Rais Magufuli atumia Ikulu ya Arusha!

Rais Magufuli atumia Ikulu ya Arusha!

Chakaza,taarifa zilizopo ni kwamba State Lodge yetu ya Arusha ilikuwa haitumiki.Raise aliyepita alikuwa akilala kwenye hotel za kifahari na kupoteza fedha za walipa kodi.JPM amekataa utaratibu huo.
Katimiza wajibu wake, hatuwezi kumpongeza kwani ubadhilifu wa mtangulizi wake haikuwa kwamba na huyu afanye
 
Hapo ndo shida imapokuja old school vs new school
Hakuna cha old wala nini hapo, ni full kujikomba tuu. Watu wa zamani hatukwepeshi na kupeana vilemba vya ukoka.
 
Awamu ya nne walikuwa wakitumia mahoteli makubwa na kuingia gharama zisizo za lazima. Issue iko hapo.
So what ?
Si hiyo awamu ya nne mlikuwa kutwa kucha Mnaiimbia Mapambo ya sifa
 
TAARIFA KWA UMMA -PRESS RELEASE

Nimevutiwa zaidi na taarifa kwa umma toka Ikulu ikiandamana na picha kibao za Ikulu Ndogo, Arusha kuwa Marais hawa wawili wa Tanzania na Uganda wamekubaliana ujenzi wa bomba la mafuta toka bandarini, Tanga mpaka Uganda la urefu wa kilometa 1,120 litajengwa na fursa kibao zitapatikana kutokana na mradi huo ikiwemo ajira 15,000.
 
Kikwete aliwahi kufikia na kulala nyumbani kwa Anna Tibaijuka huko Muleba badala ya kulala Bukoba au ikulu ndogo ya Muleba. Rais unalala nyumbani kwa mtu!!
Na alisifiwa
 
safi sana magufuli ..Hii ikulu na ikulu ndogo zingine zilizo kila wilaya /mkoa ni moja ya zile muhimu ambapo ziingine ni ya Chamwino,Mwanza,Mbeya na Lushoto...zote zilikuwa zimetekelezwa ...kwa miaka yote 10....hiii ikulu ilibidi kujengwa upya kimsingi kwakuwa Paa lilikuwa limeanguka , linavuja,garden ilikuwa kichaka ...nyumba za staffers zimeezuliwa paa ...utafikiri palipigwa bomu ...kwa miezi karibu mitatu pamekuwa kwenye marekebisho makubwa ..
Kimsingi rais ana uhuru wa kufanya kazi akitokea ikulu yeyoyte kwenye jamuhuri ...lakini marais wote ukiondoa Kikwete walikuwa wakipenda kuwa Chamwino na Arusha kama wakihitaji utulivu .....Mwalimu na Mkapa pia walipendelea Ikulu ya Lushoto ....ambayo ni kama camp david ya Tanzania enzi za Mwalimu. Hata magavana wa Kijerumani na UINGEREZA walipenda hapo pia

Kwenye utawala wa Kikwete ....alipenda zaidi kukaa mahotelini ....na baadhi ya mikoa ambayo hakuna hoteli nzuri alifikia hata kufikia kwenye nyumba za mawaziri mfano alikaa kwa mama tibaijuka ....
Pale dodoma alikaa state lodge ya mjini ambayo zamani walifikia makamu wa rais na kuiacha Chamwino ikijeuka pango la nyoka
Makazi rasmi ya waziri mkuu ambayo yalijengwa toka mwaka 2008 ya hali ya juu kabisa hayajahamiwa hadi sasa pamoja na kukamilika ....nadhani Majaliwa naye ataona umuhimu wa kuhamia pale
 
Kweli huu ni wakati wa mabadiliko nchini mwetu, picha kama hizi sikuwahi kuziona huko nyuma za Raisi wa nchi kutumia Ikulu zetu ndogo za Mikoani kwa shughuli za kiserikali!
Kama inavyoonekana pichani chini Raisi Magufuli akiwa na mgeni wake wa Raisi Museveni waUganda aliyewasili mjini Arusha kwenye mkutano wa AM!



MHA3.jpg




MHA1.jpg



MHA5.jpg

JAK.jpg


20160301090557.jpg


HAPA KAZI TU!
kwani Ikulu zilijengwa kwa kazi gani?
 
Ukawa kaa majuha vp mbona lowasa kahamishia ofisi kule mikocheni na sio ufipa tena
 
Hayo uliyoyataja ni matunda ya utawala wa CCM.

