Proper recording: Nini kilimbadili Mzee Mwanakijiji?

Proper recording: Nini kilimbadili Mzee Mwanakijiji?

Naona kuna mpambano kati ya Chadema Die Hard, Chadema Puppet, Chadema Great Thinkers, na Chadema Tantararira.
Mkuu kuna watu humu wamegeuka kuwa watabiri...ma-shekhe Yakhaya. hawakawi kusema atakae simama na Lowasa/Membe atakufa...
 
Pasco, ingawa ulimpaka mafuta kwa mgongo wa chupa mgombea "wetu" ENL, wakati uleeee kua kachafuka sana tumpake mafuta ameremete.

Nakuhakikishia kua 2015 ni CCM tena! Kwa hili tupo pamoja unless CDM wabadilike sana. Kwa style hii ya kukosa nidhamu ya viongozi wakuu (ZItto mmojawapo) CDM hawana chao 2015.

Rusheni mawe ila ENL all the way!

Mkuu FP,
Vipi kuhusu afya ya Edward Ngoyai Lowassa, maana hadi konyagi kashauriwa aache kunywa, vipi ataweza mikikimiki 2015?
 
Mwaka 2005, Mwanakijiji alifanya kosa ambalo baadhi tulilifanya pia mwaka 1995. Mimi nilimuamini sana Mwalimu. Na kwa kuwa amekwishafariki nitaendelea kumwamini kwa mambo mengi aliyoyasimamia isipokuwa jambo moja tu: Kumsimamia Mkapa achaguliwe kuwa Rais wa NCHI hii. Nilipoona Mwalimu ameinuka na kuzunguka nchi nzima akimfanyia Mkapa kampeni nikadhani hapa tunampata Rais Msafi, mwadilifu, mtu, binadamu, mchapakazi na mkweli sana kama alivyokuwa Mwalimu. Nilidhani Mwalimu anamwelewa vizuri Mkapa na kwamba asingemwangusha wala kumbadilikia akishayapata madaraka ya URAIS. Haikuwa hivo.

Mwanakijiji naye aliamini Kikwete angeweza kuwa chachu ya mabadiliko kwenye safu ya viongozi wengi walioko CCM. Haikuwezekana. Mimi nilimshtukia Kikwete mapema tu baada ya kuona matumizi makubwa mno ya pesa katika kuusaka Urais wa JMT. Nakumbuka mwaka 1995 yeye na Lowasa walikodi ndege kwenda Dodoma kuchukua na kurudisha fomu za kuteuliwa na CCM ili wagombee Urais. Nikaangalia pia na aina ya watu wanaomzunguka Kikwete kumsaidia aupate Urais. Wengi wetu tuliomo humu nchini tukashangaa Kikwete na genge lake kutouvunja MTANDAO wake tangu mwaka 1995. Mtandao huu ukazidi kujiimarisha zaidi kimkakati, kimbinu na kifedha huku ukienea NCHI nzima. Wakafanikiwa mwaka 2005 kumuweka Kikwete madarakani. Nitashangaa kwa Mwanakijiji na weledi wake wote hakuwemo kwenye mtandao huu ambao ulienea hadi kwa baadhi ya Watanzania walioko nje ya nchi!

Kikwete hakuwa na jinsi. Alipoanza UTEUZI tu ikabidi amteue Lowasa kuwa Waziri Mkuu. Rostam akawa mweka hazina wa CCM! Wenye akili timamu tukajua NCHI inakwenda kusiko. Hawa jamaa wawili wameondoka kwenye nyadhifa hizi. Madhara na majeraha walioacha hayataki kupona. Hivi watu makini kama Mwanakijiji wangeacha kubadilika kweli?

Kwa ujumla sio Mwanakijiji peke yake aliyebadilika. Tupo wengi na wengine bado wamo ndani ya CCM kwa taabu na njaa zao tu. Nampongeza Mwanakijiji kwa kuwa yeye akibadilika anaandika. Anaonyesha wazi msimamo wake MPYA. Mwanakijiji wanafanana kidogo na Jenerali Ulimwengu.
 
