Rafiki niliyemsaidia wakati wa shida akanitosa nilipopatwa shida, leo kanifanyia surprise ya kufungia mwaka

Bongotunacheza

JF-Expert Member
Dec 7, 2018
718
1,643
To cut short story huyu jamaa ni rafiki yangu wa tangu utotoni.

Mwaka 2012 nikiwa vizuri sana kiuchumi alipatwa na msiba wa baba yake mzazi. Yeye kwao ndio wa kwanza na ndio mtoto anae tegemewa na familia nzima. Kwao ni Dar ila msiba ulimkuta akiwa kaenda kufanya interview ya kazi Kigoma (alikuwa ndio kamaliza chuo)

Jamaa hakuwa na option zaidi ya kujaribu msaada kutoka kwangu. Nilimlipia nauli ya gari kutoka Kigoma to Dar na alivyofika mjini nikampa Milioni moja na laki nane ili asimamie zoezi lote la msiba. Kwao ni uswazi, michango ya wananzengo haikufika hata 80. Wanaukoo wao njaa tupu. Wote wanamuangalia yeye kwa sababu " alikuwa anasoma chuo kikuu Udsm ambapo huwa wanasoma na kulipwa( bumu) so atakuwa na hela nyingi tu huyu jamaa"

Insha'allah msiba uliisha salama.

Miaka miwili baadae jamaa alipata kazi Serikalini (wizara ya ardhi) hapa hapa mjini Daslamu. Maisha yakasonga.

Mwaka 2020 wakati huo vyuma vikiwa vimekaza kweli kweli kuna mtu mmoja alisema anataka kuuza eneo lake. Kwa bahati nzuri kwangu nilipata mteja ambae alikuwa analihitaji hilo eneo na alikuwa na uwezo wa kulinunua. Ila kabla ya kulinunua jamaa alitaka kujiridhisha kwamba hilo eneo linamilikiwa kihalali na muuzaji.

So nilitakiwa kwenda wizara ya ardhi pale kufanya online search kuona kama huyu jamaa ndio mmiliki halali wa eneo na kama halina mgogoro wowote. Mtu ambae angenisaidia kwa haraka haraka ni huyu jamaa yangu rafiki wa tangu utotoni.

Nilichotaka kwake ni yeye kuingia kwenye system kisha anipe taarifa za hiyo plot.

Ebwana eeh jamaa kasema yeye hana access ya kutazama hizo taarifa ila mtu wa juu yake ndio ana access. So kama nataka suala hilo liende natakiwa nitoe laki mbili. (duh jamaa aliniona kama boya vile) I told him sipo vizuri sina chochote ila eneo likiuzwa basi nitampa hiyo laki mbili anayo akaniambia ngoja aongee kwanza na basi wake.

Majibu boss kagoma anataka laki mbili. Nikamwambia ngoja nikatafute hiyo pesa ikiwa tayari nitamtafuta huku moyoni nikisikitika yaani huyu mwamba anataka kunipiga kwa ishu ambazo hutolewa bure kabisa na Serikali.

Nilikuwa nna mtu mwingine ninae mfahamu ambae alikuwa hapo hapo wizara ya kazi nikamvutia waya wala haikuchukua hata lisaa akanipa taarifa za hicho kiwanja bila kudai hata senti tano.

Jamaa nilimuwekea alama ya x kwenye nafsi yangu.

Novemba 2023: Jamaa kaja na ngonjera sijui kasimamishwa kazi blah blah blah nyumbani hakuna chakula. Nikamwambia sina hata senti tano hela yote Nimetoka kulipa ada (Nilivyo kwama niliwapelekaga hadi watoto wangu shule ya kayumba kutoka English Medium nikaanzisha hadi Uzi hapa JF now nimewarudisha tena English Medium mambo ya hela yamekaa sawa tena.

# Tujifunze kulipa fadhila kwa watu waliowahi kutusaidia.
 
Tenda wema nenda zako usisubiri shukrani
Nope but alini shangaza sana mkuu kukomalia nimpe rushwa licha ya kumlilia shida. Walahi sintomsaidia chochote maisha yangu yote. Nyumba yao ya urithi walishauza akaenda kupanga akanunua kiwanja hakujenga kakiuza hela mbuzi baada ya kupigwa chini kazi hela imekata. Anaishi nyumba ya kupanga ndani hana vitu analala chini ila sintomsaidia tena
 
Sawa mkuu umeniazishia uzi, kweli hali yangu ni mbaya mkuu nipe ata ten ya kula, kule ardhi nilikuwa nakutania nikijua ni utani wetu toka utotoni, nikajua utarudi tena ofisini na namba yako sikuwa nayo mkuu, sema ntakuja home hapo na familia yangu yote tukae😪
 
Mda haujawai kudanganya,
Shida ndo kipimo sahihi cha kuwajua watu walio kwenye circle vizuri
Yes kabisa mkuu na mimi wote walio nitosa nilipokuwa napitia shida nasema sintowasaidia chochote maisha yangu yote nitawasaidia wale tu walio nisaidia. Hata kwenye Biblia imeandikwa Mungu anawapenda wale wampendao
 
To cut short story huyu jamaa ni rafiki yangu wa tangu utotoni.

