Rafiki yangu amekuwa tajiri mkubwa Dodoma, ninafuata njia zake. Tuzifuate

Kwahy mkuu unataka wote tukimbilie kibaigwa ndio shida ya sisi wabongo ukiona mwenzio anauza mandaz na anakwambia anapata 10k faida kwa siku na ww unataka upike maandaz uweke jiran yake
Niliweka angalizo hapo mapema Sana, Soma Tena
 
Chamsingi ukiona fulsa sehem kaa kmya ukija humu utashambuliwa mpka bas, kibaigwa kweli wapo matajiri wengi wanaolima na kulangua mahindi mf cripsian mguri mudy pale kwny ofs ya tra n.k chamsingi pale uwende mwnyw ukiwa mgeni wanaogopa kukufanyia Kaz za shamba wanaogopa kutaopeliwa
Nimekuelewa, ni Kama Kuna watu wamekata tamaa hawajui wafanye nini
 
Mkuu unataka tuje kununua mahindi yako yenye sumu? Tulisha tangaziwa kwamba mahindi ya huko Dodoma ya SUMU KUVU, wewe hilo tangazo halikukufikia?
Mwanzoni kabisa hapo kwenye post nimeweka angalizo Soma tena vizuri.
Maana nilijua watu Kama wewe watakuja
 
Trust mi hio 25m unaenda pigwa! Unless kuna biashara nyingine ya kificho ndani ya biashara ya mahindi!
Hiyo ikipotea hakuna shida, nasisitiza nishaweka zaidi yahoyo kwenye business nyingine.
Mfano hardware niliweka Mara 3 ya hiyo, kwani sikujua Kama Kuna kuunga Moto nyumba na Mali yote kwenda?
 
Mimi wazee naona fulsa ipo kwenye kilimo cha alzeti.
Msimu ujao nataka nijitupie, mwaka huu nimejaribu nimeona changamoto zake nilichogundua alzet ni zao safi sana aisee.
Fanya hivyo, nitaendelea kuwapa moyo vijana wote weye uthubutu wa kutafuta.
Usichelewe weka pesa hapo, muombe Mungu Mambo yatakuwa safi
Sera yangu ni utajiri.
 
Kila fursa ina changamoto zake iwe kilimo au biashara so huwez kuacha kufanya Jambo lako kwa ajiri ya kupata changamoto,ila watanzania bwana ukifankiwa kwnye kilimo utaambiwa unaela za kilinge,au unauza nadawa chamsingi Kila mtu ahamini Jambo lake linaloweza kumtoa,kimaisha bas
Nimekuelewa, ni Kama Kuna watu wamekata tamaa hawajui wafanye nini
 
Binafsi napenda kuweka wazi kabisa kuwa Mimi Sera yangu ni utajiri, ninahubiri utajiri tu. Tafadhali Kama wewe una mawazo ya kimaskini hii post inaweza kukuletea shida ya msongo wa mawazo.
Rafiki yangu yupo dodoma muda mrefu Sana tokea tumalize wote chuo kipindi hicho.
Kwao ni dodoma na alianza harakati za maisha hata kipindi tunasoma, tulipomaliza alikuwa tayari kwenye mstari na Sasa hivi ni tajiri mkubwa tu huko dodoma.
Huyu amepata pesa kwenye mahindi kule kibaigwa, ni mahindi tu hakuna kingine zaidi ya hicho kilichompa utajiri. Ila Sasa hivi ana vingine(Malori).
Unaweza kupita sehemu na kudharau kumbe ndipo pesa inapatikana kirahisi hapo. Niseme ukweli sijawahi kupaelewa kibaigwa na nilipomueleza hili alinishangaa Sana.
Amenieleza kibaigwa Kuna pesa nyingi Sana ya mahindi, na hapa tunapoongea nimeomba kuweka pesa kwa kutumia mgongo wake.
Kijana mwenzangu kama upo jirani na kibaigwa hebu jaribu kwenda kufanya research uwekeze ulichonacho kwenye mahindi hata kwa kuanza mdogomdogo, tusidharau Sana sehemu hizi.
Binafsi nimetoa tayari mil 25 kwa ajili ya hii kitu na ninaeleza kupata mil 60 Kama mambo yakikaa vizuri. Najua Sana biashara na najua Kuna kupata na kukosa Ila ni lazima kchukua "risk".
Bila kuchukua risk huwezi kufanikiwa kabisa, huu ni ukweli mchungu.
Kijana mdogo(38) anamiliki Lori 6, na zote anajaza mzigo unaenda Kenya na sehemu zingine.
Nipo tayari kufuata hii njia pia, tukubali tukatae ni lazima tufanye vitu vingi ili tuweze kuwa matajiri bila hivyo tusahau kuwa matajiri.
Umaskini ni mbaya Sana ndugu zangu, na kitu kibaya zaidi ni mawazo ya kimaskini.
Ukiwa maskini hata ukiongea jambo la kuchekesha watu hawacheki.
Hivyo naongeza nguvu nyingine kwenye sekta hii na haswa kupitia mgongo wa huyu jamaa yangu
Naona ndoto nyingi Ila muda nahisi hautoshi kuzitimiza.................!
Pesa ipo sana, ila yapaswa kutumia akili kuipata...!
A stitch in time saves nine.
 
Hapana sio kwamba tunamuomba. Halaf unaelewa bro uliekuzwa nae pamoja, mkikosa mnalala mkipata mnakula, sjui unaelewa? Ila tatizo hatutambui familia nzima hataki mazoea. Ila tushamuacha.

Umefurahi?

Kwanini ma bro wanaotajirikia kwenye kilimo wanakuaga na spiriti hii??
Ninae bro wangu katajirikia mpunga huko mbalali. Ni hivi hivi tuu.
 
Kwanini ma bro wanaotajirikia kwenye kilimo wanakuaga na spiriti hii??
Ninae bro wangu katajirikia mpunga huko mbalali. Ni hivi hivi tuu.
Chunguza vizuri Inaweza kuwa mke or else labda mambo ya masharti. Ila bro wangu ye alitekwa na kitu ya kimbulu sjui Imemuendea Nigeria maana ni shida.
 
Kwa wazee wa kubeti tunasema hizo ni odds 2.7 ambazo ndani ya dakika chache tu bila kukanyaga jaruba hata moja la mahindi unaweza kuwa umetia kibindoni hio hela

Tatzo hela unazopata kubeti sio hela halali.

So utajiri wako unakua una walakini.

Siku ukimrudia Mungu uchumi wako lazima utetereke. Sababu Mungu ataondosha vyote ulivyonavyo visivo na pumzi yake..

Sijaokoka ila nipo makini saana kucheki pesa nnazoingiza. Najitahid saana kila shilingi nnayoipata nimeitolea jasho. Sio ya wizi, kamari, rushwa, biashara haramu nk.

Kulko hiyo kubeti sijui odd 1,
Mara mia niingia majarubani

Nasema uongo ndugu zangu???
 
Naona jamaa umeanza dharau si ndio kwahy mm napigwa miti au lugha za kihuni unazijua sana si ndio?
HAKUNA dharau hapo, Wala hiyo sio lugha ya kihuni bali nashangaa mnapolalamika kuwa mtapigwa wakati uamuzi wa kwenda kufanya ni wako. Na Wala hakuna atayekuja kukulaumu usipoenda. Nilichofanya ni kuwakumbusha tu kwa wale wanaopenda hizo mishe
Nisamehe Kama nimekukosea
 
Back
Top Bottom