Rais Samia Hakuhitaji Kiapo cha Urais

- - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - -
Makala hii ilitoka July 13, 2021 kwenye RAIA MWEMA ukurasa wa 13
- - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - -
Rais John Magufuli alifariki saa 12:00 jioni ya tarehe 17/03/2021, Rais Samia Suluhu Hassan aliapishwa masaa 40:15 baadaye, yaani tarehe 19/03/2021 saa 04:15 asubuhi.

Kiapo hiki kilifanya Chama cha Wanasheria nchini (TLS) kishauri ateuliwe waziri mkuu kwa kuwa ndivyo inavyoelekeza ibara ya 51(2) ya katiba yetu Tanzania.

Makundi yaliibuka ya kuipinga na kuiunga mkono TLS, lakini yote hayakuonyesha historia ya viapo. Makala hii inaonyesha historia hiyo ilivyo msingi usioepukika wa jambo hili.

Kuanzia mwaka 325 ukatoliki ulikuwa dini rasmi Ulaya na serikalini kulikuwa na maaskofu, mapadri na watawa.

Kuanzia mwaka 793 Ulaya ilikumbwa na vita za kila mara. Hivyo mtawala wa jamii alilazimika kuwa jasiri anayeweza kupigana vita. Jasiri huyo aliitwa "amiri jeshi mkuu", yaani mfalme au malkia.

Kwa kuwa dini ilitawala maisha, mtu aliaminika alipotoa tamko la kidini linaloitwa "oath" yaani "kiapo". Hivyo kila ajira ilianza kwa kuapa kumtii mfalme, yaani "oath of allegiance".

Kiapo cha watawala Ulaya kilianza mfalme Phocas wa Roma alipopishwa mwaka 602 kikaitwa "oath of coronation". Hata hivyo siku ya kuapishwa haikuwahi kuhesabika kama tarehe ya kuanza utawala wake.

Karne ya 16 ukatoliki ukaanza kutokuwa dini rasmi, maisha hayakuhitaji kuapisha kila mtu. Kiapo cha utii ("oath of allegiance") kikabaki tu kwa wanaoomba uraia na wasaidizi wa mfalme kama askari na wabunge.

Katika kiingereza neno "office" asili yake ni kilatini “opus” na “facere” yaani "kazi inayotendwa". Hata hapa limetafsiriwa mara 302 kwenye katiba kuwa ni "kazi" au "shughuli" au "majukumu" au "madaraka" au "kiti".

Hivyo ubunge, uwaziri, ujaji, urais zote ni "ofisi" ambazo Marekani zina kiapo kinachoitwa "oath of office", si kama Uingereza ambako serikali inaanza kazi pale waziri mkuu anapobusu mkono wa mfalme au malkia.

Hivyo mtawala alikosekana ofisini iwapo tu amefariki au kajiuzulu na mrithi alirithi ofisi sekunde ileile "kiti hakikubaki wazi". Mrithi wa mfalme aliitwa "prince" au "princess".

Je nini hutokea rais wa Tanzania akikosekana ofisini? Rais akikosekana ofisini ibara ya 47(1)(c) ya katiba inasema makamu atafanya "kazi zote za urais".

Bado watu duniani huuliza je, mrithi huanza kazi siku anapoapishwa au siku alipofariki mtangulizi? Hadi hapa unaweza kujibu swali hili ila tuone wataalam wanavyolijibu.

Mwaka 1984 "Tume ya Kurekebisha Sheria" ya Australia ilitoa ripoti iitwayo "Relating to the Demise of the Crown" ikieleza kwamba mrithi huitawala Australia kuanzia sekunde anapofariki mtawala na si lazima aapishwe.

Hata wasomi wa Uingereza wanaeleza hivyohivyo katika kitabu chao "Swearing in the new King, (ISBN: 9781903903810)". Sasa tuone mifano ya waliotawala Uingereza tangu sekunde waliyofariki baba zao.

Edgar aliyeitawala Uingereza tangu mwaka 959 aliapishwa mwaka 973. Elizabeth II ameitawala tangu Februari 1952 aliapishwa Juni 1953. Mfalme Edward VIII ameitawala mwaka 1936 na hakuapishwa kabisa.

Hata Marekani, makamu wa rais ndiye mrithi wa urais, hahitaji kuapishwa anaporithi urais. Mwaka 1841 William Harrison alifia madarakani wakati katiba ikisema, rais akifariki au kujiuzulu makamu "atafanya kazi zote za urais".