2010 mnasema chadema haikujipanga kiuongozi na hili hamkulisema wakati ule na mpaka mlishiriki kuandika ilani ya chadema ya uchaguzi ..wala hamkushauri ..leo mnasema chadema haijajipanga na bado wanaendelea na makosa yale yale na mnadiriki kusema hawawezi kushinda ...sasa je ni kwamba chadema wanakataa ushauri wenu? .....mnawauma kisha mnawapuliza!!.....

Watu wengi wanaopinga CDM kwa mgondo wa ushauri wapo too vulnerable.Wanatumia nguvu nyingi sana kulinda vitu vidogo.Ktk Logic ulichotumia hapa tunaita counter example, na zipo nyingi sana zinazoweza mpa MMK shida sana kuliko angesema sasa naikubali CDM na nitajitahidi ipa ushirikiano.Its a matter of ego tuu.Nani hajui kuwa CDM mmoja bila kujali elimu yake na uzoefu ni effective kuliko CCM wangapi?Na mwana CDM ana chance kubwa sana kufanya kitu kipya vyema kuliko mwana CCM.Sasa leo rais wa CCM na waziri wake wamejifunza Oman jinsi ya kutumia rasilimali vyema kwa manufaa ya raia.Kitu mabcho ni very obvious na kinasemwa sana humu nchini.Kitu kinachoonesha kuwa CCM pamoja na kuwa na miaka 50 bado wahahitaji jifunza toka kwa "people power".Kuna wajinga walikuwa wakimpinga mtu ktk dili ya kusupply software.Wao walijikita kutaja uzoefu wao ktk kuwepo katika technology, na waliitumia kama sila ha ya kuwashambulia wengine.Sikuona haja tena ya kuvumilia huo ujinga ,nikawauliza Microsoft na yahoo wana nini cha Kujivunia mbele ya google kampuni yenye miaka chini ya 8 ktk soko?Umri wa ttcl una nini cha kujivunia mbele vodacom ktk mobile money transfer and banking?

Ni kutokana na issue kadiri zinavyotokea na maeneo yake ndipo utaweza linganisha uzoefu, uimara na ubunifu.Dunia ya leo inahitaji akili tafiti na mipango ya muda mrefu na mfupi.CDM wameonyesha hayo mbele ya CCM ambao wamewekeza kuficha uovu kuliko kutetenda makosa.CDM wamewekeza kutokufanya makosa na hivyo kutohitaji kuficha kitu.CCM wapo tayari kuua ili kufucha makosa na si kutotenda .
 
Mzee Mwanakijiji, hilo la kuhitaji more nalikubali sana ndio maana mimi nawakomalia sana Chadema to do the right thing and doing the things right,!. Ila pia nimeshajifunza humu kuhusu ukosoaji wowote wa Chadema what does that mean na I won't stop because 2015 is do or die!, tutawakosoa na tutawapitisha kwenye tanuru la moto bila huruma, ili wasiostahili, wateketee mbali na moto, ili nchi nchukuliwe na wale tuu wanaostahili na ikishindikana, basi wataendelea waliopo japo hawastahili mpaka wanaostahili watakapo kuwa tayari!.

More of what?Kwetu sisi more is harmful.More food kuvimbiwa na obesity, more sex (less love,less working time,more inachosha), more of islam(alqaeda,taliban),more of christianity(more kukemea mapepo na kuwafanya wengine matajiri),more ujamaa(more uovu na kuabudu serikali).Urais si factor kubwa kwa CDM ndio maana miaka yote walikuwa wakijenga level za chini,Thisi time wana option ya kukamilisha kila level chini na kuchua urais, au hata kutouchukua na bado wakaongoza nchi.Sasa hivi CCM wanakwenda kwa kusikiliza walichosema CDM(kinyume chake au kama kilivyo), CCM vitu vingine wanafanya huku wakihisi CDM yupo pembeni yao anawangoja awaadhibu.Last week nilikuwa AR nilibahatika pitia maeneo walipokuwa wana CCM waliokuwa katk chaguzi zao.Wote walikuwa wakitafutana mchawi,kila mmoja alikuwa akiona kuwa mwingine ni pandikizi la CDM kuliko hata la kambi zao.na hii ni nchi nzima.Hata hao mawaziri wa CCM wengi tuu wanahisiwa kuwa mapandikiri ya CDM au wana uwezekano wa kutumika kwa vile wanapenda madaraka na ni wabahatishaji tuu ambao wameshajipendekeza CDM kuwa kikitokea cha kutokea CCM basi wasiachwe.
 
HIvi watu mnaposema CHADEMA hawajajipanga mnamaanisha nini hasa:
-Kwamba mnaogopa nguvu ya UCHAGGA iliyoko mle?
-Kwamba mnahofia nguvu ya UKRISTO iliyoko mle?
-Kwamba CHADEMA yenyewe sio TAASISI ni mali ya mtu au kikundi flani cha watu?
-Kwamba vyombo vya DOLA vimeshindwa kupenya mle ndani ya CHADEMA?
-Kwamba CHADEMA bado sio chama cha KITAIFA?
Mnataka wajipangeje hasa! Kuweni wawazi basi. Uongozi huu wa sasa wa CHADEMA wanaweza kujipanga tofauti na walivyo sasa? Kumbukeni CHADEMA ni chama pekee mbali na CCM ambacho tunasikia wanafanya CHAGUZI na VIKAO katika ngazi mbalimbali za muundo wake.
 
Naona mkuu MMK anaingia na kutoka, nilidhani angeweza jibu haraka haraka ili angalau yake tuliyoanzisha nae tuyakamilishe ktk session hii na watu wandelee na mambo mengine.Wel, nami nahitaji fanya vitu vingine offline.Pengine nitaendelea nikirudi.Ningeomba tuu MMK arudie kupitia mazungumzo ili aje na majibu au maelezo mazuri pale aliporukaruka.Natetagemea atakuwa tofauti na ZZK ambaye huwa anafanya mambo bila kujua nini anakiweka ktk stake,nategemea kuwa atajua uzito wake ktk fikra za watu kisiasa na jinsi gani vizazi vijavyo vitakavyopata shida yagundua makosa ktk anchofanya hasa ikizingatia kuna maandiko mengi sana ambayo si rahisi mtu kuyapata yote na kuweza linaganisha mambo.Nategemea pia katk machapisho yake basi aweke stage ya kupitisha kwa critics na kwa washabiki au slanderers atakaowaita critics.Nimeona vitabu kibao vya kitanzania vina makosa mengi sana ndani yake achilia mbali hayo ya kuwa na cover hovyo, page zimepandana, etc.Na hivi vyote vimezinduliwa na watu wakubwa na kuchapishwa na best printing press nchini.Yote haya ni kwa vile watu wapo very careless,MMK naye aisangukie huko alipoangukia ZZK kwani sasa hivi wafuasi wake wanatoka povu km ZZK mwenyewe pale anapojikuta kuwa kakosea na hawezi jitetea,wanaishia kuleta sababu za kitoto zozote zitakazokuwa karibu yao.
 
HIvi watu mnaposema CHADEMA hawajajipanga mnamaanisha nini hasa:
-Kwamba mnaogopa nguvu ya UCHAGGA iliyoko mle?
-Kwamba mnahofia nguvu ya UKRISTO iliyoko mle?
-Kwamba CHADEMA yenyewe sio TAASISI ni mali ya mtu au kikundi flani cha watu?
-Kwamba vyombo vya DOLA vimeshindwa kupenya mle ndani ya CHADEMA?
-Kwamba CHADEMA bado sio chama cha KITAIFA?
Mnataka wajipangeje hasa! Kuweni wawazi basi. Uongozi huu wa sasa wa CHADEMA wanaweza kujipanga tofauti na walivyo sasa? Kumbukeni CHADEMA ni chama pekee mbali na CCM ambacho tunasikia wanafanya CHAGUZI na VIKAO katika ngazi mbalimbali za muundo wake.
Nadhani umeongea vyema zaidi yetu kwa lugha nzuri.Pengine waliowekeza ktk uandishi kam MMK wangeweka fikra zao hivi.
 
