Rais Magufuli yashamshinda?

Rais Magufuli yashamshinda?

tena atashinda kwa kura nyingi mnoo. hawa wapinzani hawana ajenda pumzi imekata mapema sana. wamebaki kufanya siasa za kinafiki mitandaoni
Katika hili mi naweka akiba ya maneno. Wakati utasema, hatimaye!
 
Ukipita mitaani watu washachoka na story zake...
biashara haziendi.....mood iliyopo ni kusubiri labda mambo yatanyooka soon...
sasa sijui yasiponyooka itakuaje....
Watumishi tuko hoi lakini wateule wameamuru tuchangie mbio za mwenge.
 
Mbona sijawahi tukana humu?

Mleta mada kaja na kichwa cha habari chenye mfano wa maneno ya Kanga...hajaweka ni matamko gani ya kukurupuka ...

By the way kushindwa kwa Magufuli kutaelezewa na kushindwa kutekeleza ilani aliyoiahidi...so far ameshagusia maeneo mengi ya Ilani haswa haswa kwenye Elimu bure,Mahakama ya mafisadi,Ushuru usio na tija,na utumbuaji wa watendaji wabuvu.

Ukimpinga Magufuli fanya hivyo kwa data na rejea ilani ya Ccm.
Nimeona post yako nikachefukwa
 
na wenye akili ndio walikua wanatafuna Nchii hii. sasa Magufuli anawanyoosha. vyovyote iwavyo ataawanyosha tu na Nchi itanyoka
Thubutuu amnyooshe nani? Watu wanajuwa ni roho yake mbaya hawezi kufanya lolote.sisi tunachoshindwa kumuelewa matamko yake hayaeleweki.
 
Watanzania kwa kuchagua hovyo tumevunja rekodi. Kila uchaguzi tunachagua hovyo zaidi na hatujifunzi. Mtu hata mkewe alikuwa anasita kuungana naye kwenye kampeni hatugutuki! Tumelikoroga na sasa yabidi tulinywe...watakaobakia hadi 2020 labda watakuwa wamepata aikili za kuchagua kwa umakini zaidi.

Swahiba...

Kitu ambacho sikielewi kabisa ni hiki: tokea tupate uhuru hatujawahi kuongozwa na chama kingine chochote kile zaidi ya CCM [tukizingatia na ubadilishwaji wa jina].

Kwa msingi huo, CCM ndo inawajibika moja kwa moja na hali tuliyonayo leo - dhiki iliyokithiri, huduma za jamii mbovu zilizo chini ya viwango, ufisadi, rushwa, maradhi, na mengineyo.

Cha ajabu, chaguzi baada ya chaguzi watu huishia kuwapa kura walewale ambao ndo wameileta hali tuliyonayo licha ya kutuaminisha kwamba eti sisi ni nchi tajiri sana. Tunaenda kufikia miaka 60 ya kutawaliwa na chama kilekile. Aibu.

Sasa, mtu unaweza kujenga hoja ya kwamba CCM huwa hawashindi kihalali kwa sababu mazingira ambayo chaguzi hufanyika si ya huru, haki, na uwazi.

Sawa, hiyo ni hoja nzuri na yenye mashiko. Lakini mimi binafsi bado naamini kabisa kuwa kwamba watu kwa umoja wetu tukiamua kabisa kutokuipigia kura CCM tunaweza, hata kama CCM itaamua kuchakachua matokeo au kuleta mizengwe [kama ilivyofanyika Zanzibar].

Na ikitokea tukafanya hivyo na CCM kuchakachua na kuendelea kung'ang'ania madarakani walau tutakuwa kwenye nafasi nzuri zaidi ya kuishinikiza mpaka itoke. Ila kwa sasa inakuwa vigumu kwa sababu hata bunge limejaa hao hao CCM na hivyo kuifanya hoja ya chaguzi kutokuwa huru na haki kukosa nguvu kidogo.

Yaani kwa kweli ingekuwa ni juu yangu mimi basi ningependa sana kujaribu na watu wengine [zaidi ya CCM] ili tuone na wao wana nini la kutupa Watanzania.
 
Opinions. Uncle Ngosha yuko sawa. Ninamuelewa kwa sababu nilishamuelewa kabla hajawa Raisi. Ni ngumu kuielewa management style yake, mimi huwa naiita "JUST DO IT style"
Management By Walking About (MBWA)
 
Na sasa hivi hospital hakuna chanjo ya watoto,,kila kitu shidaa,vijana wanabaniwa kusoma aajiandae kukabiliana na majambazi ,,maana vijana wengi wapo tu na hawana pa kwenda
 
Rais ni Magufuli na ataendelea kuwa magufuli. huko anakopita ni shangwe na vigelegele. wananchi wanatamani aseme neno roho zao zifrahi. huku mko busy kutunga ngonjera na hadithi zisizo na vichwa wala miguu......
Mmmh nahisi unaishi nje ya Tanzania,sio kwa mahaba haya. Duuuh
 
Mimi kila siku naomba asifike kituo cha mabasi cha Ubongo saa kumi na mbili asubuhi. Maana akiona mabasi yanavyokwenda mikoani na idadi kubwa ya wasafiri, anaweza kusema " Marufuku mabasi kuondoka Dar, watu wote hawa wakiondoka nani atafanya kazi?"
 
Yakimshinda wewe unafaidika na nini? Tuambie Watanzania ili tujue. Toa lugha za kumpa moyo sio kuwazia mabaya.. Yule ni Rais wako na pia ni baba yako, lazima uwe na fikra za kinidhamu.
 
leo mpaka huyu jamaa kasema kitu! ni sawa na kumkuta chief mkwawa anahubiri siasa
 
Hivi ni mimi tu au na wengine mpo mnaoona kama vile mambo yashamshinda huyu Magufuli?

Kuna hali fulani hivi naiona ambapo jamaa ni kama anaamka tu kila asubuhi na kutoa maamuzi ya kukurupuka kurupuka.
Yaani yeye ni amri tu....fanya hivi....fukuza huyu....twende kule...nk.

Yapo baadhi ambayo ni mazuri ambapo mtu unaona kabisa hapa nia ni nzuri lakini kuna mengine yenye ukakasi sana hadi kunifanya nianze kuhoji hekima na busara za huyo bwana!

tusiwe wajinga..hata yeye mwenyewe alisema kwa hali ilivyosasa ni bora kufanya maamuzi kama kunamakosa basi yatarehekebishwa kuliko kutofanya maamuzi yeyote kwa kuogopa
 
Jamaa nchi kaiweza. Mfano jana nilikwenda beach escape 1 moja ya beach yenye wapenzi wengi lkn kwajana mambo yalikuwa ni kinyume . Nilikuta viti havina watu. Nikasogea mchangani bahari imekuwa tupu. Nikitupa jicho baharini. Hakuna hata meli moja iliyosubiri kutia nanga.

Jamaa nchi kaiweza. Na inaonekana kama nchi kasusiwa hata naawaziri wake. Na kwakweli anaejua tunakoelekea aje atufafanulie.
 
Back
Top Bottom