Mawaziri waliona makamu wa Rais John Tyler hajageuka kuwa rais ingawa anafanya kazi za urais. John Tyler akaona haiwezekani afanye "kazi zote" za urais halafu asiitwe rais, hivyo akajitangaza kuwa rais wa Marekani.

Japokuwa John Tyler aliapa kiapo cha urais yeye alikiita "superfluous" yaani hakikuhitajika, aliapa tu kupunguza ubishi uliokuwepo, kama kinavyoeleza kitabu "John Tyler, Champion of the Old South", ukurasa wa 202-203.

Mwaka 1967 Marekani iliingiza hoja za John Tayler kwenye katiba. Marekebisho hayo ya 25 yanasema rais akifariki au kujiuzulu, makamu anageuka kuwa rais, hayasemi aapishwe, ninayanukuu, "In case of the removal of the President from office or of his death or resignation, the Vice President shall become President".

Hivyo, hakuhitajiki kumuapisha mrithi anayerithi utawala, kote Uingereza na Marekani tulikorithi miundo yao.

Sasa tuirejee ibara ya 51(2) inayosema rais "akishashika madaraka" atateua waziri mkuu. Je, Rais Samia alishika lini madaraka ya urais? Mfumo wa urithi tuliouona na pia katiba yetu vinajibu swali hili kama ifuatavyo.

Moja, makamu wa rais ni mrithi kama "prince" na "princess", hivyo, si tu madaraka aliyarithi sekunde ya kifo cha Rais Magufuli, bali pia hakulazimika kuapishwa.

Mbili, kwa kuwa anapofanya "kazi zote" za rais ibara ya 47(1)(c) ya katiba haimuhitaji aapishwe, ndivyo pia haikumuhitaji aapishwe sekunde Rais Magufuli alipokosekana kazini kwa kufariki.

Kiapo alichoapa Rais Samia hakikuongeza jukumu jipya nje ya aliyoyapata sekunde ile aliyofariki Rais Magufuli. Hivyo Samia Suluhu ameanza urais tangu sekunde aliyofariki Rais Magufuli.

Hata inapotokea anapishwa, japo si lazima, ile mifano ya Uingereza imetuonyesha kwamba haapishwi wakati wa maombolezo kwani ni rahisi kusahau protokali kama ilivyotokea Tanzania na Marekani.

Mwaka 1963 Rais John Kennedy wa Marekani alipofariki waandaaji walisahau Biblia hadi Rais Lyndon Johnson akaapishwa kwa kutumia kitabu cha "Misale ya Waumini" wakati hakuwa mkatoliki.

Hata alipoapishwa Rais Samia ule mkuki na ngao ya taifa vilisahauliwa hivyo hatuna picha ya Rais Samia akiwa ameshika mkuki na ngao kama marais waliomtangulia.

Hata siku ya mazishi ya Rais Magufuli, Generali Venance Mabeyo, kwa maneno yake, alitaabika kumpongeza Rais Samia kwa kuwa haikuwa siku ya kupongeza.

Hitimisho ni kwamba hatujawahi kukosa amiri jeshi mkuu hata kwa robo sekunde. Hivyo tuache kuamini kwamba Samia alianza urais siku aliyoapishwa kwani aliuanza sekunde ileile aliyofariki Rais Magufuli, tarehe 17/03/2021.

Kinachotakiwa ni kuiondoa ibara ya 37(5) na 50(2)(d) ili hata asiyetafiti atambue kirahisi kwamba rais anapofariki basi sekunde hiyohiyo makamu anakuwa rais ("automatically") kama Marekani walivyojirekebisha mwaka 1967.

Pia, maneno kiti cha "kuwa wazi" yaondolewe kwenye katiba kwani muundo wenye mrithi hauachi kiti wazi. Kitakachotusaidia ni katiba ya Marekaniambamo hayajawahi kuwemo maneno hayo.
Sababu ya kiapo kwa Rais, au Jaji, au Waziri, au RC, au DC, au mbunge, nk. si kutangaza lini madaraka ya mhusika yanaanza; bali ni kuwathibitishia wananchi mbele ya Mungu kwamba mhusika anaahidi kutimiza majukumu anayokabidhiwa kama ipasavyo. Tarehe ya kuanza majukumu hutangazwa pekee na huenda ikawa tofauti na siku ya kula kiapo. Ndiyo maana hutangazwa kwamba uteuzi huo utaanza tarehe fulani. Kwa hiyo madhumuni hasa ya kula kiapo ni hilo la kuahidi kutimiza kazi kiadilifu. Siyo kuashiria madaraka yanaanza lini.
 
