Huyo ni mwandishi, mtafiti au mtabiri? Je alikuwa anaishi wapi ktk miaka hii ya utawala wa giza wa ccm? Maoni au ushauri wake kwa ccm yalikuwa ni yapi muda wote huo?
Sio kwamba tunapenda kusikia tunayoyataka, au kwamba CDM ni perfect sana. Hapana. CDM ndio kwanza inamea, bado hatujaona itakavyokuwa (stature growth) yake sasa huu uchuro unatoka wapi?
Ok kama anadhani ccm ina wapenzi/wanachama wengi ajiulize hivi; enzi za chama kimoja ilikuwa ni shurti kuwa mwanachama wa ccm. Leo hii wao ccm wanasema (wakijisifu) kuwa wana wanachama milioni tano nchi nzima. Ktk miaka ya uhai wa ccm (miaka 36 peke yake) ina maana kama ingekuwa inapendwa, kama anavyotaka kutuaminisha Mwananzela, basi ccm ingekuwa na wanachama zaidi ya maradufu ya idadi yao. So ccm haikuwahi kupendwa kihivyo nchi nzima....ni dhana ya kusadikika tu.
Kwa mwendo huu wa CDM (opersheni Sangara, M4C nk) inawezekana kabisa kufikia mwakani, 2014, CDM itakuwa na zaidi ya wanachama 5m nchi nzima. Moja ya sababu ni kuwa kuna pool kubwa ya watu ambao hawajawahi kuwa wanachama wa chama cha siasa na hasa vijana, ambao wamezipenda sera, mwenendo na msimamo wa CDM na ambao hawatasimama wala kuyumba popote mpaka wahakikishe CDM imeshika dola ili waweze kutimiza ahadi na sera zao. Hapo ndipo mwandishi angepaswa kuanzia kulinganisha na kuonya NK NK