technically
JF-Expert Member
- Jul 3, 2016
- 13,555
- 57,854
Africa kusini haijawai kuongozwa kidicteta ila ni ubaguzi wa rangiWaafrika ni watu wa ajabu sana. Afrika kusini imefika hapo ilipo kwa sababu ya udikteta wa makabulu. Leo hii waafrika wenyewe wanapoamua kutumia udikteta japo kwa kipindi kifupi ili kuinyoosha nchi na mambo yaende watu wanaona wanaonewa. Tanzania ilipokuwa imefikia ilihitaji mtu mkali kidogo ili arekebishe mapungufu yaliyopo, aweke misingi mizuri ya nchi ndiyo mambo mengine yafuate. Inawezekana Magufuli ndoto yake kubwa ni kuifanya Tanzania iwe kama Libya ya Gadafi! Tumpe muda afanye anachotaka kwa sababu anadhamira ya dhati na Tanzania. Huu ukata na mambo mengine yanayojitokeza ni kwa sababu anajenga msingi wa kuiongoza Tanzania, ndio maana watu wanakua katika mgumu. Kwa kifupi tumpe muda na tumruhusu aendelee na kuishape Tanzania anayo itaka baadae mambo mengine yatafuta kiulaini tu.
Kama mnavyojinasibu kwamba rais hawezi kutoka kasikazini