field marshall1
JF-Expert Member
- Sep 17, 2017
- 1,171
- 2,730
Mheshimiwa Rais, naomba nichukue nafasi hii nikupongeze kwa mambo mengi mazuri unayoyafanya ila kwa hili la watu kuanza kupotea kwenye utawala wako tayari ni doa kwenye serikali yako. Wiki mbili zilizopita kuna habari zimetokea magazeti kuwa kuna vijana watano wamepotea wakiwa wanaenda kusherekea Krismasi kwenye fukwe hapa Dar es Salaam.
Kwa maelezo yao ni kuwa walikamatwa na Police na wakawa wanapelekwa central police, baada ya hapo hawakusikika tena hadi leo wiki ya tatu licha ya jitihada za kuwatafuta kwenye vituo vya police zote za Dar, kwenye mahospitali na mortuaries zote. Hii style tuliona wakati wa utawala wa awamu ya tano ya Magufuli na wewe ukiwa makamo wa rais, tumeona yaliyompata Azory Gwanda, Ben Saanane, Roma Mkatoliki na wengine wengi waliokuwa wakiokotwa kwenye magunia na viroba.
Mheshimiwa Samia, nikuulize swali moja. Je, bado unayaendeleza yale yale ya kupoteza watu na kuwatupa mtoni? Mbona wewe unajifanya muislamu safi? Je, dini yako inaruhusu uue na kupoteza watu?
Au unashindwa kuwakemea huyo Sirro na polisi wake? Haya ndiyo yale mambo yaliyofanyika miaka iliyopita ya akina Abdallah Zombe na wenzake walivyowauwa vijana wasio na makosa wafanyabiashara wa madini na kuwaibia pesa zao? Haya ndiyo yale yale ya kuwaua vijana wapatao 7 Arusha waliokamatwa na polisi kwa kushukiwa kuwa wanapanga kuvizia na kuiba kwenya gari la benki lililokuwa likipeleka pesa Kiteto?
Inasikitisha kuona wananchi wanatoka majumbani mwao lakini hawarudi. HATA KAMA NI WASHUKIWA NA WAMEKAMATWA, KUNA TARATIBU ZAKE ZA KUPELEKWA MAHAKAMA NA FAMILIA ZAO KUFAHAMISHWA. Wewe mheshimiwa Rais Samia kwenye hotuba moja ulisema ulikamatwa kwa kosa la taa ya gari kutokuwaka. Je, ungewekwa mahabusu au kuumizwa, je familia yako ingefanyaje? Haingekuwa simanzi? Usifurahie mkuki kwa nguruwe ila kwa binadamu uchungu!
Hivi rais Samia unaona raha gani raia wako wakipotezwa au wakiuawa? Kweli una roho ngumu kiasi hiki kama Adolf Hitler! Onea huruma raia wako. Usifurahie unayoyaona, kama unafurahia ujue kuna KARMA.
HADI LINI WATU WATAENDELEA KUPOTEA?
Kwa maelezo yao ni kuwa walikamatwa na Police na wakawa wanapelekwa central police, baada ya hapo hawakusikika tena hadi leo wiki ya tatu licha ya jitihada za kuwatafuta kwenye vituo vya police zote za Dar, kwenye mahospitali na mortuaries zote. Hii style tuliona wakati wa utawala wa awamu ya tano ya Magufuli na wewe ukiwa makamo wa rais, tumeona yaliyompata Azory Gwanda, Ben Saanane, Roma Mkatoliki na wengine wengi waliokuwa wakiokotwa kwenye magunia na viroba.
Mheshimiwa Samia, nikuulize swali moja. Je, bado unayaendeleza yale yale ya kupoteza watu na kuwatupa mtoni? Mbona wewe unajifanya muislamu safi? Je, dini yako inaruhusu uue na kupoteza watu?
Au unashindwa kuwakemea huyo Sirro na polisi wake? Haya ndiyo yale mambo yaliyofanyika miaka iliyopita ya akina Abdallah Zombe na wenzake walivyowauwa vijana wasio na makosa wafanyabiashara wa madini na kuwaibia pesa zao? Haya ndiyo yale yale ya kuwaua vijana wapatao 7 Arusha waliokamatwa na polisi kwa kushukiwa kuwa wanapanga kuvizia na kuiba kwenya gari la benki lililokuwa likipeleka pesa Kiteto?
Inasikitisha kuona wananchi wanatoka majumbani mwao lakini hawarudi. HATA KAMA NI WASHUKIWA NA WAMEKAMATWA, KUNA TARATIBU ZAKE ZA KUPELEKWA MAHAKAMA NA FAMILIA ZAO KUFAHAMISHWA. Wewe mheshimiwa Rais Samia kwenye hotuba moja ulisema ulikamatwa kwa kosa la taa ya gari kutokuwaka. Je, ungewekwa mahabusu au kuumizwa, je familia yako ingefanyaje? Haingekuwa simanzi? Usifurahie mkuki kwa nguruwe ila kwa binadamu uchungu!
Hivi rais Samia unaona raha gani raia wako wakipotezwa au wakiuawa? Kweli una roho ngumu kiasi hiki kama Adolf Hitler! Onea huruma raia wako. Usifurahie unayoyaona, kama unafurahia ujue kuna KARMA.
HADI LINI WATU WATAENDELEA KUPOTEA?