Rais Kikwete; Watanzania tukukumbuke kwa lipi ulilotufanyia?

naninibaraka

JF-Expert Member
Oct 13, 2011
910
668
Mh. Rais wangu,nikupongeze kwa kuchaguliwa kumaliza awamu yako ya pili na ya mwisho kabla hujaanza kuitwa mstaafu,ni ahadi nyingi sana ulizotuahidi watanzania mwaka 2005 na baadaye 2010.

Kwa mtizamo wangu kipingi ulichokaa madarakani ni kirefu zaid kuliko kipindi ulichobakiza kumalizia mda wako.

Hoja yangu ni kuwa kama ni vigumu kwa muda uliobaki kufanya lolote la kukumbukwa na watanzania,watanzania tumekata tamaa ya maisha,hakuna wa kutuma matumaini kwa siku zijazo baba umekaa kimya,nchi imekatikatika kwa mijadala isiyoisha.

Mh. Rais, 10yrs bila maendeleo ni jambo gumu ambalo athari zake kwa jamii ni kubwa!,kwa madogo uliyofanya kama kwenye michezo tutakukumbuka daima!

Naomba kuwasilisha.


Jakaya Mrisho Kikwete mwana wa msoga anastaafu, -anaacha taasisi ya Urais anaacha Serikali na hatimae ataacha Chama...

Kama ilivyo Ada kuwa kila anayemaliza atakumbukwa nae tutamkumbuka. Kwa maana nae ataacha kumbukumbu iwe mbaya ama nzuri, wapo watakaolia kwa furaha kuondoka kwake na watakaolia kwa majonzi kwamba hawajui kesho yao...

Kikwete atakumbukwa kwa mambo makubwa na mazuri aliyowafanyia Watanzania lakini vilevile wapo wataomkumbuka kwa jinsi alivyowaangusha kwa kutenda kinyume cha ahadi zake na kaulimbiu zake za Ari mpya, Kasi Mpya na Nguvu mpya na ya Maisha bora kwa kila Mtanzania.

Watanzania wa kada mbalimbali wanazo sababu za kumkumbuka Rais Kikwete atakapong'atuka madarakani. Hii itatokana na jinsi walivyonufaika au kuumizwa kwa namna moja ama nyingine na utawala wake.

WANAWAKE:

Watamkumbuka Rais Kikwete kwa jinsi alivyothamini mchango wao na uwezo wao kiutendaji.

Ktk Awamu ya nne, Rais aliongeza kasi ya kuwaamini na akawateua kwa wingi baadhi yao kuingia kwenye vyombo vya uamuzi kama uwaziri, Ukuu wa mikoa na wilaya na nafasi za uwakilishi.

Ktk kipindi chake idadi ya majaji wanawake iliongezeka, ikiwamo hata kufanikisha Anne Makinda kuwa mwanamke wa kwanza kushika nafasi ya juu ya Uspika wa Bunge.

Swali ninalojiuliza ni je.., atawaachia zawadi wanawake kwa kupendekeza mmoja wao kuwa mgombea urais..???

VIJANA:

Kundi hili nalo litakuwa na kila sababu ya kuhuzunika KIKWETE atakapoondoka madarakani. Hii ni kwa sababu kila alipofanya uteuzi, hakuwaacha vijana.

Tangu alipojitosa katika kinyang'anyiro cha urais kwa mara ya kwanza mwaka 1995, Mkakati wake ulikuwa kuwapa vijana fursa za uongozi na aliposhinda mwaka 2005 aliwateua bila hofu katika nyadhifa mbalimbali

WAZEE:

Mbali na kuendelea kuamini busara za wazee, kila alipotaka kutangaza jambo zito au kutoa hotuba ya mwisho ya mwezi iliyotikisa nchi, alikutana na wazee wa Dar es salaam au Dodoma. Lakini vile vile wazee wamo katika nafasi mbalimbali za uongozi, uwaziri, ukuu wa wilaya na Mikoa.


WAZANZIBARI:

Rais Kikwete alijitahidi kadri ya uwezo wake kupatanisha wananchi wa unguja na pemba waliotofautiana kwa misingi ya siasa.

Chini ya ushawishi wake Wazanzibari walikubali kuongoza nchi kwa ushirikiano, wakaunda Serikali ya Umoja wa Kitaifa. UHASAMA uliondoka japokuwa kuna viashiria vya uhasama kurudi.

WASOMI

Hakuacha nyuma kundi la wasomi, kwani miongoni mwao ndio wanaoongoza wizara nyeti na taasisi mbalimbali. Aliwateua katika nafasi mbalimbali za uongozi japokuwa baadhi yao wamemwangusha.