Mto
- - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - -
Makala hii ilitoka July 13, 2021 kwenye RAIA MWEMA ukurasa wa 13
- - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - -
Rais John Magufuli alifariki saa 12:00 jioni ya tarehe 17/03/2021, Rais Samia Suluhu Hassan aliapishwa masaa 40:15 baadaye, yaani tarehe 19/03/2021 saa 04:15 asubuhi.

Kiapo hiki kilifanya Chama cha Wanasheria nchini (TLS) kishauri ateuliwe waziri mkuu kwa kuwa ndivyo inavyoelekeza ibara ya 51(2) ya katiba yetu Tanzania.

Makundi yaliibuka ya kuipinga na kuiunga mkono TLS, lakini yote hayakuonyesha historia ya viapo. Makala hii inaonyesha historia hiyo ilivyo msingi usioepukika wa jambo hili.

Kuanzia mwaka 325 ukatoliki ulikuwa dini rasmi Ulaya na serikalini kulikuwa na maaskofu, mapadri na watawa.

Kuanzia mwaka 793 Ulaya ilikumbwa na vita za kila mara. Hivyo mtawala wa jamii alilazimika kuwa jasiri anayeweza kupigana vita. Jasiri huyo aliitwa "amiri jeshi mkuu", yaani mfalme au malkia.

Kwa kuwa dini ilitawala maisha, mtu aliaminika alipotoa tamko la kidini linaloitwa "oath" yaani "kiapo". Hivyo kila ajira ilianza kwa kuapa kumtii mfalme, yaani "oath of allegiance".

Kiapo cha watawala Ulaya kilianza mfalme Phocas wa Roma alipopishwa mwaka 602 kikaitwa "oath of coronation". Hata hivyo siku ya kuapishwa haikuwahi kuhesabika kama tarehe ya kuanza utawala wake.

Karne ya 16 ukatoliki ukaanza kutokuwa dini rasmi, maisha hayakuhitaji kuapisha kila mtu. Kiapo cha utii ("oath of allegiance") kikabaki tu kwa wanaoomba uraia na wasaidizi wa mfalme kama askari na wabunge.

Katika kiingereza neno "office" asili yake ni kilatini “opus” na “facere” yaani "kazi inayotendwa". Hata hapa limetafsiriwa mara 302 kwenye katiba kuwa ni "kazi" au "shughuli" au "majukumu" au "madaraka" au "kiti".

Hivyo ubunge, uwaziri, ujaji, urais zote ni "ofisi" ambazo Marekani zina kiapo kinachoitwa "oath of office", si kama Uingereza ambako serikali inaanza kazi pale waziri mkuu anapobusu mkono wa mfalme au malkia.

Hivyo mtawala alikosekana ofisini iwapo tu amefariki au kajiuzulu na mrithi alirithi ofisi sekunde ileile "kiti hakikubaki wazi". Mrithi wa mfalme aliitwa "prince" au "princess".

Je nini hutokea rais wa Tanzania akikosekana ofisini? Rais akikosekana ofisini ibara ya 47(1)(c) ya katiba inasema makamu atafanya "kazi zote za urais".

Bado watu duniani huuliza je, mrithi huanza kazi siku anapoapishwa au siku alipofariki mtangulizi? Hadi hapa unaweza kujibu swali hili ila tuone wataalam wanavyolijibu.

Mwaka 1984 "Tume ya Kurekebisha Sheria" ya Australia ilitoa ripoti iitwayo "Relating to the Demise of the Crown" ikieleza kwamba mrithi huitawala Australia kuanzia sekunde anapofariki mtawala na si lazima aapishwe.

Hata wasomi wa Uingereza wanaeleza hivyohivyo katika kitabu chao "Swearing in the new King, (ISBN: 9781903903810)". Sasa tuone mifano ya waliotawala Uingereza tangu sekunde waliyofariki baba zao.

Edgar aliyeitawala Uingereza tangu mwaka 959 aliapishwa mwaka 973. Elizabeth II ameitawala tangu Februari 1952 aliapishwa Juni 1953. Mfalme Edward VIII ameitawala mwaka 1936 na hakuapishwa kabisa.

