Rais Magufuli na Lissu wakutanishwe

Rais Magufuli na Lissu wakutanishwe

Mpasuko gani wewe unaouongelea? Huyo aliyepata kura milioni 2 ndiyo wa kuleta mpasuko ? I mean, chadema imepeta
13% vs > 85% ya CCM, sasa kuna mpasuko gani hapo ? Huo mpasuko upo vichwani mwenu tu labda na akina tundu, ...
Mahera anakupoteza, ukweli ni Lissu kura mil 7 Jiwe mil 6, waliojitokeza hawakuzidi mil 15
 
Tuijenge nchi yetu, Uchaguzi umepita Watanzania wamefanya uamuzi hakuna sababu ya kupendekeza kutaka kwenda kinyume na Watanzania! Chapa kazi Kwa masilahi ya taifa letu uone Kama wazungu hawatatuogopa!
Uamuzi kwenye mabegi
 
Tuijenge nchi yetu, Uchaguzi umepita Watanzania wamefanya uamuzi hakuna sababu ya kupendekeza kutaka kwenda kinyume na Watanzania! Chapa kazi Kwa masilahi ya taifa letu uone Kama wazungu hawatatuogopa!
Kuna vitu ukisoma unashia kucheka kifupi mchango wako unachekesha
 
View attachment 1627158
Baada ya kula kiapo, urais unaanza kupata joto.
FB_IMG_1605430308082.jpg
 
Duuh.. kwa hiyo ashapanda cheo, saivi tunaweza kumuita "Fashisti jiwe"?
Fascist / Fashisti ina maana kubwa na siyo kama inavyotumiwa kiutani utani. Utawala wa kifashisti kwa mfano unalazimisha sote kuunga juhudi hata kama juhudi hizo zinazofanyika tunaona kabisa zinatupeleka pabaya.

Utawala wa kifashisti hututaka tusihoji au kutumia bongo zetu bali 'tukishachagua' chama au mtawala basi hatuna tena nafasi ya kuhoji au kutumia bongo zetu bali kutekeleza maagizo ya mheshimiwa. Kwenda kinyume na hivyo tutahesabiwa wasaliti, tunakwamisha maendeleo, hatuna mapenzi na nchi, uzalendo wa mashaka n.k

Utawala wa kifashisti huenda mbali na kulazimisha viongozi wa dini kuunga na kutetea juhudi za mtawala na chama-dola, maana ktk utawala wa kifashisti hakuna chama cha kisiasa cha kweli ( hapa ikiwemo CCM pia ambayo tayari imeuliwa ) bali chama-dola CCM Mpya kinachoendeshwa kama idara ya serikali na watawala wachache wakubwa.

Tujiulize Tanzania haijafika hapo? Hatuoni viongozi wa kidini mmoja mmoja au kwa makundi ktk 'Kamati za Amani' au ' Kongamano za Viongozi wa Kidini kuzungumzia mafanikio ya miaka mitano' lakini huwasikii viongozi hao wa kidini wakikosoa kama haki haitendeki, raia kuumiza n.k

Wenye viwanda, biashara , wachimbaji Madini, Wasafirishaji wa Mizigo kwa Malori, Bodaboda n.k wote wanaundiwa 'Makongamano huru' kusifia hali nzuri ya kibiashara na mazingira mazuri yaliyopo kufanyia shughuli zao.

Tutafakari kuhusu utawala wa kifashisti kama upo au haupo Tanzania kufuatana na yanayoendelea toka mwaka 2016.
 
Napenda sana siasa za upinzani wenye hoja ila upinzani unaopinga maendeleo na kukejili maendeleo kila kukicha nasema hapana narudia tena hapana.

Tulionya humu mara kadhaa kwa spidi ya JPM inabidi wapinzani wabadili mbinu za kumchallenge kama kweli wanataka kuendelee kusikika lakini wao hawakusikia. Wakaendelea na mbinu zile zile walizozitumia enzi za utawala wa JK. Bahati mbay kipindi hiki wakajikuta wanaishia kuzusha mara kuna upotevu wa 1.5 tril, na kutengeneza matukio madogo madogo ya kutafuta huruma kwa wananchi kitu ambacho wananchi wengi waligundua ni uzushi.

Taifa ambalo wananchi wake bado wanashida kubwa ya maji eti wapinzani wanadai democracia, Taifa ambalo wanananchi wake zaidi ya asilimia 80 ni wakulima wanatumia zana duni za kilimo ikiwemo pembejeo eti wapinzani agenda yao kubwa ni democracia, taifa ambalo mpaka sasa kuna shule ambazo hazina milango sakafu wala madirisha achilia mbali umeme na miundombinu ya kujifunzia eti wapinzani agenda yao kuu ni democracia.

Wakati JPM akipambana kuimarisha maisha ya raia kwa siku zijazo kwa kuimarisha sekta ya miundombinu, ikiwemo ununuzi wa ndege, ujenzi wa reli SGR, ukarabati wa reli MGR, ujenzi wa bwawa kubwa la la umeme la Nyerere 2115Mw, ujenzi wa daraja la Tanzanite, ujenzi wa dara refu kuliko yote EA daraja la Busisi nk, badala ya wapinzani kumuunga. mkono au hata kutoa ushauri wao wanapinga na kukejeli kana kwamba kinachofanyika hakina maana.

Kifupi wapinzani wa Tanzania hasa wa awamu hii ya tano wameshindwa kabisa kutoa mawazo mbadala wametumia mda mwingi kukosoa, kukejeli, kutukana na kutaka kukwamisha juhudi za serikali katika kuwaletea wananchi maamendeleo, ni vyema wakatafakari na wakaja na sura ya kizalendo sio kupandikiza chuki miongoni mwa raia ndani ya taifa hili, Namna viongozi wa upinzani walivyounzungumzia muuungano wetu ni jambi ambalo halikubaliki kabisa na sio jambo la kuzungumzwa na chama kilichojiandaa kuchukua dola.
 
