Mkuu nipo Nje ya NchiMkuu una Milioni 7
Saafi sana Rais kipenzi cha Watanzania.
Muda mwingine walau uwe unaanza kujihoji kabla ya kupost hata swali moja tu kuwa "hivi muda huu ni saa ngapi?"Watanzania wapo karibu milioni 50,kumwita aliyechaguliwa na watu milioni 8 kuwa ni kipenzi cha Watanzania nayo yaweza kuwa "ishara ya msalaba" yenye kuashiria mwanzo wa Sala za "Ritania ya watakatifu".Endelea kumsifu na kumwabudu ana uwezo wa kutengua uteuzi wa yeyote akakupa nafasi wewe.
Ndo sheria inavyosema hivyo...angeenda kinyume mngemuita diktetaWana haki ya kuwaweka watu mahabusu,hapa rais simuungi mkono
ubunge wa viti maalum nimatumizi mazuri ya hela?Vyeo vingine ni matumizi mabaya tu ya hela za kulipa mishahara.
Mtanzania yupi unayemzungumzia?Yule anaenunua sukari elf 4?Saafi sana Rais kipenzi cha Watanzania.
Kama rais anasema kuteua ma-DC haikuwa kazi rahisi halafu anamteua ABDALLAH NJWAYO kuwa DC. Nipoteza imani na JPM kaisa. CCM ni ile ileLeo Tarehe 29 Rais Magufuli anawapisha wakuu wa mikoa na wilaya asubuhi hii live from Azam two na TBC1.
Rais Magufuli: Gondwe ninajua unatangaza,sasa utakwenda kutangaza maendeleo unakokwenda,ufanye kama unatangaza tangaza tu.
Rais Magufuli: Mchakato wa kuwapata Ma-DC haukuwa rahisi, ilibidi tutizame historia ya kila mmoja wao.
Rais Magufuli: Kuna mabadiliko madogo tuliyoyafanya kutokana na jina lilikosewa, kwa hiyo aliyestahili tumeshamuweka.
Rais Magufuli: Ningeweza nikataja majina yote mliopo hapa mpaka yule aliyepigwa fimbo na mtani wangu, karibu kila jina nalifahamu na sifa yake.
Rais Magufuli: Mna mamlaka makubwa ya kumuweka mtu Mahabusu ila msiende tu kuonea watu.
Rais Magufuli: Mnaweza kufikiri tumewachagua sisi lakini inawezekana Mungu ametutumia sisi kuwachagua ninyi.
Rais Magufuli: Nilikuwa namuona DC wa Iringa anabeba watoto wakamsema sana, na mimi nikasema abaki hapa hapa
Rais Magufuli: Nilitegemea sana baada ya kuwateua, nilitegemea labda mngekuja robo tu, ninawashukuru sana kwa kuja.
Rais Magufuli: Watanzania wengi tumezoea kulalamika, tunapenda tu kupewa, hatutaki kufanya kazi.
Rais Magufuli: Ni matumaini yangu hamtaniangusha, hata sura zenu zinaonyesha ni wachapa kazi, nendeni mkachape kazi.
Rais Magufuli: Nyinyi wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya mna mamlaka hata ya kuweka watu mahabusu, ila msiende kuonea watu.
Rais Magufuli: Mkasimamie yale tuliyowaahidi sisi wana CCM, mkayatekeleze kwa nguvu zote
Rais Magufuli: Watanzania wengi wana changamoto nyingi, nina imani hamtaiangusha serikali hii.
Rais Magufuli: Nataka niseme ukweli, wale ma-DC tuliowaacha hawakufikia vigezo
Mchakato wa kuwapata ma-DC ulikuwa mgumu, ilibidi tuangalie historia ya kila mmoja, tuliangalia mambo mengi sana.
Rais Magufuli anazungumza kwenye sherehe za kuwaapisha kiapo cha uadilifu wakuu wa wilaya na wakuu wa mikoa wapya.
Na uwe ni mil 7Naogopa kusema neno, kesho nikaamkia mahabusu...!
ubunge wa viti maalum nimatumizi mazuri ya hela?
ukawa waonyeshe mfano kuugomeaNao matumizi mabaya tu.
Mkuu tangu lini umepewa Cheo cha kuwa msemaji wa watanzania wote?Saafi sana Rais kipenzi cha Watanzania.
Rais kishadema mtani wewe inachukulia seriousDuh kumbe ukipigwa na mtani wa rais unapata udc!
Tunaanza kukushambulia wewe labda na wewe utaumakonda ukaseselaMi nilisema mtu akisemwa sana kwa ubaya JPM ndo humteua na kumuongezea na cheo pia! Eg Kasesela na Makonda sasa sijui Mzee Mwanakijiji hamuoni au bado muda wake.