Rais Magufuli yashamshinda?

Rais Magufuli yashamshinda?

Kila analo fanya ni kwa nia nzur ila Aproach yake sasa.....

Nilishangazwa sana Uteuz wa maDAS kutoka kwa makada*!! Wakati dasi anatakiwa awe mtumishi wa Umma. Pia ni lini Rais amewai kuteuwa maDAS??? Utumishi wa umma una taratibu zake na kanuni zake.....sasa rais anavyo vunja kanuni, sheria na taratibu walizo jiwekea wenyewe mchana kweupe ni jambo moja baya sana...na hii haikukemewa hata! Ukiona Rais anavunja sheria na kanuni walizo jiwekea wenyewe juwa inch inakuwa kama shamba la watumwa.
 
Hivi kuna kiongozi wa Tanzania ambaye keshawahi kupingwa na kukosolewa humu kumzidi Kikwete?

Uhai karibu wote wa JF Kikwete ndo alikuwa rais na watu tumemsema sana humu.
Ni kweli. Tulimsema sana na hata mimi nilimsema sana sana! Na kusema kweli mtu kama wewe au Kiranga akimsema naona kabisa ni katika kukosoa kwa haki kusiko na makandokando kwani hata Kikwete mlikuwa mnamchambua vilivyo. Ila mimi nina niko kwnye site na naona wengi ya waliokuwa kimya wakati wa Kikwete sasa hivi hawaishi kupiga kelele. Na hawa wako wengi sana sana!
 
Hivi ni mimi tu au na wengine mpo mnaoona kama vile mambo yashamshinda huyu Magufuli?

Kuna hali fulani hivi naiona ambapo jamaa ni kama anaamka tu kila asubuhi na kutoa maamuzi ya kukurupuka kurupuka.
Yaani yeye ni amri tu....fanya hivi....fukuza huyu....twende kule...nk.

Yapo baadhi ambayo ni mazuri ambapo mtu unaona kabisa hapa nia ni nzuri lakini mengine yana ukakasi kidogo.
Yamshinde mara ngapi?
 
Hakuna namna kwa mujibu wa katiba,ya kumtoa kabla hajaleta madhara makubwa?
Mkuu OKW BOBAN SUNZU, napenda tu jinsi unavyopenda kuweka katiba,sheria,kanuni na taratibu mbele katika nyuzi zako,iwe maswali,taarifa au uchokonozi.
Ubarikiwe sana.
 
Rais ni Magufuli na ataendelea kuwa magufuli. huko anakopita ni shangwe na vigelegele. wananchi wanatamani aseme neno roho zao zifrahi. huku mko busy kutunga ngonjera na hadithi zisizo na vichwa wala miguu......
Ukifanya utafiti mdogo utagundua huko mtaani wanaomshangalia magufuli ni " layman's " ambao wanafurahishwa na uropokaji wake.watu wenye akili wote washamgundua jamaa siyo.
 
Swala siyo kuhamia Dodoma ila hiyo bajeti kaitoa wapi?anakurupuka kama kwamba tayari fedha ilisha pangwa na miundo mbinu yote muhimu tayari kaazi ipo.
Kila siku husema alikuwa hayupo tayari kuwa rais kakurupuka tu. Ndio maana kila kitu hajui nini anafanya
 
Wengi kina nani?

Mimi nimepiga kelele tangu Enzi za Mkapa.

Rais yeyote aliye madarakani atapigiwa kelele tu. Urais una mengi, na rais hawezi kupatia yote hata siku moja.

Kila siku inayopita kutakuwa cha kukosoa kuhusu serikali. Sasa watu wakimpigia kelele utasemaje kwamba walikuwa kimya wakati wa Kikwete?

Hao wengi kina nani? Unaweza kuwataja majina?

Na kwa nini huangalii hoja zao wanazomkosoa Magufuli tuzichambue kama zina msingi au hazina msingi unaanza kuangalia nani kasema nini?
Hakika kwenye neno ''wengi'' mtu kama wewe hutahusika hata kidogo. Nimekuwa nakufuatilia tangu wakati wa Kikwete na naweza kusema pasi shaka kuwa wewe ni mmoja ya watu wanaokosoa kwa kuwa kuna kasoro na sio vinginevyo.
 
