HOJA MURUA katika ubora wake,tatizo inachangiwa kikada mno,labda kwa kuwa makada wana maslahi binafsi na vyama vyama vyao,yaani wana ajira huko zinazowapa mkate.Pengine ni wanufaika huko ndiyo maana wanatoa hoja zenye ukakasi,kejeli,kiburi,majivuno,dharau zisizoakisi amani na mshikamano wa Taifa.Hizi si siasa ni uhuni,Lissu ni Mtanzania anayeipenda nchi yake kizalendo si adui wa Taifa,propaganda chafu dhidi yake ni ulimbukeni tu usio na tija kwa Taifa.Hoja hapa ni kuwepo kwa maridhiano no matter msuguano ni mkubwa au mdogo kiasi gani.Kutegemea viongozi wa dini waone hili ndiyo watoe wito wa maridhiano ni nadra sana kutokana na wengi wao kuwa waoga.Hili suala la maridhiano linataka haiba na utashi wa kisiasa,ni jambo muhimu ambalo litatoa muelekeo chanya wa Taifa