Rais Magufuli akijibu maswali haya atakuwa Rais bora wa Afrika wa karne ya 21

Raisi bora iwe Afrika au popote duniani hapimwi kwa uwezo wa kujibu maswali hupimwa kwa uwezo wa kuletea wananchi maendeleo yanayoonekana

Kazi ya uraisi sio kujibu maswali
Empty set ya Lumumba maskini , ona inavyohangaika kujibu ,Jiwe a .k.a Zanzimana hana uwezo wa kujibu haya maswali sembuse we kibaraka wake .
 
Huwa najiuliza na sipatigi jibu, ni nani aliyependekezwa magu apitishwe kuwa rais? Kiuhalisia hana sifa ya kuwa rais na huenda ana tatizo kubwa linalohitaji matibabu ya haraka kabla hajaliangamiza kabisa taifa letu
My daughter's sacrifice made me a president .
 
Nawasalimu wanabodi!

Tunaposema haya si kwamba tunamchukia Rais wetu, hapana. Tunampenda sana. Tunampenda afanikiwe maana akifanikiwa Taifa limefanikiwa kwa ujumla. Hivyo basi, hata wapambe wake wajue hivyo.

Aliyekuwa Mwanasheria Mkuu wa Marekani Robert Jackson anasema, "Si kazi ya Serikali kuwafanya raia wasianguke kwenye makosa Bali ni kazi ya raia kuifanya Serikali isianguke kwenye makosa" na kwa mantiki hiyo ni jukumu la raia kuifanya Serikali isifanye makosa ni kupitia ukosoaji, ushauri na usifiaji inapostahili.

Kwa mantiki hiyo, ukimya wa raia kuhusu mambo ya hovyo yanayotendwa na Serikali ni kuiangamiza umma, ni kuua watu. Binafsi ninaamini Dk. John Pombe Magufuli akinijibu maswali yafuatayo atakuwa Rais muungwana na wa pekee sana Afrika na duniani kwa ujumla.

(1). Magufuli ni Mkatoliki Safi aliyekataa hata kusaini hati za kunyonga watu. Je, Rais wangu unaamini kwa moyo wa dhati kabisa ulishinda Urais 2015 na 2020?

(2). Rais wangu, tunaimbiwa mapambio ya "uchumi wa viwanda", "hapa kazi tu", "uchumi wa kati", hivi, nini falsafa ya utawala wako?

(3). Rais wangu, kuna vijana Ben Saanane na Azory Gwanda "walipotea". Wapo wanaosema wamejipoteza, wapo wanaoamini walitekwa na wanausalama wako. Wewe unaamini au kudhani vijana hawa wako wapi?

(4). Rais wangu, ni lini uchunguzi au upelelezi kuhusu kushambuliwa kwa mwanasiasa mwenzio Tundu Lissu utakamilika? Je, huoni kuna haja ya kuhusisha wataalamu kutoka nje kwa gharama ya familia kama CIA, Mosad au Scotland Yard kusaidia kuwatambua "wasiojulikana"?

(5). Rais wangu, unadhani uamuzi wa kuwatimua wale wanafunzi 8000 kutoka UDOM na kuwaita vilaza ulikuwa sahihi?

(6). Rais wangu, unadhani uamuzi wa kupora hela za watu katika maduka ya kubadili fedha kwa kutumia JWTZ na kuwafilisi ulikuwa sahihi?)

(7). Rais wangu, tumechelewa Maendeleo lakini ulikabidhiwa nchi inayohishimu Sheria. Je, unadhani uamuzi wako wa kununua madege bila kufuata Sheria ya ununuzi kupitia Bunge ulikuwa sahihi? Unajua unadaiwa chenchi?

(8). Rais wangu, ule muswada uliopeleka Bungeni kwa hati ya dharura kwamba wewe, jaji Mkuu na Spika wa Bunge wasishitakiwe kwa makosa yao enzi za uongozi wao ulimaanisha nini? Je, unahisi kuna kosa umetenda ukistaafu ungeweza kushitakiwa kwayo?

(9). Rais wangu mpendwa, hupangiwi kazi, lakini, ni kwa makosa gani walifanya ukawatimua kazi Ernesti Mangu na Kapilimba? (IGP) na DG-TISS?

(10). Rais wangu, unaamini kuwa kuwachukia, kuwabagua na kuwatenga wanaokoaoa utawala wako ni uamuzi sahihi wenye busara na hekima? Unaamini katika kutesa wanasiasa wa upinzani?

(11). Rais wangu, bado unaamini kuwa kila aliyefanikiwa kimaisha ni mpiga dili? Utawapata wapi mabilionea wa kitanzania unayohubiri?

(12). Rais wangu, ulivyoingia madarakani ulikuta kuna shimo la Tanzanite maarufu kama "shimo la Mwarabu" linalotema madini hayo kuliko mashimo yote. Shimo hilo Jakaya alimpa mzungu wa Afrika Kusini aliyemsaidia fedha za kampeni 2005. Umempora mzungu huyo ukajimilikisha wewe kama wewe kupitia kwa kijana wako Dotto Biteko. Umevuna madini ya thamani ya 7T Kagame akakuzima mazima baada ya kumpa akuuzie. Je, ni kweli taarifa hizi?

