Tunaweza kukataa na kupinga Ila dalili zote ziko bayana Taifa limemegeka kisiasa, kihisia, kimitazamo, na kivitendo.
Kuna roho ya ubinafsi na majivuno inazidi kusimika mizizi katika taifa hili. Kuna wanojiona ni bora na wanastahili vyote, na wengine wanajiona kuchukiwa, kutotambulika, kutokuwa na haki hata ya kuheshimiwa mitazamo yao.
Kilichotufikisha hapa hakijaanza leo wala jana. Tunachokishuudia ni matokeo ya roho iliyopaliliwa na kunyeshewa maji kwa muda Sasa. Na kadri tunavyochelewa kuchukua hatua hali itakua mbaya Sana.
Siasa zetu zimekua chanzo Cha utengano huu. Sio kwetu tu siasa imekua chanzo Cha anguko la umoja wa kitaifa bali duniani kote siasa ugawa watu. Hili utokea kwa kuwa siasa pasina shaka ni ulaji na mamlaka. Wahenga husema palipo na ulaji hapakosi fitina, Ila ni wajibu wetu kuonyesha ustaarabu na utu.
Wazee wako kimya, watumishi wa Mungu tayari wamekubali ku take side na kuendeleza mpasuko huu. Wasomi wamekubali kubaki neutral. Wengine wamechagua kuwa kimyaa kabisaa ili kuzipa amani fake familia zao na kujihakikishia mkate mezani. Kifupi njaa na uchu wa madaraka umefubaza kalamu zao na kuamua kuisariti Taifa hili.
Nani anaweza kututoa kwenye janga hili?
Bila kupepesa macho JPM na LISSU wanaweza kulisahidia Taifa hili.
JPM- unazo nyenzo, unawajibika kikatiba, unawajibika kisiasa, na unawajibika kiimani kuongoza juhudi za kulijenga taifa hili na kuziba mpasuko. Kuchukua wajibu huu sio udhaifu na kujishusha Ila ni kuonyesha njia na kuwajibika. Utakumbukwa zaidi ukilifanikisha ili kuliko kuamua kukaa kimyaa. Heri wapatanishi maana wataitwa wana wa Mungu.
LISSU- Kama mwanasiasa unawajibika kikatiba kuilinda amani ya taifa hili. Unawajibika kiimani kusamehe na kuachilia. Unawajibika kiraia kutii na kukubali kunyenyekea mamlaka. Utakumbukwa zaidi kwa kuongoza maridhiano ya kitaifa kuliko kufanikisha mashindano .
Kwa wanaowazunguka wawili hawa, mnao wajibu wa kutuliza majeraha, kuponya nafsi zao, na kusisitiza malidhiano, na sio kuwajaza sifa, hasira na viburi.
Msione kwa kuwa mnafaidika leo kwa kushabikia umwamba huu mkaona haya ndo maisha. Hakika hiyo itakua dhambi kubwa sana mbele za Mungu na Jamii ya watanzania.
Tunapenda kuona umoja na mshikamano wa taifa hili kuliko uhasama na maumivu tunayoyashuudia leo katika kona nyingi za taifa hili.
Mwisho wa waraka huu, nitoe rai kwa wanajeshi wanobeba silaha kwa jina la Tanzania kamwe mtusaidie kurejesha tumaini na heshima ya taifa hili. Tulisifiwa na mataifa mengi duniani coz jeshi letu liliheshimu uhai wa raia zake , na liliwalinda kwa adui awaye yote. Ila leo ni haibu kuona raia zetu wanauawa na wanajeshi wetu na maafisa usalama. Tafadhari mjizuie, mtangulize weledi na utu na muwalinde raia wa taifa hili bila upendeleo.
Nashusha kalamu yangu chini. Nimetimiza wajibu wangu na ninaomba record iwekwe bayana.
Heri mpatanishi maana ataitwa mwana wa Mungu.