Kwa namna ulivyo-comment ni wazi wewe ni mtu anayeangalia mabaya tu ya CCM na serikali yake. Hutambui kuwa uhuru ulio nao wa kuandika utakavyo ni matunda ya CCM. Nenda China uandike kama mnavyofanya humu JF uone kitakachowapata. Nenda Russia ufanye kejeli hizo kwa PUTIN. Nenda RWANDA umdhalilishe KAGAME. Hata huko Marekani kwenye kile kinachoitwa uhuru mkubwa wa kutoa mawazo hawawezi kutamka hayo mnayosema kuwa Obama ameenda au ameingia....Sana Sana ikibidi, tena basi kwa nadra sana, wanaweza wakasema 'washing room' na hata hivyo sidhani kama wanaweza wakasema kuwa Rais ameenda au ameingia 'washing room'. Wana heshima na adabu kwa viongozi wao, sio kama sisi hapa tunaodandia demokrasia na kudhani kuwa demokrasia ni kudhalilisha wengine na hasa viongozi.
 
Kumbuka Chakaza uwe na adabu kwa Rais, hata kama humpendi nyamaza...usitaje ovyo ovyo kuwa Rais anaingia ...huo sio utamaduni wa kiafrika. Kuna namna ya kutamka hayo uliyosema...sijui nyie vijana wa siku hizi mkoje, hamna adabu kabisa. kwa kweli inaudhi sana. Mnaifanya nafasi ya Rais ionekane kuwa ni nafasi ya mzaha mzaha.
Huo ndiyo ukweli japo unaweza kuuona kuwa una sura mbaya. Sifa zisizo sufa zipunguzwe.
 
Awamu ya nne walikuwa wakitumia mahoteli makubwa na kuingia gharama zisizo za lazima. Issue iko hapo.
Na mlikuwa mnasifia haswa kaja huyu nae mnamsifia haswa akija mwingine akilala chooni mtamsifia mno mno.

Hapo ndipo naposhindwaga kuwaelewa kabisa.

Muone mwenzako Simiyu Yetu hapo juu.
Mnalipwaga kusifia ujinga ujinga nini?
 
Sina hakika sana na lengo la Barbarosa katika kuanzisha mada hii. Lakini ukweli ni kwamba JK na wasaidizi wake kazitumia hizo Ikulu ndogo alipokuwa akifanya ziara za mikoani. Si vizuri kujaribu kupotosha watu kwa mihemko ya kimahaba. Fanyeni utafiti kidogo.
 
Dahhh Kuna jua kali hapo ikulu.
Hiyo kofia ya Museveni hatari.
 
Chakaza,taarifa zilizopo ni kwamba State Lodge yetu ya Arusha ilikuwa haitumiki.Raise aliyepita alikuwa akilala kwenye hotel za kifahari na kupoteza fedha za walipa kodi.JPM amekataa utaratibu huo.
Siyo taarifa zilizopo mkuu, taarifa rasmi ndiyo hiyo kwamba Ikulu ilikuwa hata panya hakai coz nothing was there ingawaje Rais alitakiwa awe anafikia pale ktk shughuli zake za kikazi akija Arusha.

Mleta mada naona ni hawa vijana wa Academia, St. ... Schools, kwamba kipindi JK analala Mahotelini walikuwa wanamsifia leo hii Magu analala ikulu wanamsifia sada hapa nashindwa kuwaelewa.

So hata akija mwingine akalala chooni mtamsifia, hivi upambe ndiyo imekuwa kazi ya Watanzania siku hizi?
 
Inanikumbusha mchekeshaji maarufu wa marekani,anasema manigga wanavituko! Eti nigga anajisifu "mi natunza familia yangu" AMA "mi nasomesha mtoto wangu". Icho SI chakujisifu,hayo Ni majukumu ya kawaida na ya lazima. Kusifu Rais kutumia ikulu ndogo nikama mtu mzima kujisifu kuwa unaogaga. That's normal bra.
 
vipi kama alikuwa anatumia lakini alikuwa atangazi kwenye vyombo vya habari kama huwa anatumia na ikilu ndogo za mikoani,au wewe ndo mama salma unajua mlikuwa mkienda hotel
Ulikuwa unaishi Mbekenyela usijue kwamba zilikuwa hazitumiki? Hakuna magazeti wala Internet?
 
Back
Top Bottom