(13). Rais wangu, ni kweli Rostam Aziz amekutapeli mabilioni za Uchaguzi akatokomea Canada na sasa hamuongei? Kwamba ulimruhusu kuingiza pesa nchini kumsapoti Lissu ili zipigwe akapiga yeye?

(14). Rais wangu, ni kweli Tanzania jakuna janga la Corona? Je, una mpango wa kuagiza chanjo ya ugonjwa huo?

(15). Rais wangu, kelele za kutaka kuifanya Chato kuwa Ulaya badala ya Tanzania unazichukuliaje? Ni kweli au uzushi za wasiokupenda?

(16). Rais wangu, kuna taarifa kuwa baraza lako la Mawaziri umejaza Wakatoliki wa Kanda ya Ziwa, ni kweli mambo haya?

(17). Rais wangu, mtu anayeitwa NAJIM ZUBERI MSENGA ni katika utawala wako? Nani bosi kati yake na Dotto James wa Hazina?

(18). Rais wangu, ni kweli ulimwekea "bambi" Bernard Membe asiwe Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Madola 2016 licha ya kukubalika na wenzio wote wa EAC na ndio ugomvi wenu uliofikia ngazi ya familia?

(19). Rais wangu, kwa nini unataka kumfukuza kazi Dk. Bashiru Ally? Je, ni kwa sababu amekataa kuondoa ukurasa unaogusa #$@&+ kwenye ripoti ya Mali za chama?

(21). Rais wangu, ni kweli unatumia ripoti hii kama rungu kudhibiti wanaotaka Urais 2025 kwa kuwatishia "tukutane Kisutu" kwa uhujumu uchumi?

(22). Rais wangu, ni kweli wapinzani hawakushinda Ubunge nchi nzima?

(23). Rais wangu, ni kweli umeachana na wazungu kasoro Ufaransa (kuwapa gesi Total) na sasa maisha ni Uchina?

(24). Rais wangu, ni kweli umeteka nyara fedha za mwekezaji kutoka Oman bilioni 480 aliyetaka kuwekeza huko nyumbani Arusha kwenya madawa ya binadamu?

(25). Rais wangu, katika moyo wako wa ndani kama Mkristo, unadhani unaongoza vizuri inavyostahili? Unadhani wananchi wanakufurahia au unashambuliwa na ugonjwa wa. "huwezi kupendwa na wote" ambao ni ndwele ya waliofeli uongozi?

Rais wangu, maswali yako 101. Naomba leo niishie hapo. Unaweza kujibu hadharani au sirini au kwa kutumia washangwena wako.

Ahsante Rais wangu. Ukiyajibu maswali hayo, hakika utakuwa kiongozi wa aina yake Afrika. Tujenge nchi yetu.
Kuanzia S.12 hadi la mwisho ni lazima yatakuwa yasomeka moyoni mwake kama vile herufi zake zimeumbwa kwa msumari wa moto.
 
Oxygen ya Tanzania ni tofauti na nchi zote jirani pamoja na kwamba ambulance zinapishana kama daladala mitaani. Saa chache zijazo naenda kumzika mtu aliyekufa kwa approved covid-19.
Unaliwa kweli wewe hivi mtu mwenye covid anaruhusiwa kuzikwa hata kuagwa tu na watu hao ndugu zake wenyewe hawaruhusiwi kumuona,ukitaka kujua corona haipo au ipo lakini haituadhiri angalia ukali wa uo ugonjwa,angalia maisha yetu tangu miezi miwili iliyopita,
Usiwe mbumbumbu hao madokta ma nurse hawachukui tahadhari yoyote na wao wapo jikoni unafikiri corona kama ingekuepo ingekua na huruma kiasi gani?
 
Inafurahisha. Eti virusi vya CORONA viruka weeeee lakini vikifika Namanga, Sirare, Rombo nakadhalika vinakufa. Havivuki mpaka wa Tanzania. Na ukiwa na Corona ukiingia tu Tanzania unapona. Mi nadhani Ulaya wahamie tu Bongo watapona wote. Nchi ya matahira!

Matahira ni wewe Na ukoo wako, shwaini!
 
1610624447306.png
 
Swali la nyongeza, hivi Rais unaamini kabisa kuwa Tanzania hakuna COVID licha ya majirani zetu wote kusumbuliwa na hili tatizo?
Askofu Bagonza ameshamwambia kuwa Tanzania siyo makao makuu ya Mungu. Asijilimbikie dhambi ya kufuru eti maombi yake yamefukuza corona. Kwani nchi jirani hawasali?
 
Askofu Bagonza ameshamwambia kuwa Tanzania siyo makao makuu ya Mungu. Asijilimbikie dhambi ya kufuru eti maombi yake yamefukuza corona. Kwani nchi jirani hawasali?
Kwani huyo Askofu Bagonza ndio msemaji mkuu wa Mungu!?
🤔🤔🤔
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom