Rais Magufuli unawatesa walinzi wako

Rais Magufuli unawatesa walinzi wako

Raisi hulindwa na walinzi wanaoonekana na wasioonekana.Wasioonekana ni wengi kuliko wanaoonekana.Hapa naona wengi wanaongelea tu ulinzi unaoonekana!!!!!
Ni kweli mkuu Marais wengi wa Afrika walinzi wasioonekana huwa wengi zaidi ya wale wanaoonekana live , mila na desturi huzingatiwa zaidi.
 
Hadi kuanzisha thread kama hii Kumbe watanzania tunampenda Rais wetu, basi tumshauri afanye nini sio kusema unamtesa mlinzi sijui nn kimekuaje!
#Tumshauri
 
Hawateseki, wanalipia nights.

HAPA KAZI TU.
 
mleta mada yupo sahihi wanavamiwa france ukiona wale makomandoo na teknologia walionayo still inakua shida kuzuia uhalifu wa kiwango cha juu..dunia haipo salama sana Mh. tunakupenda badili na hayo magari pis sio salama kuriko ndege ni mbingu na ardhi..
 
Magufuli anawatesa kila mtu kwa moja kwa moja au indirect..... mambo mtaani magumu .... biashara haziend... mzigo hautoki kama zamani dukani... ni miez sita tu kashika hatamu na mambo yashaanza kuzingua.
wadhamini wetu washaanza kusepa, bandarini shughuli za kibiashara zinashuka kwa asilimia kubwa tu....

niko nje ya mada lakini Rais wangu inabidi aangalie vizuri kuhusu kupunguza government expenditure kuna athali gani kwa sekta binafsi
Wataanza na NSSF kisha NHC na kuendelea mpaka Wizara zote pesa zote zilizoibiwa zitarejeshwa na Safari hii Serikali itapata nyumba nyingi za kutaifisha toka Kwa Mafisadi huenda watumishi wa umma wakarejea Oyesterbay na Masaki Kwa style ingine kabsa,
 
mleta mada yupo sahihi wanavamiwa france ukiona wale makomandoo na teknologia walionayo still inakua shida kuzuia uhalifu wa kiwango cha juu..
Teknolojia ya kiafrika iko juu kuliko hiyo teknolojia ya wazungu kwenye maswala ya ulinzi hasa wa binafsi.
 
Tabia yako ya kusafiri kwa gari umbali mrefu hujui ni mbaya kiusalama?

Unawapa wakati mgumu sana walinzi wako kukulinda.Uwe unapokea na ushauri mheshimiwa Rais.

Hivi huko maporini mtu akijificha na Rocket-Propelled Grenade akakuvizia itakuwaje wakati unajua fika ukanda huo silaha kibao toka Congo zinapatikana.

Hujui pale unapopanga na mahasimu wako wanapanga pia?

Halafu pia kutumia masaa 6 barabarani wakati ungeweza kutumia saa 1, matano ukafanya kazi nyingine ni,jipu au uvivu.
 
Walinzi ndio washauri wake wa hayo mambo wanaoshauri hivyo kuwa asafirije.Fani za watu hizo achana nazo.

Usafiri hata wa anga kabla ya kusafiri wanausalama lazima wakwambie tumia.Hata angani si salama hujasikia maraisi ndege zao kutunguliwa.

Walinzi wanajua cha kufanya waachie kazi yao.Si watu wa kuchoka hovyo.Walinzi wa RAISI UNAFIKIRI ni sawa na walinzi wa CHADEMA wale wanaovaa miwani ya kuchomea magrill?

CHEKI WALINZI WA CHADEMA NA MIWANI YAO YA KUCHOMEA VYUMA
Mbeya3.jpg
Vipi zile pen zao za kupigia kura kwenye uchaguzi wa Meyas!!
 
mleta mada yupo sahihi wanavamiwa france ukiona wale makomandoo na teknologia walionayo still inakua shida kuzuia uhalifu wa kiwango cha juu..dunia haipo salama sana Mh. tunakupenda badili na hayo magari pis sio salama kuriko ndege ni mbingu na ardhi..
Ni kweli mkuu ndiyo maana Afrika Mizimu huwekewa Mbele zaidi , mfano Kwa Sasa kule misituni kuna Koboko Kama 1000 wapo wanalinda akikatiza mwenye nia mbaya anagongwa kimya kimya anapotea , Mizimu imeimarisha Ulunzi usioonekana Kwa speed ya radi .
 
Safi sana magufuri utuone vizuri wananchi wako barabarani watoto walivyochoka wanaomba hela barabarani au chupa ya maji sijaju sehemu gani pale mbele sana ya kahama karibu na lusumo wananchi wamechoka mpaka nilitamani kulia nikakumbuka nguo nilizozitupa dar ningejua ningewapelekea na kuwatupia fasta dilishani .nivizuri walinzi waache uvivu wafanye kazi kwelikweli! Nasio uwoga wa kufikili na kujibweteka raisi ataki majibu mepesi wanausalama wapo na wanalipwa nimajukumu yao kumlinda na tunaomba wamlinde mpendwa wetu kwelikweli.
 
M
Mkuu nenda kajaribu kujificha kichakani na propela lako kesho uje utupe mrejesho! kama kabla ya kutoka nyumban kwako ushakalishwa chini ya ulinzi
msituni atafika lakini atakutana na walinzi wasioonekana Yaani koboko watazaa nae Kwa kasi ya ajabu .
 
Tabia yako ya kusafiri kwa gari umbali mrefu hujui ni mbaya kiusalama?

Unawapa wakati mgumu sana walinzi wako kukulinda.Uwe unapokea na ushauri mheshimiwa Rais.