Hata Marekani, makamu wa rais ndiye mrithi wa urais, hahitaji kuapishwa anaporithi urais. Mwaka 1841 William Harrison alifia madarakani wakati katiba ikisema, rais akifariki au kujiuzulu makamu "atafanya kazi zote za urais".

Mawaziri waliona makamu wa Rais John Tyler hajageuka kuwa rais ingawa anafanya kazi za urais. John Tyler akaona haiwezekani afanye "kazi zote" za urais halafu asiitwe rais, hivyo akajitangaza kuwa rais wa Marekani.

Japokuwa John Tyler aliapa kiapo cha urais yeye alikiita "superfluous" yaani hakikuhitajika, aliapa tu kupunguza ubishi uliokuwepo, kama kinavyoeleza kitabu "John Tyler, Champion of the Old South", ukurasa wa 202-203.

Mwaka 1967 Marekani iliingiza hoja za John Tayler kwenye katiba. Marekebisho hayo ya 25 yanasema rais akifariki au kujiuzulu, makamu anageuka kuwa rais, hayasemi aapishwe, ninayanukuu, "In case of the removal of the President from office or of his death or resignation, the Vice President shall become President".

Hivyo, hakuhitajiki kumuapisha mrithi anayerithi utawala, kote Uingereza na Marekani tulikorithi miundo yao.

Sasa tuirejee ibara ya 51(2) inayosema rais "akishashika madaraka" atateua waziri mkuu. Je, Rais Samia alishika lini madaraka ya urais? Mfumo wa urithi tuliouona na pia katiba yetu vinajibu swali hili kama ifuatavyo.

Moja, makamu wa rais ni mrithi kama "prince" na "princess", hivyo, si tu madaraka aliyarithi sekunde ya kifo cha Rais Magufuli, bali pia hakulazimika kuapishwa.

Mbili, kwa kuwa anapofanya "kazi zote" za rais ibara ya 47(1)(c) ya katiba haimuhitaji aapishwe, ndivyo pia haikumuhitaji aapishwe sekunde Rais Magufuli alipokosekana kazini kwa kufariki.

Kiapo alichoapa Rais Samia hakikuongeza jukumu jipya nje ya aliyoyapata sekunde ile aliyofariki Rais Magufuli. Hivyo Samia Suluhu ameanza urais tangu sekunde aliyofariki Rais Magufuli.

Hata inapotokea anapishwa, japo si lazima, ile mifano ya Uingereza imetuonyesha kwamba haapishwi wakati wa maombolezo kwani ni rahisi kusahau protokali kama ilivyotokea Tanzania na Marekani.

Mwaka 1963 Rais John Kennedy wa Marekani alipofariki waandaaji walisahau Biblia hadi Rais Lyndon Johnson akaapishwa kwa kutumia kitabu cha "Misale ya Waumini" wakati hakuwa mkatoliki.

Hata alipoapishwa Rais Samia ule mkuki na ngao ya taifa vilisahauliwa hivyo hatuna picha ya Rais Samia akiwa ameshika mkuki na ngao kama marais waliomtangulia.

Hata siku ya mazishi ya Rais Magufuli, Generali Venance Mabeyo, kwa maneno yake, alitaabika kumpongeza Rais Samia kwa kuwa haikuwa siku ya kupongeza.

Hitimisho ni kwamba hatujawahi kukosa amiri jeshi mkuu hata kwa robo sekunde. Hivyo tuache kuamini kwamba Samia alianza urais siku aliyoapishwa kwani aliuanza sekunde ileile aliyofariki Rais Magufuli, tarehe 17/03/2021.

Kinachotakiwa ni kuiondoa ibara ya 37(5) na 50(2)(d) ili hata asiyetafiti atambue kirahisi kwamba rais anapofariki basi sekunde hiyohiyo makamu anakuwa rais ("automatically") kama Marekani walivyojirekebisha mwaka 1967.

Pia, maneno kiti cha "kuwa wazi" yaondolewe kwenye katiba kwani muundo wenye mrithi hauachi kiti wazi. Kitakachotusaidia ni katiba ya Marekaniambamo hayajawahi kuwemo maneno hayo.
Mtoa mada ametoa hoja zake kwa uadilifu na kukariri mambo kadhaa kutia nguvu hoja anayojenga. Hii ni mada nzuri na hivyo ndivyo inavyotakiwa katika uwanja hu wa JF wa Great Thinkers. Badala yake, nimeona baadhi ya wachangiaji wanaingiza mambo ambayo hayahusiani kabisa na mada. Kwa mfano, mmoja amesema 'tunahitaji katiba mpya'. Sasa hili linahusika vipi na mada husika? Mwingine akasema kama CCM ingekuwa inafuata Katiba, ingekuwa imekwishatoweka zamani. Tafsiri ya kauli hiyo ni kwamba Katiba ni nzuri. Kasoro ni kwamba haifuatwi. Vivyo hivyo michango mingi imejikita katika mambo ya Katiba, kitu ambacho mtoa mada hakukidhamiria katika uzi huu. Michango kama hiyo inashusha hadhi ya jukwaa hili la Great Thinkers. Kama una tatizo na Katiba, anzisha uzi wako juu ya somo hilo. Siyo kuchafua uzi wa mwenzako.
 
Asante kaka,

Hata mim sitaki kupata sifa ya mtoa mada. Nimeeleza kwamba hii makala niliiona niliposoma gazeti la RAIA MWEMA.

Makala iliandikwa na Joseph Magata.


Mto

Mtoa mada ametoa hoja zake kwa uadilifu na kukariri mambo kadhaa kutia nguvu hoja anayojenga. Hii ni mada nzuri na hivyo ndivyo inavyotakiwa katika uwanja hu wa JF wa Great Thinkers. Badala yake, nimeona baadhi ya wachangiaji wanaingiza mambo ambayo hayahusikani kabisa na hoja za kwenye mada. Kwa mfano, mmoja amesema 'tunahitaji katiba mpya'. Sasa hili linahusikana vipi na mada husika? Mwingine akasema kama CCM ingekuwa inafuata Katiba, ingekuwa imekwishatoweka zamani. Tafsiri ya kauli hiyo ni kwamba Katiba ni nzuri. Kasoro ni kwamba haifuatwi. Vivyo hivyo michango mingi imejikita katika mambo ya Katiba , kitu ambacho mtoa mada hakukidhamiria katika uzi huu. Michango kama hiyo inashusha hadhi ya jukwaa hili la Great Thinkers. Kama una tatizo na Katiba, anzisha uzi wako juu ya somo hilo. Siyo kuchafua uzi wa mwenzako.
 
Asante kaka,

Hata mim sitaki kupata sifa ya mtoa mada. Nimeeleza kwamba hii makala niliiona niliposoma gazeti la RAIA MWEMA.

Makala iliandikwa na Joseph Magata.
Asante kwa ufafanuzi. Kwa ufupi ni kwamba makala ya Magata ilikuwa ya kisomi hasa. Hata kama msomaji hukubaliani na hoja zilizotolewa, ruksa kwako kuzikosoa hoja hizo. Siyo kuanza kulalamikia mambo ambayo hayakudhamiriwa kwenye mada.
 
Makala yako ni nzuri kwa sababu za kihistoria ila kuhusu Samia kuwa alianza kazi mara moja Magufuli alipokufa ninakupinga.

Magufuli alifariki tarehe 9/ 03/ 2021 au kabla ya hapo. Na Samia alitangaza msiba tarehe 17/ 03/ wa na aliapishwa tarehe19/ 03/ 21.

Kwa kipindi cha siku 8 Serikali ilikuwa imetekwa nyara na kikundi cha wasiri wa Magufuli ( Bashiru, Chamuriho, Prof Mchembe, Dotto James) ambao walikuwa ndiyo watendaji wakuu wa Serikali.

Bila hisani ya Mabeyo CDF, Tanzania ingekuwa ni mahali tofauti kabisa na tulivyo sasa.

Kwa mazingira hayo ilikuwa lazima Samia aapishwe ili Sukuma Gang watengwe
Kwenye list umemsahau Pole Pole, Gwajima na yule DPP wa zamani!
Hakika CDF na JK walicheza kuliokoa Taifa.
Nakumbuka pilika pilika kabla ya ule usiku wa tangazo la msiba na yaliyojiri baada ya pale.. Yaani unaona kabisa serikali ilikuwa imetekwa nyara!
 
Ni lini Tanzania imeanza kutumia katiba? Tungekuwa tunatumia katiba japo robo tu hiyo ccm ingekuwa imeshafutwa siku nyingi ni genge la kigaidi tu sawa na Al qaeda tu.

