KARLO MWILAPWA
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 2,590
- 4,603
Tukiwa na watu wenye mtazamo huu tulionao wa uzembe, kusukumwa na uvivu basi tusitegemee mabadiliko yoyote chanya kwa kubadili katiba maana watekelezaji wakubwa wa katiba ni watu.
Kwa mfano, mtazamo mkubwa wa wapinzani kwenye mabadiliko ya katiba ni kubadili vifungu vinavyoelezea mamlaka ya Rais na Tume huru ya Taifa ya uchaguzi kitu ambacho ni tofauti kabisa na mtazamo wa mkulima, mfanyakazi au mwingine yoyote hivyo kwa tofauti ya mitazamo hii mabadiliko ya katiba itakuwa ni bure.
Katika kubadilisha mitazamo kwa kuwajengea uelewa wananchi juu ya katiba, Serikali ya Rais Samia imekuja na mpango kabambe wa kutoa elimu ya katiba. Mpango ambao unakubaliwa na kila mwanamabadiliko na mwanamageuzi.
Kwanza, kutoa elimu ya katiba itasaidia Kujenga mtazamo wa pamoja wa mabadiliko ya katiba. Kila mtu atafahamu umuhimu wa mabadiliko ya katiba kwa upande wake binafsi na sio kwa upande wa wanasiasa. CHADEMA inataka mabadiliko ya katiba wakiamini katiba mpya itawasaidia kushinda wakati mkulima anaamini katiba itamsaidia kwenye kilimo, mitazamo miwili tofauti.
Pili, kutoa elimu kutasaidia kutoandika katiba katika mtazamo wa kundi Fulani wakati katika ni Kwa ajili ya watanzania wote na ushiriki wa Kila mmoja unahitajika. Kwa Sasa mchakato wa katiba mpya umeshikiliwa sana na wanasiasa na kuna hatari kama wanasiasa wakaendelea kuhodhi mchakato huu katiba mpya itatatua matatizo ya kisiasa pekee.
Tatu, Baada ya elimu ya kutosha na Kila mtu kufahamu lengo la katiba Kwa upande wake baada ya hapo tutakuwa tumefanikiwa pakubwa kuwa na mtazamo wa pamoja.
Kwa mfano, mtazamo mkubwa wa wapinzani kwenye mabadiliko ya katiba ni kubadili vifungu vinavyoelezea mamlaka ya Rais na Tume huru ya Taifa ya uchaguzi kitu ambacho ni tofauti kabisa na mtazamo wa mkulima, mfanyakazi au mwingine yoyote hivyo kwa tofauti ya mitazamo hii mabadiliko ya katiba itakuwa ni bure.
Katika kubadilisha mitazamo kwa kuwajengea uelewa wananchi juu ya katiba, Serikali ya Rais Samia imekuja na mpango kabambe wa kutoa elimu ya katiba. Mpango ambao unakubaliwa na kila mwanamabadiliko na mwanamageuzi.
Kwanza, kutoa elimu ya katiba itasaidia Kujenga mtazamo wa pamoja wa mabadiliko ya katiba. Kila mtu atafahamu umuhimu wa mabadiliko ya katiba kwa upande wake binafsi na sio kwa upande wa wanasiasa. CHADEMA inataka mabadiliko ya katiba wakiamini katiba mpya itawasaidia kushinda wakati mkulima anaamini katiba itamsaidia kwenye kilimo, mitazamo miwili tofauti.
Pili, kutoa elimu kutasaidia kutoandika katiba katika mtazamo wa kundi Fulani wakati katika ni Kwa ajili ya watanzania wote na ushiriki wa Kila mmoja unahitajika. Kwa Sasa mchakato wa katiba mpya umeshikiliwa sana na wanasiasa na kuna hatari kama wanasiasa wakaendelea kuhodhi mchakato huu katiba mpya itatatua matatizo ya kisiasa pekee.
Tatu, Baada ya elimu ya kutosha na Kila mtu kufahamu lengo la katiba Kwa upande wake baada ya hapo tutakuwa tumefanikiwa pakubwa kuwa na mtazamo wa pamoja.