Rais Magufuli na Libya

Rais Magufuli na Libya

Waafrika ni watu wa ajabu sana. Afrika kusini imefika hapo ilipo kwa sababu ya udikteta wa makabulu. Leo hii waafrika wenyewe wanapoamua kutumia udikteta japo kwa kipindi kifupi ili kuinyoosha nchi na mambo yaende watu wanaona wanaonewa. Tanzania ilipokuwa imefikia ilihitaji mtu mkali kidogo ili arekebishe mapungufu yaliyopo, aweke misingi mizuri ya nchi ndiyo mambo mengine yafuate. Inawezekana Magufuli ndoto yake kubwa ni kuifanya Tanzania iwe kama Libya ya Gadafi! Tumpe muda afanye anachotaka kwa sababu anadhamira ya dhati na Tanzania. Huu ukata na mambo mengine yanayojitokeza ni kwa sababu anajenga msingi wa kuiongoza Tanzania, ndio maana watu wanakua katika mgumu. Kwa kifupi tumpe muda na tumruhusu aendelee na kuishape Tanzania anayo itaka baadae mambo mengine yatafuta kiulaini tu.
Africa kusini haijawai kuongozwa kidicteta ila ni ubaguzi wa rangi
Kama mnavyojinasibu kwamba rais hawezi kutoka kasikazini
 
Wakati mwingine unaweza kuwa mtu wa aina fulani lakini ukakosa sifa kutokana na kile unachokitetea. Ngabu unahoja dhaifu, hoja ambayo huwa naifananisha na nyimbo za mipasho. Umekuwa mmoja kati ya wenye kuziba macho na kujitia upofu hata pale linapofanywa jambo lililosahihi. Umekuwa na hulka ya kujifanya unajua kila kitu lakini hutambui kuwa hujui. Mwana Africa yoyote asiyetambua kile alichokifanya GADAFI katika uhai wake na kile kinachoendelea baada ya kuondoka kwake Ni muongo na mtu wa kuogopwa

Unafki hausaidii katika kutafuta kilicho cha kweli. Mipasho kama hii haipaswi kuandikwa na wewe. lakini kwa kuwa umekuwa muimbaji wa taarab endelea kutawala jukwaa ipo siku utapata ufalme kama sio umalikia. TANZANIA NI YA KWETU
Badala ya kuonyesha mstari kwa mstari udhaifu wa hoja yangu/ zangu, unaishia kunishambulia mimi badala yake.

Wewe si tu huna hoja. Wewe ni dhaifu.

Tena dhaifu wa akili.

Miaka nenda rudi humu watu tunahubiri kuwa hoja hujibiwa kwa hoja.

Wewe hujafanya hivyo. Umejibu hoja kwa viroja!

Alamsiki.
 
Kwa kauli zako basi sisi waTz na wa Africa tunapotezewa muda na chaguzi zisizo real
Sio kwamba tunapoteza mda, vyama vingi vya upinzani havina dira. Utaona viongozi wao hawana tofauti na viongozi walioshika dola, na wao pia wanang'aninia vyeo vile vile. Vyama vinatumika kama kampuni binafsi, wanachama hawana nguvu ya kuhoji ndani ya vyama vyao vya siasa. Unategemea utapewa dola? Huo Uhuru mnaoutaka nyie uko wapi ndani ya vyama vyenu? Ukiwa muwazi utaona taswira ya vyama vya siasa vya upinzani, havina malengo ya Masafa marefu wao ni kutumia ruzuku tu.

Angalia Kenya Odinga anavyofanya, asipopendekezwa kugombea anaanzisha chama chake alafu anagombea urais. Angalia Uganda besigye ni mara ya ngapi kugombea urais, INA maana hamna mwingine ndani ya chama? Twende Zimbabwe Morgan ni mara ngapi anagombea urais, INA maana hakuna wengine? Huku kwetu kuna vyama mwenyeviti wamekua ni wa milele, wanachama hawapaswi kuhoji? Angalia leo CUF rafu zinavyofanyika, alafu upime mwenyewe. Demokrasia mnayoitaka kwenye uchaguzi mkuu huko kwenu IPO? Uhuru mnaoutaka huku uraiani huko ndani ya vyama vyenu upo?
Hakuna nchi au taasisi unayoweza kuwa huru tu bila ya kufata sheria husika. Haipo!
 
