Rais Kikwete amuumbua John Tendwa

Rais Kikwete amuumbua John Tendwa

Sijui kwanini unawaamini viongozi wa Tanzania hadi uhalalishe matamshi yao kwa kutumia quotes zao. Wakati hao hao ni mabingwa wa kuchakachua hizo quote zenyewe na kutumia msemo maarufu 'Sikumaanisha hivyo, mmenielewa vibaya"

Bongo tambarare bwana...unasema mwenyewe afu unageuza habari. Hivyo ndivyo walivyosema, nasi baadhi yetu tuliwasikia.

Sasa kama kwetu viongozi ni wepesi wa kugeuza kauli, hili linaongeza kabisa umuhimu wa kuzinasa hizi kauli neno kwa neno, ili kesho wakitaka kuturuka tuweze kusema kauli yako hii hapa, umesema hivi na vile.

Tukizungumza kwa maneno jumla jumla bila direct quotes ndo hapo mtu anapokuja kuruka.

Kwa kutokutoa direct quote mnampa nafasi Tendwa aweze kujitetea "Mimi sikupiga marufuku maandamano na mikutano ya CHADEMA kwani hiyo ni haki yao ya kikatiba, ila nilikuwa nawahimiza kuhakikisha usalama wa wananchi unazingatiwa katika mikutano yao"

Kama hamtaki kumpa loopholes kama hizi inawabidi mrekodi vilivyo neno baada ya neno ili kesho akija kukanusha mmuonyeshe maneno halisi aliyosema.

Point yako inaongeza umuhimu wa kuwa na direct quotes, haipunguzi.
 
Huwa napata shida ninapokutana na mawazo ambayo ni ya watu wanaojiona wanjua kumbe ni mbumbumbu. Hivi wewe comment kama hii unaona umeandika kitu cha maana??. Quates zinatusaidia nini?. Je unataka kutwambia kwamba huyu bwana anachokisema ni uongo mpaka aweke quates. Kuwa muelewa usiuweke usiku watu wana mambo mengi ya kufanya

Nukuu zinasaidia si tu katika kuelewa muktadha wa kilichosemwa bali pia huwa ni ithibati kwamba kweli kinachodaiwa kusemwa kilisemwa kama kilivyo na si uzushi wala tafsiri ya mleta mada.
 
Chadema mmechanganyikiwa na safu ya mashambulizi. Nyie mlikuwa mnahamasisha furugu na kujidai eti mnafungua matawi na hata kutaka kuvuruga zoezi la sensa. Hapa hamtwambii kitu tendwa siyo mtoto anajua mbivu na mbichi. Mkuhubiri vurugu mtaipate kama yule jamaa yenu yule yule na niiiii hahaha



Mtoto kazi yake kucheza na mikojo kwenye chupi,M4C sasa ndio inamaliza kazi,Tendwa ni sawa na changu doa tu anayekuwa wa kwanza ndio huyo hajui wanyuma kama ana mazuri au mabaya zaidi.Chama chochote cha siasa ni lazima kiwe active na kinafanya kazi ya siasa kama walivyokuwa wanafanya CDM,CCM wanajua madhara ya kutokuwa sughuli za kisiasa ndio maana wanapita jia ileile ya CDM,Tendwa ni masikini wa akili na hajitambui wala hatambui siasa na vyama vya siasa vinatakiwa kufanya nini,kama wata kua treated equally hakutakuwa na fujo ya aina yoyote.
Hasa huyu mtu anayeitwa Tendwa anatabia gani?siku zote huyu jamaa ni mtu asiyejitambua,hivi ile kauli yake ya kuvifuta vyama ambavyo havifanyi sughuli za kisiasa ila vinaibuka katika uchaguzi tu alimalizaje?Huyu jamaa namuombea kwa mungu asije sababisha vurugu sidhani kama atakuja kuzizima,CDM marufuku kuna Sensa huku CCM wana kampeni za ubunge baya!!!!!!!!!!!!!!!!! CCM wanataka kupiga jaramba vitongojini,wilayani na mikoani,je hii ni sawa wengine waangalie tu?ngoma inogile.

mmwaisoba ukisoma maneno yangu hapo juu utajua hakika unachezea mikojo bila ya kujitambua.
 
Huwa napata shida ninapokutana na mawazo ambayo ni ya watu wanaojiona wanjua kumbe ni mbumbumbu. Hivi wewe comment kama hii unaona umeandika kitu cha maana??. Quates zinatusaidia nini?. Je unataka kutwambia kwamba huyu bwana anachokisema ni uongo mpaka aweke quates. Kuwa muelewa usiuweke usiku watu wana mambo mengi ya kufanya

Mie sina ninachokijua ndo maana nauliza, wewe unayejua unazo hizo quotes nilizouliza?

