makoye2009
JF-Expert Member
- Jun 12, 2009
- 2,638
- 1,219
Huyu mama umeambiwa kuwa ana zaidi ya miaka 25 kazini chini ya utendaji wake ni vijana wengi sana wamepata elimu kupitia kwake,si ajabu ukakuta wengine waliopata elimu chini ya huyu mama ni hawa hawa wanaowaita wenzao watumishi hewa au wanaweza wakawa ni ndugu zao au wanaweza wakawa ni watumishi katika serekali hihi ya kuwaita wenzao watumishi hewa,sasa je kama huyu mwalimu ana itwa mtumishi hewa na wale waliopata mafanikio kwa kupitia elimu yake waitwe akina nani?.
Twende mbele turudi nyuma.
Watu wanachanganya HEWA na KUGHUSHI CHETI. Kiuhalisia huyu mama anastahili kusamehewa na kulipwa mafao yake kwa utumishi wake wa miaka 25. Nitaeleza.
Huyu mama alitumia cheti cha shule cha marehemu shangazi wa mleta hoja. Hivo alisoma chuo akamaliza, akafaulu na kupangiwa kazi/shule ya kufundisha. Kwa maana ya HEWA huyu siyo MWALIMU HEWA!! Mwalimu hewa(ghost worker) ni yule asiyekuwepo kazini kwa maana ya jina lililoko kwenye Payroll lakini huyo mtumishi hayupo popote lakini kuna Afisa Utumishi, Mkurugenzi, Mhasibu au yeyote aliyetengeneza hilo jina anachukua huo mshahara!!!
Kwa kesi ya huyu mama alifaulu Chuo cha Waalimu na kafanya kazi kwa miaka yote zaidi ya 25. Je, ni wanafunzi wangapi wamepitia mikononi mwake?Bila shaka ni maelefu kwa maelfu wengine ni Waalimu,Madaktari, Wahandisi,Wahasibu n.k.
Hivo kumfukuza kazi mtu kama huyu ni Uonevu uliopitiliza na wa kinyama. Mbona kuna Watumishi wengi tu kwa ngazi za Uwaziri, u-RC, u-DC n.k huwa wanafanya makosa na kinachotokea Wanahamishwa sehemu ya kazi au Wanastaafishwa kwa Manufaa ya Umma lakini wanalipwa HAKI ZAO. Kwanini basi huyu mama naye kwa misingi hiyo hiyo akastaafishwa kwa manufaa ya Umma na akalipwa stahili zake ukizingatia kuwa bado mwaka 1 tu astaafu!!!
Tatizo la Viongozi wetu ni roho mbaya na kutopenda kusamehe. Wazungu huwa wanasema USITAKE KUMFANYIA MTU JAMBO AMBALO WEWE MWENYEWE HUTAKI UTENDEWE!!! Yaani watu wanaangalia kosa moja tu kati ya 100 mema aliyofanya mtu basi wana amua kuchukua hatua za kudhulumu mtu haki zake. Mbona kuna Mafisadi wamekomba MABILIONI ya Fedha za EPA,ESCROW, KAGODA n.k lakini mpaka leo wanatanua tu mitaani? Huyu maskini mwalimu na vimilioni vyake vya HELA YA MBOGA kama mara kumi hivi imekuwa nongwa!!!!Hebu tujaribu na kumwogopa Mungu sote tu binadamu.