Rais Magufuli unamuua mama yangu

Rais Magufuli unamuua mama yangu

Hebu tukague vyeti vya viongozi nao tukianza na Mtukufu wafuate wengine....itapendeza sana
 
Tunajua yawezekana ni kweli amekosea kutumia cheti cha mtu kazini lakini tutumie ubinadamu mama huyu kafanya kazi miaka zaidi ya 25 na alikuwa anategemea mafao yake karibia million 100 mwakani halaf leo hii ziyeyuke kirahisi hivi??

Rais Magufuli watu wa aina hii ya mama waonee huruma jamani mama atakufa hivi hivi tunamuona!
Dah..Yaani miaka 25 alikuwa anawajaza watu ujinga? halafu tunakuja kulalamika hapa eti watanzania wengi wana uelewa mdogo...Afungwe tu tu huyu hakuna namna,,,,,😎😎
 
Mkuu pamoja Na kwamba kweli mama pressure inaweza kumwondoa na polee kwa Hilo pia fikiria serikali imepoteza kiasi gani kwa miaka hiyo 25 ya udanganyifu? Mm ngoja nikupe mfano Nina mdogo wangu wa damu hakuwa Na cheti cha form four my bro akafanya ujanja wakapata cheti exactly chenye jina Kama la mdogo wangu mwenye cheti alishafariki. Mm nikawaambia I'm not part of the plan maana alikuwa anakuja kusoma pale nilipokuwa nafanya kazi. MUNG mkubwa akafeli nikashangilia nikamwambia umefeli kwa sababu hicho cheti siyo chako Na ilikuwa certificate. Nikamwambia kasome QT upate credit akasoma kwa miaka miwili akapata nikamwambia aingie Chuo kingine certificate Na mwaka huu kamaliza diploma. Tumuunge Rais kwa zoezi hili hata Kama Ni chungu.
 
Duuh! Inauma sana! Ila ndo hivyo sasa! Amshukuru ata Mungu kia amekifanyia kazi hicho cheti miaka yote hiyo.
 
Hii ni kweli jamani ni story imemkuta mama mdogo

Mamdogo ni mwalimu wa msingi na anatarajia kustaafu mwakani hivyo kwenye akili yake alishajiandaa kustaafu

Kitu ambacho hatukujua ni kuwa muda wote aliofanya kazi hakuwa akitumia cheti chake halisi( shangazi alifariki zaman sana hivyo ukoo ukakubaliana kumpa mama mdogo cheti cha shangazi akaingilia chuo cha ualimu miaka hiyo ya sabini na..
Mpk akaajiriwa)

Sasa kwa hesabu ya haraka mwakani anapaswa astaafu!! Ila ukaguzi huu wa Magufuli umemkumba

Mama anateseka presure inapanda asubuhi na jioni, vyeti vimehangaikiwa mpaka viapo vya kubadilisha jina ila wapi? Baraza wamekaba kooo!

Tunajua yawezekana ni kweli amekosea kutumia cheti cha mtu kazini lakini tutumie ubinadamu mama huyu kafanya kazi miaka zaidi ya 25 na alikuwa anategemea mafao yake karibia million 100 mwakani halaf leo hii ziyeyuke kirahisi hivi??

Rais Magufuli watu wa aina hii ya mama waonee huruma jamani mama atakufa hivi hivi tunamuona!
Inabidi akamatwe na aamriwe kulipa gharama zote za mishahara maana ni mwizi alikuwa anaiibia serikali. Kwanini alitumia cheti cha mwingine kwenda chuo??? Maana yake ni kuwa uwezo wake darasani ulikuwa mdogo na hakufaa hata kuwa mwalimu.
 
Hamna namna yeye angestaafu kwa hiari pale aliposikia Rais anataka kushughulikia tatizo la watumishi hewa. Sasa ni too late lazima atastaafishwa kwa kosa la fojari au kutumia cheti siyo chake. Nampongeza sana RAIS kwa zoezi hili Pendwa na kupunguza hewa kila sehemu. Ushauri wangu kwa Admin JF waangalie namna ya kupambana na WANAJUKWAA au WANAJAMVI HEWA .
Kweli ubinadamu kazi
 
Mkuu daktari feki akisababisha kifo kimoja lakini akaokoa maisha ya watu sita bado tutamwacha aendelee kutibu watu hadi astahafu apate mafao ya kustaafu kwa vile tunamuonea huruma na aliokoa maisha ya mtu?
Kwanza mkae mkijua huyo mama amefanya kosa la jinai, kwa sheria zetu kosa la jinai halina kikomo cha muda kwamba ikipita miaka kadhaa hawezi kushitakiwa kwa kosa hilo. Mwambieni tena akimbie asirudi kazini asijefungwa.
Sasa kama wakati huo dakitari hawapo mnafanyaje, lazima mumuache aendelee kuokoa na maisha ya wengine. Je inaingia akilini kumuondoa ili wale wote saba wafe ?
HERI NUSU SHARI KULIKO SHARI KAMILI
 