Atakumbukwa alivyohamasisha ujenzi wa shule za Sekondari kukidhi ongezeko kubwa la wanaofaulu kutoka shule za msingi na alivyojenga chuo kikuu cha Dodoma, upanuzi wa Chuo Kikuu huria na vyuo vya kati.

WANACHAMA WA CCM.

Tofauti na vyama vingine vya siasa, CCm wanajivunia kumpata mtu aliyekuwa kete ya ushindi kwa vipindi viwili mfululizo 2005 - 2010 na 2010 - 2015.

Watamkumbuka alivyowabeba, alivyofanyia marekebisho katiba ya chama kuwa na wajumbe wa Halmshauri kuu kutoka Wilayani, alivyohuisha chama hadi kuwa na mvuto kuliko awali.

HOFU yao ni je, watampata mgombea ambaye atakuwa KETE ya USHINDI..???
 
Yapo mengi,kubwa kuliko yote waliohukumiwa kifo kwa kosa la kumuua Kombe kuachiwa,ili hali kina Babu Say Yer wanaozea Gerezani,kwa hayo tutamkumbuka!.
 
Hakika Jk karuhusu uhuru wa vyombo vya habari kiasi kwamba hata baadhi ya watu wasiokuwa na adabu wanamtukana humu jamvini na yeye akiwa mkuu wa nchi hawachulii hatua huu ni uvumilivu wa kuigwa
 
  • Thanks
Reactions: Omr
Atakumbukwa kwa mengi sana.
1. Chuo kikuu cha dodoma.
2. Kuhamasisha kilimo, rejea sera Kilimo Kwanza.
3. Uhuru wa vyombo vya habari.
4. Uvumilivu wa kisiasa.
5. Ujenzi wa shule za sekondari.
N.k.

Japo ana mapungufu ya kibinadamu, ila amefanya mema mengi tu yakukumbukwa.
 
  • Thanks
Reactions: Omr
Hakika Jk karuhusu uhuru wa vyombo vya habari kiasi kwamba hata baadhi ya watu wasiokuwa na adabu wanamtukana humu jamvini na yeye akiwa mkuu wa nchi hawachulii hatua huu ni uvumilivu wa kuigwa

Makupa Makupa Makupa usije kuwa makupe jamani Makupa
 
  • Thanks
Reactions: BMT
Kigoma Will be like Dubai in Three years coming!
He will build three International Airports as he Promised during his 2010 presidential campaign!
Without forgetting better life to every Tanzanian.
I think Tanzanian will Remember our behated President for that!
............................................
I was Just Joking...nothing like that will be done that is politics!
 
Kigoma Will be like Dubai in Three years coming!
He will build three International Airports as he Promised during his 2010 presidential campaign!
Without forgetting better life to every Tanzanian.
I think Tanzanian will Remember our behated President for that!
............................................
I was Just Joking...nothing like that will be done that is politics!
Anasubiri cement ya sh.500 kutoka kwa Slaa ili akajenge magorofa huko kigoma
 
Hakika Jk karuhusu uhuru wa vyombo vya habari kiasi kwamba hata baadhi ya watu wasiokuwa na adabu wanamtukana humu jamvini na yeye akiwa mkuu wa nchi hawachulii hatua huu ni uvumilivu wa kuigwa
Kikwete is a Dictator in making hajijui na wengi hawajui.
 
Hakika Jk karuhusu uhuru wa vyombo vya habari kiasi kwamba hata baadhi ya watu wasiokuwa na adabu wanamtukana humu jamvini na yeye akiwa mkuu wa nchi hawachulii hatua huu ni uvumilivu wa kuigwa

Ibara ya 18 uhuru wa kutoa maoni
 
Ngoja nikusaidie! ni shs 5000. Halafu nikukumbushe Dr.Slaa alitoa ahadi hizo na angezitekeleza iwapo angekuwa Rais!
Sasa hiyo dubai itajengwa vipi kama hiyo cement haiji? Tunaomba umuulize hiyo cement angeishushaje bei mpaka kufikia hiyo bei?
 
alishasema kwamba mumkumbuke kwa kuwatoa pale na kuwafikisha hapa.
 
  • Thanks
Reactions: BMT
Sasa hiyo dubai itajengwa vipi kama hiyo cement haiji? Tunaomba umuulize hiyo cement angeishushaje bei mpaka kufikia hiyo bei?
Cement kushuka bei hiyo rahisi tu! hata kichaa ukimpa nchi anaweza kuifanya bei kuwa 3500 kwa mfuko mmoja! ondoa kodi kwa wazalishaji wa cement na ongeza kodi maradufu kwa waizi wa madini yetu! thats all!
 
Back
Top Bottom