Rais Magufuli na Libya

Rais Magufuli na Libya

Gadafi hajawahi kuwa roll model ya utawala mzuri si kwa africa tu hata huko Libya kwenyewe, mambo yanayofanyika chini ya carpet kwa viongozi kama hao usipime, of course kuna watu wanafaidika na tawala kama hizo na watazisifia sana. Watu wanashindwa kuelewa kwamba aliyesababisha kutoweka kwa amani Libya ni Gadafi mwenyewe wala hakuna mtu mwingine, hata kufa alijisababishia yeye. Bila udikteta wake Gadafi angeweza kuifanya Libya ikawa nchi ya amani na utulivu daima na yeye akaishi kama Farther of the Nation hata baada ya kutoka madarakani.
 
Mi namsifu Rais magufuli kumsifia Gaddafi alivyoifanya libya.
Maisha yalikuwa shwari libya. Tupa kule propaganda za wazungu. Mwafrika yoyote mpenda nchi yake angetaman nchi yake iwe kama ilivyo kuwa libya. Full misosi japo wapo jangwani. Nyumba na huduma zingine safi sana. Maisha murua. Utake nini zaid!

Kufanikisha hilo alikuwa anawapenda watu wake na alitaka na kuwa na njia za kunyanyua hali za watu wake. Hakuwa na tamaa na ubinafsi


Huduma za afya na Elimu pia shwari zilikuwa

Wazungu wanatufundsha kuwa jamaa alikuwa mwovu. Badala yake wanaona aibu kumsifia mobutu, kipenzi chao. Naamini Zaire ingekuwa kama libya ya Gaddafi kama si hila za wazungu wakimtumia mobutu.

Maendeleo ya Libya hayajaanza zamani sana. Yameanza kipindi Gaddafi ameishika nchi ile

Naamini tuna vitu kama vya libya, na hivyo tukimpata mtu mwenye akili kama ya Gaddafi lazima tufanikiwe

Tatizo Lita kuwa watu wenye mawazo kama ya kwako. Na wabaya wetu hawatopenda maana wanapendelea watu wa kuwatumia kama mobutu
Tangu Mobutu ameondoka madarakani ni miaka 20 sasa. Wamefanya nini cha maana zaidi ya migogoro ambayo haiishi. Natarajia utaniambia machafuko Zaire yameanzishwa na Wazungu pia maana wao kila mahali wanaanzisha machafuko as if sisi waafrika hatuna akili timamu.
 
Nchi ili iweze kuendelea pasipo shaka lazima udikteta utumike ,,mfn Libya,U.S,Uk,Russia,Israel,Egypt,Cuba,Venezuela na nyingine nyingi tu,udikteta ulitumika.Hivyo basi JPM ana malengo mazuri na Nchi yake
 
Gadafi hajawahi kuwa roll model ya utawala mzuri si kwa africa tu hata huko Libya kwenyewe, mambo yanayofanyika chini ya carpet kwa viongozi kama hao usipime, of course kuna watu wanafaidika na tawala kama hizo na watazisifia sana. Watu wanashindwa kuelewa kwamba aliyesababisha kutoweka kwa amani Libya ni Gadafi mwenyewe wala hakuna mtu mwingine, hata kufa alijisababishia yeye. Bila udikteta wake Gadafi angeweza kuifanya Libya ikawa nchi ya amani na utulivu daima na yeye akaishi kama Farther of the Nation hata baada ya kutoka madarakani.
Watanzania wenzetu wanatushambulia na kutuita tusiojua as if wao ni waLibya.
 
Ila maandamano ya kusifia yanakubalika kufanyika kwa maana yanatoa pongezi na wanaoandamana si watu ila visiki. Yake maandamano ya kukosoa baadhi ya mambo si sahihi.
 
Umesema vyema sana.

Sasa maswali ya kujiuliza

1. Tanzania tunatoa Scholarship ?
2. Tanzania tunasaida Africa kulipia Matumizi ya Sattelite ?
3. Raia wa Tanzania tuna Maisha bora kuwazidi watu wengine wote barani Africa ?

Ukijbu haya Maswali utajua kuwa hatupaswi kujifananisha na Libya ya enzi za Gadafi,hatufanani nayo hata Chembe...
Bado hatujafikia huko ila Magufuli ndiyo anataka tuelekee huko
 
Marekani nchi ina uhura na ina maendeleo
Uk, France, Germany, canada huwezi kusikia radio imefungiwa kwasababu ya kumkosoa raisi au serekali lakini kuna amani na maendeleo. Sasa Mtukufu raisi ameona libya tu ndio mfano wa amani na utawala bora, na kama libya ya gadafii ilikua ina amani sana ile vita ilitoka wapi? Kama kila mtu ambae anaikosoa serekali anatupwa jela hio sio amani huo ni udikteta. Tanzania hatuna cha kujifunza kutoka kwa libya. Tuna mfumo wa utawala ambao ni bora sana kuliko libya japo magu anataka kuuharibu. Sisi tunatakiwa kuziangalia nchi kama marekani au UK ili siku moja tuwe kama wao sio libya.
 
Nchi ili iweze kuendelea pasipo shaka lazima udikteta utumike ,,mfn Libya,U.S,Uk,Russia,Israel,Egypt,Cuba,Venezuela na nyingine nyingi tu,udikteta ulitumika.Hivyo basi JPM ana malengo mazuri na Nchi yake

Cuba imeendelea?
 
% alizopata Magufuli hadi tunafika 2020 atabakiza 20% tu !!
 