Quotes kwa sie tusio na dini wala chama zitatusaidia kujua kilichosemwa hasa na primary source, ili tujue kama hii habari ni ya ukweli au ni chumvi za siasa.

Of course if you are a CHADEMA fanboy, chochote cha kuwatananga CCM kitakuwa ni fair game kwako. Which is sad.
 
Unamfanyia reference Dhaifu! Basi na wewe dhaifu
 
Tatizo lako ni kwamba unapinga vitu kwa unazi bila kujenga hoja au na wewe ndo wale mnaosoma tu magazeti ya Uhuru na Mzalendo???!!!!! Alichosema mtoa mada ndo ukweli wenyewe. kwa wana JF makini sidhani kama hawatakuwa aware na alichosema John tendwa kuhusu mikutano ya kisiasa wakati ambao sio wa uchaguzi. kama hujui si uulize????? na sio kubisha usichojua!!!!!

Kati yangu mie ninayetaka kuangalia maneno halisi yaliyotumika niyapime kwa undani na wewe unayechukua maneno jumla jumla nani anaendekeza unazi?

Mie sijamtetea yeyote hapa kati ya Tendwa, Kikwete, CCM, CHADEMA.

Naonyesha tu kwamba kuna umuhimu wa kuyachambua maneno halisi yaliyosemwa maana hizi habari za kuambiwa na aliyeambiwa na aliyesikia kwa aliyesikia unakuja kupata habari imepinduka mara saba mara sabibi na saba.

Sasa kukataa hayo, naomba maneno halisi ili nijue kama kweli Kikwete kamuumbua Tendwa au ni hadithi za kisiasa tu.

Sasa nitakuwaje mnazi mtu hata sijachagua upande?

Mnazi wewe unayerukia kushabikia maneno usiyoyajua.
 
Unamfanyia reference Dhaifu! Basi na wewe dhaifu

To the contrary, kwanza hapa kinachotakiwa ni quotation, siyo reference, know the difference.

Pili, kama mtu ni dhaifu, halafu unataka kuonyesha kwamba yeye dhaifu, ukashindwa hata kujenga hoja dhaifu kwa kutumia quotations dhaifu kutoka kwa dhaifu, wewe utakuwa dhaifu zaidi ya dhaifu mwenyewe.
 
Mkuu kiwososa

Nimefurahi sana kukusoma jinsi ulivyomjibu huyu jamaa asiye na kumbukumbuku.

Inavyoelekea yeye anasoma tu magazeti ya Uhuru na Mzalendo.Ni kweli magazeti haya hayawezi kuwa na habari niliyoandika.

Kati yako wewe usiyejua umuhimu wa direct quotations na mimi ninayesisitiza umuhimu wa direct quotations nani anasoma magazeti ya maana hapa?

Magazeti ya maana unayoyasoma wewe ndo yanasema habari iletwe tu bila direct quotations from primary sources?
 
Nukuu zinasaidia si tu katika kuelewa muktadha wa kilichosemwa bali pia huwa ni ithibati kwamba kweli kinachodaiwa kusemwa kilisemwa kama kilivyo na si uzushi wala tafsiri ya mleta mada.

Wengine hata wakielewa hawataki kukiri kwamba ili uchambuzi madhubuti kufanyika nukuu za moja kwa moja ni muhimu.

And when cooler heads prevail in seeing this as an issue, they quickly distort the narrative without addressing the fundaments of the discourse.
 
Tendwa has been more of a liability to Tanzania than anything else.Kama Tanzania itaingia kwenye machafuko yeyote yale,wakati wowote ule,Mungu aepushie mbali,Tendwa atakuwa amechangia sana.
Mwenyekiti wa chama cha Mapinduzi Rais Jakaya Kikwete amewataka wajumbe wapya wa NEC wa CCM kutokulala bali kuzunguka kila kona ya nchi kufanya mikutano ya hadhara,kuingiza wanachama wapya na kueneza sera za chama hicho.

Rais Kikwete amesema kazi hiyo ikamilike kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2014 kisha iendelee mpaka uchaguzi mkuu wa 2015.Rais Kikwete amesema hiyo ndiyo njia pekee itakayokipa ushindi mkubwa chama hicho kwenye chaguzi zijazo.Rais amesema kamwe chama kisichozunguka kwa wananchi kuhutubia na kueneza sera lazima kitaangamia.

Itakumbukwa ni hivi karibuni Msajili wa vyama vya siasa nchini John Tendwa alitishia kupiga marufuku chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA kuendelea na operesheni yake ya M4C kwa kile alichodai amesitisha operesheni zote mpaka nyakati za uchaguzi.Alisema akiwa kama msajili wa vyama kamwe hatakubaliana na operesheni za CDM za kujijenga.

