Pulchra Animo
JF-Expert Member
- Jun 16, 2016
- 3,398
- 2,990
Kitendo cha Mh Rais kutamka hadharani kuwa mtu yeyote aliyemzidi umri asijidanganye kuomba nafasi hiyo ni kwenda kinyume kabisa na katiba ya Nchi.
Hakuna sehemu katika katiba ya Nchi yetu inayomkataza mtu yeyote kugombea nafasi ya Urais kwa kigezo cha umri mkubwa.
Washauri wa Rais jaribuni kumshauri Bwana Mkubwa kuna kauli akizisema ninaleta mtafaruku mkubwa sana katika jamii.
Unwritten rules zina nguvu kubwa kuliko unavyofikiria! Hapo JPM amekumegea tu kipande cha portfolio ya unwritten rules.
Kumnyima mtu form ya kugombea kwa sababu ya kuwa na umri mkubwa kuliko wa Rais anayemaliza muda wake ndiyo kinyume cha Katiba. Hakika CCM hawatafanya hivyo. Anayetaka kuchukua form ruksa, lakini kama CCM wakiamua wazee wasipenye, kweli wazee hawatapenya.
Kumbuka, kura ya mjumbe wa kikao cha maamuzi au kura ya mwananchi katika uchaguzi huwa haina maelezo. Mtu anaweza kumnyima kura mgombea kwa sababu ambazo ni kinyume kabisa cha Katiba (kama vile dini yake, kabila lake, rangi yake, jinsia yake), lakini ndiyo imetoka hiyo; hakuna mahakama inayoweza kuhoji utashi wa mpigakura!