Mwaka 2012 nikiwa vizuri sana kiuchumi alipatwa na msiba wa baba yake mzazi. Yeye kwao ndio wa kwanza na ndio mtoto anae tegemewa na familia nzima. Kwao ni Dar ila msiba ulimkuta akiwa kaenda kufanya interview ya kazi Kigoma (alikuwa ndio kamaliza chuo)

Jamaa hakuwa na option zaidi ya kujaribu msaada kutoka kwangu. Nilimlipia nauli ya gari kutoka Kigoma to Dar na alivyofika mjini nikampa Milioni moja na laki nane ili asimamie zoezi lote la msiba. Kwao ni uswazi, michango ya wananzengo haikufika hata 80. Wanaukoo wao njaa tupu. Wote wanamuangalia yeye kwa sababu " alikuwa anasoma chuo kikuu Udsm ambapo huwa wanasoma na kulipwa( bumu) so atakuwa na hela nyingi tu huyu jamaa"

Insha'allah msiba uliisha salama.

Miaka miwili baadae jamaa alipata kazi Serikalini (wizara ya ardhi) hapa hapa mjini Daslamu. Maisha yakasonga.

Mwaka 2020 wakati huo vyuma vikiwa vimekaza kweli kweli kuna mtu mmoja alisema anataka kuuza eneo lake. Kwa bahati nzuri kwangu nilipata mteja ambae alikuwa analihitaji hilo eneo na alikuwa na uwezo wa kulinunua. Ila kabla ya kulinunua jamaa alitaka kujiridhisha kwamba hilo eneo linamilikiwa kihalali na muuzaji.

So nilitakiwa kwenda wizara ya ardhi pale kufanya online search kuona kama huyu jamaa ndio mmiliki halali wa eneo na kama halina mgogoro wowote. Mtu ambae angenisaidia kwa haraka haraka ni huyu jamaa yangu rafiki wa tangu utotoni.

Nilichotaka kwake ni yeye kuingia kwenye system kisha anipe taarifa za hiyo plot.

Ebwana eeh jamaa kasema yeye hana access ya kutazama hizo taarifa ila mtu wa juu yake ndio ana access. So kama nataka suala hilo liende natakiwa nitoe laki mbili. (duh jamaa aliniona kama boya vile) I told him sipo vizuri sina chochote ila eneo likiuzwa basi nitampa hiyo laki mbili anayo akaniambia ngoja aongee kwanza na basi wake.

Majibu boss kagoma anataka laki mbili. Nikamwambia ngoja nikatafute hiyo pesa ikiwa tayari nitamtafuta huku moyoni nikisikitika yaani huyu mwamba anataka kunipiga kwa ishu ambazo hutolewa bure kabisa na Serikali.

Nilikuwa nna mtu mwingine ninae mfahamu ambae alikuwa hapo hapo wizara ya kazi nikamvutia waya wala haikuchukua hata lisaa akanipa taarifa za hicho kiwanja bila kudai hata senti tano.

Jamaa nilimuwekea alama ya x kwenye nafsi yangu.

Novemba 2023: Jamaa kaja na ngonjera sijui kasimamishwa kazi blah blah blah nyumbani hakuna chakula. Nikamwambia sina hata senti tano hela yote Nimetoka kulipa ada (Nilivyo kwama niliwapelekaga hadi watoto wangu shule ya kayumba kutoka English Medium nikaanzisha hadi Uzi hapa JF now nimewarudisha tena English Medium mambo ya hela yamekaa sawa tena.

# Tujifunze kulipa fadhila kwa watu waliowahi kutusaidia.
Kaa mbali na wahaya na waha
 
Nope but alini shangaza sana mkuu kukomalia nimpe rushwa licha ya kumlilia shida. Walahi sintomsaidia chochote maisha yangu yote. Nyumba yao ya urithi walishauza akaenda kupanga akanunua kiwanja hakujenga kakiuza hela mbuzi baada ya kupigwa chini kazi hela imekata. Anaishi nyumba ya kupanga ndani hana vitu analala chini ila sintomsaidia tena
Duniani kuna watu wa hovyo sana. Wengine ukiwafanyia wema wanakuona fala.
 
Na Mimi Kuna rafiki yangu kanikacha kisa kapata kazi wakati Mimi Niko vyema nilimsaidia sana kavaa nguo zangu sana Mama yake kala vyangu sana jamaa ata simu yake sina nina miaka saivi hila sina shaka naye namuombe kila la kheri uko alipo Dunua duara.
Mimi naendelea kukomaa na connection nitoboe
 
Jua ukitenda wema unajitendea mwenyewe, na ukitenda ubaya unajitendea mwenyewe.

Malipo ya mungu ni makubwa kuliko binadamu, ukitenda wema pita hivi, mungu atakulipa tu wema wako, iwe hapa duniani au kesho akhera malipo yapo costant, haijalishi uliyemtendea nae atakutendea wema au lah, akitenda wema nae atakuta malipo yake, na akikutendea mabaya nae atakita malipo ya ubaya wake.
 
Na Mimi Kuna rafiki yangu kanikacha kisa kapata kazi wakati Mimi Niko vyema nilimsaidia sana kavaa nguo zangu sana Mama yake kala vyangu sana jamaa ata simu yake sina nina miaka saivi hila sina shaka naye namuombe kila la kheri uko alipo Dunua duara.
Mimi naendelea kukomaa na connection nitoboe
All the best mkuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom