Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
Wewe ni lini Mtanzania akawa na maisha bora zaidi ya wakati huu? Kwa mara ya kwanza Tanzania tumepata tuzo ya Umoja wa Mataifa ya uongozi bora, jee unajuwa vigezo vinavyotumika?
Kama mnangoja Kikwete aje kuwajaza fedha mfukoni bila kufanya kazi basi mmekosea na mtangoja sana tena sana, si kwa Kikwete tu hata aje nani, hilo msahau. Njooni muone nje watu wanavyojituma, kwa utajiri walionao utadhani kuwa kila mtu atakuwa anazembea, si nchi wanzo fedha, lakini la hasha, kila mmoja yuko mbioni kufanya kazi kwa bidii ili maisha yake yaendelee kuboreka na apate mustakabali wake.
Watanzania wengi bado mnaongelea kufanyiwa, ongeleeni kufanya. Na wale wanaofanya tunawaona ndio wanakuwa waajiri. Watu kama wewe mtabaki kulalamikia mafanikio ya wenzenu daima. Na kwa kuwa ni wavivu kila mnapoona mafanikio ya wenzenu mnafikiri wameiba tu. Hapo ndipo mnaponishangaza mimi. Wewe hufanyi unategemea vipi kupata? utaokota? zitakuangukia kutoka mbinguni? au Serikali itakuja ikuambie chukuwa hizi?
Hapana, Serikali inakufanyia njia za kujiwezesha kuwa ni rahisi, kama ni mfanya kazi kafanye kazi, kama mkulima kalime, kama ni mpiga porojo tu JF, mitandao ndio hiyo bwereree, njoo tu tupige soga hapa halafu usilalamike kuwa "mimi sina". Fanya kazi!
Pia usasahau rekodi yenu ya kuwa Rais wa kwanza kuingiza Kiduku Ikulu na kuwazalisha wanawake wengi mitaani