Rais Magufuli na Libya

Rais Magufuli na Libya

Gaddafi's Last Speech!!! .

In the name of Allah, the ...beneficent, the merciful...
For 40 years, or was it longer, I can't remember, I did all I could to give people houses, hospitals, schools, and when they were hungry, I gave them food. I even made Benghazi into farmland from the desert, I stood up to attacks from that cowboy Ronald Reagan, when he killed my adopted orphaned daughter, he was trying to kill me, instead he killed that poor innocent child. Then I helped my brothers and sisters from Africa with money for the African Union.
I did all I could to help people Understand the concept of real democracy, where people's committees ran our country. But that was never enough, as some told me, even people who had 10 room homes, new suits and furniture, were never satisfied, as selfish as they were they wanted more. They told Americans and other visitors, that they needed "democracy" and "freedom" never realizing it was a cut throat system, where the biggest dog eats the rest, but they were enchanted with those words, never realizing that in America, there was no free medicine, no free hospitals, no free housing, no free education and no free food, except when people had to beg or go to long lines to get soup.
No, no matter what I did, it was never enough for some, but for others, they knew I was the son of Gamal Abdel Nasser, the only true Arab and Muslim leader we've had since Salah-al-Deen, when he claimed the Suez Canal for his people, as I claimed Libya, for my people, it was his footsteps I tried to follow, to keep my people free from colonial domination - from thieves who would steal from us.
Now, I am under attack by the biggest force in military history, my little African son, Obama wants to kill me, to take away the freedom of our country, to take away our free housing, our free medicine, our free education, our free food, and replace it with American style thievery, called "capitalism" ,but all of us in the Third World know what that means, it means corporations run the countries, run the world, and the people suffer.
So, there is no alternative for me, I must make my stand, and if Allah wishes, I shall die by following His path, the path that has made our country rich with farmland, with food and health, and even allowed us to help our African and Arab brothers and sisters.
I do not wish to die, but if it comes to that, to save this land, my people, all the thousands who are all my children, then so be it.
Let this testament be my voice to the world, that I stood up to crusader attacks of NATO, stood up to cruelty, stoop up to betrayal, stood up to the West and its colonialist ambitions, and that I stood with my African brothers, my true Arab and Muslim brothers, as a beacon of light.
When others were building castles, I lived in a modest house, and in a tent. I never forgot my youth in Sirte, I did not spend our national treasury foolishly, and like Salah-al-Deen, our great Muslim leader, who rescued Jerusalem for Islam, I took little for myself...
In the West, some have called me "mad", "crazy", but they know the truth yet continue to lie, they know that our land is independent and free, not in the colonial grip, that my vision, my path, is, and has been clear and for my people and that I will fight to my last breath to keep us free, may Allah almighty help us to remain faithful and free.
Too touchy, brave and courageful nashangaa sana wajinga wanaompinga huyu jamaa
 
Sasa hivi Tanzania mtu kioa hapewi nyumba wala gari wala Pesa yoyote ya kuanzia Maisha kama alivyokuwa anafanya Gadafi.
Sasa Tanzania kuifananisha na Libya ya enzi za Gadafi sio sahihi
Wamesema bado hajamaliza mwaka tusuburiii
 
Labda Watanzania tumesahau jinsi Gadaffi alivyoungana na Idd Amin kuivamia Tanzania. Kuna Watanzania walipoteza maisha yao kwenye ile vita!!
Sisi tunaangalia alivyotumia rasilimali za nchi yake na ubunifu kuwasaidia watu wake hayo mengine unajua wewe
 
N
Ni mara kadhaa sasa nimemsikia mtukufu rais Dkt.John Pombe Joseph Magufuli, akiwa anazungumzia suala la amani, akiitolea mfano nchi ya Libya kipindi cha Gadafi.

Kwamba mambo huko Libya yalikuwa safi tu. Vijana waliokuwa wanaoa walipewa hela, nyumba, na mengineyo.

