Rais Samia, haya mambo ya kupotea watu ni doa kwenye serikali yako

Hao uliowataja kipind kile walikuwa wanateka watu kwa sababu gani?
Na Sasa wanaendelea kuteka kwa sababu gani?
Mfumo wowote ulioasisiwa, ukishasimama na ukajizatiti, kamwe hauwezi kupotea au kuondoka mara moja.

Tukumbuke wakati wa Magufuli, siyo Magufuli aliyekuwa akiteka au akiua kwa mkono wake, bali aliuimarisha na kuupa nguvu mfumo uliokuwa ukiteka, kupoteza na kuteka watu (naamini kuwa huo mfumo hakuasisi yeye, ulikuwepo hata kabla yake). Hii ina maana kuna watu waliajiriwa na kazi yao ilikuwa ni kuteka, kupoteza na kuua watu.

Wengi wa hawa wauaji na watekaji, baada ya kuteka na kuua sana, wakati wa marehemu, walipandishwa vyeo. Hawa watu bado wapo, na wengi wao wanashikilia ofisi zile zile au za juu zaidi, huku wakijua kuwa ni utekaji na uuaji ndivyo vilivyowapandisha mpaka kufika walipo sasa. Akina Kingai, Goodluck, Mahita, Jumanne , etc, mnawaona wakiendelea kwenye ofisi za umma, tena wakiwa na madaraka makubwa zaidi. Kama kazi zao ndizo hizo, na bado wapo maofisini, mnafikiri wanafanya nini?
 
Mama wale wale tu,Kamnada Ciro hakupaswa kuwepo alipo, kwenye wigo wake yamefanyika mengi tu ya hovyo!!!

Kitengo Cha supika kufokewa hadi kukimbia kazi kisa kahoji madeni,hatuna tofauti na Magufuli alivyomnyanyasa Assad kisa kasema kuna hela imepigwa!!!

Tunaenda kuweka historia ya kua na uchwara wa kike!!
Huyu ndo uchwara kamili...yule alikuwa kamanda
 
Pia kuna wapumbavu wanaodhani wengine wakiua basi wanafuta ule uuaji uliokuwa ukifanywa na mkono wa chuma wa utawala wa Jiwe.
Endeleni kujifariji wengi waovu na wema hufa na kwa kuwa hamtaki kujua ya kuwa matukio hayana utawala ila pia utawala unaweza kuwafanya waharifu a mauaji washamiri kama hali ilivyo sasa! Leo umesikia tena Arusha dada kaokotwa Ikiwa ameuawa na mwili wake kutupwa bustanini! Juzi ulisikia wanawake watatu mwanza miili yao iliokotwa Ikiwa imechinjwa! Sasa jiulize haya yanatokea? Wenye hekima wanajua ila wajinga hujadili haya kwa mihemko tu!
 
Endeleni kujifariji wengi waovu na wema hufa na kwa kuwa hamtaki kujua ya kuwa matukio hayana utawala ila pia utawala unaweza kuwafanya waharifu a mauaji washamiri kama hali ilivyo sasa! Leo umesikia tena Arusha dada kaokotwa Ikiwa ameuawa na mwili wake kutupwa bustanini! Juzi ulisikia wanawake watatu mwanza miili yao iliokotwa Ikiwa imechinjwa! Sasa jiulize haya yanatokea? Wenye hekima wanajua ila wajinga hujadili haya kwa mihemko tu!
Wajinga ni wale ambao mauaji ya watu huyachukulia ki wepesi, watu kutekwa au kupigwa risasi mchana kweupe na uchunguzi haufanyiki kuna uhalali gani hapo. Iwe bi Urojo au mwendazake wa Chato muuaji ni muuaji tu na wala haiangiliwi muuaji anatokea wapi au ni wa utawala wa awamu ipi.
 
Mfumo wowote ulioasisiwa, ukishasimama na ukajizatiti, kamwe hauwezi kupotea au kuondoka mara moja.

Tukumbuke wakati wa Magufuli, siyo Magufuli aliyekuwa akiteka au akiua kwa mkono wake, bali aliuimarisha na kuupa nguvu mfumo uliokuwa ukiteka, kupoteza na kuteka watu (naamini kuwa huo mfumo hakuasisi yeye, ulikuwepo hata kabla yake). Hii ina maana kuna watu waliajiriwa na kazi yao ilikuwa ni kuteka, kupoteza na kuua watu.

Wengi wa hawa wauaji na watekaji, baada ya kuteka na kuua sana, wakati wa marehemu, walipandishwa vyeo. Hawa watu bado wapo, na wengi wao wanashikilia ofisi zile zile au za juu zaidi, huku wakijua kuwa ni utekaji na uuaji ndivyo vilivyowapandisha mpaka kufika walipo sasa.

Akina Kingai, Goodluck, Mahita, Jumanne , etc, mnawaona wakiendelea kwenye ofisi za umma, tena wakiwa na madaraka makubwa zaidi. Kama kazi zao ndizo hizo, na bado wapo maofisini, mnafikiri wanafanya nini?
Waliajiriwa miaka 5 tu iliyopita??? Wale waliopiga bomu likasambaratisha kabisa mwili wa mtu pale iringa wao pia waliajiriwa na jiwe sio, yule kiongozi wa Dr nae pia alikuwa jiwe?? Eti kubambikia watu kesi, kesi zimeisha sasa??
 
Kitu kimoja tu Ambacho nina uhakika nacho LEGACY ALIYOIACHA MAGUFULI hakuna rais anaweza fika hata nusu yake...!!! Alivyothamini watu wenye vipato vya hali ya chini ilikuwa namna ya kipekee sana.. Leo tunakatwa buku buku kila kona na bado mtu akiongelea kuhusu Kukopa anaonekana ni Adui.. Safari ni ndefu sana bado yani tutafika hoiii
 
Yap, aliua sana na hata baadhi ya waliomtangulia waliua lakini si kwa kiwango chake. Jiwe aliua bila woga kwani alikuwa ruthless na alitengeneza mfumo wa kiimla uliofanya yeye kuogopwa na watu na hata media pia.
Nitajie watu 3 waliouliwa na jiwe
 
Yaani hawa wao ni kusakama tu! Sasa si hayupo yakitokea wanasema kundi lake JPM lililobaki! Je wakati wa Kikwete lilikiwa la Magufuli pia? Hawana majibu.!
Sasa nyie ccm mbona mnawaua watu bila hatia?
Toeni majibu.Hili jambo halihitaji siasa zenu za CCM na CHADEMA.
 
  • Thanks
Reactions: Qwy
Back
Top Bottom