Rais Magufuli atumia Ikulu ya Arusha!

Rais Magufuli atumia Ikulu ya Arusha!

Na mlikuwa mnasifia haswa kaja huyu nae mnamsifia haswa akija mwingine akilala chooni mtamsifia mno mno.

Hapo ndipo naposhindwaga kuwaelewa kabisa.

Muone mwenzako Simiyu Yetu hapo juu.
Mnalipwaga kusifia ujinga ujinga nini?
Kwa hiyo ulitaka aje fisadi?
Nilikuwa CDM hadi walipolipokea fisadi kuu. Haikuwa lazima. Si lazima Dr Slaa lakini la fisadi kuu was an own goal
 
Ha ha kweli museveni ni shida, anatabasam tu kwa raha zake, haki ya kristo lol
 
Ikulu ndogo zote zimejengwa kwa ajili ya Rais. Ni aibu kubwa na ujinga uliovuka mipaka kwa watu kudiriki kumsifia Rais kwa kutumia makazi ambayo kimsingi yamejengwa na yanatunzwa kwa ajili yake. Mbona wakati waliomtangulia wakiepa makazi hayo na kukimbilia kwenye hoteli za gharama kubwa watu hawakuhoji hayo?

Kuna mengi yanatakiwa kufanywa kwa sasa na sio kupoteza muda kusifia mambo yasiyo na faida yoyote kwa taifa
 
Ikulu ndogo zote zimejengwa kwa ajili ya Rais. Ni aibu kubwa na ujinga uliovuka mipaka kwa watu kudiriki kumsifia Rais kwa kutumia makazi ambayo kimsingi yamejengwa na yanatunzwa kwa ajili yake. Mbona wakati waliomtangulia wakiepa makazi hayo na kukimbilia kwenye hoteli za gharama kubwa watu hawakuhoji hayo?

Kuna mengi yanatakiwa kufanywa kwa sasa na sio kupoteza muda kusifia mambo yasiyo na faida yoyote kwa taifa


wote walizitumi kasoro Kikwete
 
Kwa hiyo ulitaka aje fisadi?
Nilikuwa CDM hadi walipolipokea fisadi kuu. Haikuwa lazima. Si lazima Dr Slaa lakini la fisadi kuu was an own goal
Siasa za maji taka still zimekutawala.
Fisadi ni Yona, Mramba na wale jamaa wawili walifungwa kuhusu EPA nadhani.

Otherwise no other fisadi au labda kwa tafsiri yako fisadi ni mtu aliye above the law in TZ yaani huyo ni untouchable, anafanya lolote na hakuna anayemgusa.

Sasa wewe akija Rais anayekula majalalani na wewe utamsifia tu kisa ni Rais coz watu mlimsifia sana JK akila maisha huko mahotelini sasa JK kukaa ikulu kama inavyotakiwa imekuwa ni kumsifia tena?

Nashindwa kuwaelewa vijana Wa kisasa
 
wanapongezana kwa kushinda uchaguzi kihalalii na kidemokrasiaa
 
Kwa namna ulivyo-comment ni wazi wewe ni mtu anayeangalia mabaya tu ya CCM na serikali yake. Hutambui kuwa uhuru ulio nao wa kuandika utakavyo ni matunda ya CCM. Nenda China uandike kama mnavyofanya humu JF uone kitakachowapata. Nenda Russia ufanye kejeli hizo kwa PUTIN. Nenda RWANDA umdhalilishe KAGAME. Hata huko Marekani kwenye kile kinachoitwa uhuru mkubwa wa kutoa mawazo hawawezi kutamka hayo mnayosema kuwa Obama ameenda au ameingia....Sana Sana ikibidi, tena basi kwa nadra sana, wanaweza wakasema 'washing room' na hata hivyo sidhani kama wanaweza wakasema kuwa Rais ameenda au ameingia 'washing room'. Wana heshima na adabu kwa viongozi wao, sio kama sisi hapa tunaodandia demokrasia na kudhani kuwa demokrasia ni kudhalilisha wengine na hasa viongozi.
Nakubaliana na wewe kwa upande mmoja lakini ni viongozi wenyewe ndio waliojipotezea heshima hiyo. Mbona kwa Nyerere au Mwinyi vijana tuliwaheshimu kwa kusikia tu habari zao japokuwa hatukuwepo au tulikuwa wachanga enzi zao?!

Lakini baada ya hapo Awamu zilizofuata, viongozi walikosa heshima kwa wananchi wao. Inapofikia kiongozi kuweza kuwatusi au kuwakejeli wananchi wake ujue lazima heshima yake itashuka, hawatamheshimu!

Waanze kubadilika wao, na kizazi hiki kitawaheshimu!
 
Nikweli aisee, sasa
Haya bhana mtabishana na kujibizana sana lkn jamaa ndiyo anachanja mbuga hivyo. Km kweli wenzake walikua wakilala mahoteli ya gharama wakati ikulu ipo anastahili kusifiwa.
Ni kweli sasa kuna mijitu humu haielewi. Yaani hujui ipo upande gani. Kusifia haitaki, kila kiti ni kukashifu tu. Kiukweli mnaboa sana. Mtu akitenda jema kwanini asisifiwe.
 
Kutumia ikulu Ndogo ya arusha hakubadirishi chochote maana hiyo ndo ofisi yake, ni sawa na ww uingie ofisini kwako au nyumbani kwako halafu mtu akusifie hivi utakuwa umefanya jambo la nadra au?? Mh. Rais kutumia ikulu Ndogo zilizopo mikoani si ajabu maana ndo ofisi zake,
 
Haya bhana mtabishana na kujibizana sana lkn jamaa ndiyo anachanja mbuga hivyo. Km kweli wenzake walikua wakilala mahoteli ya gharama wakati ikulu ipo anastahili kusifiwa
Upo sahihi. Yaani kuna mijitu kila jambo na kukashifu. Sasa mheshimiwa katumia ikulu mwenzake alikuwa anatumia ngurdoto je hasitahili kusifiwa?
 
serikali ya CCM imeifilisi sana nchi hii
Ni kweli lakini ccm ni watu. Tumpe JPM at least miaka miwili. Tutakuwa tumeisha jua kama ni mvinyo ule ule kwenye chupa mpya au ni mvinyo mpya kwenye chupa ya zamani.
 
Ni kweli lakini ccm ni watu. Tumpe JPM at least miaka miwili. Tutakuwa tumeisha jua kama ni mvinyo ule ule kwenye chupa mpya au ni mvinyo mpya kwenye chupa ya zamani.
YEAH..Uko sahihi...lakini kiukweli kwa dalili zinavyoonesha hakuna kipya...mfano angalia upuuzi unaofanywa kuhusu uchaguzi wa mayor
 
Upo sahihi. Yaani kuna mijitu kila jambo na kukashifu. Sasa mheshimiwa katumia ikulu mwenzake alikuwa anatumia ngurdoto je hasitahili kusifiwa?
Binadamu wengine hawafadhiliki, bora umfadhili mbuzi manake kuna siku utaambulia hata supu ya utumbo.
 
Ni kweli lakini ccm ni watu. Tumpe JPM at least miaka miwili. Tutakuwa tumeisha jua kama ni mvinyo ule ule kwenye chupa mpya au ni mvinyo mpya kwenye chupa ya zamani.
Miaka miwili ya nini tena? Dunia inaenda haraka sana mkuu yaani tunajifanya kuzoea shida kiasi hiki? Hatari sana. Kawaulize NOKIA
 
Kwani hiyo Ikulu ndogo ilikuwa kwa ajili ya Rais au kufugia mbuzi?
Nyie kuna siku mtamsifia hata akiingia chooni
Inabidi uvumilie tu maana kuna miaka mingine KUMI ya Ngosha. Au kajinyonge tu ili usione hii nchi inaendelea.
Weye lazima unammiss Mzee wa Msoga. Umebanwa kweli kweli.
 
Hivi mwenye nyumba kulala nyumbani kwake ni ajabu? Au mimi sielewi jamani. Ikulu ni kwa ajili ya nani labda?
 
Kweli huu ni wakati wa mabadiliko nchini mwetu, picha kama hizi sikuwahi kuziona huko nyuma za Raisi wa nchi kutumia Ikulu zetu ndogo za Mikoani kwa shughuli za kiserikali!
Kama inavyoonekana pichani chini Raisi Magufuli akiwa na mgeni wake wa Raisi Museveni waUganda aliyewasili mjini Arusha kwenye mkutano wa AM!



MHA3.jpg




MHA1.jpg



MHA5.jpg

JAK.jpg


20160301090557.jpg


HAPA KAZI TU!
Yeye rangi mpya haimdhuru? Maana inaonekana vizuri. Na wafanyakazi wa ikulu ndogo anatoka nao Dar au wako huko permanently? Sina nia mbaya najaribu tu kuona kama kuna matumizi ambayo yanaweza kubanwa.

Hiyo ikulu kuu ilikuwa haikaliki sembuse hiyo ya pembezoni, wakati ngurdoto iko. Kwa mahesabu ya haraka haraka unadhani bilioni ngapi au trilioni zilipotea. Na pengine upendekeze tutazirudishaje.
 
Back
Top Bottom