Naye Mhadhiri wa chuo kikuu cha DSM Dr Benson Banna alimuunga mkono Tendwa kwa kusema Operesheni ya CDM ya M4C haikubaliki kwani ni kuwasumbua wananchi na kuwanyima muda wa kufanya kazi na kuwataka CDM wasubiri kipindi cha uchaguzi.

Kama vile ni mpango mahususi ulikuwa umepangwa nayo Kamati ya kuchunguza kifo cha Daudi Mwangosi maarufu kama kamati ya Nchimbi iliungana na Tendwa katika moja ya mapendekezo yake kuitaka serikali kupitisha sheria ya kuzuia mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa mpaka nyakati za uchaguzi.Pendekezo hilo lilisema shughuli zote za siasa baada ya chaguzi zihamie bungeni.

Kauli ya Rais Kikwete ya leo imeonekana waziwazi ni kupingana na kauli ya msajili wa vyama vya siasa John Tendwa na Msajili huyo ameonekana wazi hafai kuendelea kushikilia wadhifa huo.

Source: ITV/Chanel Ten.
 
Tendwa anatoa matamko yake huku akisikisikiliza tumbo lake linahitaji nini, akisema kinyume lazima CCM wamnyime ajira. Uenda ana akili timamu lakini kutokana na katiba ya nchi anajikuta hawezi kwenda against na chama tawala
 
Mkuu Kiranga
Umesahau habari yenyewe imeandikwa na Molemo wa JF?


Chama
Gongo la mboto DSM

Part of the issue is I don't necessarily keep up with all these little two bit activists.

So are you saying that this guy is an irrelevant ignoble ignoramus bent on imbecilic idiocracies?
 
si tendwa tuu,pinda, Nape, Lowasa na wengine huona joto la Jiwe mkulu anaposema apendacho bila kulinda hawa jamaa.
 
Tendwa anatoa matamko yake huku akisikisikiliza tumbo lake linahitaji nini, akisema kinyume lazima CCM wamnyime ajira. Uenda ana akili timamu lakini kutokana na katiba ya nchi anajikuta hawezi kwenda against na chama tawala

Matamko gani? Unalo tamko la Tendwa kwa maneno yake mwenyewe tuukaate mzizi wa mzozo?
 
Ukweli haujali demokrasia, hata dunia nzima ikisema moja ni mbili moja haigeuki mbili.

Nimeandika hapo juu kwamba sifagilii habari za kuangalia macho ya watu.

Serious claims require serious evidence
, uneshindwa kutoa hata direct quote tu.

Unakubaliana na hoja katika thread ya propaganda? Do you even know the difference?

Nani anaye-define seriousness ya claim, wewe?. Na kwa nini definition yako iwe sahihi?. Kwa mwingine ni moderate. Kwa hiyo hitaji la direct quote linategemea nani ana-define terms na siyo lazima tufuate definition yako.
 
Nani anaye-define seriousness ya claim, wewe?. Na kwa nini definition yako iwe sahihi?. Kwa mwingine ni moderate. Kwa hiyo hitaji la direct quote linategemea nani ana-define terms na siyo lazima tufuate definition yako.

You just can't discount the importance of direct quotes by injecting subjectivity.
 
Kati yako wewe usiyejua umuhimu wa direct quotations na mimi ninayesisitiza umuhimu wa direct quotations nani anasoma magazeti ya maana hapa?

Magazeti ya maana unayoyasoma wewe ndo yanasema habari iletwe tu bila direct quotations from primary sources?

Mleta maada yupo katika kiwango cha juu katika kup-resent issues. Maelezo yako ni ya kiwango cha chini cha uandishi ya "Kiranga amesema", kumbe mwandishi yupo juu katika analysis na exploration, kup-resent relationship ya ideas. Uko kwenye basis level ya thinking wakati mwandishi yupo kwenye advanced level hasa kwa great thinkers.
 
Nani aliyekwambia kuwa direct quote haina subjectivity?

Direct quote ni direct quote, period. Baada ya hapo subjectivity of opinions and judgement kuhusiana na hiyo direct quote ndiyo vinaweza kufuatia.
 
Wengine hata wakielewa hawataki kukiri kwamba ili uchambuzi madhubuti kufanyika nukuu za moja kwa moja ni muhimu.

And when cooler heads prevail in seeing this as an issue, they quickly distort the narrative without addressing the fundaments of the discourse.

Unaangalia habari katika miwani ya aina moja. Nani aliyekwambia kuwa direct quote inakuwa na fundamental discourse. It can as well be acquired discourse siyo fundamental.
 
Back
Top Bottom