Huu mkakati anotumia JK naona kama umepitwa na wakati, nionavyo mimi unatakiwa ubunifu uchukue mkondo wake, suala la kujitambulisha halina manufaa kwa taifa, amekuwa mwaziri wa mambo ya nje kwa miaka 10 anafamika vilivyo.JK awaamini watendaji wake na akazimu madaraka kwa taasisi zinazo husika zifanye kazi yake matokeo tutayaona, kwa mtindo huu anaokwenda nao atashindwa kubeba miziko ya kashfa kwani mikataba ikibuma hatakuwa na kisingizio.
Nionavyo mimi,
mosi, kwa upande wa kutafuta wawekezaji Tanzania Investment Centre inafanya kazi gani, mabalozi walioko huko ng'ambo wanafanya kazi gani, kama hizi taasisi hazifanyi kazi ni bora zifutwe ili JK awe na kisingizio cha kusafiri, baadhi ya mikutano si lazima aende yeye akasimu madaraka kwa mabalozi au waziri wa mabo ya nchi za nje, akifanya hivyo taifa litaokoa gharama, na kufanya shuguli za maendeleo.
pili, mkakati wa kupata wawekezaji unaweza kufanikiwa hata JK akiwa hapa nchini si lazima asafiri, serikali ya marekani haina pesa, pesa wanazo wamarekani, balozi zetu kushirikiana na TIC wapewe jukumu na malengo, kuwashawishi wafanya biashara wakubwa watembelee nchi yetu kwa mwaliko wa Rais, wawekezaji hawa watapata furasa ya kuona sehemu watakayo wekeza badala ya kwauzia mbuzi kwenye gunia.
tatu, utaratibu wa raisi kutembea na utitiri wa wawafanya biashara umeshaanza kuleta wasiwasi kwa wananchi, hatujatangaziwa ni utaratibu gani unatumika kuwachagua hao wafanya biashara wanaongozana na muheshimiwa, wamachinga wamekuwa wa kwanza wanataka nao wakaone wenzao wanafanya biashara ng'ambo nao pia wataka kuingia ubia na wamachinga wenzao ng'ambo, kesho utasikia mama lishe, keshokutwa wabeba mizigo watalalamika wanaumia migongo kubeba lumbesa watataka kutafuta wabia ng'ambo ili wapate vifaa vya kubebea mizigo, malamiko haya yanakwenda mbali wengine wahisi labda JK analipa fadhila kwa wafanya biashara walio muwezesha kupita mchokato mzima wa uchaguzi, na pengine anajaribu kujenga uwezo kwa kuwazesha hawa wafanya biashara ili waje wamchangie pesa za uchaguzi 2010.
haya si maneno yangu na nisiukumiwe, ni maneno yanayosemwa mitaani