HOJA MURUA katika ubora wake,tatizo inachangiwa kikada mno,labda kwa kuwa makada wana maslahi binafsi na vyama vyama vyao,yaani wana ajira huko zinazowapa mkate.

Pengine ni wanufaika huko ndiyo maana wanatoa hoja zenye ukakasi,kejeli,kiburi,majivuno,dharau zisizoakisi amani na mshikamano wa Taifa.

Hizi si siasa ni uhuni,Lissu ni Mtanzania anayeipenda nchi yake kizalendo si adui wa Taifa,propaganda chafu dhidi yake ni ulimbukeni tu usio na tija kwa Taifa.

Hoja hapa ni kuwepo kwa maridhiano no matter msuguano ni mkubwa au mdogo kiasi gani.Kutegemea viongozi wa dini waone hili ndiyo watoe wito wa maridhiano ni nadra sana kutokana na wengi wao kuwa waoga.

Hili suala la maridhiano linataka haiba na utashi wa kisiasa,ni jambo muhimu ambalo litatoa muelekeo chanya wa Taifa
 
Mwizi wa kura, mjivuni, mjenga chuki, muuaji, mzandiki,na asiyefuata demokrasia hatufai. Tunataka Uhuru, Haki, na Maendeleo ya Watu. Atuachie Ikulu yetu.
 
Ningeelewa kana mtu angependekeza Rais akutane na viongozi wa vyama vya upinzani walioko nyumbani, Mbowe, Zitto, nk; lakini siyo Lissu. Yeye aachwe atimize nia yake aliyonayo kwa taifa let, then tutaona kama atatia mguu Tanzania tena.
Are you sitting on your brain?
 
...
Siasa zetu zimekua chanzo Cha utengano huu. Sio kwetu tu siasa imekua chanzo Cha anguko la umoja wa kitaifa bali duniani kote siasa ugawa watu. Hili utokea kwa kuwa siasa pasina shaka ni ulaji na mamlaka. Wahenga husema palipo na ulaji hapakosi fitina, Ila ni wajibu wetu kuonyesha ustaarabu na utu.
...

Sikubaliani na ushauri wako kwa sababu ya aya hiyo hapo. Umekiri na huo ndio ukweli.

Nimekuwa nikisisitiza kuwa Siasa katika demokrasia ya vyama vingi kwenye Nchi maskini au zinazoendelea ni dhana ya "wagawanye watawalike" (divide and rule). Upinzani si wa kupanua wigo wa Itikadi, Sera na Mikakati ya kimaendeleo ila wa wanasiasa kupata nafasi ya kuingia madarakani. Ushahidi ni kauli na matendo ya wanasiasa wa upinzani, kwa mifano ifuatayo:

1) Wamekuwa wakiitisha mikutano na wanahabari au kuandika kwenye kurasa za mitandao ya kijamii kudai Tume Huru ya Uchaguzi - nia ni kuwa na Tume itayowaweka madarakani na siyo wapiga kura.

2) Wameshindwa Uchaguzi kwenye sanduku la kura wakahamasisha "maandamano yasiyo na kikomo" wakisahau kuwa kuna makundi ya jamii wanayodai yanaonewa (kutekwa, watumishi kunyimwa nyongeza za mishahara, nk) lakini hawakuhamasisha "maandamano yasiyo na kikomo".

3) Walioshindwa kwenye sanduku la kura wanajikusanya DSM kuanzisha "maandamano yasiyo na kikomo" badala ya kwenye majimbo yao wanakodai wameibiwa kura ili wapiga kura wao wawaunge mkono, hakika nia yao ni ovu ya uvunjifu wa amani.

Je, hili kundi la wanasiasa unaotaka Serikali na vyombo vyake wakae meza moja ya majadiliano litawakilisha jamii au maslahi yao binafsi?
 
Rais akutanishwe na kibaraka wa mabeberu ili iweje? Acheni kumtafutia promo za kitoto hapa. Amekimbia, amejipanga kuichafua nchi yetu kwa kutumiwa na mabeberu wanotaka kuja kuchuma. Hana uzalendo wowote kwa nchi yetu. Yeye aishi huko huko, hatumhitaji.
Tutaijenga upya chadema aliyoibomoa. Let him go to hell
Kuna majitu mataahira kule CCM yanamjaza ujinga yule mwizi wa kura!
 
Mwambie Lissu awe na siasa za heshima, lugha nzuri.akajifunze kwa Slaa

Nje ya hapo mtaomba po sana, mtaongea lugha zote, watu washa wa ignore

Kama Lissu wazazi wake wako ubelgiji sawa

Aache kuongea shits, mpaka anakufa baadae ata loose kabisa popularity kama Mrema

Yeye ndio ajishushe
 
Rais akutanishwe na kibaraka wa mabeberu ili iweje? Acheni kumtafutia promo za kitoto hapa. Amekimbia, amejipanga kuichafua nchi yetu kwa kutumiwa na mabeberu wanotaka kuja kuchuma. Hana uzalendo wowote kwa nchi yetu. Yeye aishi huko huko, hatumhitaji.
Tutaijenga upya chadema aliyoibomoa. Let him go to hell
linawezekana ukawa ni mmoja wa wanufaikao na mpasuko huu.............. JITAFAKARI .
 
Bila DEMOKRASIA maendeleo ya kweli hayawezi kuwepo, labda kwa kikundi kidogo cha watawala wezi, na vibaraka wao
 
Back
Top Bottom