Rais Magufuli unawatesa walinzi wako

Rais Magufuli unawatesa walinzi wako

aka2030

JF-Expert Member
Joined
Jan 5, 2013
Posts
2,672
Reaction score
3,737
Tabia yako ya kusafiri kwa gari umbali mrefu hujui ni mbaya kiusalama?

Unawapa wakati mgumu sana walinzi wako kukulinda.Uwe unapokea na ushauri mheshimiwa Rais.

Hivi huko maporini mtu akijificha na Rocket-Propelled Grenade akakuvizia itakuwaje wakati unajua fika ukanda huo silaha kibao toka Congo zinapatikana.

Hujui pale unapopanga na mahasimu wako wanapanga pia?

Halafu pia kutumia masaa 6 barabarani wakati ungeweza kutumia saa 1, matano ukafanya kazi nyingine ni,jipu au uvivu.
 
Kwa hiyo mtazamo wako unadhani, yeye Rais ameamua kutumia barabara hivi hivi tu bila kujiandaa na kuandaliwa?!

Unafikiri suala la kumlinda anajiamulia yeye!?

Naiamini system yetu ya usalama! Ukiona wameruhusu, jua wamejiandaa; Wanajua wanachokifanya.

Au movie za porini za akina Van Damme zinakupa mawazo hayo?!

Bachi! Mimi nichicheme mengi (In mmakonde's voice)!
 
tabia yako ya kusafiri kwa gari umbali mrefu hujui ni mbaya kiusalama? unawapa wakati mgumu sana walinzi wako kukulinda.uwe unapokea na ushauri mheshimiwa rais. Hiv huko maporini mtu akijificha na Rocket-Propelled Grenade akakuvizia itakuwaje wakati unajua fika ukanda huo silaha kibao toka congo zinapatikana
Hujui pale unapopanga na mahasimu wako wanapanga pia?
halafu pia kutumia masaa 6 barabaran wakati ungeweza kutumia saa 1 matano ukafanya kazi zingne ni,jipu au uvivu

Walinzi ndio washauri wake wa hayo mambo wanaoshauri hivyo kuwa asafirije.Fani za watu hizo achana nazo.

Usafiri hata wa anga kabla ya kusafiri wanausalama lazima wakwambie tumia.Hata angani si salama hujasikia maraisi ndege zao kutunguliwa.

Walinzi wanajua cha kufanya waachie kazi yao.Si watu wa kuchoka hovyo.Walinzi wa RAISI UNAFIKIRI ni sawa na walinzi wa CHADEMA wale wanaovaa miwani ya kuchomea magrill?

CHEKI WALINZI WA CHADEMA NA MIWANI YAO YA KUCHOMEA VYUMA
Mbeya3.jpg
 
kiukweli tunapishana,kwa mfano kwenye mpira sisi tunakaba mtu ,wenzetu mpira wao wanakaba nafasi,hivyo hivyo kwa wazungu ulinzi wao hulinda eneo zima na sio kikitokea tukio. Sasa eneo la kysafiri masaa6unaweza kulidhibiti lote? Atumie ndege tu.
 
Magufuli anawatesa kila mtu kwa moja kwa moja au indirect..... mambo mtaani magumu .... biashara haziend... mzigo hautoki kama zamani dukani... ni miez sita tu kashika hatamu na mambo yashaanza kuzingua.
wadhamini wetu washaanza kusepa, bandarini shughuli za kibiashara zinashuka kwa asilimia kubwa tu....

niko nje ya mada lakini Rais wangu inabidi aangalie vizuri kuhusu kupunguza government expenditure kuna athali gani kwa sekta binafsi
 
muheshimiwa rais anasabau zake nyingi tu,labda angekuwa ameziweka wazi naiman tungepata chakuongea!! Tofauti na hapo,tz ulinzi upo wakutosha tena sana
 
tabia yako ya kusafiri kwa gari umbali mrefu hujui ni mbaya kiusalama? unawapa wakati mgumu sana walinzi wako kukulinda.uwe unapokea na ushauri mheshimiwa rais. Hiv huko maporini mtu akijificha na Rocket-Propelled Grenade akakuvizia itakuwaje wakati unajua fika ukanda huo silaha kibao toka congo zinapatikana
Hujui pale unapopanga na mahasimu wako wanapanga pia?
halafu pia kutumia masaa 6 barabaran wakati ungeweza kutumia saa 1 matano ukafanya kazi zingne ni,jipu au uvivu


