupa maneno ya ujasiri,kutuongoza,kutupatia matumaini,kutupa Tabasamu na matumaini pamoja na kutujengea ujasiri wa kusonga mbele pasipo kukata Tamaa.

Ndio maana Leo hii watanzania Wanatazama Mbele kwa matumaini na siyo hofu,ndio maana watanzania wanasonga mbele kwa ujasiri pasipo Shaka,ndio maana Taifa Lina amani, utulivu na upendo huku likiwa limeshikamana.ndio maana uchumi wetu unaendelea kupaa na kumgusa kila mtanzania,ndio maana kila mtanzania Anayo matumaini makubwa ya kutimiza Ndoto zake, ndio maana watanzania tunazungumza lugha moja,ndio maana watanzania tunapendana ,kuheshimiana,kusaidiana , kushirikiana na kuvumiliana tunapotofautiana kimtizamo,ndio maana kila mmoja wetu anaiona kesho iliyo Bora zaidi ya Leo na kila mmoja anaiona nuru machoni pake.

Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
 
Ndugu zangu watanzania,

Mtu kufikia hatua ya ukomandoo anakuwa amepitia mafunzo mengi Sana magumu,yenye kuhitaji nguvu na akili,maarifa na upeo,ufahamu na utambuzi,uvumilivu na ujasiri,ukakamavu na ushupavu,Dhamira na malengo,Dira na muelekeo.

Hivi Ndivyo alivyo Rais wetu mama Samia suluhu Hassani

Kazi iendeleee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627
Naunga mkono hoja
P
 
Ndugu zangu watanzania,

Mtu kufikia hatua ya ukomandoo anakuwa amepitia mafunzo mengi Sana magumu,yenye kuhitaji nguvu na akili,maarifa na upeo,ufahamu na utambuzi,uvumilivu na ujasiri,ukakamavu na ushupavu,Dhamira na malengo,Dira na muelekeo.
a Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa, kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.

0742-676627

Chawa katika ubora wako.
 
Back
Top Bottom