Rais Magufuli na Libya

Rais Magufuli na Libya

Kinachotuponza watanzania ni kukosoa jambo bila kuchunguza uhalisia wake. Uhuru mnaoutaka nyinyi haupo dunia kote. Kila nchi ina sheria na taratibu zake ambazo huwezi kuziepuka.
Kuhusu Libya ni suala ambalo linatakiwa kufundishwa hata mashuleni ili wanaokuwa waelewe kile kilichotokea Libya kabla historia haijaanza kupotoshwa. Jamaa kweli alikuwa dikteka, dikteka ambaye aliandaliwa na Uingereza kuja kuitawala Libya kwa kufanya mapinduzi lakini ni kiongozi aliyependa watu wake. Na waliompinga aliwapoteza. Aliuwa mapandikizi kama 2000, lakini baada ya kutoka madarakani ni watu wangapi wamekufa huko Libya?
Dunia leo inashuhudia idadi ya wakimbizi wengi kuwahi kutokea tangu dunia ianze Huko Syria! Hivi vitu huwezi kuvielewa kama hujaamua kuvielewa...
Gaddafi alitoa skolashipu bure kwa wanafunzi kutoka afrika, na alisaidia afrika katika tozo ya satelaiti tunayotumia leo kwenye mitandao. Pia hiyo Libya ya Gaddafi ilikuwa na maisha bora kwa kila raia kuliko nchi zote za mashariki ya kati. Sasa shida ya Gaddafi iko wapi hapo? Aliowaua ni kawaida kwa wahaini katika nchi yoyote ile, hata Tanzania Nyerere alikuwa anawapoteza watu waliokuwa wanahatarisha usalama wa serikali yake.
Uhuru mnaotaka nyinyi haupo dunia kote! Serikali lazima isimamie sema ni kwa namna tofauti. Kuna nchi zingine hata uchaguzi hautakiwi kuwepo, sababu za kiusalama na kuepusha vurugu. Ni nafuu kiongozi yule yule aendelee kutawala ili kuepusha machafuko, hii inatokea sana nchi za uarabuni.

Umesema vyema sana.

Sasa maswali ya kujiuliza

1. Tanzania tunatoa Scholarship ?
2. Tanzania tunasaida Africa kulipia Matumizi ya Sattelite ?
3. Raia wa Tanzania tuna Maisha bora kuwazidi watu wengine wote barani Africa ?

Ukijbu haya Maswali utajua kuwa hatupaswi kujifananisha na Libya ya enzi za Gadafi,hatufanani nayo hata Chembe...
 
Ni mara kadhaa sasa nimemsikia mtukufu rais Dkt.John Pombe Joseph Magufuli, akiwa anazungumzia suala la amani, akiitolea mfano nchi ya Libya kipindi cha Gadafi.

Kwamba mambo huko Libya yalikuwa safi tu. Vijana waliokuwa wanaoa walipewa hela, nyumba, na mengineyo.

Inawezekana kweli walikuwa wanapewa hivyo vitu lakini je, walikuwa wako huru kiasi gani?

Gadafi alikuwa dikteta. Tena dikteta mkubwa tu aliyeng'ang'ania madaraka kwa muda mrefu sana hadi walipomfurumsha.

Mtukufu rais Magufuli naye watu wengi wameshaanza kumwona kuwa ni dikteta. Hataki watu wafanye siasa kwenye maeneo yasiyo yao.

Tumeshaona na kusikia watu wakikamatwa na kufunguliwa mashitaka kwa makosa ya kumtukana/ kusema maneno mabaya dhidi yake.

Tumeona vyombo vya habari vikifungiwa kwa sababu zisizo na mashiko.

Sasa haya mambo ya yeye kuisifia Libya ya Gadafi mimi yananitatiza.

Nabaki najiuliza maswali tu. Ina maana yeye Magufuli alikuwa anamwona Gadafi kuwa ni kiongozi bora aliyeweza kutunza amani huko Libya hadi awe anaisifia sifia hivyo?

Kama Gadafi ndo mmoja wa viongozi ambao Magufuli anawaona kama mfano mzuri wa utunzaji wa amani, watu wakimwona na yeye dikteta watakuwa wanakosea kweli?

Ndo mambo ya ndege wafananao hayo au..?