Ndugu yangu wowowo napenda kuwa muwazi kwako juu ya upinzani wako kwa hoja za MM mimi pia ninamuunga mkono MM kwa msimamo wake kwani Watanzania hawataki mabadiliko yeyote bali wanataka mabadiliko yenye dira itakayo likomboa TAIFA
wameikosoa serikali tumeona sasa ni wakati wakuwaeleza Watanzania wenye kiu ya Maendeleo mipango yao ni ipi dhidi ya adui umasikini unaowakabili Watanzania. Mimi kama mtanzania mzalendo mzawa nataka kuiona Tanzania yangu ikistawi katika kila nyanja kwa mikakti itakayo wekwa na iweze kutekelezeka bila kushindwa kwa kutumia rasilimali tulizonazo nahili linawezekana
Ni vyema vyama vya upinzani vikajipambanua juu ya siasa zao za uchumi kwani ndio msingi wa dira itakayotukwamua kiuchumi. Ninawasiwasi wanasiasa wetu wengi ni wachumia tumbo na hawana chochote wanachofikiri juu ya mapinduzi ya kiuchumi unyonge wa watanzania kwa ujumla kwa mtazamo wangu kukosoa bila kuwa na mipango mkakati mbadala sio suluhisho la tatizo tulilonalo. Wapinzane wajipange kama ambavyo Mh. Zito ambae naomba nimtofautishe na wanasiasa wengine uchwara wachumia tumbo, kijana jasiri mwenye vision ya nini anataka kuifanyia nchi yake kwangu mimi huyu ni mtu ambae angeweza kuwakomboa Watanzania nimesoma makala zake hivi karibuni kuhusu marehemu Zenawi aliekuwa Waziri mkuu wa Ethiopia kwa hakika ninaona kiongozi shupavu na mwenye mapenzi na nchi yake na mwenye mawazo mbadala ambayo yaweza kabisa kuwa suluhisho la matatizo tulionayo.
 
Inabidi wakati mwingine tuwe tayari kushauriwa,kukosolewa pamoja na kuambiwa ukweli mchungu ambao wengi hapa mnajaribu kuzijibu hoja za MMK NA PASCO kwa hoja dhaifu bdala ya kukubali ukweli wanaousema mm ni MWANACHADEMA lakini ni ukweli uliodhahiri 2nahtaj kuwaambia wananchi 2tawafanyia nn wakitupa dola sio kuwaeleza mabaya ya CCM ilhali hatuwaambia tutawafanyia nn ili kuondokana na lind la umasikini unaowafanya waichukie CCM. CHADEMA WANAHITAJ MABADILIKO MAKUBWA YA KISERA KATIKA KUELEKEA UCHAGUZ MKUU 2015.NAKUBALI WANANCH WANAHTAJ MABADILIKO LAKIN CDM HAWAJAJIPANGA
 
MMK... be the change you want to see..
nimakukubali kwa hoja.. hebu simama na CHADEMA kwa ajili yetu wanyonge.
Asante.
 
Mkuu MMM,
Hoja yako kuu ni kuwa CDM haijajipanga, hujaelezea kuhusu M4C inayoendelea kama sehemu ya kujipanga! Pia unalalamikia migawanyko iliyopo CDM huku ukisahau kuwa CCM ni chanzo kikuu cha migawanyiko kwenye vyama vya upinzani! Nakuona kama mtu wa kukata tamaa haraka sana japokuwa unataka kujiaminisha kuwa "hushabikii matukio" bali fikra! Ukisoma between the lines kwenye hoja zako zimejaa matukio zaidi kuliko kile unachokiita fikra, ndio maana umeanza na kabla ya uchaguzi na baada ya hapo, huku ukionesha kuchanganyikiwa kuwa ubaki CCM au CDM! Sijui kama wewe ni mtu wa msimamo kama ulivyofanikiwa kuwaaminisha wengi! Mada yako kwa ufupi imenishangza sana, unatumiwa na CCM kama ilivyo kwa akina Zitto Kabwe, usitudanganye, huwezi kuwatumikia mabwana wawili (CCM vs CDM)!
Mimi awali alikuwa ananivutia sana na uandishi wake lakini baada ya kusoma sana makala zake nikagundua ni za kijanja kijanja sana za kuvizia matukio na kujifanya utabiri siku hizi nikiona makala zake wala sipotezi muda kuisoma mapaka nitakapo maliza za wabdishi wengine
 
1.MKJJ yuko katika payroll ya Serikali katika kazi ya usalama wa Taifa. Majukumu yake hayafuati muundo wa kawaida(organogram) uliopo.

