Guselya Ngwandu
Member
- Sep 17, 2021
- 39
- 84
David McAllister, alipotosha kwamba viongozi wengi wa upinzani wamekamwta na kuwekwa katika magereza tofauti tofauti, wakati inafahamika kwamba tangu Rais Samia Samia Suluhu aingie madarakani kesi nyingi zilizokuwa zikipigiwa kelele na vyama vya upinzani zilifutwa ( Septemba 22,2021 Tundu Lissu alifutiwa kesi ya uchochezi, June 28,2021 Mdude Nyangali aliachiwa huru kisha akatoka na kwenda kumtukana Rais hadharani lakini yuko huru hadi leo, bila kusahau kuachiwa huru kwa Mashekhe wa Uamsho ambalo lilikuwa ombi la Wapinzani kwa miaka mingi).
David MacAllister ambaye amekiri kufahamiana na watu kadhaa ndani ya Tanzania, huku kukiwa na ushahidi kwamba Rafiki yake ni Tundu Lissu anayefahamika kwa kutunga uwongo mwingi dhidi ya Tanzania, alijiegemeza katika kesi ya Freeman Mbowe. Alitumia maneno mengi, lakini hiyo pekee ndiyo ilikuw ahoja yake, huku akilazimisha kwamba Rais wa Tanzania akiuke misingi ya Kidemokrasia na kuingilia uhuru wa Mahakama.
Hoja za kubumba za David McAllister ziligonga mwamba baada ya ukweli kuelezwa ndani ya Bunge hilo , baada ya ukweli wa mabo kusemwa.
Mbunge Rita Laranjinha alieleza kwamba, Rasis Samia Suluhu Hassan ameleta tumaini jipya ndani ya Tanzania katika kipindi kifupi alichoingia madarakani.
Tanzania imepongezwa kwa namna ilivyofaulu kubadilisha uongozi kwa amani na kufuata Katiba kufuatia kifoi cha Hayati Magufuli aliyekuwa Rais.
Lakini pia Bunge la Ulaya limeelezwa kuhusu hatua zinazochukuliwa na Rais Samia Suluhu katika kuimarisha Demokrasia, bila kusahau maamuzi yake ya kukabiliana na janga la Corona kwa njia za kisayansi zinazokubalika duniani kote.
Kung’ara huko kwa Tanzania katika Bunge la Ulaya ni muendelezo wa mema yanayoendelea kuchipua ndani ya Tanzania baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kuifungua nchi kupitia diplomasia, na kulinda misingi ya demokrasia ambapo hivi sasa vyama vya siasa vinaendelea kufanya shughuli zao za ndani kwa uhuru mkubwa.