Inawezekana kweli walikuwa wanapewa hivyo vitu lakini je, walikuwa wako huru kiasi gani?

Gadafi alikuwa dikteta. Tena dikteta mkubwa tu aliyeng'ang'ania madaraka kwa muda mrefu sana hadi walipomfurumsha.

Mtukufu rais Magufuli naye watu wengi wameshaanza kumwona kuwa ni dikteta. Hataki watu wafanye siasa kwenye maeneo yasiyo yao.

Tumeshaona na kusikia watu wakikamatwa na kufunguliwa mashitaka kwa makosa ya kumtukana/ kusema maneno mabaya dhidi yake.

Tumeona vyombo vya habari vikifungiwa kwa sababu zisizo na mashiko.

Sasa haya mambo ya yeye kuisifia Libya ya Gadafi mimi yananitatiza.

Nabaki najiuliza maswali tu. Ina maana yeye Magufuli alikuwa anamwona Gadafi kuwa ni kiongozi bora aliyeweza kutunza amani huko Libya hadi awe anaisifia sifia hivyo?

Kama Gadafi ndo mmoja wa viongozi ambao Magufuli anawaona kama mfano mzuri wa utunzaji wa amani, watu wakimwona na yeye dikteta watakuwa wanakosea kweli?

Ndo mambo ya ndege wafananao hayo au..?

Nyani ngabu kweli wewe ni nyani fikiria maisha chini ya gadafi libya yalikuaje fananisha na ss hivi, uhuru unakusaidia katika nchi ambayo ukioa unapewa.na mtaji
 
siwezi kujibu kuegemea alipo mtoa bandiko kwa kuwa hata yeye ameonyesha wapi upande alipo.
mkuu kuna mada aliyo ianzisha huyu huyu aliye anzisha mada hii inasema "nani atawaamini tena chadema" tambua upande wake pia.
 
Sasa kama mtu Role model wake ni Kagame unategemea na yeye atakuwaje?
Moja wapo ya alama ya udiketa ni matamshi ya vitisho kama haya "mtu akikuchezea niambie, haitachukua hata dakika 5"

Huyu ilashaonekana toka anagombea kwake msamiati Demokrasia haupo na haamini kama upo.

Kama vipi simama upinge basi kamanda?
 
Nimesoma hoja zako hapa na nimekuelewa...Lakini ni wazi kuwa kuna issues nyingine inabidi ujiongeze zaidi...Kwa mfano katika masuala ya uhuru wa watu na suala la kuvifungia vyombo vya habari kwa kutaja machache tu....

Anayozungumza JPM kuhusu Libya ni kweli tupu...binafsi nilibahatika kufika Libya wakati wa Gadhafi na nikakaa Tripoli na maeneo mengine machache kwa karibu wiki mbili hivi...Ni siku chache kuweza kuifahamu nchi, lakini ni wazi Libya wakati wa Ghadafi ilikuwa ni 'heaven' ukilinganisha na hali ya sasa....Ni kweli Libya wakati wa Ghadafi walikuwa wanakosa mambo mengi ya anasa kwa vigezo vya nchi za magharibi...kama pombe, vyombo huru vya habari kwa, na yale mambo mengine ya anasa ambayo siwezi kuyaweka hapa...Lakini Libya wakati huo walikuwa na karibu kila kitu kwa bidhaa madukani..vyakula, nguo za bei rahisi kutoka Italy, Spain, Turkey na kadhalika...Kulikuwa hakuna tatizo la ajira..maji na umeme karibu ni wa bure na wanaume kulipiwa mahali wakati wa kuoa...

Ni kweli walikuwa hawana uhuru kwa maana ya kukosoa uongozi...sikuona pia uhuru katika masuala ya internet...hakukuwa na madawa ya kulevya...vyombo vya habari vilikuwa controlled na kadhalika...