2. MKJJ ni mhitimu wa shahada ya kwanza (BA in Political Science)- Tanzania na pia Shahada ya uzamili (MA in Mass Communication & Media Arts)- USA. Baadaye alifaulu vizuri sana mafunzo ya upelelezi (Intensive course in Nationalism & Espionage) – Cuba chini ya Mwalimu wake gwiji aliyempenda sana kwa jina Mosses Powel . Hii inaeleza sababu ya MKJJ kupewa nafasi ya kuwa muhudumu (Usher) mmojawapo katika mazishi ya Powell 22.01.2005. Alipelekwa pia Trinidad & Tobago kwa ajili ya mafunzo ya ukakamavu na ulinzi wa kujikinga chini ya kitivo cha Powell ambaye ndiye mwanzilishi wa mashambulizi ya Sanuces Ryu Jujutsu lakini bahati mbaya MKJJ hakuwa mzuri sana katika somo hili.

MKJJ baada ya kushauriwa , alichagua kuendelea zaidi kubobea katika mbinu za kipepelezi za steganografia (steganography), Saitografia (Cytography) na Utafiti (Research) siraha zilizompa nafasi kupata mazoezi kwa njia ya vitendo katika Wizara ya Ulinzi ya Marekani (Ministry of Defence).


3. Kwa sasa MNKJJ anafanya kazi ya kunusa na kuwachanganya Watanzania kwa kuandika na kuongea kwa style ya kukandia Serikali kwa sana kupitia majamvi na majukwaa mbalimbali kama vile JF na magazeti mbalimbali yaliyo katika mtandao.

4. Kwa kutumia utaalamu wake wa sanaa na fani ya uandishi na utangazaji, MKJJ anajificha ndani ya mbinu ya kijasusi ijulikanayo kama ‘The Italian Strategy of Tension with False Flag’. Ingawa ni mwanachama CCM lakini anapokuwa mtandaoni huvaa ngozi ya mbwa mwitu na kujiita Mkuu wa Taasisi ya Kitanzania ya Demokrasia, Maendeleo na Amani (TAKIDEMA). Kazi zake ni kama ifuatavyo:-

a. Kuanzisha mada chokozi (provocative topics) zenye kuleta hisia kali akisukuma makombora kwenye Serikali ikiwa ni namna ya kuwachokoza wananchi ili mnapoanza kusema au kuandika basi yeye anachukuwa notisi zake na kuwakabidhi waliomtuma kwa ajili ya kurekebisha panapotakiwa haraka iwezekanavyo mfano katika moja ya jibu lak leo humu katika thread hii amesema aliyependekeza IGP Mahita aondolewe na ndie alitoa pendekezo la kugawa Dar-es-Salaam kama mikoa ya polisi (kanda). Pendekezo hili lilichukuliwa mara moja.. Hadhira yake kusudiwa ni hasa Watanzania walioko nje na hususani wasomi ambao wanaweza kuleta upinzanina ndio hawa aliokwaruzana nao wakati anapinga swala la uraia wa nchi mbili. sababu iko wazi nayo ni “you are either with us or against us.....I'M out!!

Kilichoandikwa hapo juu kina ukweli fulani lakini si ukweli wote. Kwa hiyo hili ni kasa mnalishwa na Edson halafu nashangaa kuona MM hajalipinga.

Mimi nimesoma darasa moja na MM hapa Tanzania. Na alikuwa mwanamapinduzi wa dhati nilipokuwa naye. Hakusoma BA pale UDSM, bali alisoma kozi nyingine( kwa sasa naihifadhi). MM amesoma Masters ya Uchumi USA. Lakini sasa MM amebadilika. Tulipokuwa chuo kaka zetu waliotupika kuwa wazalendo ni kina Kitila Mkumbo ambaye wakati huo alikuwa Rais wa DARUSO. Jakaya Kikwete ni sisi tumechangia kwa kiasi kikubwa kumweka madarakani na ndio maana tunatamani tumtoe hata leo kwa jinsi alivyotusaliti. RIDHIWANI ANALIJUA VYEMA HILI. NCHIMBI NDIYO KINARA HASWA(MBA UDSM!!!!)

MMM alikuwa ni kiongozi wa DARUSO Kwenye wizara nyeti ( Naihifadhi kwa sasa). MM alifukuzwa pamoja nami kwenye mgomo wa mwaka ambao kulikuwa na uchaguzi wa Rais, Hivyo MM hakumaliza masomo yake TZ. Alipoenda marekani kwa jitihada za kuuza ng'ombe wa mama yake kijijini ndipo alipobadilisha masomo.

MM hakupitia Mbweni hivyo si mwajiriwa wa TISS hata kidogo! Huwezi kuwa Ofisa wa jeshi kwa kupitia kwa amiri jeshi mkuu bila kupita Monduli kwa JWTZ au Mbweni kwa kupitia TISS. Japo sikatai kuwa anaweza kutumiwa na TISS kama anavyotumiwa mgombea Urais wetu Zitto Zuberi Kabwe.( Sijui kama anakumbuka kiapo chetu pale nyumbani kwa mama yake Magomeni mwembechai- kwa sababu tume ya madini ya Kikwete ilimvuruga kabisa)

Kwa kifupi niseme tu hapa mnalishwa kasa na Edson, na jambo la pili ni kuwa kina MMM wana msemo wao huko wanakotumiwa kuwa 'every head has got a price tag on it'.
 
Mkuu Mzee Mwanakijiji,ebu kuwa fair kwa chadema tafadhali,ni ombi tu mkuu!Ebu ona unavyojichanganya na kutuchanganya at the same time...Hapo chini ni kigezo kuhusu mgombea ama kiongozi wa chadema.

Lakini tena kipimo chako wakati wa JK kilikuwa hicho hapo chini...


Mkuu hizo ni double standards zinazoonyesha uonevu wa wazi kabisa!

Hakuna chaguzi iliyosumbua fikra zangu kama uliompa ushindi wa kishindo JK 2005 , niliwahurumia sana watanzania lakini nilimuhurumia sana MM baada ya kuingia naye kwenye mtego wa kuweka matumaini yake kwa JK , kwa watu ambao tulijua mbinu za JK kuingia madarakani zisinge weza kumfanya kuwa rais bora yeye MM alimuona JK kama nabii aliyetabiriwa sasa leo anakuja na story tofauti, so MM siyo mtu wa kumtumaini kwa kila jambo leo anaweza kusema hili akiona hali imebadlika anatumia maneno ya kiujanja ujanja kuaminisha umma tofauti.
 
Mkuu FP,
Vipi kuhusu afya ya Edward Ngoyai Lowassa, maana hadi konyagi kashauriwa aache kunywa, vipi ataweza mikikimiki 2015?
Hili la afya linajulikana wazi ndio maana nguvu kubwa sasa inaelekezwa kwa Membe!. EL ataendelea kutumika kwa "mass mobilization" na kuileta kambi yake kwa Membe, then anakuwa disposed he is done!.
P.
 
Nimesoma thread hii na maoni ya members nikakakumbuka mbali sana....sijawahi kusema mahali ila leo ntawaeleza kisa hiki.....

Wakati niko form six zaidi ya miongo miwili iliyopita (tosamaganga sec) kulikuwa na mashindano ya mpira kati ya timu ya shule na wanakijiji....wale wanakijiji walipenda sana kutufunga mara kwa mara .binafsi nilikuwa sio mchezaji bali mtazamaji na mpenzi wa timu yangu ya shule na nilikuwa sipendezwi na namna wale wanakijiji walivyokuwa wanatufunga kila mara.


Siku moja tukawa na mechi na hawa wanakijiji na mshindi wa mchezo ule alikuwa anaondoka na Mbuzi (beberu)... asubuhi wakati watu wanajiandaa kwa ile mechi na baada ya mwl wa michezo kupanga kikosi ..wazo likanijia kichwani na kusema kuwa sitaki hawa wanakijiji wamchukue mbuzi maana niliamini kabisa kuwa wanaweza kutufunga.. .
Bila kumwambia yeyote nilienda ipamba hosp na kufanikiwa kupata bomba la sindano kisha nikarudi shule na kumfata mzee aliyekuwa anatunza funguo za maabara na kuingia maabara na kujifanya nafanya mafunzo ya practical(chemistry)..lengo langu kuu lilikuwa ni kuiba acid (conc. Sulphuric acid na conc. Hcl)..nilifanikiwa...
Mda wa michezo ukafika tukashuka uwanjani(msiwasi) na mechi ikaanza mda wa jioni saa kumi na nusu....mpaka inafika dakika ya 70 timu ya shule (tosaboys) walikuwa nyuma kwa magolli mawili na dalili za kurudisha magoli hazikuwepo maana walielemewa sana...huku uwanja ukiwa umefurika watu(wanakijiji na wanafunzi+ walimu) nilijipenyeza hadi meza kuu walipokuwa viongozi wa kijiji na walimu na pembeni yake alikuwa amefungwa yule mbuzi...

Pasipo mtu yeyote kuniona wala kutambua na kwa njia ninayoijua mimi nilimchoma yule mbuzi sindano ya acid na kuondoka kuelekea upande mwingine wa uwanja . mbuzi alilala chini na badae kidogo alikufa na wengi pale uwanjani hasa wlaiokuwa karibu na mbuzi walidhani amelala usingizi kumbe alikuwa amelala kweli!!
Timu ya kijiji ilimkosa mbuzi na mpaka leo hawakujua chanzo cha kifo cha mbuzi yule..walimzika...


Ukiniuliza leo kwa nini nilimchoma sindano ya acid mbuzi yule ntakwambia sikutaka kombe(mbuzi) achukuliwe na wanakijiji....ukiniuliza maswali zaidi juu ya ubora wa timu yetu, formationa ya timu uwanjani, na ubora wa timu ya shule na mazoezi naweza nikawa sina jibu ila sikuwapenda tu hawa wanakijiji wamchukue yule mbuzi.....

Sasa nikija kwenye mada hii inayojadiliwa humu hasa upande wa majibu (coments)toka kwa members inaonyesha wtanzania wengi wanaweza kuwa kama mimi juu ya kitendo nilichomfanyia mbuzi!! ..kama mtu unaamua kumsapoti mtu eti kwa sababu imeonekana anapendwa na wengi basi kuna shida kubwa sana nap engine ni kuwadanganya na kuupindisha ukweli....au mwingine akisema chama hiki hakijajipanga pasipo kusema hawajajipanga vipi na nini hasa mnataka wafanye ili 2015 washinde siyaoni majibu hayo..isipokuwa maneno maneno tu kuwa 2015 ni kufa au kupona na kwamba ccm itashinda tena... waleze watu kwanini washinde na hawa wengine hwajajipanga vipi?

Bado naona kuna shida kubwa sana miongoni mwa wananchi wa Tanzania na tatizo kubwa liko kwa wasomi wa nchi hii na hawa ndio wanaoyumbisha wananchi kwa maneno maneno yao yasiyokuwa yamsingi.. na kama wananchi wasipotambua na kuchambua ni nani hasa anawafaa kutoka kwenye hivyo vyama vya siasa basi huko mbele si ajabu atachaguliwa mtu ambaye hatadumu kenye kiti hicho ...''ataondolewa kwa namna itakayofaa ili kulinda amani ya YERUSALEMU''...lakini hatua hiyo itafanyika pale tu upuuzi unaondelea sasa utaendela baadaya 2015.. watu wamechoka!


Ni jikumu la wanasiasa kunadi sera zao na wananchi wafanye kuchagua wanayeamini na si kudhani atawafaa.. msiwapoteze na kuwadanganya...

Kuna siku wakati wa mwinyi akiwa ni rais wa nchi hii...mwalimu nyerere alimuta rais (mwinyI) , waziri mkuu(malecela) na kama sikosei makamu wa rais... walikwenda hadi kwa mwalimu pale msasani na hawakujua nini mwalimu amewaitia ..msafala ukafika pale na mwalimu akaarifiwa kuwa wageni waheshimiwa wamefika.... mwalimu akawapokea na wala hakuwangiza ndani ..baada ya salamu tu aliwapeleka kwenye bustani yake ..kisha akaangua mapapai matatu makubwa na mazuri kisha akawagawia wale waheshimiwa watatu kila mmoja la kwake na kuwambia '' haya ni matunda toka katika bustani yangu, chukueni mwende mkale na familia zenu ndicho nilichowaitia''... msafara uliondoka pale msasasani kwa mwalimu huku waheshimiwa wakiwa na maswali mengi na kila mmoja aliongea la kwake... nampaka leo sijui kama walielewa hasa sababu ya kuitwa pale...ulikuwa mwito wa kupewa mapapai?!!


Nawapa kisa hiki nikiwa na maana kwamba mwaka 2015 mnaweza kuchagua mtu na kumsimika pale huku yeye mwenyewe asijue yuko pale kwa sababu ipi hasa na kakaapale kwa kipindi chote na kinachomuweka zaidi ni nguvu ya pesa na upuuzi wa kununua watu na kujaza propaganda zauongo miongoni mwawananchi....epukeni hili na epukeni kabisa wananchi....

Kwa upande wa ccm kazi siyo ndogo ya kumpata mgombea sabubu kubwa ni makundi na mabaka mabaka ambayo chama hicho kinayo....lazima chama kijipange sana ..na kuanzia mwakani ni mwaka mgumu zaidi kwa ccm huu ugumu utaenda hadi 2014 mwanzoni..hili linawahusu sana viongozi wa juu na wale wanaoutaka urais...


Kwa chadema warekebishe migogoro ya chini kwa nchini ndani ya chama chao na wajiangalie sana juu ya magugu yanayokinyemelea chama. .nitazungumza zaidi mara baada ya kazi inayofanyika sasa juu ya vyama hivi viwili (chadema na ccm) kukamilika..

Vinginevyo wasomi na wataalamu wa uchambuzi ninaowaona humu msiwapotoshe wananchi juu ya ukweli wanaouona kwa macho na hivyo na wao kufanya kama mimi nilivyomfanyia mbuzi eti kisa sikutaka wanakijiji wamchukue pasipo kuangalia uwezo wa timu yangu, formation ya mchezo,moyo wa kujituma, kucheza kitimu, na mazoezi...
 
CDM haiwezi uliza watu wenye loosing spirit chochote.kama wote hapa hamkuweza ona ilipoanzia CDM na vikwazo vilivyorukwa, ni vipi mnaweza elewa vision ya waanzilishi wa chama?Ni kama mazaramo anayefikiria kwenda mcheza ngoma binti yake akitaka mshauri mchaga kuhusu shule na biashara.

Jamani acheni ujinga na uzembe,hizi nafasi mnazojipa za ushauri wakati hakuna mlichoweza achieve ni kufuru na matusi.Kuna mwenye pilot chama aliweza kitoa hata hatua moja kwenda nyingine?My friend aliapa kutowatumia consultants wa kitanzania wanaoganga njaa halafu wanataka mshahuri mtu aliyetafuta hela from the scratch to somewhere ambapo kila mtu anawakubali.Atakushauri nini zaidi ya kukupa ma theory kibao ambayo hata wao hawajui kuyatumia.

Nimekuta mjinga mmoja anamshauri mtu afungue akaumti bank na kufuata sheria ili a qualify kwa mkopo.Huyu jama ambaye hajaenda shule alikuwa na dreamz za kuifanya bank ndio equalify kumpa mkopo, na kwanini akapoteze muda kupanga foloeni ktk bank kwa transaction zinazoweza pitia ktk M-Pesa?Wakati huyu msomi anapiga blah balah kuwa ni Impossible,jama akampa clue kuwa maafisa mauzo wa bank wanashinda ktk office yake kila siku,bado mshauri hakuanza ona kuwa demand imeshift kutoka kwa mfanyabiashara na kwenda kwa bank.Hivyo mfanya biashara sasa anweza weka conditions zake kwa bank.Jamaa yangu akampatia jamaa bia na pombe.na hela kidogo huku akimwambia kamkubali san aelimu yake.Ikawa misho.Hivyo hivyo CDM inaendelea waonyesha critics kwa vitendo ,wakati wao wakiwa busy kutoa plan kichaa nyingi, na kutafuta conspirancy theories nyingi za kuelezea mafanikio ya CDM kama by chance na sijui mapenzi ya watu, mara sijui mapungufu ya CCM.

Ulisoma maelezo yako ukayaelewa kabla ya kuituma kweli?
 
Sawan mkuu Mwanakijiji. Nazikubali fikra zako. Natumaini sasa kwa ujumbe huu na hizo link kadhaa, tumekuelewa zaidi. Nachoomba utuwekee link ya maoni yako ya mgawanyo wa jiji la dar katika mikoa ya kipolisi.

Anakunywa chai akimaliza atakuja kukujibu Boss
 
Back
Top Bottom