Rais Samia anasifiwa kupita kiasi

Rais Samia anasifiwa kupita kiasi

Kila siku utasikia,"Rais kajenga barabara hapa:Rais katujengea zahanati."
Watu wanamwabudu Rais,na yeye hafanyi kitu chochote kuwazuia. Haya ndiyo mambo yanayomchukiza Mungu.

Kwa ajili Uchaguzi Mkuu unakaribia,acha watu wanisifie zaidi na zaidi.

Magufuli hakuwa anasifiwa namna hii; ingawa watu walikuwa wanasema huyu mtu kaongoza nchi siku kidogo tu,lakini nchi yetu imepata maendeleo kama Ulaya.

Marekani utasikia mara moja moja wanasema,"The Biden Education Programme,au The Biden Housing Project,lakini hii ni kwa sababu Kuna strong Opposition Party,na wanataka kutofautisha mambo.

Kikwete mara moja tu walikuwa wanaongea kuhusu " mamilioni ya Kikwete". Lakini kila siku tunasikia kuhusu " mamilioni ya Samia".

Hata ukimpa mtoto mdogo peremende,lazima uhakikishe kwamba yule mtoto anamsifu Mungu.

Kwa hiyo wajihadhari hawa watu wote wanaotaka kuitwa "superstar"
Haifanyiki kwa bahati mbaya ni mkakati maalum wa wale wanaofaidika na utawala wake
 
Mwingine huyu hata usingizi hapati, akilala anaota kusifia, akiamka ni kusifia tu mchana kutwa, hii tabia inaweza kuwaathiri kisaikolojia, iacheni kwa usalama wa afya zenu.
Magufuli aliiharibu sana hii nchi
 
dharau ni jambo zuri, la muhumu na la maana sana kwa mtu asie na dira wala uelekeo na ndio hua chimbuko la mihemko, ghadhabu na unyumbu wake baada ya kuangukia poa kwa kila kitu mwisho wa siku, kwasababu anakua anakua na liburi na amepotoka....

sie hatunaga dharau, mzaha, wala haya, kwa mtu au chama chochote tunapokua tunapotafuta tunacho hitaji kwa maslahi mapana ya waTanzania wote....

Rais Comrade Dr.SSH ndie kiongozi anaependwa zaidi barani Africa kwa sasa...
Madaraka mnayotafuta kwa mbeleko ya vyombo vya Dola. Yaani tunawaona ni makhanithi wa hali ya juu.
 
Niwakumbushe kitu tu kwamba chimbuko la praise team.

Sote tuliohai tunatambua kwamba siku zote serikali inawajibika kwa raia wake na inaeleweka vyema kupitia chama tawala kwa awamu ya kwanza hadi ya 3 serikali ilikuwa imara ila ilipofika awamu ya 4 mambo yalibadilika kwa namna flani ikawa viongozi wamefocus zaidi kwenye matumbo yao kuliko mahitaji ya raia ikafikia stage kila mdau ni mpiga dili au dalali wa kuuza rasilimali zetu kwa wageni kujilimbikizia utajiri tu. Haki za wanyonge kuporwa na wenye mali zikakithiri. Kiufupi taswira ya chama ikachafuka sana na hakuna mtu alikuwa anataka kuisikia CCM so ilibidi waje na masterplan mpya.

Katika kikili kakara ndio akapitakana Magufuli maana ndie angalau alikuwa na haiba ya kukubalika na raia. Kwa kua watu walikuwa na chuki sana na chama ndipo Magu akaamua kujiposition yeye kama yeye ili kuleta relevance kwa chama. Ndio mfumo wa praise team ulianzia hapo. Lengo lilikuwa kuleta relevance ya uongozi wa CCM ili raia nyongo ziwapungue maana walikuwa washaichoka mno na ilibaki nukta tu waipe chadema nchi.

Magu alikubalika na kuirudisha CCM kwenye chart baada ya kuamua kutawala kinyume na awamu ya 4 kabisa kutokana na mfumo wake wa ku favour wananchi zaidi kuliko wanasiasa na matajiri. So wengi walimsifia sana na alikuwa akijinadi yeye kama kiongozi mkuu wa serikali.
Mkuu, kumbu kumbu zako zipo 'hot' sana, pamoja na ufafanuzi uliouweka ni sahihi 100% .

Na kwenye uchaguzi mkuu wa 2015 nembo ya mgombea wa Ccm, haikuwa na jina la chama bali ilikuwa na picha ya mwenge, Magufuli pamoja na M kubwa kumaanisha Magufuli, siyo Ccm.

Baada ya kuwa Rais, aliendelea kutawala kama Rais aliyetokana na mgombea binafsi, akiitaja Ccm kwa nadra sana, nadhani kiubinadamu aliona haya kuitaja na kuinadi Ccm ya mafisadi, hadi pale kwenye mkutano wa marais wastaafu, Mkapa alipoikaripia kanuni hiyo ya kutawala anayoifuata Magufuli ya kujitaja yeye badala ya chama, lakini kanuni hiyo tayari ilikuwa imekwisha kutamalaki.

Baada ya hapo ndipo Magufuli akaanza kuiweka Ccm mdomoni mwake, ingawa vitendo vyake havikuendana kabisa na viongozi na makada wa Ccm watangulizi wake tunaowajua sisi.

Ni kweli kabisa kuwa huu 'msamiati' mpya wa ...'Rais kafanya, Rais kajenga, Rais katoa mabilioni'... ulianzia kwake.

Sasa, kwa walamba viatu kauli hizi zimefika mahali pake maana zinafupisha na kurahisisha maneno ya kujikomba.

Je ni kweli pamoja na sifa za usomi walizonazo Mawaziri pamoja na Wabunge wote, hawana uelewa wa lugha sahihi ya kuelezea uwajibikaji wa Serikali katika kutekeleza miradi mbali mbali ya maendeleo hadi wammwagie sifa Rais kama anatoa fedha zake za binafsi mfukoni mwake?

Tena hawataji 'title' ya Rais tu, ni lazima wamtaje kwa title pamoja na majina yake yote matatu kanakwamba yupo mTz asiye elewa jina la Rais!
 
Madaraka mnayotafuta kwa mbeleko ya vyombo vya Dola. Yaani tunawaona ni makhanithi wa hali ya juu.
hayo maneno na malalamiko ya wanaotegemea kushundwa uchaguzi , yamezoeleka sana sio tu kwa wanaoshindwa uchaguz Tz, bali pia EA na Africa kwa ujumla na kwahiyo hayadhoofishi malengo wala mipango ya ushindi wa kishindo kwa wenye mikakati madhubuti...

kwahiyo wewe pamoja na kibaraka wenu,
muendelee kubabaika na kuzubaa hivyo hivyo na sababu hizo hizo miaka nenda miaka rud, huku na sisi tusonge mbele kwa bidii na mipango ya ushindi na kuwatumikia wananch....
 
hayo maneno na malalamiko ya wanaotegemea kushundwa uchaguzi , yamezoeleka sana sio tu kwa wanaoshindwa uchaguz Tz, bali pia EA na Africa kwa ujumla na kwahiyo hayadhoofishi malengo wala mipango ya ushindi wa kishindo kwa wenye mikakati madhubuti...

kwahiyo wewe pamoja na kibaraka wenu,
muendelee kubabaika na kuzubaa hivyo hivyo na sababu hizo hizo miaka nenda miaka rud, huku na sisi tusonge mbele kwa bidii na mipango ya ushindi na kuwatumikia wananch....
Nasema hivi, hakuna mwanaume anayesimamisha vizuri anaweza kujisifia ushindi wa mbeleko ya vyombo vya Dola. Mipango madhubuti ya ushindi haijawahi kufanywa kwa kutegemea mbeleko ya vyombo vya Dola.
 
Usiwe mgeni basi katika hii country, kuna kipindi kuliibuka wimbi la kila anaesifia ,anaibuka na moja ya nafasi serikalini,
Kwaiyo wote hao unaowaona ni walenga faida , wakiwa vyumbni mwao ambapo hawaonwi na Makada na waimba pambio wenzao wanasonya tu
 
Anayo cult of worship and dedicated praise singers utadhani Kim Il Sung wa Korea. Usiwashe radio au TV maana utakutana na uharo non-stop wa shukrani zisizoisha kwa "Mheshimiwa Dokta Rais Samia Suluhu Hassan" kwa kufanya hiki na kuteletea kile. It's complete utter nonsense!
 
Magufuli hakuwa anasifiwa namna hii; ingawa watu walikuwa wanasema huyu mtu kaongoza nchi siku kidogo tu,lakini nchi yetu imepata maendeleo kama Ulaya.

N
Nakubaliana na wewe kwenye hoja ya msingi kuwa hatuna haja ya kumsifu sana Rais.

LAKINI nakupinga kwa NGUVU zote kwenye hiyo paragraph ya Magufuli. Magufuli ndiye aliyeasisi mambo ya Rais kusifiwa. Awamu 1-4 hatukuwa na mambo haya. Magufuli alitengeneza wajinga na misukule. Kuna akina Prof Kabudi, Aggrey Mwanri, Sheikh Alhad wa Bakwata waliwahi kusema Magufuli ni kama Mungu au ni maarufu kuliko Yesu na Muhammad!!

Wakati Mimi najuwa Magufuli alikuwa muuaji tu, katili asiyetumia akili, kila wakati anapanda kichaa, mwizi, mwongo na kimsingi ni TAKATAKA
 
Magu alikubalika na kuirudisha CCM kwenye chart baada ya kuamua kutawala kinyume na awamu ya 4 kabisa kutokana na mfumo wake wa ku favour wananchi zaidi kuliko wanasiasa na matajiri. So wengi walimsifia sana na alikuwa akijinadi yeye kama kiongozi mkuu wa serikali.
Kwa mfumo wa Magufuli wa alivyoendeasha siasa ndani ya chama na Serikali ni kwamba CCM ilikuwa inategemea Police na NEC kubaki madarakani.

Hakukuwa na demokrasia ya kuhesabu kura wala hamna anayejua CCM inakubalika kiasi gani kwa wananchi. Hivyo Magufuli alikuwa anajidanya tu kuwa eti mwaka 2020 aliishinda uchaguzi kwa 82%.
Alikuwa anadhalilisha wenzie kwa kuwafanya bidhaa. Kimsingi aliwanunua akina Mtulia, Silinde, Gekul, Mollel, kwa mtindo wa human trafficking.

Eti unasema alikijenga chama? Alijenga vipi ? Lile DUBWASHA nafuu lilikufa
 
mnyonge mnyongeni haki yake mpeni 🐒

ili kutofatisha na wengine, rais comrade Dr SSH anapiga kazi na for sure ana mipango na ana malengo na waTanzania,

ukweli usemwe,
kiuchumi Dr.SSH yupo mstari wa mbele kabisa kuupaisha,
kisiasa Dr SSH yupo mstari wa mbele sana kuimarisha demokrasia,

kijamii Dr.SS yupo mstari wa mwanzo kabisa kuhakikisha miundombinu na huduma za jamii zinawafikia waTz wote kwa uhakika na zinawatisheleza 🐒

anaachaje kusifiwa kila uchwao 🐒

na vip wale wa mihemko na malalamiko kwa kila lililo jema kwao baya 🐒
Huu upumbabu uliasisiwa na mwenda zake na viongozi wa tanzania walivyo wajinga wajinga huwa wana copy na ku paste huwa hawajiongezi wao ni kuiga tuu na wakaona ndio njia fariki ya kujipendekeza kwa watawala
 
Kila siku utasikia,"Rais kajenga barabara hapa:Rais katujengea zahanati."
Watu wanamwabudu Rais,na yeye hafanyi kitu chochote kuwazuia. Haya ndiyo mambo yanayomchukiza Mungu.

Kwa ajili Uchaguzi Mkuu unakaribia,acha watu wanisifie zaidi na zaidi.

Magufuli hakuwa anasifiwa namna hii; ingawa watu walikuwa wanasema huyu mtu kaongoza nchi siku kidogo tu,lakini nchi yetu imepata maendeleo kama Ulaya.

Marekani utasikia mara moja moja wanasema,"The Biden Education Programme,au The Biden Housing Project,lakini hii ni kwa sababu Kuna strong Opposition Party,na wanataka kutofautisha mambo.

Kikwete mara moja tu walikuwa wanaongea kuhusu " mamilioni ya Kikwete". Lakini kila siku tunasikia kuhusu " mamilioni ya Samia".

Hata ukimpa mtoto mdogo peremende,lazima uhakikishe kwamba yule mtoto anamsifu Mungu.

Kwa hiyo wajihadhari hawa watu wote wanaotaka kuitwa "superstar"
Watanza ni wapumbavu tu
 
Kila siku utasikia,"Rais kajenga barabara hapa:Rais katujengea zahanati."
Watu wanamwabudu Rais,na yeye hafanyi kitu chochote kuwazuia. Haya ndiyo mambo yanayomchukiza Mungu.

Kwa ajili Uchaguzi Mkuu unakaribia,acha watu wanisifie zaidi na zaidi.

Magufuli hakuwa anasifiwa namna hii; ingawa watu walikuwa wanasema huyu mtu kaongoza nchi siku kidogo tu,lakini nchi yetu imepata maendeleo kama Ulaya.

Marekani utasikia mara moja moja wanasema,"The Biden Education Programme,au The Biden Housing Project,lakini hii ni kwa sababu Kuna strong Opposition Party,na wanataka kutofautisha mambo.

Kikwete mara moja tu walikuwa wanaongea kuhusu " mamilioni ya Kikwete". Lakini kila siku tunasikia kuhusu " mamilioni ya Samia".

Hata ukimpa mtoto mdogo peremende,lazima uhakikishe kwamba yule mtoto anamsifu Mungu.

Kwa hiyo wajihadhari hawa watu wote wanaotaka kuitwa "superstar"
Mwenye mbwa ndiye huelekeze mbwa wake wamlambe wapi!
 
Mkuu hajamfikia Mwendazake! Hata robo ya mwendazake haijafika!

Mwendazake mwenyewe ilijipachika unyapala wa malaika!

Wengine sasa, wakadiriki kumuita Mungu! Umesahau mara hii???

Umesahau sifa za Musiba??!
Naona huyu Poppy Hatonn anaandika kama raia wa kigeni. Hakuna mtu alipenda masifa kama Magufuli
 
Back
Top Bottom