Rais Magufuli yashamshinda?

Rais Magufuli yashamshinda?

Mimi kila siku naomba asifike kituo cha mabasi cha Ubongo saa kumi na mbili asubuhi. Maana akiona mabasi yanavyokwenda mikoani na idadi kubwa ya wasafiri, anaweza kusema " Marufuku mabasi kuondoka Dar, watu wote hawa wakiondoka nani atafanya kazi?"
umenichekesha mkuu. (Ila inawezekana kabisa hilo ulilosema)
 
Na kwanza tuliosema huyu ni One term president inawezekana hata asikamilishe One Term

Ofcourse sio lazima akae madarakani miaka 5.
Je unamjua mteuliwa wa CCM wa nafasi ya urais na baada ya kusimikwa hapo ambaye hajamaliza 5? au 10?
Kwa tume ipi ya uchaguzi? Ya Kivuitu?

Uchaguzi mkuu Tz ni changa la macho tu. Wenyewe wanateuana, kusimikana na kupokezana kijiti tu.
 
Bunge linaweza mfukuza kazi Rais
Lkn Bunge hili la TZ ambalo Rais anaogopwa hata kuhojiwa kwa kauli zake za hovyo kama hizi?
Bunge hili ambalo ni jipu? Bunge, jimbo la Ikulu?
Nioneshe Mbunge mmoja wa chama cha majipu, ufisadi na unafiki anayeweza kupeleka hoja ya kumtumbua Rais.

Ile Rasimu ya katiba ya Mzee wa vijisenti na Sitta iliyodhaminiwa na CCM inatoa nafasi hiyo ya kumtumbua Mkulu?
 
Si mlisema Kikwete dhaifu, haya hangaikeni na Magufuli mbabe. Mlisema nchi hii inataka Rais mwenye uthubutu wa kidikteta kama Kagame ili mambo yaende. Mkamsifia Kagame mkamponda Kikwete, haya Magufuli huyo sasa mmebadili gia angani mnataka Rais asiye dikteta. Kiongozi hawezi kuwaridhisha waongozwa wooote. At least waliompigia kura ya hapana watampinga hata afanye mazuri yote, watayapinga tu..

Magufuli chapa ilale...
 
Bunge hili ambalo ni jipu? Bunge, jimbo la Ikulu?
Nioneshe Mbunge mmoja wa chama cha majipu, ufisadi na unafiki anayeweza kupeleka hoja ya kumtumbua Rais.

Ile Rasimu ya katiba ya Mzee wa vijisenti na Sitta iliyodhaminiwa na CCM inatoa nafasi hiyo ya kumtumbua Mkulu?
Katiba ya Sitta inampa nguvu Rais kuliko hii ya sasa!Kuna kipengele mle kinasema Rais anaweza kukuweka Mahabusu"akihisi wewe ni tatizo la usalama wa Taifa"

Ahahaha kazi sana kuishi Africa
 
Si mlisema Kikwete dhaifu, haya hangaikeni na Magufuli mbabe. Mlisema nchi hii inataka Rais mwenye uthubutu wa kidikteta kama Kagame ili mambo yaende. Mkamsifia Kagame mkamponda Kikwete, haya Magufuli, bado mnataka Rais asiye dikteta. Kiongozi hawezi kuwarudhisha waongozwa wooote. At least waliompigia kura ya hapana watampinga hata afanye mazuri yote, watayapinga.

Magufuli chapa ilale...
Huku kitaa wanakosa usingizi kwa kukosa sukari kwa bei elekezi.

Wanasema wameuziwa mbuzi ndani ya gunia.
 
Rais ni Magufuli na ataendelea kuwa magufuli. huko anakopita ni shangwe na vigelegele. wananchi wanatamani aseme neno roho zao zifrahi. huku mko busy kutunga ngonjera na hadithi zisizo na vichwa wala miguu......
Shangwe zakununuliza izo nazo niza kujisifia?
 
Je unamjua mteuliwa wa CCM wa nafasi ya urais na baada ya kusimikwa hapo ambaye hajamaliza 5? au 10?
Kwa tume ipi ya uchaguzi? Ya Kivuitu?

Uchaguzi mkuu Tz ni changa la macho tu. Wenyewe wanateuana, kusimikana na kupokezana kijiti tu.
Hilo changa la macho hilo, suluhisho lake ni dogo sana..!!
Wana jitahidi sana kupunguza makali ya wapinzani kwa kuwarudisha nyuma huku wakiwasahaulisha ajenda muhimu zilizokuwa zinaelekea kuzaa matunda.