Unajua Nyani Ngabu, binadamu ni kiumbe wa tofauti sasa kwa watawala wetu kudhani kuwa wanaweza kutuweka kwenye "zoo" ni sawa na kujaribu kuonja sumu kwa kulamba.
 
Unajua Nyani Ngabu, binadamu ni kiumbe wa tofauti sasa kwa watawala wetu kudhani kuwa wanaweza kutuweka kwenye "zoo" ni sawa na kujaribu kuonja sumu kwa kulamba.
Yaani katika mataifa yote hapa duniani yeye mtukufu Ngosha Libya ndo ya kuitolea mfano?

Nchi iliyoongozwa na dikteta toka mwaka 1969 ndo nchi ya kuitolea mfano wa amani?

Mwenyewe huwa anasema alikaa huko kwa wiki mbili.

Au jamaa hajawahi kwenda nchi zingine zaidi ya Libya, Rwanda, Kenya na Uganda?

Manake tunaweza tukawa tunamlaumu bure kumbe mwenzetu hana ufunuo wa kutosha....
 
Sio kwamba tunapoteza mda, vyama vingi vya upinzani havina dira. Utaona viongozi wao hawana tofauti na viongozi walioshika dola, na wao pia wanang'aninia vyeo vile vile. Vyama vinatumika kama kampuni binafsi, wanachama hawana nguvu ya kuhoji ndani ya vyama vyao vya siasa. Unategemea utapewa dola? Huo Uhuru mnaoutaka nyie uko wapi ndani ya vyama vyenu? Ukiwa muwazi utaona taswira ya vyama vya siasa vya upinzani, havina malengo ya Masafa marefu wao ni kutumia ruzuku tu.

Angalia Kenya Odinga anavyofanya, asipopendekezwa kugombea anaanzisha chama chake alafu anagombea urais. Angalia Uganda besigye ni mara ya ngapi kugombea urais, INA maana hamna mwingine ndani ya chama? Twende Zimbabwe Morgan ni mara ngapi anagombea urais, INA maana hakuna wengine? Huku kwetu kuna vyama mwenyeviti wamekua ni wa milele, wanachama hawapaswi kuhoji? Angalia leo CUF rafu zinavyofanyika, alafu upime mwenyewe. Demokrasia mnayoitaka kwenye uchaguzi mkuu huko kwenu IPO? Uhuru mnaoutaka huku uraiani huko ndani ya vyama vyenu upo?
Hakuna nchi au taasisi unayoweza kuwa huru tu bila ya kufata sheria husika. Haipo!
Mr. Silas kwa yote haya uliohoji unataka Malaika wa mbinguni ashuke kutuwekea mfumo mzuri wa kuongozana ?! Kwanini iwe kazi ya watu wengine na siyo sisi kukaa na kujiwekea utaratibu mzuri wa kufuata kufikia kuupata huo uongozi bila mizengwe hii inayotokea Africa ?!

Pia si sahihi kung'ang'ania kutokutenda haki kwa sababu mpinzani wako ana mapungufu unayoyaona wewe ni vema wananchi wakahukumu na si system
 
Sio kwamba tunapoteza mda, vyama vingi vya upinzani havina dira. Utaona viongozi wao hawana tofauti na viongozi walioshika dola, na wao pia wanang'aninia vyeo vile vile. Vyama vinatumika kama kampuni binafsi, wanachama hawana nguvu ya kuhoji ndani ya vyama vyao vya siasa. Unategemea utapewa dola? Huo Uhuru mnaoutaka nyie uko wapi ndani ya vyama vyenu? Ukiwa muwazi utaona taswira ya vyama vya siasa vya upinzani, havina malengo ya Masafa marefu wao ni kutumia ruzuku tu.

