Rais Samia anafanya usanii wa demokrasia. Maridhiano ni janja tu ya kujisafisha kimataifa

Sexless

JF-Expert Member
Mar 11, 2017
21,563
50,415
Nimefuatilia kauli na Matendo ya rais Samia nimejiridhisha kwamba siyo mpenda demokrasia kama anavyojinadi majukwaani.

Amejigamba kwamba ana ngozi ngumu na kusema anaruhusu uhuru wa kusema, kukosoa na kujieleza. Kwa taarifa yako ndugu msomaji huyu mama hana ngozi ngumu kwa Mambo yasiyomuumiza tu. Mifano ipo mingi:

1. Aliwaasa wandishi wa habari kuwa "wasimparure".

2. Ndugai akiwa spika, alitoa maoni yake lkn bahati mbaya yakamparura mhe rais. Kilichompata Ndugai sote tunakijua.

3. Amekubali mazungumzo na CHADEMA ili kuleta maridhiano na yameanza kufanyika. Lakini matendo ya serikali yake hayaoneshi kama kuna kujali ama kuheshimu mazungumzo hayo. Tunayaona haya kwenye suala la wabunge 19 waliofukuzwa uanachama na Chadema.

Hapa ni dhahiri kwamba mama anataka maridhiano mdomoni tu lakini moyoni mwake ana ajenda ya siri. Siri yenyewe ni ama anafanya danganya toto (dangany wapinzani) au anatafuta kuaminiwa na mataifa wahisani.

5. Mhe Rais hata katika suala la Loliondo ameonesha jeuri ya hali juu sana. Achilia mbali asasi za kiraia na wanaharakati lakini hata wabunge na wananchi wa Loliondo wamepiga kelele sana kuhusu kupinga maamuzi ya kuwaondoa wamasai toka ardhi yao. Amekaa kimya na kuwapuuza.

Mwisho. Nawashuri chadema kujiondoa kwenye mazungumzo yanayoendelea kwani hayatazaa matunda yoyote. Wanachezeshwa ngoma wasiojua mwisho wake.
 
Mimi huwa nacheka sana hivi mtu mwenye akili timamu unaweza kumwamini SA100
emoji856.png
emoji856.png
Kiukweli haaminiki
 
Mwisho. Nawashuri chadema kujiondoa kwenye mazungumzo yanayoendelea kwani hayatazaa matunda yoyote. Wanachezeshwa ngoma wasiojua mwisho wake.
Watake wenyewe "kuchezeshwa ngoma", lakini kama wakienda kwenye hayo mazungumzo wanajua aina ya mtu wanayejadili naye, sioni tatizo kabisa.

Ukitaka kujua tabia ya Samia, jikumbushe alivyofanya kazi na kuishi ndani ya serikali ya Magufuli.

Ukichambua Samia huyo, utakuwa umemfahamu vizuri zaidi Samia ni mtu wa namna gani.

Huwezi kwenda na kujiondoa akili yote wakati ukijadili na mtu wa aina ile, eti kwa vile amepaka wanja na kulegeza macho.
 
Alikuwa Makamu Mwenyekiti wa Bunge la Katiba ya Warioba chini ya Samuel Sitta , alijionyesha wazi kupinga maoni ya wananchi , leo mtu yuleyule amebadilikaje ?
Sema mkuu, sema watu wasikie.

Usisahau kitu. Mtu huyu huyu alikuwa Makamu wa nani vile? Mtu anayeweza kuhimili mazingira yale atakuwa tofauti na yanayotendeka na mkubwa wake? Tofauti inaweza kuwa mwonekano tu wa utendaji wa mabo yaleyale.
 
Nimefuatilia kauli na Matendo ya rais Samia nimejiridhisha kwamba siyo mpenda demokrasia kama anavyojinadi majukwaani...
Wanasiasa ni mwana SII hasa maneno na matendo yao hata SII ya kuyaamini,usemalo Lina ukweli japo Kwa upande mwingine panaweza kuwa na matokeo ila SII yanayolengwa.
 
Wanasiasa ni mwana SII hasa maneno na matendo yao hata SII ya kuyaamini,usemalo Lina ukweli japo Kwa upande mwingine panaweza kuwa na matokeo ila SII yanayolengwa.
Kwa tafsiri yetu ya kiafrica ni kwamba Sii-hasa ni uongo unaofanana na Ukweli !!!
 
Back
Top Bottom