Hivi huko maporini mtu akijificha na Rocket-Propelled Grenade akakuvizia itakuwaje wakati unajua fika ukanda huo silaha kibao toka Congo zinapatikana.

Hujui pale unapopanga na mahasimu wako wanapanga pia?

Halafu pia kutumia masaa 6 barabarani wakati ungeweza kutumia saa 1, matano ukafanya kazi nyingine ni,jipu au uvivu.
Walinzi hawateseki, hiyo ndiyo kazi yao waliyosomea, tofauti na unavyofikiri, wanafurahia kazi yao
 
Ana kazi pia pale Mpakani Rusumo Afungue stop boarder za TRA na Uhamiaji....pande zote 2 watakuwa kwenye jengo moja! Then ndio ataenda Kigali!
 
Usalama wa rais ni muhimu sio kubishana pasipo na mana tatizo sifa ndiyo zinatuponza sawa ulinzi tunao wakutosha lakini ni kujitafutia tatizo rais ni mtu muhimu sana siyo wakutembea na gari kwa masaa sita ni hatari hafadhari ingalikuwa ndani ya nchi lakini nje ya nchi mmm haya bana kila la kheri rais wetu safari njema
 
yehodaya nazungumzia ulinzi wa rais sio wako huo wa kuchanjiwa usilogwe harafu unakufa kwa kipindupindu au malaria..
 
yehodaya nazungumzia ulinzi wa rais sio wako huo wa kuchanjiwa usilogwe harafu unakufa kwa kipindupindu au malaria..

Kwani raisi wa Tanzania huwa anapatikanaje si lazima akubalike na wote wanaoonekana na wasioonekana? Ili akipata uraisi alindwe na wote.
 
Tabia yako ya kusafiri kwa gari umbali mrefu hujui ni mbaya kiusalama?

Unawapa wakati mgumu sana walinzi wako kukulinda.Uwe unapokea na ushauri mheshimiwa Rais.

Hivi huko maporini mtu akijificha na Rocket-Propelled Grenade akakuvizia itakuwaje wakati unajua fika ukanda huo silaha kibao toka Congo zinapatikana.

Hujui pale unapopanga na mahasimu wako wanapanga pia?

Halafu pia kutumia masaa 6 barabarani wakati ungeweza kutumia saa 1, matano ukafanya kazi nyingine ni,jipu au uvivu.

Tena Kwa TAARIFA Yako Presidential Protection TEAM Yake Inafurahi Mno Kutembea Kwa Barabara Na Mkubwa Wao Ili Wamwonyeshe Kuwa SERIKALI Yake Kamwe Haikupoteza Pesa Zake Kuwapekeleka Kusoma au Kufanya Hayo MAFUNZO Yao Ya KIULINZI. Sitaki Niende Deep Kwani Watakuja Humu Wenyewe WABOBEZI Wa Hii Kitu Ila Kwa UPEO Wangu Mdogo au Haba Wa Masuala Ya ULINZI Wa Marais Ni Kwamba KIITIFAKI Kila Kitu Chake HURATIBIWA Mapema Sana Na Kwa UANGALIFU Mkubwa Wa Madhara au Faida Na Ukiona Mpaka Rais Anapita Mahala Fulani Basi Jua WANAMUME Walishajiridhisha KIUSALA Kwa Mapana Yake. Na Usisahau Pia Kuwa Hata Anapokuwa Anasafiri Kwa Barabara AMINI USIAMINI Humo Njiani Kote Hasa Yale Maeneo HATARISHI ( Kijajusi Huita POTENTIAL TARGETS ) Zote WANAMUME Huwa Hapo Huku Maeneno Mengine Na Hata Katika MSAFARA Wake Wakiwemo WANAMUME Kadhaa Wa Njia Panda Na Mdaula au Bwawani Ambao WAKIAMUA Dar es Salaam Wote TULALE Saa 12 Jioni Inakuwa Hivyo Kutokana Na Shughuli Yao Ya KUTUKUKA Ambayo Hata WAASI Wa M23 Kule Congo Kinshasa WANAIJUA Na KUITAMBUA. Mwisho Usisahau Mkuu Kuwa Hakuna Watu LOYAL Na Patriotic Kwa Nchi Yao au AMIRI JESHI MKUU Wao Kama Hao ( WANAMUME ) Wa Makumbusho Na Makao Makuu Upanga Na Amini Kuwa Rais Wako Yupo 100% Safe Na Hakuna TAKATAKA Yoyote Awe Yupo Tanzania au Nje Ya Tanzania Anaweza KUMDHURU Kwa Njia Yoyote Ile. INTELLIGENCE Ya TANZANIA Ni Very Extraordinary Hasa Katika VIP PROTECTION. Sisi Wenyewe Huku Kwetu Nchini Rwanda Nilipo Sasa Tunawaonea WIVU!
 
Walinzi ndio washauri wake wa hayo mambo wanaoshauri hivyo kuwa asafirije.Fani za watu hizo achana nazo.

Usafiri hata wa anga kabla ya kusafiri wanausalama lazima wakwambie tumia.Hata angani si salama hujasikia maraisi ndege zao kutunguliwa.

Walinzi wanajua cha kufanya waachie kazi yao.Si watu wa kuchoka hovyo.Walinzi wa RAISI UNAFIKIRI ni sawa na walinzi wa CHADEMA wale wanaovaa miwani ya kuchomea magrill?

CHEKI WALINZI WA CHADEMA NA MIWANI YAO YA KUCHOMEA VYUMA
Mbeya3.jpg
duuh! we jamaa haufai!! hapo mwishoni umenivunja mbavu kinyama!
 
Back
Top Bottom