Ainone:
1: Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. Jonh Pombe Magufuli
2: Mh. Tundu Antipas Lissu
3: Marais wastaafu
4: Wakuu wa majeshi ya Tanzania
5: Viongozi wa vyama vya siasa
6: Raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Pureman2
Umemaliza kusema tu, lakini tuna watu "conservative" kama hawa jamaa hapa👇👇👇 chini...
Lissu hapana kabisa huyo nia yake ovu ni dhahiri mbele ya macho ya kila mmoja ni bora Mbowe ana uzalendo fulani sema amepigwa pin sababu amekuwa mlezi wa vibaraka na mawakala wa shetani huku Lissu na genge lake la kina Robert Amsterdam wakina ndio vinara
Rais akutanishwe na kibaraka wa mabeberu ili iweje? Acheni kumtafutia promo za kitoto hapa. Amekimbia, amejipanga kuichafua nchi yetu kwa kutumiwa na mabeberu wanotaka kuja kuchuma. Hana uzalendo wowote kwa nchi yetu. Yeye aishi huko huko, hatumhitaji.
Tutaijenga upya CHADEMA aliyoibomoa. Let him go to hell
1. Hivi wewe Dp800 na mwenzio UmkhontoSizwe, mnaelewa hata maana ya "beberu ama ubeberu" kweli ama mmelishwa tu maneno hayo nanyi mnabugia? Kaeni vizuri na tumieni vichwa vyenu vizuri kufikiria..
2. Na hebu tuweni honest, ndugu zangu, tujaribu kuusema ukweli japo hata kwa dakika moja..
Kwamba kwa kilichotokea na kinachoendelea kutokea, ni nani kati Tundu Lissu na CHADEMA upande huu na John Pombe Magufuli, serikali yake na CCM upande huu wenye NIA OVU na nchi na wananchi wa nchi hii?
Tukiwaomba mthibitishe NIA OVU ya Tundu Lissu na CHADEMA, mimi nina hakika hamtaweza kufanya vile...!!
Lakini kama mnataka sisi tunaopinga matokeo ya uchaguzi huu wa juzi wa kuiweka serikali hii iliyopo sasa madarakani tuthibitishe NIA OVU ya watawala hawa waliopo hapo kwa nguvu ya dola kwa kutumia kivuli cha uchaguzi wa damu, tunaweza kufanya vile mchana kweupe...!!
Kwa kuanzia, hebu tazama "series" ya matukio maovu ambayo Rais Magufuli ametendea huyu ndugu Tundu Lissu tangu alipoingia madarakani 2015...
Amejaribu mpaka kutaka kuuchukua uhai wa Tundu Lissu, bahati nzuri kuwa Mungu Yehova ni mkuu sana na amemkatalia kutimiza nia yake hiyo...
Kasa kwa hilo tu, mtu yeyote anaweza kui - define NIA OVU ya Magufuli kwa urahisi na ufasaha kabisa...
Kumbukeni kuwa huyu ni Rais mwenyewe "supreme powe and authority" katika nchi na anaweza kuamuru chochote KIOVU ama KIZURI kifanyike na kikafanyika..
Ndiyo alivyofanya kwa Tundu Lissu..
On the other hand, tujiulize, hivi kosa la Tundu Lissu ni nini hasa hata astahili such harsh treatment kutoka kwa Rais wa nchi yake?
Kiukweli HAKUNA KOSA LOLOTE isipokuwa ni KUWAKOSOA WATAWALA TU baasi....!
Hii ndiyo imezaa uchaguzi mkuu 2020 wa hovyo kabisa kuwahi kutokea. Uchaguzi uliojaa wizi mtupu mwanzo mwisho kwa sababu wanaogopa kitawaliwa na mtu mwingine ili asije akaanza kuwahukumu kwa madhambi yao ya tangu mwaka 1961...!
Kama kuna makosa ya Tundu Lissu hebu yawekeni hapa tulinganishe na makosa ya John Pombe Magufuli kisha tuombe Mungu wa haki amhukumu kila mmoja...