Kitu cha kwanza kinachoniudhi ni utumiaji wa jina la mtukufu, nafikiri sisi watanzania tuna tabia ya kutukuza watu sana. Kwani kumuita mheshimiwa haitoshi?
Halafu kumuita mta kilaza sidhani kama kuna makosa yeyote. Kilaza kwa ninavyoelewa ni mtu asiye na elimu na sidhani hilo ni tusi la kumpeleka mtu kortini.
 
!
!
watu wote huwa na busara kabla hawajazungumza kitu chochote kile. Busara huanza kupotea na mtu kuonekana wa hovyo paleee anapoanza kutokwa na povu. Poor Africans.
 
Ni mara kadhaa sasa nimemsikia mtukufu rais Dkt.John Pombe Joseph Magufuli, akiwa anazungumzia suala la amani, akiitolea mfano nchi ya Libya kipindi cha Gadafi.

Kwamba mambo huko Libya yalikuwa safi tu. Vijana waliokuwa wanaoa walipewa hela, nyumba, na mengineyo.

Inawezekana kweli walikuwa wanapewa hivyo vitu lakini je, walikuwa wako huru kiasi gani?

Gadafi alikuwa dikteta. Tena dikteta mkubwa tu aliyeng'ang'ania madaraka kwa muda mrefu sana hadi walipomfurumsha.

Mtukufu rais Magufuli naye watu wengi wameshaanza kumwona kuwa ni dikteta. Hataki watu wafanye siasa kwenye maeneo yasiyo yao.

Tumeshaona na kusikia watu wakikamatwa na kufunguliwa mashitaka kwa makosa ya kumtukana/ kusema maneno mabaya dhidi yake.

Tumeona vyombo vya habari vikifungiwa kwa sababu zisizo na mashiko.

Sasa haya mambo ya yeye kuisifia Libya ya Gadafi mimi yananitatiza.

Nabaki najiuliza maswali tu. Ina maana yeye Magufuli alikuwa anamwona Gadafi kuwa ni kiongozi bora aliyeweza kutunza amani huko Libya hadi awe anaisifia sifia hivyo?

Kama Gadafi ndo mmoja wa viongozi ambao Magufuli anawaona kama mfano mzuri wa utunzaji wa amani, watu wakimwona na yeye dikteta watakuwa wanakosea kweli?

Ndo mambo ya ndege wafananao hayo au..?
Ukituliaga unatoa vitu vyenye akili wew
 
Tukisema ni dicteta watu wanabisha kwanini utolee nchi za kidicteta mfano asipoongelea Libya ataongelea Rwanda
Rafiki kuna watu humu wanamonitor each and everything going on over here! Be careful usije pata matatizo na wa kukutetea ni wachache
 
Amekomaliaa mfano mfu wa dikteta mwenzake! Hajui diplomacy yeyote ameshikilia mfano mbovu na dhaifu kulinganis amani! Libya walikuwa wameminywa uhuru wao kwa kuzibwa mdomo na utajiri wa nchi yao! Ile haikuwa amani ulikuwa woga kwa mkono wa chuma! Walipochoka kunyimwa haki na uhuru wao hasa wa kukosoa mfalme Juha wakalianzisha
 
Binadamu sisi ni waajabu na wanafiki tusioridhika hata kidogo. Imagine bila aibu watu wanaolilia demokrasia ndio hao hao wanaogeuzana nyuma! Uhuru wanaoudai ndoo huo huo unaowapelekea hata kubadilisha matumizi ya miili yao. Kila kitu lazima kiwekewe sheria na zuio. Hauwezi kufanya chochote ukiulizwa demokrasia. Watu wa Libya watasumbuka sana tena sana. Hawana shukrani. Ss hiyo demokrasia waliyoililia ndiyo wana enjoy
Hivi ulishawahi kusikia nchi ya amani watu wake wanazuiwa kuandamana!?

Hivi kweli unafikiri maandamano yanaweza kuhatarisha amani kwenye nchi ya amani!!?
 
Autocracy
Democracy
Theocracy
Oligarchy
 
..unajua majeshi ya Gaddafi yaliua vijana wetu wa jwtz wakati wa vita vya Uganda.

..mimi nashangaa Amiri Jeshi wetu mkuu anamsifia kiongozi wa aina hiyo.

..Je amesahau? Je hajali? Au ni kukosa uelewa wa uzito wa dhamana aliyonayo?