Wamarekani na nchi za magharibi hawakupenda ustawi wa Libya...na pale Ghadafi alipojaribu kupendekeza kuwa dhahabu ndiyo itumike kwenye biashara ya mafuta, ndipo walipokula njama za kumuodoa....

Sijafika Libya ya sasa lakini kwa kupitia vyombo vya habari ni wazi Walibya wanajuta...hakuna serikali pale..Kule Benghazi nadhani wana serikali yao...kuna makundi mengi yenye silaha yenye itikadi tofauti na yanapambana yenyewe kwa wenyewe...mafuta yanachotwa ovyo na mabepari wa nchi za magharibi...

Ndiyo maana walibya wengi wanajuta kwa kuona kuwa walihadaiwa.....Pengine ni vema tujiulize hivi tunapodai uhuru tunamanisha nini???? Libya sasa wana uhuru wa kutukana viongozi, kuchukua silaha na kupigana na kuuana wao kwa wao...Yaani kilichoko Libya sasa ni vurugu...Je, sisi Tanzania ndio uhuru tunaoutaka??? Yaani tunataka uhuru wa kutotii mamlaka??? Tunataka uhuru wa ghasia???? Je, sisi watanzania tunataka hayo??? Uhuru ni jambo jema lakini uhuru pasipo wajibu ni vurugu....

Vyombo vya habari vina nafasi ya kujenga mshikamano na kukemea maovu, lakini vyombo hivyo vikianza kutumika katika kuhakikisha kuwa amani na usalama wa nchi unapotea ni lazima vyombo hivyo vya habari 'vishughulikiwe' kwa mujibu wa taratibu, kanuni na sheria za nchi yetu.....
mkuu Hata Rais akifungia vyombo vyote vya habari...kubana Uhuru wa kuongea Tanzania haiwezi kuwa kama Libya enzi za Gadafi..... Serikali imeshindwa kunyanyua uchumi...sukari bei juu...biashara zimedoda..ajira hakuna sasa wanachofanya ni kuwatisha wananchi kwa kigezo cha amani ili waendelee kuwatawala....Hao wanaosema wanataka kuvuruga amani hawana hata fimbo
 
N


Nyani ngabu kweli wewe ni nyani fikiria maisha chini ya gadafi libya yalikuaje fananisha na ss hivi, uhuru unakusaidia katika nchi ambayo ukioa unapewa.na mtaji
Tanzania sasa hivi tuna amani mbona sasa hatifanani na libya chini ya Gadafi? Usifananishe Tanzania na Libya ni nchi mbili tofauti sana amani yetu haijatusaidia kitu chochote
 
Mi namsifu Rais magufuli kumsifia Gaddafi alivyoifanya libya.
Maisha yalikuwa shwari libya. Tupa kule propaganda za wazungu. Mwafrika yoyote mpenda nchi yake angetaman nchi yake iwe kama ilivyo kuwa libya. Full misosi japo wapo jangwani. Nyumba na huduma zingine safi sana. Maisha murua. Utake nini zaid!

Kufanikisha hilo alikuwa anawapenda watu wake na alitaka na kuwa na njia za kunyanyua hali za watu wake. Hakuwa na tamaa na ubinafsi


Huduma za afya na Elimu pia shwari zilikuwa

Wazungu wanatufundsha kuwa jamaa alikuwa mwovu. Badala yake wanaona aibu kumsifia mobutu, kipenzi chao. Naamini Zaire ingekuwa kama libya ya Gaddafi kama si hila za wazungu wakimtumia mobutu.