Na huu ndio tunaita uozo wa mawazo

Mnakaa kufikiri hiyo katiba mpya ndio suluhu na njia pekee ya kuwatoa CCM madarakani na kuwaweka wapuuzi wasiojielewa madarakani na sio kufikiri namna gani Katiba mpya inaweza kuleta chachu na tija ktk maendeleo ya nchi
 
Kwenye list umemsahau Pole Pole, Gwajima na yule DPP wa zamani!
Hakika CDF na JK walicheza kuliokoa Taifa.
Nakumbuka pilika pilika kabla ya ule usiku wa tangazo la msiba na yaliyojiri baada ya pale.. Yaani unaona kabisa serikali ilikuwa imetekwa nyara!
Kabisa Mkuu, bila CDF Mabeyo tulikuwa tumekwisha poteana
 
Kila kitu kuhusu urais wa Samia ulivyokuja kimeelezwa huku kwenye huu uzi.

Kifo cha Magufuli kimethibitisha pasipo shaka kuwa sisi kama nchi hatuna utaratibu wowote rasimi wa kikatiba, kisheria au usio wa kisheria unaotuongoza katika kuhesabu au kuzitambua awamu za serikali.

Kama utaratibu rasimi huo, basi ni wazi hauleweki na unapaswa kutazamwa upya ili kuondoa huu mkanganyiko unaojitokeza sasa tena ukiwahusisha viongozi wakubwa tu katika nchi yetu.

Hivyo, tunapaswa kuwa na utaratibu unaotamka rasimi kama awamu ya serikali inahesabiwa pale anapoingia Raisi mpya hata ikitokea Raisi aliepo madarakani anafariki na kurithiwa na makama wake au vinginevyo. .

Tujiulize, ikitokea tunapata Raisi mwingine kutokana na sababu zilizoainishwa na katiba yetu, Raisi huyo atakuwa ni wa serikali ya awamu ya tano, ya sita at saba?

Kwakuwa hatuna utaratibu unaoeleweka, hata awamu ya Nyerere inaweza isiwe ni awamu ya kwanza kwani zilikuwepo serikali za kikoloni kabla ya Nyerere kuwa Raisi.

Tujifunze kutokana na makosa kwa kuupatia suluhisho huu mkanganyiko uliopo sasa.
 
Mto

Mtoa mada ametoa hoja zake kwa uadilifu na kukariri mambo kadhaa kutia nguvu hoja anayojenga. Hii ni mada nzuri na hivyo ndivyo inavyotakiwa katika uwanja hu wa JF wa Great Thinkers. Badala yake, nimeona baadhi ya wachangiaji wanaingiza mambo ambayo hayahusiani kabisa na mada. Kwa mfano, mmoja amesema 'tunahitaji katiba mpya'. Sasa hili linahusika vipi na mada husika? Mwingine akasema kama CCM ingekuwa inafuata Katiba, ingekuwa imekwishatoweka zamani. Tafsiri ya kauli hiyo ni kwamba Katiba ni nzuri. Kasoro ni kwamba haifuatwi. Vivyo hivyo michango mingi imejikita katika mambo ya Katiba, kitu ambacho mtoa mada hakukidhamiria katika uzi huu. Michango kama hiyo inashusha hadhi ya jukwaa hili la Great Thinkers. Kama una tatizo na Katiba, anzisha uzi wako juu ya somo hilo. Siyo kuchafua uzi wa mwenzako.
Hawataelewa
 
- - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - -
Hitimisho ni kwamba hatujawahi kukosa amiri jeshi mkuu hata kwa robo sekunde. Hivyo tuache kuamini kwamba Samia alianza urais siku aliyoapishwa kwani aliuanza sekunde ileile aliyofariki Rais Magufuli, tarehe 17/03/2021.

Kinachotakiwa ni kuiondoa ibara ya 37(5) na 50(2)(d) ili hata asiyetafiti atambue kirahisi kwamba rais anapofariki basi sekunde hiyohiyo makamu anakuwa rais ("automatically") kama Marekani walivyojirekebisha mwaka 1967.