..suala la kilichotokea Libya ni very complex. Gaddafi alifanya makosa na wapinzani wake nao walifanya makosa.

..Je, hakuna viongozi wengine wa kusifiwa zaidi ya Gaddafi aliyeuwa askari wa Tanzania?

NB:
 
Rafiki kuna watu humu wanamonitor each and everything going on over here! Be careful usije pata matatizo na wa kukutetea ni wachache
Matatizo kwa unajua Mimi nani au ni mtoto wa nani waambie waje wanitafute !!
Kwanza kwa lipi?
Kwa kosa gani baada washugulikie sukari kwa wananchi wao wao wanaangaika na Mimi !!
Waje tu mi siwaogopi!!
 
Ni mara kadhaa sasa nimemsikia mtukufu rais Dkt.John Pombe Joseph Magufuli, akiwa anazungumzia suala la amani, akiitolea mfano nchi ya Libya kipindi cha Gadafi.

Kwamba mambo huko Libya yalikuwa safi tu. Vijana waliokuwa wanaoa walipewa hela, nyumba, na mengineyo.

Inawezekana kweli walikuwa wanapewa hivyo vitu lakini je, walikuwa wako huru kiasi gani?

Gadafi alikuwa dikteta. Tena dikteta mkubwa tu aliyeng'ang'ania madaraka kwa muda mrefu sana hadi walipomfurumsha.

Mtukufu rais Magufuli naye watu wengi wameshaanza kumwona kuwa ni dikteta. Hataki watu wafanye siasa kwenye maeneo yasiyo yao.

Tumeshaona na kusikia watu wakikamatwa na kufunguliwa mashitaka kwa makosa ya kumtukana/ kusema maneno mabaya dhidi yake.

Tumeona vyombo vya habari vikifungiwa kwa sababu zisizo na mashiko.

Sasa haya mambo ya yeye kuisifia Libya ya Gadafi mimi yananitatiza.

Nabaki najiuliza maswali tu. Ina maana yeye Magufuli alikuwa anamwona Gadafi kuwa ni kiongozi bora aliyeweza kutunza amani huko Libya hadi awe anaisifia sifia hivyo?

Kama Gadafi ndo mmoja wa viongozi ambao Magufuli anawaona kama mfano mzuri wa utunzaji wa amani, watu wakimwona na yeye dikteta watakuwa wanakosea kweli?

Ndo mambo ya ndege wafananao hayo au..?
Yaani wewe nyani, hata sijui nisemeje, yaani umezungumza pumba tu. Hujaelezea udikteta wa gadafi sawa sawa, Toa ufafanuzi kamili kwa nini gadafi alikuwa dikteta? au kwa kuwa ulisikia tu ma wester walikuwa wakimuita hivyo basi na wewe kumba kumba unachukulia hivyo hivyo? sasa eleza hapa halafu tukupe shule kamili.
 
Kawaulize wananchi wa libya leo hii kati ya Gadafi na sasa kipi kizuri
 
Swali la kujiuliza tulifikaje hapa, yote haya yanaletwa na tabia za wanasiasa wasaka sifa, kutukana viongozi bungeni, kwenye mitandao, kwenye mikutano na magazetini.

La kushangaza viongozi waliothubutu kuwafunga na kuwapoteza wawatukanao au wanaowajaribu kama Nyerere na mkapa walikuwa wanaogopwa na kuheshimiwa. Waliokuwa wavumilivu na wasikilizi kama Mwinyi na Kikwete walitukanwa na kubezwa hata wafanyapo mazuri. Msukuma naye hataki kubezwa period.
 
Tangia huyu mzee wa Iraq aingie madarakani sioni kilichobadilika. Hospitali zimeendelea kukosa madawa, amesabisha uhaba wa baadhi ya mahitaji ya kijamii kama sukari, mzunguko wa fedha umekuwa finyu na hivyo kusababisha hali ngumu kwa wananchi, kukosekana kwa ajira, kupungua kwa maslahi kwa watumishi wa umma kutokana na kutopewa nyongeza ya mishahara na kutopandishwa madaraja, wananchi kurundikiwa mzigo wa kodi kwa mfano VAT kwenye miamala ya kibenki na miamala kwenye kampuni za mitandao ya simu, kuwagawa wananchi kwa kauli za kichochezi na zinazoudhi n.k, n.k.
 
Back
Top Bottom