Angalia Kenya Odinga anavyofanya, asipopendekezwa kugombea anaanzisha chama chake alafu anagombea urais. Angalia Uganda besigye ni mara ya ngapi kugombea urais, INA maana hamna mwingine ndani ya chama? Twende Zimbabwe Morgan ni mara ngapi anagombea urais, INA maana hakuna wengine? Huku kwetu kuna vyama mwenyeviti wamekua ni wa milele, wanachama hawapaswi kuhoji? Angalia leo CUF rafu zinavyofanyika, alafu upime mwenyewe. Demokrasia mnayoitaka kwenye uchaguzi mkuu huko kwenu IPO? Uhuru mnaoutaka huku uraiani huko ndani ya vyama vyenu upo?
Hakuna nchi au taasisi unayoweza kuwa huru tu bila ya kufata sheria husika. Haipo!
Kwa hiyo kusigana Katiba ndiyo kitu sahihi kwako?
 
Kifupi ni kwamba Mheshimiwa huwachukulia Muammar Ghadaffi na Saddam Hussein kama 'role models' wake. Anawasifia na kuwarejea kila anapoongelea suala la amani. Kwake amani huletwa kwa 'fimbo ya chuma'. Na kwake uhuru na amani ya nafsi si mambo ya msingi sana kama mtu anapata 'huduma muhimu'. Kifupi ni kwamba kwa mtazamo wake mtumwa ambaye 'bwana' wake anamhudumia kwa mavazi, malazi na chakula ni bora kuliko mtu huru anayehangaika kupata mkate wake wa kila siku kadiri anavyojaaliwa.
 
Mr. Silas kwa yote haya uliohoji unataka Malaika wa mbinguni ashuke kutuwekea mfumo mzuri wa kuongozana ?! Kwanini iwe kazi ya watu wengine na siyo sisi kukaa na kujiwekea utaratibu mzuri wa kufuata kufikia kuupata huo uongozi bila mizengwe hii inayotokea Africa ?!

Pia si sahihi kung'ang'ania kutokutenda haki kwa sababu mpinzani wako ana mapungufu unayoyaona wewe ni vema wananchi wakahukumu na si system
Hatuwezi kuwa na demokrasia kama taasisi za siasa hazifati demokrasia. Hii ni kwa chama vyote tawala na upinzani. Lakini vyama vya upinzani wana nafasi ya kuonesha jamii kuwa wako tofauti na chama tawala. Lakini hakuna tofauti iliyopo kati ya vyama tawala na vyama pinzani.
Hapo ndo kuna kosa, jamii ni kama ombwe.Huwezi kuwaachia waamue wenyewe, hii ni kanuni duniani kote. Ukiacha wananchi waamue hata leo diamond platinum akingombea urais atampita yule mama wa act kwa kura. Sasa shida yote ya nini, ni lazima kuwa na vigezo
 
Kwa hiyo kusigana Katiba ndiyo kitu sahihi kwako?
Katiba IPI inasiginwa?leo unaitisha maandamano ya kupinga serikali, alafu unataka huyo huyo kiongozi aliyeko madarakani awaruhusu mumpinge, inakuja kweli?
 
Mleta uzi unataka Rais magufuli atolee mfano nchi gani zaidi ya Libya hapa afrika? Libya ni mfano mzuri wa nchi ya kiafrika iliyo tumia rasilimali zake bila misaada kunyanyua maisha ya wananchi wake

Kuna mfano bora kama huo hapa afrika? Mi siuoni
Botswana
 
Tunampenda rais magufuli,nyinyi mshazoea wizi ndio maana hamumpendi
Aaaaah wapi ...hii inakula kote !! Sasa maisha mbona magumu sana kuliko kipind cha nyuma. acha zako wewe huyo magufuli nani yako mbona ubamtetea anapokosea
 
Katiba IPI inasiginwa?leo unaitisha maandamano ya kupinga serikali, alafu unataka huyo huyo kiongozi aliyeko madarakani awaruhusu mumpinge, inakuja kweli?
Ukitaka kuongoza vizuri ukubali kukusolewa pale kwenye marekibisho yafanyike zote tutafika. Kupewa uongozi si maana yake unajua sana kuliko wengine.
 
Ukitaka kuongoza vizuri ukubali kukusolewa pale kwenye marekibisho yafanyike zote tutafika. Kupewa uongozi si maana yake unajua sana kuliko wengine.
Kukosoa sio kwa kuweka watu barabarani. Alafu unaishinikiza serikali ikae kwa makubaliano?hakuna serikali ya hivyo
 
Sio kwamba tunapoteza mda, vyama vingi vya upinzani havina dira. Utaona viongozi wao hawana tofauti na viongozi walioshika dola, na wao pia wanang'aninia vyeo vile vile. Vyama vinatumika kama kampuni binafsi, wanachama hawana nguvu ya kuhoji ndani ya vyama vyao vya siasa. Unategemea utapewa dola? Huo Uhuru mnaoutaka nyie uko wapi ndani ya vyama vyenu? Ukiwa muwazi utaona taswira ya vyama vya siasa vya upinzani, havina malengo ya Masafa marefu wao ni kutumia ruzuku tu.

Angalia Kenya Odinga anavyofanya, asipopendekezwa kugombea anaanzisha chama chake alafu anagombea urais. Angalia Uganda besigye ni mara ya ngapi kugombea urais, INA maana hamna mwingine ndani ya chama? Twende Zimbabwe Morgan ni mara ngapi anagombea urais, INA maana hakuna wengine? Huku kwetu kuna vyama mwenyeviti wamekua ni wa milele, wanachama hawapaswi kuhoji? Angalia leo CUF rafu zinavyofanyika, alafu upime mwenyewe. Demokrasia mnayoitaka kwenye uchaguzi mkuu huko kwenu IPO? Uhuru mnaoutaka huku uraiani huko ndani ya vyama vyenu upo?
Hakuna nchi au taasisi unayoweza kuwa huru tu bila ya kufata sheria husika. Haipo!

Tatizo sio vyama vingi (oppositions), tatizo kubwa ni vyama tawala.

Kwa mfano angalia Zambia ambapo Dr. Kaunda alikubali kwa moyo mkunjufu mfumo wa vyama vingi, na katika uchaguzi wa Zambia 1991 laiti kama Serikali ya Dr. Kaunda au chama chake cha UNIP vingekuwa kama CCM ilivyo na serikali yake basi Kaunda asingeshindwa na Chiluba.

Lazima pawepo na Tume Huru ya Uchaguzi + Sheria za Uchaguzi kama moja ya mambo ya msingi sana katika kuwa na chaguzi huru na zenye tija kwa nchi zetu. Lakini kwa nchi nyingi za Afrika, mfumo wa saiasa ya vyama vingi ni kama vile tulilazimishwa.

Je unakumbuka maoni ya Tume ya Jaji Nyalali kuelekea mwaka 1991-92? Ni mangapi ya msingi yaliyotekelezwa na watawala wetu? Ni kama vile tuliogopa/tunaogopa Wazungu zaidi ndio maana tuna hii mifumo lakini ki-uhalisia hakuna utayari upande wa watawala wetu. Na kwa bahati mawazo yako na ya watawala wengi yanafanana i.e. kutoheshimu au kupalilia demokrasia na uhuru wa kweli kwa kuona kuwa oppositions hawana jipya wala nafasi ya kuleta maendeleo au fikra mpya.

Hivyo badala ya kulaumu jumla jumla ni vema kuchunguza na kubaini chanzo cha tatizo.
 