Pia, maneno kiti cha "kuwa wazi" yaondolewe kwenye katiba kwani muundo wenye mrithi hauachi kiti wazi. Kitakachotusaidia ni katiba ya Marekaniambamo hayajawahi kuwemo maneno hayo.
Nadhani tulikuwa chini ya Kaimu Rais, immediately baada ya JPM kuwa ametwaliwa na Bwana.
Je, Kaimu Rais anahitaji kuapishwa?
By the way, bila kuapishwa Kaimu Rais hana mamlaka ya kufanya baadhi ya mambo fulani fulani mithili kusaini au kufuta hati za hukumu za vifo; kwa watu waliohukumiwa kunyongwa.

Umeandika hapa mengi na ninadhani wewe ni mwanasheria. Unadhani ilikuwa ni busara kwa Kaimu Rais kuapishwa immediately, after an hour or so, baada ya JPM kutwaliwa na Bwana? Huoni kwamba hapa Katiba ingetumika kuu-override ubinadamu, na hivyo sheria kuwa ya muhimu zaidi kuliko ubinadamu? Au hoja yako hapa ni kwa sababu Wamarekani wana mechanism yenye mchakato ambao si sawa na wa kwetu?
Issue unayojaribu kutuleleza sisi hapa ni ipi hasa? Ni kwamba tulifanya makosa kwa sababu tu tulifanya tofauti na wanavyofanya Marekani, au?
 
Nilikwambia, hawataelewa na wengine hawatasoma kabisa kama huyu anaishia kudhani.

Nadhani tulikuwa chini ya Kaimu Rais, immediately baada ya JPM kuwa ametwaliwa na Bwana.
Je, Kaimu Rais anahitaji kuapishwa?
By the way, bila kuapishwa Kaimu Rais hana mamlaka ya kufanya baadhi ya mambo fulani fulani mithili kusaini au kufuta hati za hukumu za vifo; kwa watu waliohukumiwa kunyongwa.

Umeandika hapa mengi na ninadhani wewe ni mwanasheria. Unadhani ilikuwa ni busara kwa Kaimu Rais kuapishwa immediately, after an hour or so, baada ya JPM kutwaliwa na Bwana? Huoni kwamba hapa Katiba ingetumika kuu-override ubinadamu, na hivyo sheria kuwa ya muhimu zaidi kuliko ubinadamu? Au hoja yako hapa ni kwa sababu Wamarekani wana mechanism yenye mchakato ambao si sawa na wa kwetu?
Issue unayojaribu kutuleleza sisi hapa ni ipi hasa? Ni kwamba tulifanya makosa kwa sababu tu tulifanya tofauti na wanavyofanya Marekani, au?
 
- - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - - -
Makundi yaliibuka ya kuipinga na kuiunga mkono TLS, lakini yote hayakuonyesha historia ya viapo. Makala hii inaonyesha historia hiyo ilivyo msingi usioepukika wa jambo hili.
?????????????!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Kwa hiyo Katiba inasema pia kuwa TLS ndiyo wana mamlaka ya kushauri nani anatakiwa kuapishwa, au waliamua kushauri tu kwenye swala hili specific kwa sababu wao ni mahiri wa mambo ya sheria?
 
Ndiyo maana Samia anasema Katiba mpya si hitaji la wengi maana hamuijui hata ya sasa, kama wewe.

?????????????!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
Kwa hiyo Katiba inasema pia kuwa TLS ndiyo wana mamlaka ya kushauri nani anatakiwa kuapishwa, au waliamua kushauri tu kwenye swala hili specific kwa sababu wao ni mahiri wa mambo ya sheria?
 
Ndiyo maana Samia anasema Katiba mpya si hitaji la wengi maana hamuijui hata ya sasa, kama wewe.
Hujajibu swali. Ungejibu swali kwanza halafu ndiyo unituhumu kuwa sijui. Nauliza tena; je; Katiba inasema pia kuwa TLS ndiyo wana mamlaka ya kushauri nani anatakiwa kuapishwa, au waliamua kushauri tu kwenye swala hili specific kwa sababu wao ni mahiri wa mambo ya sheria?
 
Hujajibu swali. Ungejibu swali kwanza halafu ndiyo unituhumu kuwa sijui. Nauliza tena; je; Katiba inasema pia kuwa TLS ndiyo wana mamlaka ya kushauri nani anatakiwa kuapishwa, au waliamua kushauri tu kwenye swala hili specific kwa sababu wao ni mahiri wa mambo ya sheria?
Muulize mwandish wa makala.
 
Back
Top Bottom