Kama namwelewa Mtukufu Rais, anamlaumu Ghadafi kwa kutochukua hatua kuzima chokochoko kutoka nje. Kwamba hakuwaadhibu watu waliokuwa wamepewa ahadi za uongo. Matokeo yake aliangamia. Kwa kutumia mfano huo, hatovumilia chokochoko yoyote kutoka nje. Na anasema huko Zanzibar kuna chokochoko. Anawajua wanaofanya chokochoko na ameagiza waadhibiwe kwa kuwa wasipoadhibiwa yatampata yaliyompata Ghadafi.

Na sijui Mtukufu Rais alijuaje kuwa Libya kuna raha kwa ziara ya siku chache tu.
 
Ni mara kadhaa sasa nimemsikia mtukufu rais Dkt.John Pombe Joseph Magufuli, akiwa anazungumzia suala la amani, akiitolea mfano nchi ya Libya kipindi cha Gadafi.

Kwamba mambo huko Libya yalikuwa safi tu. Vijana waliokuwa wanaoa walipewa hela, nyumba, na mengineyo.

Inawezekana kweli walikuwa wanapewa hivyo vitu lakini je, walikuwa wako huru kiasi gani?

Gadafi alikuwa dikteta. Tena dikteta mkubwa tu aliyeng'ang'ania madaraka kwa muda mrefu sana hadi walipomfurumsha.

Mtukufu rais Magufuli naye watu wengi wameshaanza kumwona kuwa ni dikteta. Hataki watu wafanye siasa kwenye maeneo yasiyo yao.

Tumeshaona na kusikia watu wakikamatwa na kufunguliwa mashitaka kwa makosa ya kumtukana/ kusema maneno mabaya dhidi yake.

Tumeona vyombo vya habari vikifungiwa kwa sababu zisizo na mashiko.

Sasa haya mambo ya yeye kuisifia Libya ya Gadafi mimi yananitatiza.

Nabaki najiuliza maswali tu. Ina maana yeye Magufuli alikuwa anamwona Gadafi kuwa ni kiongozi bora aliyeweza kutunza amani huko Libya hadi awe anaisifia sifia hivyo?

Kama Gadafi ndo mmoja wa viongozi ambao Magufuli anawaona kama mfano mzuri wa utunzaji wa amani, watu wakimwona na yeye dikteta watakuwa wanakosea kweli?

Ndo mambo ya ndege wafananao hayo au..?
We Nyani acha uchochezi
 
Hao uliokaa nao wakakwambia hivyo leo hii kawaulize tena wanaonaje maisha kipindi cha Gadaffi na sasa?
Ni kawaida ya binadamu kuona alicho nacho sio bora akatamani asichokuwa nacho mpaka kile alichokuwa nacho kikimponyoka ndipo huona umuhimu wake.
JK si alitukanwa sana akaitwa dhaifu na wapinzani na watanzania wengi, lakini sasa wanamtamani.
Same applied to Gadaf na Magu muda wake ukiisha atasifiwa.
Ndugu yangu kesi ya libya na tanzania ni tofauti....kule serikali ya familia ya gadafi na watu hawakuridhika ...nchi ni ya watu wote.
Hapa kwetu kuna mfumo tofauti. Tuna katiba na hatuna ufalme.
Tunafanya uchaguzi anayeshinda anatuongoza ...ndo katiba yetu inavo sema .
Hatuna ugomvi na hilo na raia wote wanali elewa ...ila ccm wao hawako huko wao mawazo yao kumbe ni ya ki gadafi gadafi...kuwa uchaguzi ni geresha tu lakini tukishindwa sisi hatutoi hii nchi ni mali yetu...wamefanya zanzibar. Sasa ndo hii mifano ya gadafi inapo tolewa.
Maana yake nini ? Maana yake hata kama ikitokea watanzania wameichoka ccm ..hawaitaki tena ..basi wao waendelee tu kututawala.... na hata kwa nguvu watatutawala...sasa wao ndo watatuchafulia ..ukaidi wao ndo utatuharibia...
Hivyo hiivi vya libya mfano tumtake mtawala wetu tukimkataa tutageuka libya.
Hii sio sahihi...ni wazi ccm bara bado wana mbavu za kuendelea kuchaguliwa..lakini ushawishi unapungua. Wakishinda sawa sawa hamna tabu...tujenge nchi
Wakushundwa sawa wakae pembeni...hapo tutafika hakutakua na gadafi wala syria...tutakua ma tanzania imara yenye umoja na upendo
 
tatizo la gadafi nikukaakatika cheokwamudamrefu miyaka 40 simchezo
Hao wanaokaa miaka kumi kumi wanaleta maendeleo ya nchi na wanawajali wananchi wao? mimi nadhani tatizo si kukaa muda mrefu, muhimu ni maendeleo yapatikane na wananchi wasisote, japokuwa hao wanaotetea "demokrasia" hawalikubali hilo. Ila kama kiongozi anakaa miaka mingi halafu hakuna maendeleo, njaa tupu, elimu ni shida, mahospitali hakuna dawa nk. basi hafai na hata kama atakaa miaka kumi tu halafu hamna kitu (kama hapa kwetu wameshabadilisha maraisi mara ngapi?) basi pia huyo kiongozi hafai.
 
Sawa mkuu vile inategemea uungwana wa viongozi!! wengine wanafikiri wakiwa maamiri jeshi ni kutawala tu kwa mkono wa chuma. Hawa wanaosema waombewe huku wakiwa na roho za visasi ni majanga tu hata ungeweka tume huru!! damu itamwagika kuliko waachie kwa sanduku la kura!!
Nimechukizwa mno na kauli zake huko pemba na ZNZ nina uhakika kuwa huyo muungwana Dr Shein analazimishwa tu dhambi lakini hayuko hivyo!!
Nakubaliana nawe
 
Back
Top Bottom