Ni kweli. Tulimsema sana na hata mimi nilimsema sana sana! Na kusema kweli mtu kama wewe au Kiranga akimsema naona kabisa ni katika kukosoa kwa haki kusiko na makandokando kwani hata Kikwete mlikuwa mnamchambua vilivyo. Ila mimi nina niko kwnye site na naona wengi ya waliokuwa kimya wakati wa Kikwete sasa hivi hawaishi kupiga kelele. Na hawa wako wengi sana sana!

Kama mtu alifaidika na Kikwete haimuondoi uhalali wa kumkosoa Magufuli....

Urais wa Magufuli usiupime kwa kigezo cha Urais wa Kikwete

Urais wa Magufuli unapimwa kwa matatizo yanayojitokeza awamu hii ya tano
haijalishi Kikwete aliweza au hakuweza......
 
Hakika kwenye neno ''wengi'' mtu kama wewe hutahusika hata kidogo. Nimekuwa nakufuatilia tangu wakati wa Kikwete na naweza kusema pasi shaka kuwa wewe ni mmoja ya watu wanaokosoa kwa kuwa kuna kasoro na sio vinginevyo.
Asante kwa kunitoa.

Bado hujajibu swali. Wengi kina nani?

Tunataka kujadili hoja kwa detail, sio kwa general statements tu.
 
Bunge linaweza mfukuza kazi Rais
Lkn Bunge hili la TZ ambalo Rais anaogopwa hata kuhojiwa kwa kauli zake za hovyo kama hizi?
Mkuu,na hapa ndipo tunapoona kete ya CCM ya kumpa Raisi kofia ya Mwenyekiti wa chama.
Absolute power...
 
Ukipita mitaani watu washachoka na story zake...
biashara haziendi.....mood iliyopo ni kusubiri labda mambo yatanyooka soon...
sasa sijui yasiponyooka itakuaje....
Waliochoka n wapga dili.. Sisi maskini akhaaaaah tunamkubali ajabu.
 
Kama mtu alifaidika na Kikwete haimuondoi uhalali wa kumkosoa Magufuli....

Urais wa Magufuli usiupime kwa kigezo cha Urais wa Kikwete

Urais wa Magufuli unapimwa kwa matatizo yanayojitokeza awamu hii ya tano
haijalishi Kikwete aliweza au hakuweza......
And it is really interesting! Mimi ni wewe tujiulize ni kwanini kuna watu wanaona makosa upande mmoja tu!
 
Kama mtu alifaidika na Kikwete haimuondoi uhalali wa kumkosoa Magufuli....

Urais wa Magufuli usiupime kwa kigezo cha Urais wa Kikwete

Urais wa Magufuli unapimwa kwa matatizo yanayojitokeza awamu hii ya tano
haijalishi Kikwete aliweza au hakuweza......
Na hapo ndipo ugumu wa kulinganisha marais wawili tofauti bila kuwa very detailed unalinganisha nini unapokuja.

Kwa sababu kuna matatizo mengine ya Magufuli anapambana nayo kwa sababu Kikwete kayalea.

Na kuna matatizo mengine Magufuli hakutani nayo kwa sababu Kikwete alishayamaliza.

Sasa hapo utawalinganishaje wawili hawa kwa jumla jumla tu wakati huyo Magufuli political career yake iliyompa uzoefu alionao sasa hivi kaipata kwa appointment za Kikwete? Mtu akikwambia Magufuli ni zao la Kikwete na hivyo kumlinganisha Magufuli na Kikwete si sawa kwa sababu kwenye wimbo wa Kikwete Magufuli alishiriki kuimba chorus na kwenye wimbo wa Magufuli Kikwete ndiye alikuwa producer utakataa?
 
Nimekuelewa hasa mistari miwili ya mwisho ila kwa wale jamaa wanaolipwa kwajili ya kupinga ukweli na kung'ang'ania uongo kwao hii ni shida
 
Ukifanya utafiti mdogo utagundua huko mtaani wanaomshangalia magufuli ni " layman's " ambao wanafurahishwa na uropokaji wake.watu wenye akili wote washamgundua jamaa siyo.
na wenye akili ndio walikua wanatafuna Nchii hii. sasa Magufuli anawanyoosha. vyovyote iwavyo ataawanyosha tu na Nchi itanyoka
 
Back
Top Bottom