Maendeleo ya Libya hayajaanza zamani sana. Yameanza kipindi Gaddafi ameishika nchi ile

Naamini tuna vitu kama vya libya, na hivyo tukimpata mtu mwenye akili kama ya Gaddafi lazima tufanikiwe

Tatizo Lita kuwa watu wenye mawazo kama ya kwako. Na wabaya wetu hawatopenda maana wanapendelea watu wa kuwatumia kama mobutu

kwa hiyo wewe utakula udikteta?
So far 'hayo mabadiliko' yamembadilishia nini mwananchi?
Elimu bora iko wapi? na hizo dawa hospitalini ziko wapi mbona hata ukienda na watoto wadogo wanaotakiwa kutibiwa bure dawa zinazopatikana hospitalini ni zile za bei rahisi tu, na zile ghali wanasema hawana inabidi ukanunue nje?
Sikia, uwe na akili timamu. Hatuongelei uhuru wa bendera hapa. kama ni hivyo, wewe unadhani nchi za Afrika zilipata uhuru huo mapema kuliko za Ulaya na Amerika? Au unataka kusema kwamba Tanzania, Kenya, Uganda, Zambia, Ghana, etc "zilipata uhuru" kabla ya Marekani, Uingereza, Ujerumani, Norway, Uholanzi, Canada, etc?
 
Kama watanzania miaka 50 baada ya uhuru bado tuna watu wanafikiri kupatwa kwa jua kumeletwa na mtu huoni kuwa tuko karne nyingi nyuma?
Hivyo watu kuelewa kuwa uhuru wa kutoa mawazo yako una faida nyingi za kimaendeleo itachukua miaka mingi.
Hivyo watawala wetu wanatumia ujinga wa watu wao kwa jusema kuwa kutoa mawazo tofauti ni uvunjivu wa amani. Kwamba mkuu anaweza kujenga amani nchini kwa kutumia mtutu wa bunduki. Ka mikakati ya bunduki haikusaidia Libya, Iraq, Syria na pengine ni kwa nini yeye anataka
kulazimisha?
 
mkuu kuna mada aliyo ianzisha huyu huyu aliye anzisha mada hii inasema "nani atawaamini tena chadema" tambua upande wake pia.
hata hapo mwanzo alikuwa mmoja kati ya waliunga mkono ule mkakati wa kuidai demokrasia. Lakini kwangu mimi huwa naisemea Tanzania, sisemei chama chochote cha SIASA.

Huyu mwandishi ni mmoja kati ya wanaopinga hata kile kizuri kinachofanywa na SERIKALI. na hilo bandiko kuhusu chadema ni aibu baada yq kuona kile alichokuwa akikipigania kushindikana
 
Ndo wazungu wanavyo wadanganya? Tafuteni habari kupitia vyanzo vingi

Majuzi Obama amesema kuwa katika jambo analolijutia zaidi ni kuiingiza marekani kuibomoa libya bila kuwa na mpango thabiti wa jinsi ya kuirejesha nchi hiyo katika hali ya kawaida, ya kutawalika

Nchi zingine za kiafrika zina mengi mazuri ya kujifunza kutoka libya na Gaddafi wake. Na ya msingi ni haya - kutumia rasilimali zilizopo kuiendeleza nchi, kuacha kubabaikia mataifa ya nje, kuacha uroho wa mali na ubinafsi

Mengine mengi ni ngonjera tu, tena za kupotezeana muda.


Gadafi alikuwa ni dikteta wa kutisha.Watu kuuwawa katika mazingira ya kutatanisha ilikuwa ni kawaida mnoo wakati wa Gadaffi.Ukiwa mpinzani wa Gadaffi ata ukiwa nje ya Libya alikuwa anakutumia majasusi wakumalize.Rejea "Lockerbie bombing" ya mwaka 1988 ambapo Gadaffi alitumia majasusi wake kulipua ndege iliyouwa watu takribani 270 na wengine 10 waliongukiwa na ndege hiyo pale Lockerbie, Scotaland.
Gadafi alikuwa ana bahati Libya ina utajiri mkubwa wa mafuta.Ndio maana aliweza kutoa huduma nyingi za kijamii bure.

Libya ingekuwa na utawala wa kidemokrasia tangu enzi za Gadaffi ingekuwa ni nchi tajiri kuzidi Morocco na Algeria.

Siku zote unapomg'oa dikteta unaacha ombwe la uongozi kwa maana uongozi wote unakuwa umeteuliwa na mtu mmoja na sio na wananchi.Ombwe la uongozi lilitokea pia Uganga baada ya kung'olewa Iddi Amini mpaka alipokuja kupatikana Museveni.Pia Iraq imekumbwa na ombwe la uongozi baada ya kung'olewa Dikteta Sadam Hussein.
 

Nawewe nawe! Una shangaa mtu kutokujua kuhusu hilo? Wew unafikiri hajui kila kitu? Wew unajua kila kitu?

Unaongeleaje kudhoofishwa kwa libya, Syria na Iraq katika mtizamo wa kuifananisha na Tanzania? Libya na Syria iraq zilikuwa na tifutifu na wazungu, kimaslahi zaidi wakati Tanzania hamna kitu kama hicho

Eti bunduki, kuna mtu amepigwa shaba hapa? Au kiongozi wa upinzan kubanwa alipe kodi unafananisha Na mtu kupigwa risasi?

Kama watanzania miaka 50 baada ya uhuru bado tuna watu wanafikiri kupatwa kwa jua kumeletwa na mtu huoni kuwa tuko karne nyingi nyuma?
Hivyo watu kuelewa kuwa uhuru wa kutoa mawazo yako una faida nyingi za kimaendeleo itachukua miaka mingi.
Hivyo watawala wetu wanatumia ujinga wa watu wao kwa jusema kuwa kutoa mawazo tofauti ni uvunjivu wa amani. Kwamba mkuu anaweza kujenga amani nchini kwa kutumia mtutu wa bunduki. Ka mikakati ya bunduki haikusaidia Libya, Iraq, Syria na pengine ni kwa nini yeye anataka
kulazimisha?
 
Anatumia Libya km kigezo cha kuendelea kubana demokrasia

Hakika magufuli ataaibika vibaya, siku zaja
 
Kuhusu kutolewa mfano Gadaffi, hata mm siliungi mkono...!!

Pia kusema nipe taarifa anayesumbua hatachukua dak. 5 siungi mkono..!!

Haya maneno sio mazuri sana Mh. Rais kutoa..
 
hata hapo mwanzo alikuwa mmoja kati ya waliunga mkono ule mkakati wa kuidai demokrasia. Lakini kwangu mimi huwa naisemea Tanzania, sisemei chama chochote cha SIASA.

Huyu mwandishi ni mmoja kati ya wanaopinga hata kile kizuri kinachofanywa na SERIKALI. na hilo bandiko kuhusu chadema ni aibu baada yq kuona kile alichokuwa akikipigania kushindikana
ok, yawezekana chadema wamefeli kama baadhi wanavyo amini, lakini mi naona madai yao yataendelea kuishi kama selekali haitajirekebisha.
 
Wakati mwingine unaweza kuwa mtu wa aina fulani lakini ukakosa sifa kutokana na kile unachokitetea. Ngabu unahoja dhaifu, hoja ambayo huwa naifananisha na nyimbo za mipasho. Umekuwa mmoja kati ya wenye kuziba macho na kujitia upofu hata pale linapofanywa jambo lililosahihi. Umekuwa na hulka ya kujifanya unajua kila kitu lakini hutambui kuwa hujui. Mwana Africa yoyote asiyetambua kile alichokifanya GADAFI katika uhai wake na kile kinachoendelea baada ya kuondoka kwake Ni muongo na mtu wa kuogopwa

Unafki hausaidii katika kutafuta kilicho cha kweli. Mipasho kama hii haipaswi kuandikwa na wewe. lakini kwa kuwa umekuwa muimbaji wa taarab endelea kutawala jukwaa ipo siku utapata ufalme kama sio umalikia. TANZANIA NI YA KWETU
bora umemchana asee mm mwenyewe nlkua nafkiria maneno ya kumwambia kama hayo big up kiongozi....
 
Back
Top Bottom