ndugu yangu hapo unachojaribu kukisema ni tutumie ubinadamu na tuweke pembeni sheria,mpaka lini tutaendelea kuchukuliana na kubebana hivi???mbona kama unajaribu kuturudisha kulekule enzi za rais msataafu maana yeye alikua anawachukulia watu na kuwabeba watu lakini bado hatukumuona
anafaa na watu wakawa wanafanya watakavyo...inabidi tubadilike hakuna kumwangalia mtu usoni wa kumuonea soni mtu,umevunja sheria twende na maji tu hakuna
namna muda wa kuconsider wewe ni nani
umekaa muda gani haupo kwa sasa.hapa tuna mzungumzia huyu mama lakini ukae ujue wapo wa aina hii wengi tuu huko maofisini tena ofisi nyeti nao tuwachukulie kama wewe
unvosuggest??

Haki bila huruma ni ukatili mkuu.... ebu fikiria mara 2 suala hili... na hata mahakamani ukiisha
onekana una kosa, mahakama hukupa nafasi ya mwisho kusema neno maana yake ndo hiyo, haki na huruma vinaenda pamoja.... watu kama hawa wote wastaafishwe na walipwe stahiki zao, serikali inaweza hold hata 20% ya pesa zao kama penalty na kuanzia sasa, inawekwa wazi hamna nafasi hiyo...
 
Lengo n kubana matumizi kwa iyo hapo imekula kwake msema ukweli mpenzi wa Mungu
 
Sidhani kama kuna ukweli wo wote kwenye hii thread. Miaka hiyo hakukua na NECTA wala NACTE. Hakukuwa na mambo ya kufoji vyeti. System ilikuwa madhubuti na mtu alikuwa hawezi kuripoti chuoni kwa cheti cha mwingine. Kwanza vyeti vilipelekwa kwenye hivyo vyuo muda mrefu baada ya wanafunzi kuanza masomo.

Halafu system ya sasa haina uwezo wa kuhakiki hivyo vyeti vya zamani vya Cambridge University East African Examination Council, incoporating GCE. Acha kudanganya watu wewe mtoto.
Huyu amefanya kazi miaka 25. Hapo ni miaka ya 1990 na NECTA ilikuwa hai. Ninakubaliana na wewe kwamba miaka hiyo watu walichaguliwa kwenda NECTA si kujiendea. Mashaka ya miaka ya 70 na 90 nami yananitatiza.
 
Hivi mwalimu kama huyo mama atafundisha 'kufanya fojari ni kubaya'?. Kama alifundisha hivyo; ahurumiwe. Lakini kama sio, alipwe haki yake ya kufoji.
 
aise
lazima atakuwa kachanganyikiwa sana, embu mtafutieni mtu wa kum counsel mapema
 
Mtoa mada hajasema elimu ya huyo mama yake mdogo ilikuwa darasa gani. Kama alikuwa darasa la saba na akakitumia cheti cha mtu mwingine, huyo mama ni hatari sana , ameshiriki kwa kiwango kikubwa kutoa vijana wengi ambao hawana uwezo mzuri kwasababu alikuwa anafundisha chini ya kiwango.Kumbuka elimu kubwa inayotolewa kwenye vyuo vya elimu ni jinsi ya kufundisha unapokuwa darasani wakiamini elimu ya awali uliyonayo tangu mwanzo ndio msingi. Sasa japo alifauli mafunzo ya ualimu lakini hakuwa na sifa za kielimu, alikosa elimu ya msingi katika maana ya secondary.
 
Hii ni kweli jamani ni story imemkuta mama mdogo

Mamdogo ni mwalimu wa msingi na anatarajia kustaafu mwakani hivyo kwenye akili yake alishajiandaa kustaafu

Kitu ambacho hatukujua ni kuwa muda wote aliofanya kazi hakuwa akitumia cheti chake halisi( shangazi alifariki zaman sana hivyo ukoo ukakubaliana kumpa mama mdogo cheti cha shangazi akaingilia chuo cha ualimu miaka hiyo ya sabini na..
Mpk akaajiriwa)

Sasa kwa hesabu ya haraka mwakani anapaswa astaafu!! Ila ukaguzi huu wa Magufuli umemkumba

Mama anateseka presure inapanda asubuhi na jioni, vyeti vimehangaikiwa mpaka viapo vya kubadilisha jina ila wapi? Baraza wamekaba kooo!

Tunajua yawezekana ni kweli amekosea kutumia cheti cha mtu kazini lakini tutumie ubinadamu mama huyu kafanya kazi miaka zaidi ya 25 na alikuwa anategemea mafao yake karibia million 100 mwakani halaf leo hii ziyeyuke kirahisi hivi??

Rais Magufuli watu wa aina hii ya mama waonee huruma jamani mama atakufa hivi hivi tunamuona!
Kwani nani aliwaambia jina la cheti sio lake?au shangazi yako alikuwa mfanyakazi wa serikalini?cheti hicho ni cha elimu gani ambacho alikitumia?kwa hyo alikuwa anapokea mshahara kwa jina lipi wakati cheti kina jina lipi?
 
Back
Top Bottom