Mungu amejibu maombi yako, na haja ya moyo wako, ni nani asiyejua kuwa wewe hutaki kabisa upinzani Tanzania?
Hujifichi kuonyesha chuki yako hadharani dhidi ya upinzani.
Naomba nikuulize Tafadhali mheshimiwa Rais, Kama nitakukosea nisamehe bure .
Risasi alizomiminiwa Tundu Lissu na watu wanaoitwa "wasiojulikana ". ingekuwa risasi hizo kwa mfano kamiminiwa mkuu wa mkoa au waziri yoyote, hao wahalifu wangekuwa hawajapatikana?
Tuna makovu ya mateso mengi, kuwa mpinzani hapa Tanzania ni kuchagua kifo, bado tunamwomboleza mawazo, Ben Saanane, Kanguye, Azori Gwanda na wengine wengi.
Mheshimiwa Rais, hatutaki kupiga kura ili tukipishe chama chako kitawale milele Kama wewe unavyotaka sasa wakuu wa mikoa na wilaya watatufanyaje?
Tumeamua kupumzika ili nyie mnaopendwa sana muendelee kupendwa na kutawala milele, ajabu tena imekuwa kero.
Na 2020 pia hatutapiga kura, tuache tupumzike, Tafadhali Tumechoka.
Wana CCM wapo wengi watapiga kura na kujipatia ushindi mnono.
Tumeshajua hata tukipiga kura hatushindi kwa sababu CCM huwa inashinda hata kabla ya kupiga kura sasa tunapiga kura za nini?
Tuache tupumzike.
KWA NINI WANANCHI HAWATAKI KUJIANDIKISHA?
Na Thadei Ole Mushi.
Mawazo yangu binafsi!!
Mwaka Jana mwezi wa kumi Katibu mkuu ccm Dr Bashiru alilalamika wapiga kura kupungua kwenye chaguzi za marudio, Dr Bashiru alinukuliwa akisema wapiga kura wanaojitokeza kupiga kura walikuwa chini ya asilimia Hamsini ya waliojiandikisha.
Namuona Mh Jafo naye akiingia kwenye issue ile ile kuwa zoezi la kujiandikisha kupiga kura kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa nao unasua sua. Hapa ndipo watafiti wanapotakiwa kufanya utafiti kwa nn wananchi hawataki kushiriki uchaguzi?
Ninapredict factor NNE hapa.
1.Chaguzi za marudio za mradi wa jiuzulu, unga mkono, gombea tena, shinda kwa lazima ni factor mojawapo ya wananchi kuchoshwa na chaguzi. Wananchi wa naona hata wakipiga kura kuna watu wapo mahali wanamatokeo yao tayari.
2. Hakuna Elimu iliyotolewa ya kutosha kati ya uandikishaji wa daftri la kudumu kwa ajili ya uchaguzi mkuu 2020 na daftari hili la ukaazi kwa ajili ya uchaguzi wa serikali za mitaa. Zoezi lilianza kabla ya Elimu hii ya kutofautisha kutolewa.
3. Mikutano ya vyama vya siasa kuwa na zuio za hapa na pale kumeshusha morali ya Demokrasia nchini. Mwanachama wa Chadema wa kawaida was Mbinga kwa miaka minne hajawahi kukutana na mwenyekuti wake wa chama kwenye mkutano. Mwenyekiti hana ruhusa ya kufanya mikutano akienda Mbinga atafanyia mikutano ndani na hapa atakutana tu na viongozi. Kwenye maandishi kikatiba tunatumia mfumo wa vyama vingi ila practically ni kimoja kinaoparete kwa mwavuli wa udola na kukagua utekelezaji wa ilani.
4. Vijana ndio chachu ya chaguzi zote duniani.... Hakuna uhusiano wa moja kwa moja uliopo kati ya vijana wanaosaka ajira usiku na mchana na viongozi wa kuchaguliwa. Mwitikio wa vijana ni mdogo sana, angalia kwenye media utaligundua hili sana.
Tunakoelekea.
Pamoja na population yetu kuobgezeka idadi ya wapiga kura itazidi kupungua. Lazma tulifanyie kazi eneo hili.
Agizo la waziri.
Waziri Jafo amesema atapeleka dokezo kwa Mh Rais kwa mikoa ambayo uandikishaji utadorora ikiwezekana waadhibiwe. Mh Rais naye kashakubali kuwa atawashughulikia. Wakuu wa mikoa wataanza kuhaha kuomba watu wajiandikishe ili wasikutane na rungu la mh Rais.
Wanaweza kujiandikisha lakini je watapiga kura ? Hili ni eneo jingine.
Ole Mushi.
0712702602