Sasa hivi swala la katiba limemezwa na swala la ukandamizaji demokrasia wakati huo siku sinasogea, na mafanikio yatakayotakana na swala la katiba ndio mwarobaini wa hilo "changa la macho"
 
Hivi ni mimi tu au na wengine mpo mnaoona kama vile mambo yashamshinda huyu Magufuli?

Kuna hali fulani hivi naiona ambapo jamaa ni kama anaamka tu kila asubuhi na kutoa maamuzi ya kukurupuka kurupuka.
Yaani yeye ni amri tu....fanya hivi....fukuza huyu....twende kule...nk.

Yapo baadhi ambayo ni mazuri ambapo mtu unaona kabisa hapa nia ni nzuri lakini kuna mengine yenye ukakasi sana hadi kunifanya nianze kuhoji hekima na busara za huyo bwana!
Kifupi tu hajajua ni jinsi gani anatakiwa kuiongoza nchi hii na sababu ni kutokana na kutokuwepo kwa maandalizi timilifu ya yeye kama yeye kabla hajakabidhiwa kijiti na mtangulizi wake.

Kuhakiki hili tunaona 80% ya maamuzi yake yana majuto mbeleni.
 
Hilo changa la macho hilo, suluhisho lake ni dogo sana..!!
Wana jitahidi sana kupunguza makali ya wapinzani kwa kuwarudisha nyuma huku wakiwasahaulisha ajenda muhimu zilizokuwa zinaelekea kuzaa matunda.

Sasa hivi swala la katiba limemezwa na swala la ukandamizaji demokrasia wakati huo siku sinasogea, na mafanikio yatakayotakana na swala la katiba ndio mwarobaini wa hilo "changa la macho"
Upinzani kwa umoja wao,wapinzani Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu kwa CCM. Tangia 1995 wanapeleka kichwa kunyolewa, mwisho wake wanaishia kama Dr. Mihogo na maharage, Prof. Nafsi imenisuta, Mrema aliamua kufanya biashara na mtumbua Majipu na Ngosha Cheyo aka "Nitawajaza Mapesa" anajisifia kuwa angalau wamepata kuwapiku wakwere kwa kutoa Mtumbua majipu.

Ukiwekeza kwa CCM wanakugawia umasikini, ukiwekeza kwa wapinzani unanunua kesi ya kubambikiziwa na polisi.
 
Upinzani kwa umoja wao,wapinzani Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu kwa CCM. Tangia 1995 wanapeleka kichwa kunyolewa, mwisho wake wanaishia kama Dr. Mihogo na maharage, Prof. Nafsi imenisuta, Mrema aliamua kufanya biashara na mtumbua Majipu na Ngosha Cheyo aka "Nitawajaza Mapesa" anajisifia kuwa angalau wamepata kuwapiku wakwere kwa kutoa Mtumbua majipu.

Ukiwekeza kwa CCM wanakugawia umasikini, ukiwekeza kwa wapinzani unanunua kesi ya kubambikiziwa na polisi.
solution ni nini mr?

Nini hasa kifanyike na kwanini?
 
solution ni nini mr?

Nini hasa kifanyike na kwanini?
Solution ni kuacha kufanya siasa.
Ukiacha kufanya siasa, unafanya nini?
Unarudi kijijini kulima kwa meno ili tu-enjoy wote.

CCM wana kitu wanaita "Mapinduzi daima". Chama cha mapinduzi, mapinduzi daima. Mpinzani gani mwenye mkakati wa kuuzidi huu wa mapinduzi daima?
 
CHADEMA ingekuwa imara kama zamani huyu easily angeondoka 2020
Lkn kwa upinzani huu wa hovyo hovyo wa kutowasikiliza wanachama na kujiona viongozi kama Mungu watu
Wapinzani wanawatumia wanachama wao kwenye maadamano tu
Kwenye teuzi wanapuuzi kauli za wanachama wa kawaida
Wao na CCM hamna tofauti
Magufuli atashinda 2020 hata kukiwa na TUME HURU
Mark my words
Mkuu pamoja na huu u hovyo wa wazi wa upinzani, nje ya dola ccm ni hovyo zaidi
 
Mkuu pamoja na huu u hovyo wa wazi wa upinzani, nje ya dola ccm ni hovyo zaidi
CCM hawafai kabisa
LKN CHADEMA sio substute ya CCM,nakataa
Oktoba 2015 CHADEMA ya Mbowe prior and post election WAMEFANYA MAKOSA MAKUBWA mno yasiyo weza samehewa
Niliondoka CHADEMA baada ya uteuzi wa viti maalum
Nikaona wao na CCM ni kaka na dada
 
Back
Top Bottom