Watanzania, bwana...kazi kwelikweli, yaani wanajua kila kitu...Hivi wewe unadhani RAIS anakurupuka tu kusafiri?! Itabidi utafutwe ili utoe ufafanuzi zaidi uwasaidie PSU kuhusu masuala ya ulinzi.
 
Tabia yako ya kusafiri kwa gari umbali mrefu hujui ni mbaya kiusalama?

Unawapa wakati mgumu sana walinzi wako kukulinda.Uwe unapokea na ushauri mheshimiwa Rais.

Hivi huko maporini mtu akijificha na Rocket-Propelled Grenade akakuvizia itakuwaje wakati unajua fika ukanda huo silaha kibao toka Congo zinapatikana.

Hujui pale unapopanga na mahasimu wako wanapanga pia?

Halafu pia kutumia masaa 6 barabarani wakati ungeweza kutumia saa 1, matano ukafanya kazi nyingine ni,jipu au uvivu.
Tuma maombi,
Usalama wa Raisi, c/o Magogoni, Dar es Salaam.
 
And that's the problem. Hao viongozi wasipotembea kwa magari..matatizo yetu watayajuaje? Mfano barabara ya Nyakanazi kwenda Rusomo imeharibika vibaya mno...naamini Magufuli akipita pale lazima kazi ifanyike....yes ndege ni nzuri lakini ni vema viongozi wetu wakatembea kwa barabara pia.wakayaona matatizo yetu huko wanakopita.
 
Kwa hiyo mtazamo wako unadhani, yeye Rais ameamua kutumia barabara hivi hivi tu bila kujiandaa na kuandaliwa?!

Unafikiri suala la kumlinda anajiamulia yeye!?

Naiamini system yetu ya usalama! Ukiona wameruhusu, jua wamejiandaa; Wanajua wanachokifanya.

Au movie za porini za akina Van Damme zinakupa mawazo hayo?!

Bachi! Mimi nichicheme mengi (In mmakonde's voice)!
Acha kusifia Ujinga. Kuna msemo unasema " Kama Elimu ni gharama, Jaribu Ujinga"

Kumbuka Usalama ni gharama. Ili uweze kuwa Salama ni lazima uwe stable, reliable and trustworthy. Ni lazima usome Mazingira na nyakati hata kama unawalinzi wa namna gani...,

Unadhani "Commando Mamadou Toure" hakuwa na walinzi pale Beni wakati anauwawa? Uliza aliuliwa na watu gani? Na kifaa gani kilimuua?

Hakuna watu wanafki kama warwanda. Nimekaa Congo na jirani ya maeneo ya Rwanda; I understand these people very well.

Kuna vitu vya kupunguza gharama , na vitu vingine sio vya kupunguza gharama.

Anachofanya Rais ni kutafuta sifa kwa kujifanya baharia ( kurisk maisha) ; kuishi kwa mazoea wakati ulimwengu umebadilika.

Waovu wa sasa wanatafuta headlines na si kitu kingine. Safari kama hizo hapaswi kuzitangaza , ; atangeze zile anazokwenda na ndege.

Mnawapa Magaidi opportunity na hamu ya kuwekeza TANZANIA...,

Ushauri; Afanye kama Rais wa Cameron, yeye huwa anasafiri , mfano ;- kutoka Mwanza hadi dodoma hupanda gari huku akiwa na wanajeshi wakutosha then wakati wa kurudi hupanda ndege; safari zake za gari huwa hazitangazwi

MAGUFULI aache kutafuta sifa mpaka kwenye mambo ya Usalama. Ukibana gharama mpaka kwenye Usalama maana yake nini?
 
Back
Top Bottom