Ni mara kadhaa sasa nimemsikia mtukufu rais Dkt.John Pombe Joseph Magufuli, akiwa anazungumzia suala la amani, akiitolea mfano nchi ya Libya kipindi cha Gadafi.

Kwamba mambo huko Libya yalikuwa safi tu. Vijana waliokuwa wanaoa walipewa hela, nyumba, na mengineyo.

Inawezekana kweli walikuwa wanapewa hivyo vitu lakini je, walikuwa wako huru kiasi gani?

Gadafi alikuwa dikteta. Tena dikteta mkubwa tu aliyeng'ang'ania madaraka kwa muda mrefu sana hadi walipomfurumsha.

Mtukufu rais Magufuli naye watu wengi wameshaanza kumwona kuwa ni dikteta. Hataki watu wafanye siasa kwenye maeneo yasiyo yao.

Tumeshaona na kusikia watu wakikamatwa na kufunguliwa mashitaka kwa makosa ya kumtukana/ kusema maneno mabaya dhidi yake.

Tumeona vyombo vya habari vikifungiwa kwa sababu zisizo na mashiko.

Sasa haya mambo ya yeye kuisifia Libya ya Gadafi mimi yananitatiza.

Nabaki najiuliza maswali tu. Ina maana yeye Magufuli alikuwa anamwona Gadafi kuwa ni kiongozi bora aliyeweza kutunza amani huko Libya hadi awe anaisifia sifia hivyo?

Kama Gadafi ndo mmoja wa viongozi ambao Magufuli anawaona kama mfano mzuri wa utunzaji wa amani, watu wakimwona na yeye dikteta watakuwa wanakosea kweli?

Ndo mambo ya ndege wafananao hayo au..?
Hatutaki rais wa kutufuga kama mifugo yake kule chato, Kwamba ukishawapa majani basi ni kuwafungia zizini. Ukipata wageni unachinja mmoja!! NO NO NO huyu hatukumchagua wa hivyo!!!
 
Tatizo sio vyama vingi (oppositions), tatizo kubwa ni vyama tawala.

Kwa mfano angalia Zambia ambapo Dr. Kaunda alikubali kwa moyo mkunjufu mfumo wa vyama vingi, na katika uchaguzi wa Zambia 1991 laiti kama Serikali ya Dr. Kaunda au chama chake cha UNIP vingekuwa kama CCM ilivyo na serikali yake basi Kaunda asingeshindwa na Chiluba.

Lazima pawepo na Tume Huru ya Uchaguzi + Sheria za Uchaguzi kama moja ya mambo ya msingi sana katika kuwa na chaguzi huru na zenye tija kwa nchi zetu.Lakini kwanchi nyingi za Afrika, mfumo wa saiasa ya vyama vingi ni kama vile tulilazimishwa.

Je unakumbuka maoni ya Tume ya Jaji Nyalali kuelekea mwaka 1991-92? Ni mangapi ya msingi yaliyotekelezwa na watawala wetu? Ni kama vile tuliogopa/tunaogopa Wazungu zaidi ndio maana tuna hii mifumo lakini ki-uhalisia hakuna mawzo yako na ya watawala wengi yanafanana i.e. kutoheshimu au kupalilia demokrasia na uhuru wa kweli.

Hivyo badala ya kulaumu jumla jumla ni vema kuchunguza na kubaini chanzo cha tatizo.
Sawa mkuu vile inategemea uungwana wa viongozi!! wengine wanafikiri wakiwa maamiri jeshi ni kutawala tu kwa mkono wa chuma. Hawa wanaosema waombewe huku wakiwa na roho za visasi ni majanga tu hata ungeweka tume huru!! damu itamwagika kuliko waachie kwa sanduku la kura!!
Nimechukizwa mno na kauli zake huko pemba na ZNZ nina uhakika kuwa huyo muungwana Dr Shein analazimishwa tu dhambi lakini hayuko hivyo!!
 
Back
Top Bottom